grand millenial
JF-Expert Member
- Jul 29, 2018
- 3,943
- 5,550
Hakuna cha "mercy killing" uuwaji ni uuwaji tu kuondoa uhai wa mtu unasema ni mercy?Pole kwa kuuguza kaka , hamna jinsi kama yeye aliwajibika ipasavyo wakati mnakua pengine mlikua hata zaidi ya watoto watatu !! Uwajibikaji umehamia kwenu hamna jinsi pambaneni mkishirikiana na madaktari wawaeleze hali halisi !!! Ingekua kwa wenzetu kuna "Mercy killing"
Neno la Muumba wetu ni amri hivyo ni amri kuwalea wazazi wawili kwa heshima na kuwajali.Na Mola wako Mlezi ameamrisha kuwa msimuabudu yeyote ila Yeye tu, na wazazi wawili muwatendee wema. Mmoja wao akifikia uzee, naye yuko kwako, au wote wawili, basi usimwambie hata: Ah! Wala usiwakemee. Na sema nao kwa msemo wa hishima
hii ni Qur'an inatuamrisha haya
kumbuka ww ulivokua mtoto huenda ulikua msumbufu sana ila wazazi wako walikuvumilia iweje leo ww huwezi kumvumilia mzazi wako?
Yawezekana angekua tajiri mkubwa tu lkn alisacrifice akakulea ww kwa pesa zake leo hii iweje yy ndio sababu ya ww kupatikana lkn unamdhalilisha kiasi hichi
Najivunia kua Muislamu kwani Uislamu umetufunza yte hya
Hoja hupingwa na hoja lete aya inayopinga aliyoyatoa huyo member ikiwa wewe unaijua dini kuliko yeye.mkuu.. wewe huujui uislamu kuliko mimi . ungenyamaza tu ili usije leta mjadala wa kidini hapa. mimi toka babu yangu alikuwa sheikh,mufti na alhaj... wewe maamuma tu unataka jifanya unaifahamu dini na mistari ya kukariri kuliko watu wenye uelewa wa dini? acha huo upuuzi hapa tunaongea kisomi siyo kimaamuma.
Jiulize kama mzazi wa diamond akiugua kama atakuwa na mawazo kama yakomatajiri huwa wanakuwa na hesabu kali zaidi
Duuh hivi mkuu unamuita mama ako maiti tarajiwa??? Kuna watu mna rohoo ngumu.Huo msala ulimkutaga brother kipindi anamuuguza maza mi nlikua skonga bado
Nilikua namuonea huruma anahudumia maiti tarajiwa
Kiukweli vizazi vya sasa hivi ni kama watoto wamepoteza kabisa mapenzi kwa wazazi wao.. yani kupoteza gari inakuuma kuliko afya ya mzee wako??Kuna kipindi pia aliumwaaaaaa.... tukafikia hatua tukasema bora tu arudishe number maana sasa inakuwa changamoto kwetu. akaja akapona.. shida ikawa pale pale. hakuna afadhali akiwa mzima shida akiugua shida. ni msumbufu sana....
sasa this time anaumwa tena. mwezi wa 3 huu amelala tumehamisha hosp zote... tunagharamia ukimwangalia age yake nayo imeenda sana. 90 plus. anataka aendelee kuishi kufanya nini hapa duniani? sasa tunatumia pesa ambazo zingesaidia wajukuu wake kumtibu mgonjwa mbaye kwa kweli ameshakula chumvi ya kutosha hapa duniani. mwisho wa siku tunamwona tu kama chuma ulete. maana kila pesa zetu zinaenda kwenye matibabu yake. meno yake yameshatoka, anaishi kwa shida... anaanikwa tu juani kama mjusi ila bado anataka aendelee kuishi. unajiuliza aishi kufanya nini hapa duniani? mbona alishamaliza kila kitu?
Sasa inafikia kipindi tunasema bora tu akapumzike nasi tupumzike kidogo maana atatufilisi kwa kweli. mimi nimeshauza gari moja. nimechukua mkopo, nimekuwa sasa nina madeni ile mbaya. kwa mabro wengine nao.. ishakuwa shida. maana tulishampeleka mpaka india kipindi flani... wakatwambia kwa huu umri asifanyiwe hayo matibabu maana kinga zake nazo zimekosa nguvu. so alilazwa tu akipewa madawa miezi mitatu. gharama kubwa ilikuja kwetu. akarudi amekuwa tia maji tia maji . kama gari la mkaa trio moja shamba nyingine gereji.
Ila bado mbishi sana, bado anataka atibiwe na kupelekwa hosp za gharama, sasa mzee si atatuacha watoto wake tumefilisika halafu ndo afe? hapo tutakuwa tumefanya nini? nahitaji ushauri wenu kwa kweli hili jambo limenifika hatua nimechoka sana.sipendi unafiki... hii hali ni ngumu sana. maana sasa hata ukiona simu toka kwa ndugu unashindwa kupokea maana huchelewi kuambiwa sasa tuchangie kila mtu atoe 700,000 kuna vipimo na maibabu flani tena yanatakiwa.
Ni kweli asisahau kabisa na anavyomfanyia mzazi wake ndiyo na watoto wake watakuja kumfanyia hivyo hivyo kwa sababu wanasoma kutoka kwake.angeyasikia haya maneno nina hakika angekufa leo leo...
huna ustaarabu hata kdg
usisahau na wewe ni mzee mtarajiwa