Gharama za Ujenzi kwa Nyumba za ‘Contemporary’ Vs ‘Traditional’ Roof

Gharama za Ujenzi kwa Nyumba za ‘Contemporary’ Vs ‘Traditional’ Roof

Black Thought

Senior Member
Joined
Feb 25, 2015
Posts
161
Reaction score
408
Habarini wakuu,

Kuna mjadala uliletwa humu kuhusu ni nyumba zipi zina gharama nafuu kwenye ujenzi kati ya hizi za kisasa za kuficha bati (‘contempoarary) na zile za kawaida. Ambapo kwa uzoefu wangu nilijaribu kuelezea kuwa kwa kawaida tunatarajia nyumba za paa la kuficha zitatumia tofali nyingi huku bati na mbao zikitumika kidogo sana (maranyingi haizidi nusu) wakati hizi za paa la kawaida zinatumia tofali chache huku zikitumia bati na mbao nyingi zaidi.

Lakini kuna mambo ya kuzingatia

1. Ongezeko la tofali kwenye contemporary house si kubwa sana kulinganisha na utofauti wa mahitaji ya mbao na bati za kupaulia baina ya aina hizi mbili za upauaji wa nyumba.

2. Gharama za mbao na bati kwa ujumla wake zinakupa ongezeko kubwa la gharama kwa nyumba za kawaida kulinganisha na contemporary house.

3. Kuna kitu kinachoongezeka kwenye nyumba za contemporary ambacho ni ‘concrete Gutter’ (mitaro ya kukusanya maji). Ambacho kwa mtazamo wangu nili commet kuwa ndio hasa kinaweza kufanya unafuu wa contempoary uliotokana na roofing ukaja kujilipa (kwa kukalibia au hata kuzidi) kulingana na idadi na namna mitaro ya maji ilivyowekwa kwenye nyumba amabyo kwa namna flani inatokana na ‘spatial arrangement’ ya ndani na namna flani za kuboresha mvuto wa jengo (Contemporary house zinaongezeka mvuto with complexity).

Hivyo basi pendekezo langu lilikuwa ni kwamba kama unataka kujenga kwa kuficha bati na huku pia ukitaka kupunguza gharama ni muhimu kuzingatia mpangilo wa nyumba utakao kufanya uepuke kujenga mitaro mingi kwenye nyumba.

Au unaweza kuepuka kabisa ujenzi wa mitaro kwa kuacha wazi upande wa nyuma ambao ndio maji yataelekezwa huko, na hii ni nzuiri zaidi maana pia itakupunguzia idadi ya tofali ambazo zingehitajika upande wa nyuma huku pia ukiepuka materials kwaajili ya ujenzi wa gutter ambalo lingehitaji zege la nondo.

Na kwakuongeza tu namna hii ya kuacha wazi upande wa nyuma iatakusaidia kupunguza risk ya nyumba kuvuja endapo hukutumia fundi mwenye uzoefu/ujuzi wa nyumba hizi, so risk ya kuvuja itabaki kuwa kwenye maungio ya bati na ukuta (kama fundi ni kimeo).
Kwa maelekezo zaidi juu ya masuala yote yahusuyo ujenzi unaweza kutucheki whatsapp 0717682856.

Unaweza kuona mfano wa hako ka ramani hapo chini (kalichorwa kwa lengo la kusave space na gharama). Kana vyumba vitatu (1master), kiStudy room kidogo, kitchen, dining na public toilet.

D62D8714-46F5-4270-9F4D-70E8CCC74157.jpeg


2B792704-3E43-49D1-959A-B6061B7CAA1D.jpeg


AAC5BB66-1B13-4998-AA9D-9B2C119B436C.jpeg
 
Hizo contemporary ni nzuri sana kwa muonekano, ila nnavosikia zinaharibika haraka zinavujisha (nadhani shida itakua kwa wataalamu wetu) hawajazijulia vizuri....
Kuna jamaa kajenga haina hata mwaka tayari ndani kunavuja
No doubt Fundi tatizo. Wabongo tunapenda sana vitu cheap badala ya vitu affordable. Mtu anataka kujenga anaungaunga kuanzia ramani mpaka mafundi ujenzi kila kitu unataka the cheapest.

Au mtu anachorewa ramani lakini atakwambia anafundi wake, kisha anaenda kutafuta fundi wa bei nafuu bila hata kuwa na uhakika juu ya ujuzi wa fundi husika. Na tatizo ni kuwa hakuna fundi atakuambia hajui kazi
 
No doubt Fundi tatizo. Wabongo tunapenda sana vitu cheap badala ya vitu affordable. Mtu anataka kujenga anaungaunga kuanzia ramani mpaka mafundi ujenzi kila kitu unataka the cheapest. Au mtu anachorewa ramani lakini atakwambia anafundi wake, kisha anaenda kutafuta fundi wa bei nafuu bila hata kuwa na uhakika juu ya ujuzi wa fundi husika. Na tatizo ni kuwa hakuna fundi atakuambia hajui kazi
Hapa kuna kitu naomba kujua mtu akikuchorea Ramani ni lazima afanye kazi? Na mchora Ramani kazi yake si kuchora tu au na kujenga anajenga?

Back to topic: hapo kwenye ucheap ndio penyewe sio kuwa hatupendi vitu vizuri ila mbuzi anakula urefu wa kamba.
 
Hapa kuna kitu naomba kujua mtu akikuchorea Ramani ni lazima afanye kazi? Na mchora Ramani kazi yake si kuchora tu au na kujenga anajenga?

Back to topic: hapo kwenye ucheap ndio penyewe sio kuwa hatupendi vitu vizuri ila mbuzi anakula urefu wa kamba.
Sio lazima aliechora ndio ajenge, lakini angalau kunakua na uhakika wakufanya kwa ubora unaotakiwa kulingana na design.

Na issue ya kupenda cheap, sio tatizo ndio maana nikasema angalau uwe na uhakika na uwezo wa mtu anayefanya kazi. Sio tu kwakuwa mtu ananusu bei basi unamkabizi kazi, kisha baadae unakuja kulalamika umeharibiwa kazi, uliokoa laki tano na unapata hasara ya million tano au zaidi.

Njia nzuri inaweza kuwa kujilizisha na uwezo wa mtu unayempa kazi kupitia watu aliowafanyia kazi. Au unaweza kumpa fundi kazi kisha ukamtumia mchora ramani (architect/engineer) kuja kukagua kwenye hatua muhimu za ujenzi kisha yeye ukamlipa hela ya site visiting tu.
 
No doubt Fundi tatizo. Wabongo tunapenda sana vitu cheap badala ya vitu affordable. Mtu anataka kujenga anaungaunga kuanzia ramani mpaka mafundi ujenzi kila kitu unataka the cheapest. Au mtu anachorewa ramani lakini atakwambia anafundi wake, kisha anaenda kutafuta fundi wa bei nafuu bila hata kuwa na uhakika juu ya ujuzi wa fundi husika. Na tatizo ni kuwa hakuna fundi atakuambia hajui kazi
Tatizo lipo kwa mafundi wenyewe! Mnatoa bei za kukomoana! Nani alikuambia ww kunijengea nyumba yangu ndio unaponea kutatua matatizo yako yote? Muwe reasonable bana mfyuuuuu 😡!
 
No doubt Fundi tatizo. Wabongo tunapenda sana vitu cheap badala ya vitu affordable. Mtu anataka kujenga anaungaunga kuanzia ramani mpaka mafundi ujenzi kila kitu unataka the cheapest. Au mtu anachorewa ramani lakini atakwambia anafundi wake, kisha anaenda kutafuta fundi wa bei nafuu bila hata kuwa na uhakika juu ya ujuzi wa fundi husika. Na tatizo ni kuwa hakuna fundi atakuambia hajui kazi
Tatizo lipo kwa mafundi wenyewe! Mnatoa bei za kukomoana! Nani alikuambia ww kunijengea nyumba yangu ndio unaponea kutatua matatizo yako yote? Muwe reasonable bana mfyuuuuu 😡!
 
No doubt Fundi tatizo. Wabongo tunapenda sana vitu cheap badala ya vitu affordable. Mtu anataka kujenga anaungaunga kuanzia ramani mpaka mafundi ujenzi kila kitu unataka the cheapest. Au mtu anachorewa ramani lakini atakwambia anafundi wake, kisha anaenda kutafuta fundi wa bei nafuu bila hata kuwa na uhakika juu ya ujuzi wa fundi husika. Na tatizo ni kuwa hakuna fundi atakuambia hajui kazi
Nyumba ya vyumba vinne standard inaweza cost shilingi ngapi?
 
Sasa kiongozi ukiacha nyuma wazi hivi nyumba si inapoteza mvuto inakuwa kama majengo ya waarabu zamani
Hata kuziba kote ilikuwepo zamani pia boss, ni kwamba zama zinajirudia tu. Suala la mvuto linategemea vitu vingi ikiwemo mtazamo wako wewe binafsi ofcoz na namna itakavyoachwa wazi kwa mujibu wa design
 
Tatizo lipo kwa mafundi wenyewe! Mnatoa bei za kukomoana! Nani alikuambia ww kunijengea nyumba yangu ndio unaponea kutatua matatizo yako yote? Muwe reasonable bana mfyuuuuu 😡!
Ingekua hivo basi watu wasingejenga boss. Mfano sisi gharama zetu umeziona wapi. Ndio maana nikasema sio mbaya mtu kutafuta namna ambayo ni more affordable lakini usikimbilie tu kwakuwa umeona ni cheap.

Ukikutana na simu ya laki nane inauzwa laki mbili kwa akili ya kawaida lazima utafute namna ya kujilizisha kuwa ni salama/nzima kweli, lakini ukikurupuka kwa kufurahia tu utajikuta umepoteza laki mbili yako na unatakiwa utafute laki nane sasa ukachukue upya😀.

Kila mtu anasababu zake kwa bei zake kamwe hatuwezi kufanana. Tafuta fundi wa gharama ya chini lakini tafuta namna ya kujiliza juu ya uwezo wake, simple
 
Mwanzoni nilianza kuwa muumini wa contemporary roofing lakini ushuhuda nnaopata kutoka kwa walioezeka kwa style hyo unanipa mashaka makubwa na jirani yangu ameijenga nyumba inavuja kama nje ,mafundi wapo ila guarantee ya kukupaulia isivuje hana, dhumuni mama la kupaua nyumba ni kukukinga na jua na mvua na uchafu unaotoka juu, sijui mambo ya contemporary au classical roofing au msouth versatile au romantile simba dumu ni namna tu ya kutafuta mvuto ili lengo mama litimie. Lengo lisipotimia na nyumba ikaanza kuvuja hakuna maana ya kupaua .
 
Back
Top Bottom