Gharama za kumuuguza Mzee zinaongezeka. Sisi tumeshachoka kwa kweli. Bora tu achukuliwe

Gharama za kumuuguza Mzee zinaongezeka. Sisi tumeshachoka kwa kweli. Bora tu achukuliwe

Mtoto kama wew ndo Bora ubadilishane na kreti la bia

Mtoto hasara kabisa pambaneni na mzee wenu mpaka mwisho
 
chaajabu babu wa watu bado anataka kuishi ndo mana anawaambia nipelekeni hospital mercy killing mpaka mgonjwa atake mwenyewe.
Mercy killing au euthanasia haipo kwa nchi nyingi ikiwemo ya kwetu. Huko Uswisi, Udachi, Ubeligiji nk ndio unaweza kwenda na kuomba kusitishiwa uhai wako.
 
Kuna kipindi pia aliumwaaa.... tukafikia hatua tukasema bora tu arudishe number maana sasa inakuwa changamoto kwetu. Akaja akapona. Shida ikawa pale pale. Hakuna afadhali akiwa mzima shida akiugua shida. Ni msumbufu sana.

Sasa this time anaumwa tena. mwezi wa 3 huu amelala tumehamisha hosp zote. Tunagharamia ukimwangalia age yake nayo imeenda sana. 90 plus. Anataka aendelee kuishi kufanya nini hapa duniani? Sasa tunatumia pesa ambazo zingesaidia wajukuu wake kumtibu mgonjwa mbaye kwa kweli ameshakula chumvi ya kutosha hapa duniani. Mwisho wa siku tunamuona tu kama chuma ulete. Maana kila pesa zetu zinaenda kwenye matibabu yake. Meno yake yameshatoka, anaishi kwa shida. Anaanikwa tu juani kama mjusi ila bado anataka aendelee kuishi. Unajiuliza aishi kufanya nini hapa duniani? Mbona alishamaliza kila kitu?

Sasa inafikia kipindi tunasema bora tu akapumzike nasi tupumzike kidogo maana atatufilisi kwa kweli. Mimi nimeshauza gari moja, nimechukua mkopo, nimekuwa sasa nina madeni ile mbaya. Kwa mabro wengine nao.. ishakuwa shida. Maana tulishampeleka mpaka India kipindi fulani. Wakatwambia kwa huu umri asifanyiwe hayo matibabu maana kinga zake nazo zimekosa nguvu. So alilazwa tu akipewa madawa miezi mitatu. Gharama kubwa ilikuja kwetu. Akarudi amekuwa tia maji tia maji kama gari la mkaa trip moja shamba nyingine gereji.

Ila bado mbishi sana, bado anataka atibiwe na kupelekwa hosp za gharama, sasa mzee si atatuacha watoto wake tumefilisika halafu ndo afe? Hapo tutakuwa tumefanya nini? Nahitaji ushauri wenu kwa kweli hili jambo limenifika hatua nimechoka sana. Sipendi unafiki... hii hali ni ngumu sana maana sasa hata ukiona simu toka kwa ndugu unashindwa kupokea maana huchelewi kuambiwa sasa tuchangie kila mtu atoe 700,000 kuna vipimo na matibabu flani tena yanatakiwa.
Tukiwaambia tuishinikize serikali Ili kila kichwa kuanzia miaka 18 kitoe 5,000 kwa mwaka Ili tupate Bima hamtaki sasa kila mtu apambane kivyake..

Nilichojifunza Bora kujiandaa kuweka hela ukiwa mzima unless yakukute ukiwa bado hujajipanga maana watoto wenyewe na ndugu ndio hao.
 
Mimi mpaka hapo sijaona ustaarabu wako pia. Mimi nimeongea uhalisia ulivyo. Kila mtu ni mzee na marehemu mtarajiwa. So hi haitoi kibali cha mtu kuwa mnafiki na mpuuzi. Kuna haja gani kutumia chakula cha wazima kumpa mtu ambaye hatoweza kuwa mzima? Wafe wote? Miaka 90 plus unadhani ni michache? Na hali yake si nzuri. Unadhani kuna mtu ataishi milele?
Huo ni mtihani wako ukitenda vinginevyo utajizolea laana kama zote..

Kama ni pesa unaweza pata overnight na pesa ni kudra sio juhudi na zinaweza potea sekunde tuu..

Mungu ndio ataamua hatima yake na si vinginevyo.
 
Kuna kipindi pia aliumwaaa.... tukafikia hatua tukasema bora tu arudishe number maana sasa inakuwa changamoto kwetu. Akaja akapona. Shida ikawa pale pale. Hakuna afadhali akiwa mzima shida akiugua shida. Ni msumbufu sana.

Sasa this time anaumwa tena. mwezi wa 3 huu amelala tumehamisha hosp zote. Tunagharamia ukimwangalia age yake nayo imeenda sana. 90 plus. Anataka aendelee kuishi kufanya nini hapa duniani? Sasa tunatumia pesa ambazo zingesaidia wajukuu wake kumtibu mgonjwa mbaye kwa kweli ameshakula chumvi ya kutosha hapa duniani. Mwisho wa siku tunamuona tu kama chuma ulete. Maana kila pesa zetu zinaenda kwenye matibabu yake. Meno yake yameshatoka, anaishi kwa shida. Anaanikwa tu juani kama mjusi ila bado anataka aendelee kuishi. Unajiuliza aishi kufanya nini hapa duniani? Mbona alishamaliza kila kitu?

Sasa inafikia kipindi tunasema bora tu akapumzike nasi tupumzike kidogo maana atatufilisi kwa kweli. Mimi nimeshauza gari moja, nimechukua mkopo, nimekuwa sasa nina madeni ile mbaya. Kwa mabro wengine nao.. ishakuwa shida. Maana tulishampeleka mpaka India kipindi fulani. Wakatwambia kwa huu umri asifanyiwe hayo matibabu maana kinga zake nazo zimekosa nguvu. So alilazwa tu akipewa madawa miezi mitatu. Gharama kubwa ilikuja kwetu. Akarudi amekuwa tia maji tia maji kama gari la mkaa trip moja shamba nyingine gereji.

Ila bado mbishi sana, bado anataka atibiwe na kupelekwa hosp za gharama, sasa mzee si atatuacha watoto wake tumefilisika halafu ndo afe? Hapo tutakuwa tumefanya nini? Nahitaji ushauri wenu kwa kweli hili jambo limenifika hatua nimechoka sana. Sipendi unafiki... hii hali ni ngumu sana maana sasa hata ukiona simu toka kwa ndugu unashindwa kupokea maana huchelewi kuambiwa sasa tuchangie kila mtu atoe 700,000 kuna vipimo na matibabu flani tena yanatakiwa.
sijajua wewe nimwenyeji wa wapi ,ila hii ni tabia ya sukumaland.
Acha laana wewe unamchokaje mzee wako. kama umechoka waachie ndugu zako wamuuguza
 
Kuna kipindi pia aliumwaaa.... tukafikia hatua tukasema bora tu arudishe number maana sasa inakuwa changamoto kwetu. Akaja akapona. Shida ikawa pale pale. Hakuna afadhali akiwa mzima shida akiugua shida. Ni msumbufu sana.

Sasa this time anaumwa tena. mwezi wa 3 huu amelala tumehamisha hosp zote. Tunagharamia ukimwangalia age yake nayo imeenda sana. 90 plus. Anataka aendelee kuishi kufanya nini hapa duniani? Sasa tunatumia pesa ambazo zingesaidia wajukuu wake kumtibu mgonjwa mbaye kwa kweli ameshakula chumvi ya kutosha hapa duniani. Mwisho wa siku tunamuona tu kama chuma ulete. Maana kila pesa zetu zinaenda kwenye matibabu yake. Meno yake yameshatoka, anaishi kwa shida. Anaanikwa tu juani kama mjusi ila bado anataka aendelee kuishi. Unajiuliza aishi kufanya nini hapa duniani? Mbona alishamaliza kila kitu?

Sasa inafikia kipindi tunasema bora tu akapumzike nasi tupumzike kidogo maana atatufilisi kwa kweli. Mimi nimeshauza gari moja, nimechukua mkopo, nimekuwa sasa nina madeni ile mbaya. Kwa mabro wengine nao.. ishakuwa shida. Maana tulishampeleka mpaka India kipindi fulani. Wakatwambia kwa huu umri asifanyiwe hayo matibabu maana kinga zake nazo zimekosa nguvu. So alilazwa tu akipewa madawa miezi mitatu. Gharama kubwa ilikuja kwetu. Akarudi amekuwa tia maji tia maji kama gari la mkaa trip moja shamba nyingine gereji.

Ila bado mbishi sana, bado anataka atibiwe na kupelekwa hosp za gharama, sasa mzee si atatuacha watoto wake tumefilisika halafu ndo afe? Hapo tutakuwa tumefanya nini? Nahitaji ushauri wenu kwa kweli hili jambo limenifika hatua nimechoka sana. Sipendi unafiki... hii hali ni ngumu sana maana sasa hata ukiona simu toka kwa ndugu unashindwa kupokea maana huchelewi kuambiwa sasa tuchangie kila mtu atoe 700,000 kuna vipimo na matibabu flani tena yanatakiwa.
Wakati unatapika kamasi ulipokuwa mchanga angelikuwa na akili butu kama hizi wala usingeweza kusurvive mpaka leo maana akili zako zinakuwezesha kuvuka barabara ya kijiji....
Mzee anahitaji matunzo na lazima mumhangaikie
 
chaajabu babu wa watu bado anataka kuishi ndo mana anawaambia nipelekeni hospital mercy killing mpaka mgonjwa atake mwenyewe.
Kikubwa wamlee mzee wao na wawe nae karibu sana dunia isitufanye tuwatenge wazee wetu kiasi hichi , huu ndiyo ule muda wa kuvuna baraka tele maana inakuwa unayapitia yale aliyoyapitia yeye na mke wake wakiwa wanakulea unaumwa kila muda yani hawapumziki wanahangaika kama wehu .

Halafu leo kuna jitu linakuja kuona pesa ina thamani sanaaa kuliko uhai na furaha ya mzazi wake hii ishu inakera sana aisee sanaaa.

Sasa kama ugonjwa tu analalamika je angekuwa amepooza ndo angeweza hata kumsafisha haja zake?
 
Unatumia IDs nyingi. ila nimeepuka tu mjadala wa kidini hapa maana kuna mambo sisi wenye hekma tunayaacha hatujazi watu ambao si sehemu yao hapo. hakuna kitu ambacho huwa najaribu kwanza kuepuka kama kuanza mchambulia mtu dini hasa ya uislamu. naifahamu sijakariri. naifahamu kwa ukaribu sana...sisi ni baadhi ya watu ambao marhamu sheikh yahya alikuwa anakuja mpaka nyumbani kukaa kuongea na mzee habari za dini ya kiislamu. nami nimesoma tena kwa kusoma Mombasa na Lamu... ila mwishowe nimebaki na akili zangu timamu.
Kuja kwa sheikh yahya hadi kwa mzee wako kusoma kwako lamu na mombasa habadilishi upumbavu wako mkuu.

Nimekuambia hoja inapingwa na hoja weka aya yoyote ya quran inayopinga maelezo ya yule aliyeku quote , haunaweka unabaki kujificha kwenye kivuli cha umetokea kwenye ukoo sijui wa mufti sijui nini.

Ingekuwa umesoma quran ungeelewa kuwa ni dhambi kubwa sana mzazi/wazazi wako waliye wazee wakikuambia jambo ukasema ile "Ah" ya kichini sana inayoonesha kukasirishwa nao na ambayo haijasikika ni dhambi mbaya sana.

Sasa leo hii wewe ambaye alikulea na kuhangaika na wewe usiku kucha na mchana kutwa yeye na mke wake hawatulii kama wehu unaumwa daily wanakutibu unaamka usiku hawalali hawa enjoy penzi lako kisa makelele na magonjwa ya utoto leo unakuja kuwaanika hapa??

Hivi ikitokea amepooza (Allah amuepishie) utaweza hata kumsafisha uchafu wake? Unaona visenti na gari na nyumba vina thamani sanaa kuliko mzazi?
 
Ulichokiongea kina maana kubwa ila wachangiaji wengi hapa watakukosoa sababu hawajastaarabika bado. Nchi Zilizoendelea Kimaarifa Mzee akifikisha umri wa kuanza kutegemea watu pale pale anapelekwa kwenye kituo cha kulea wazee, sababu ni asiwe mzigo kwa wanawe wanaohangaikia kazi masaa 12 kwa siku na kirudi kuanza kulea watoto zao.
 
Tunza sana hili andiko. Kama umejaliwa watoto basi watakuwa mashahidi wako wa kwanza.
Ni Mzazi wako kweli?
Tunamuombea uponyaji..
Mkuu kuwa na kiasi hajapenda kuugua
Mzazi wako ataumia sana akisikia haya..
 
Mimi mpaka hapo sijaona ustaarabu wako pia. Mimi nimeongea uhalisia ulivyo. Kila mtu ni mzee na marehemu mtarajiwa. So hi haitoi kibali cha mtu kuwa mnafiki na mpuuzi. Kuna haja gani kutumia chakula cha wazima kumpa mtu ambaye hatoweza kuwa mzima? Wafe wote? Miaka 90 plus unadhani ni michache? Na hali yake si nzuri. Unadhani kuna mtu ataishi milele?
Mkuu subiri ubaki naye hapo peke yako hapo hospital kumkaba na mashuka afe labda roho yako itatulia!!
 
Na Mola wako Mlezi ameamrisha kuwa msimuabudu yeyote ila Yeye tu na wazazi wawili muwatendee wema. Mmoja wao akifikia uzee, naye yuko kwako, au wote wawili, basi usimwambie hata: Ah! Wala usiwakemee. Na sema nao kwa msemo wa heshima

Hii ni Qur'an inatuamrisha haya
Kumbuka wewe ulivokuwa mtoto huenda ulikuwa msumbufu sana ila wazazi wako walikuvumilia iweje leo wewe huwezi kumvumilia mzazi wako?

Yawezekana angekuwa tajiri mkubwa tu lakini alisacrifice akakulea wewe kwa pesa zake leo hii iweje yeye ndio sababu ya wewe kupatikana lakini unamdhalilisha kiasi hiki.

Najivunia kuwa Muislamu kwani Uislamu umetufunza yote haya.

Alhamdulillah ala kul hal..uislamu una raha Sana nami najivunia kuwa muislamu
 
Kauli huumba, huyu mwamba lazima kwenye uzee wake yaje yamrudi haya! Unamsemanmzazi wako kama kiufupi mtu fulani? Kwa nini msiuze mali yake mkaenda kumtibishia?
 
Si mumkabe azime biashara imeisha.
Kuna mzee kijijini kwetu kama mgonjwa amewasumbua sana na daktari kasema kupona ni ngumu mkimwita anamaliza shughuli.
Akija mnatoka nje anaenda kumsalimia mgonjwa. Ile anatoka tu mkachukue mkaifunike maiti yenu.
Wamama wakimwona tu anakuja kumwona mgonjwa walikuwa wanaanza kulia
Huyo mzee ndio Israel mtoa roho au?
 
Hii dunia ina watu wabaya sana... Laiti wazaz wangekua wanatuambia jinsi walivyo hangaika kwa hali na mali tulivyo kuwa watoto hatujielewi, hakika tusingefikia hatua ya kuchoka kumtibia mzaz kias cha kutamani afe...
Ok usihofu soon atakufa ili pesa zako tamu zisitumike tena ktk matibabu, ila nina uhakika Mungu atakufanyia jambo na utaona ni heri hili ulilonalo
 
Vitu vingine hupaswi kuvitoa mdomoni si vizuri, muombee kwa Mungu ni baraka moja wapo, yeye aliwalea mpaka hapo
 
Back
Top Bottom