Gharama za kumuuguza Mzee zinaongezeka. Sisi tumeshachoka kwa kweli. Bora tu achukuliwe

Gharama za kumuuguza Mzee zinaongezeka. Sisi tumeshachoka kwa kweli. Bora tu achukuliwe

pole kwanza , ila ayo ni maneno makali sana , ndo mana unaeza kuta Mungu anakuadhibu.. cha kufanya. msikilize , na umtibie kwa moyo wote uyo ni mzazi wako, ukiwa huna kinyongo , na unamuhudumia kwa moyo wote ,pesa zitakuja tu kaka, pesa zinatafutwa ila mzazi akikutoka kakutoka...
 
He is a master siku 1 utaelewa hii risala yangu Mungu atakapomchukua mshua.
Na mama yako aliebaki hai anajua kuwa una element za kike?

Screenshot_20220802-132807.jpg
 
Wabongo wanakusaidia kwa maneno tu [emoji38][emoji1787][emoji1787],hao maparoko na masheikh ndio majanga watajifanya kukupa mistari ila pesa ni hapana.

Wanajidai wana ogopa laana,mbona Magufuli walikua wanamuombea kifo hawakudai ni laana,watu ni wanafiki walio kubuhu.
Mijitu minafiki hii.

Si ajabu unakuta ndio vinara wa kulawiti watoto wa sekondari.
 
Vizuri bunge lipeleke mswada bungeni wakuwarestisha watu aina kama yeye au hatayule anaamua kwa hiyari yake
 
Na Mola wako Mlezi ameamrisha kuwa msimuabudu yeyote ila Yeye tu na wazazi wawili muwatendee wema. Mmoja wao akifikia uzee, naye yuko kwako, au wote wawili, basi usimwambie hata: Ah! Wala usiwakemee. Na sema nao kwa msemo wa heshima

Hii ni Qur'an inatuamrisha haya
Kumbuka wewe ulivokuwa mtoto huenda ulikuwa msumbufu sana ila wazazi wako walikuvumilia iweje leo wewe huwezi kumvumilia mzazi wako?

Yawezekana angekuwa tajiri mkubwa tu lakini alisacrifice akakulea wewe kwa pesa zake leo hii iweje yeye ndio sababu ya wewe kupatikana lakini unamdhalilisha kiasi hiki.

Najivunia kuwa Muislamu kwani Uislamu umetufunza yote haya.
Una maana wale wote unaowaona na kuwafahamu wanauguza na kiulea wazee wao na kuwajengea mpaka sehemu nzuri za kwenda uani ili wasipate shida na kuwatunza kwa kila kitu ni WAISLAM TUU???

Hata huyo Alha wako sijui nani sidhani kama anakuelewa.
 
[emoji125][emoji125][emoji125][emoji125]nitarudi baadae.....!!!
Fikiria hapo ndo bangi haijaruhusiwa kuuzwa madukani. Je ikiruhusiwa taifa na wazazi wataingia hasara kiasi gani kwa watu wa aina hii ya mleta mada!!
 
Kuna kipindi pia aliumwaaa.... tukafikia hatua tukasema bora tu arudishe number maana sasa inakuwa changamoto kwetu. Akaja akapona. Shida ikawa pale pale. Hakuna afadhali akiwa mzima shida akiugua shida. Ni msumbufu sana.

Sasa this time anaumwa tena. mwezi wa 3 huu amelala tumehamisha hosp zote. Tunagharamia ukimwangalia age yake nayo imeenda sana. 90 plus. Anataka aendelee kuishi kufanya nini hapa duniani? Sasa tunatumia pesa ambazo zingesaidia wajukuu wake kumtibu mgonjwa mbaye kwa kweli ameshakula chumvi ya kutosha hapa duniani. Mwisho wa siku tunamuona tu kama chuma ulete. Maana kila pesa zetu zinaenda kwenye matibabu yake. Meno yake yameshatoka, anaishi kwa shida. Anaanikwa tu juani kama mjusi ila bado anataka aendelee kuishi. Unajiuliza aishi kufanya nini hapa duniani? Mbona alishamaliza kila kitu?

Sasa inafikia kipindi tunasema bora tu akapumzike nasi tupumzike kidogo maana atatufilisi kwa kweli. Mimi nimeshauza gari moja, nimechukua mkopo, nimekuwa sasa nina madeni ile mbaya. Kwa mabro wengine nao.. ishakuwa shida. Maana tulishampeleka mpaka India kipindi fulani. Wakatwambia kwa huu umri asifanyiwe hayo matibabu maana kinga zake nazo zimekosa nguvu. So alilazwa tu akipewa madawa miezi mitatu. Gharama kubwa ilikuja kwetu. Akarudi amekuwa tia maji tia maji kama gari la mkaa trip moja shamba nyingine gereji.

Ila bado mbishi sana, bado anataka atibiwe na kupelekwa hosp za gharama, sasa mzee si atatuacha watoto wake tumefilisika halafu ndo afe? Hapo tutakuwa tumefanya nini? Nahitaji ushauri wenu kwa kweli hili jambo limenifika hatua nimechoka sana. Sipendi unafiki... hii hali ni ngumu sana maana sasa hata ukiona simu toka kwa ndugu unashindwa kupokea maana huchelewi kuambiwa sasa tuchangie kila mtu atoe 700,000 kuna vipimo na matibabu flani tena yanatakiwa.
Nashindwa kukupa ushauri sababu naona maneno makali sana kwenye maelezo yako kama vile tumamuanika juani kama mjusi, tunamuona kama chuma ulete,ksms gari la mkaa
 
Una maana wale wote unaowaona na kuwafahamu wanauguza na kiulea wazee wao na kuwajengea mpaka sehemu nzuri za kwenda uani ili wasipate shida na kuwatunza kwa kila kitu ni WAISLAM TUU???

Hata huyo Alha wako sijui nani sidhani kama anakuelewa.


Hata wasio waislamu wapo wanaokuwanao bega kwa bega na kuwatunza wazee wao mpaka wanafariki, so, watalipwa hapa hapa duniani, akhera hawana kitu.
 
Unaringia Imani ya babu sijui baba yako kwani uliambiwa watakusaidia kuingia peponi? Ungekuwa imani yako unaifahamu vizuri na unawapenda na kuwaheshimu wazazi wako kama Quran Tukufu inavyosema ungeshakuwa na aibu ukafuta huo uzi kuliko ujinga uliofanya wa kulinganisha uhai wa binadamu (tena baba yako) na pesa ambazo unahonga hata bila kuombwa.
 
Jamani nikwamba ilikuaje hadi kuwaza ujinga huu?kua mmuwekee sumu mzazi kisa anawasumbua?Mungu aturehemu maana unaweza zaa ukijua umepata wakukutunza siku nguvu zimekuishia kumbe anawaza kukupa sumu hivi mnajua ilivyokazi kulea mimba hadi kitoto kilivyokidogo kijitambue?

Sent from my SM-G9250 using JamiiForums mobile app
Huwa namwangaliaga my son bado ni mchanga wife anavyohangaika nae then nikipitia huu najisemea kesho na keshokutwa anakuja kukuanzishia uzi huku wa kipumbavu
 
Hata wasio waislamu wapo wanaokuwanao bega kwa bega na kuwatunza wazee wao mpaka wanafariki, so, watalipwa hapa hapa duniani, akhera hawana kitu.
Ila nyie ndio mtakaolipwa mbinguni?,aisee hii dini ngumu sana
 
Pole sna mkuu..binafsi niliyapitia haya pale muhimbil mzee figo zilifeli..akawa anaenda chuja..hakuna rangi nilio acha iyona....kwa wiki tu ilikuwa inaenda 1 M plus...nilivurugwa haswa...ilibaki kidogo tu nianze kuchangisha lakin sikutaka...yan hapo nina kimeo cha dogo anasoma bila mkopo mliman pale...dah hapo hapo nina mavikoba plus pango la biashara kwa mwezi tu ni laki nane...nilijifunza pombe kali angalau niwe napata usingizi..nikiangali umri wa kuoa umefika 30 plus kidogo..mara nikapata kabinti nikakaweka mimba..afu nikamwambia ucjal..imefika muda wa kujifungua mwanaume nipo home peke angu...nikaplan nikaomba namba ya bimkubwa wake nikampigia nikaongea nae nikamuomba anitunzie mwanae mpaka atakapo jifungua na akimaliza tu ile miez mitatu nitamfata chapu bimkubwa akanielewa nikashukuru sana..basi nikamkimbiza mbeya nikamwachia mpunga bimkubwa wake nae kwenye akaunt yake nilimuekea 1.4M ...dadeki mahar cjatoa na baba mkwe akawa hajui nin kinachoendelea...dah maisha haya...yaan ilikuwa afe mzee au nifee mimi...nilimpqmbania pale muhimbil tokea 2019 na akaja kata moto 2021 december ..ila ndio alinipukutisha haswa...
 
Nilimuuguza mzee wangu kwa uri na thim kwa miaka miwili. Nililazimika kuahirisha mambo yangu yote ili kuhangaikia afya yake na akiwa na kesi nzito na ngumu za kansa na failure ya Figo zote mbili. Katu asilani sikukata tamaa.

Huu ndiyo wakati pekee niliokuwa nikimnyoa ndevu; kumfikisha toilet, kumfunga nepi, kumuogesha kwa kitambaa cha vuguvugu akiwa kitandani mwake, kumgeuza na kuongea nae hata kwa ishara pale kauli yake ilipokata.

Nilifarijika sana kuwa na ukaribu na mzee wangu kwa kiwango kile, nafasi ambayo sikuwahi kuwa nayo, wakati wa ugonjwa wake mapenzi yangu kwake yaliongezeka mara dufu.

Akafariki nikishuhudia kwenye visaidizi vya kupumua Hospitali ya Taifa Muhimbili. Nikapambana na kuupa mwili wake heshima stahiki na kumzika pale alipopenda azikwe.

Nikiona uzi kama huu, natambua kwamba KWELI BINADAMU tumetofautiana sana.

Nilichelea mzee angekuwa hata 100 lakini hakufika umri huo...

umekuwaje mleta sledi. Mwogope Mola wako...omba hiyo roho ya kikatili ikuondoke...
 
Kuna kipindi pia aliumwaaa.... tukafikia hatua tukasema bora tu arudishe number maana sasa inakuwa changamoto kwetu. Akaja akapona. Shida ikawa pale pale. Hakuna afadhali akiwa mzima shida akiugua shida. Ni msumbufu sana.

Sasa this time anaumwa tena. mwezi wa 3 huu amelala tumehamisha hosp zote. Tunagharamia ukimwangalia age yake nayo imeenda sana. 90 plus. Anataka aendelee kuishi kufanya nini hapa duniani? Sasa tunatumia pesa ambazo zingesaidia wajukuu wake kumtibu mgonjwa mbaye kwa kweli ameshakula chumvi ya kutosha hapa duniani. Mwisho wa siku tunamuona tu kama chuma ulete. Maana kila pesa zetu zinaenda kwenye matibabu yake. Meno yake yameshatoka, anaishi kwa shida. Anaanikwa tu juani kama mjusi ila bado anataka aendelee kuishi. Unajiuliza aishi kufanya nini hapa duniani? Mbona alishamaliza kila kitu?

Sasa inafikia kipindi tunasema bora tu akapumzike nasi tupumzike kidogo maana atatufilisi kwa kweli. Mimi nimeshauza gari moja, nimechukua mkopo, nimekuwa sasa nina madeni ile mbaya. Kwa mabro wengine nao.. ishakuwa shida. Maana tulishampeleka mpaka India kipindi fulani. Wakatwambia kwa huu umri asifanyiwe hayo matibabu maana kinga zake nazo zimekosa nguvu. So alilazwa tu akipewa madawa miezi mitatu. Gharama kubwa ilikuja kwetu. Akarudi amekuwa tia maji tia maji kama gari la mkaa trip moja shamba nyingine gereji.

Ila bado mbishi sana, bado anataka atibiwe na kupelekwa hosp za gharama, sasa mzee si atatuacha watoto wake tumefilisika halafu ndo afe? Hapo tutakuwa tumefanya nini? Nahitaji ushauri wenu kwa kweli hili jambo limenifika hatua nimechoka sana. Sipendi unafiki... hii hali ni ngumu sana maana sasa hata ukiona simu toka kwa ndugu unashindwa kupokea maana huchelewi kuambiwa sasa tuchangie kila mtu atoe 700,000 kuna vipimo na matibabu flani tena yanatakiwa.
Kweli mzazi mmoja anaweza Lea watoto kumi lakini watoto kumi hawawezi.kumlea mzazi mmoja, NI kweli unakuja lalamika hili huku JF
 
Back
Top Bottom