Gharama za Ujenzi kwa Nyumba za ‘Contemporary’ Vs ‘Traditional’ Roof

Gharama za Ujenzi kwa Nyumba za ‘Contemporary’ Vs ‘Traditional’ Roof

Nadhani ili kuepuka kuvujiwa nikuacha nyuma wazi ili maji yatiririke bila tatizo
Mwanzoni nilianza kuwa muumini wa contemporary roofing lakini ushuhuda nnaopata kutoka kwa walioezeka kwa style hyo unanipa mashaka makubwa na jirani yangu ameijenga nyumba inavuja kama nje ,mafundi wapo ila guarantee ya kukupaulia isivuje hana, dhumuni mama la kupaua nyumba ni kukukinga na jua na mvua na uchafu unaotoka juu, sijui mambo ya contemporary au classical roofing au msouth versatile au romantile simba dumu ni namna tu ya kutafuta mvuto ili lengo mama litimie. Lengo lisipotimia na nyumba ikaanza kuvuja hakuna maana ya kupaua .
 
Kwa uzoefu wangu, hamna gharama inayopongua, una save kwenye kupaua, unaumia kwenye concrete gutters na slabs za vibaraza, shughuli ni pevu
Issue ya gutter na nimeelezea hapo kuwa ili gharama ipingue inategemea sana na namna gutters zilivyo sanifiwa.
Ishu ya Vibaraza sio lazima viwefunikwe kwa slabs, Vinaweza kufunikwa kwa bati likiwa linefichwa pia.
 
Habarini wakuu,

Kuna mjadala uliletwa humu kuhusu ni nyumba zipi zina gharama nafuu kwenye ujenzi kati ya hizi za kisasa za kuficha bati (‘contempoarary) na zile za kawaida. Ambapo kwa uzoefu wangu nilijaribu kuelezea kuwa kwa kawaida tunatarajia nyumba za paa la kuficha zitatumia tofali nyingi huku bati na mbao zikitumika kidogo sana (maranyingi haizidi nusu) wakati hizi za paa la kawaida zinatumia tofali chache huku zikitumia bati na mbao nyingi zaidi.

Lakini kuna mambo ya kuzingatia

1. Ongezeko la tofali kwenye contemporary house si kubwa sana kulinganisha na utofauti wa mahitaji ya mbao na bati za kupaulia baina ya aina hizi mbili za upauaji wa nyumba.

2. Gharama za mbao na bati kwa ujumla wake zinakupa ongezeko kubwa la gharama kwa nyumba za kawaida kulinganisha na contemporary house.

3. Kuna kitu kinachoongezeka kwenye nyumba za contemporary ambacho ni ‘concrete Gutter’ (mitaro ya kukusanya maji). Ambacho kwa mtazamo wangu nili commet kuwa ndio hasa kinaweza kufanya unafuu wa contempoary uliotokana na roofing ukaja kujilipa (kwa kukalibia au hata kuzidi) kulingana na idadi na namna mitaro ya maji ilivyowekwa kwenye nyumba amabyo kwa namna flani inatokana na ‘spatial arrangement’ ya ndani na namna flani za kuboresha mvuto wa jengo (Contemporary house zinaongezeka mvuto with complexity).

Hivyo basi pendekezo langu lilikuwa ni kwamba kama unataka kujenga kwa kuficha bati na huku pia ukitaka kupunguza gharama ni muhimu kuzingatia mpangilo wa nyumba utakao kufanya uepuke kujenga mitaro mingi kwenye nyumba.

Au unaweza kuepuka kabisa ujenzi wa mitaro kwa kuacha wazi upande wa nyuma ambao ndio maji yataelekezwa huko, na hii ni nzuiri zaidi maana pia itakupunguzia idadi ya tofali ambazo zingehitajika upande wa nyuma huku pia ukiepuka materials kwaajili ya ujenzi wa gutter ambalo lingehitaji zege la nondo.

Na kwakuongeza tu namna hii ya kuacha wazi upande wa nyuma iatakusaidia kupunguza risk ya nyumba kuvuja endapo hukutumia fundi mwenye uzoefu/ujuzi wa nyumba hizi, so risk ya kuvuja itabaki kuwa kwenye maungio ya bati na ukuta (kama fundi ni kimeo).
Kwa maelekezo zaidi juu ya masuala yote yahusuyo ujenzi unaweza kutucheki whatsapp 0717682856.

Unaweza kuona mfano wa hako ka ramani hapo chini (kalichorwa kwa lengo la kusave space na gharama). Kana vyumba vitatu (1master), kiStudy room kidogo, kitchen, dining na public toilet.

View attachment 1745814

View attachment 1745815

View attachment 1745816
Mkuu Heri kwako ila twende mbele turudi nyuma, nyumba zile kweli za contemporary kweli ile contemporary house bongo ni chache sana,,kwa upeo wangu mdogo,mara nyingi nyumba za contemporary hutawaliwa almost 90% kwa concrete na glass,hata huko juu wabongo tunaforce kuweka bati tena kuna wengine wanajinasibu kuweka bati cheap zaidi kwa vile watu hawalioni ili kukwepa gharama,pasipo kuhusisha factors nyingine ikiwepo hali ya hewa,ubora wa matumizi ya material yenyewe kwa shughuli husika,kutu si rafiki baada ya miaka kadhaa,ukiacha swala la kuvuja pembeni,dawa ni kupiga zege tu,mwite fundi akupe makadirio na ushauri,fit kwny design yako, anza nondo mdogo mdogo,mifuko ya cement,gari kokoto,gari mchanga,pvc,mbao,hela ya fundi material ndogo ndogo,kata mzizi wa fitna ishi kweli kwny contemporary house.vinginevyo wabongo tunafake tu.😀
 
Mkuu Heri kwako ila twende mbele turudi nyuma, nyumba zile kweli za contemporary kweli ile contemporary house bongo ni chache sana,,kwa upeo wangu mdogo,mara nyingi nyumba za contemporary hutawaliwa almost 90% kwa concrete na glass,hata huko juu wabongo tunaforce kuweka bati tena kuna wengine wanajinasibu kuweka bati cheap zaidi kwa vile watu hawalioni ili kukwepa gharama,pasipo kuhusisha factors nyingine ikiwepo hali ya hewa,ubora wa matumizi ya material yenyewe kwa shughuli husika,kutu si rafiki baada ya miaka kadhaa,ukiacha swala la kuvuja pembeni,dawa ni kupiga zege tu,mwite fundi akupe makadirio na ushauri,fit kwny design yako, anza nondo mdogo mdogo,mifuko ya cement,gari kokoto,gari mchanga,pvc,mbao,hela ya fundi material ndogo ndogo,kata mzizi wa fitna ishi kweli kwny contemporary house.vinginevyo wabongo tunafake tu.😀
Unaweza kuwa sahihi pia mkuu. Lakini muhimu ni ujuzi/taaluna na uzoefu juu ya kitu kinachofanyika. Hata roof slabs zipo zinazovuja pia. Hizi contemporary zina mambo mengi yanayoweza kufanya zikavuja endapo yasipozingatiwa, na ishu kama bati kupata kutu yes inaweza kutokea endapo roof pitch ikiwa ndogo sana ndio maana huwa inatakiwa slope isipungue walau nyuzi kumi. Kuna vitu vingi sana vya kuzungumza hapa ikiwepo hata aina za bati zinazofaa zaidi, namna ya kutengeneza na kulinda makutano ya bati na kuta ili kusitokee uvujaji pembeni n.k
Ndio maana nikasema kupunguza gharama sio tatizo ila kukwepa gharama mara nyingi huleta gharama kubwa zaidi baadae.
 
Tunauza mbao kwa bei ya jumla.Njoo ofisini kwetu TEGETA tukuhudumie kwa gharama nafuu sana:-
2*2 fut12=2500
2*2 fut12(treated) ya dawa=2800
2*2 fut18(treated) ya dawa=5000
2*4 fut12 treated(ya dawa)=5000
2*4 fut12 isiyo ya dawa=4500
1*6 fut12=4500
1*8 fut12=8000
1*8fut12 ya fisher board(treated)=9500
1*10 fut12=13000
1*10fut 18 fisher board( treated)=15500
2*4 fut18(treated)=9500
2*6 fut12=8000
1*4 fut12=2800
2*6 fut 18=19000
Tunapatikana muda wote kwa namba za simu zifuatazo:-
----0759630751
----0687371138
----0654830416

vile vile kuna huduma ya kuchana,kuranda na kusize mbao inapatikana ofisini kwetu
 
Hapa kuna kitu naomba kujua mtu akikuchorea Ramani ni lazima afanye kazi? Na mchora Ramani kazi yake si kuchora tu au na kujenga anajenga?

Back to topic: hapo kwenye ucheap ndio penyewe sio kuwa hatupendi vitu vizuri ila mbuzi anakula urefu wa kamba.
You have spoken my mind.... Sio kuwa tunapenda cheap... Uwezo ndio shida...mkono unapoishia
 
Mkuu Heri kwako ila twende mbele turudi nyuma, nyumba zile kweli za contemporary kweli ile contemporary house bongo ni chache sana,,kwa upeo wangu mdogo,mara nyingi nyumba za contemporary hutawaliwa almost 90% kwa concrete na glass,hata huko juu wabongo tunaforce kuweka bati tena kuna wengine wanajinasibu kuweka bati cheap zaidi kwa vile watu hawalioni ili kukwepa gharama,pasipo kuhusisha factors nyingine ikiwepo hali ya hewa,ubora wa matumizi ya material yenyewe kwa shughuli husika,kutu si rafiki baada ya miaka kadhaa,ukiacha swala la kuvuja pembeni,dawa ni kupiga zege tu,mwite fundi akupe makadirio na ushauri,fit kwny design yako, anza nondo mdogo mdogo,mifuko ya cement,gari kokoto,gari mchanga,pvc,mbao,hela ya fundi material ndogo ndogo,kata mzizi wa fitna ishi kweli kwny contemporary house.vinginevyo wabongo tunafake tu.😀
Jamaa umeongea kitu cha ukweli haswaaa!! Contemporary kwa wenzetu ni zaidi ya ile style ya kupaua, ni muundo mzima wa jengo kwa maana kama ulivyosema. Na nia ya contemporary kwa wenzetu wala sio kupunguza gharama! Sasa sisi tumeivamia hiyo style ya kupaua kwa vile wengi wanaoitwa mafundi wanaiuza kwamba inapunguza gharama ya upauaji! Kitu ambacho kinaweza kisiwe sahihi sana, ndo tunaishia kuvujiwa na nyumba kisha tunalaumu kuwa hiyo style ni mbaya!
 
Jamaa umeongea kitu cha ukweli haswaaa!! Contemporary kwa wenzetu ni zaidi ya ile style ya kupaua, ni muundo mzima wa jengo kwa maana kama ulivyosema. Na nia ya contemporary kwa wenzetu wala sio kupunguza gharama! Sasa sisi tumeivamia hiyo style ya kupaua kwa vile wengi wanaoitwa mafundi wanaiuza kwamba inapunguza gharama ya upauaji! Kitu ambacho kinaweza kisiwe sahihi sana, ndo tunaishia kuvujiwa na nyumba kisha tunalaumu kuwa hiyo style ni mbaya!
Turejee kauli ya Mzee wetu Hayati Julius Kambarage Nyerere-"Ukweli haupendi kupuuzwa puuzwa"
 
Hizo contemporary ni nzuri sana kwa muonekano, ila nnavosikia zinaharibika haraka zinavujisha (nadhani shida itakua kwa wataalamu wetu) hawajazijulia vizuri....
Kuna jamaa kajenga haina hata mwaka tayari ndani kunavuja
Uko sahihi sana lakini:
1. Hutokana na kutumia watu wasio wazoefu
2. Kutokujua aina ya matirio ya finishing

Mfano kwenye mfereji na maungio ya bati ukutani kunahitaji (1) butmen nyeupe hii hupatikana NABAKI AFRIKA
(2) Membrane cloth hivi hutumika kwa pamoja na hutaona kuvuja wala unyevu.

3. Maungio ya mabati yanatakiwa overlap migongo 3 tofauti na ujenzi wa kawaida
 
Uko sahihi sana lakini:
1. Hutokana na kutumia watu wasio wazoefu
2. Kutokujua aina ya matirio ya finishing

Mfano kwenye mfereji na maungio ya bati ukutani kunahitaji (1) butmen nyeupe hii hupatikana NABAKI AFRIKA
(2) Membrane cloth hivi hutumika kwa pamoja na hutaona kuvuja wala unyevu.

3. Maungio ya mabati yanatakiwa overlap migongo 3 tofauti na ujenzi wa kawaida
Basi shida ipo hapo kwenye utaalamu, swala la kuvuja limekua kawaida kwa hizo nyumba....
Ila kwakweli kwa kutizama zinavutia ni nzuri
 
Habarini wakuu,

Kuna mjadala uliletwa humu kuhusu ni nyumba zipi zina gharama nafuu kwenye ujenzi kati ya hizi za kisasa za kuficha bati (‘contempoarary) na zile za kawaida. Ambapo kwa uzoefu wangu nilijaribu kuelezea kuwa kwa kawaida tunatarajia nyumba za paa la kuficha zitatumia tofali nyingi huku bati na mbao zikitumika kidogo sana (maranyingi haizidi nusu) wakati hizi za paa la kawaida zinatumia tofali chache huku zikitumia bati na mbao nyingi zaidi.

Lakini kuna mambo ya kuzingatia

1. Ongezeko la tofali kwenye contemporary house si kubwa sana kulinganisha na utofauti wa mahitaji ya mbao na bati za kupaulia baina ya aina hizi mbili za upauaji wa nyumba.

2. Gharama za mbao na bati kwa ujumla wake zinakupa ongezeko kubwa la gharama kwa nyumba za kawaida kulinganisha na contemporary house.

3. Kuna kitu kinachoongezeka kwenye nyumba za contemporary ambacho ni ‘concrete Gutter’ (mitaro ya kukusanya maji). Ambacho kwa mtazamo wangu nili commet kuwa ndio hasa kinaweza kufanya unafuu wa contempoary uliotokana na roofing ukaja kujilipa (kwa kukalibia au hata kuzidi) kulingana na idadi na namna mitaro ya maji ilivyowekwa kwenye nyumba amabyo kwa namna flani inatokana na ‘spatial arrangement’ ya ndani na namna flani za kuboresha mvuto wa jengo (Contemporary house zinaongezeka mvuto with complexity).

Hivyo basi pendekezo langu lilikuwa ni kwamba kama unataka kujenga kwa kuficha bati na huku pia ukitaka kupunguza gharama ni muhimu kuzingatia mpangilo wa nyumba utakao kufanya uepuke kujenga mitaro mingi kwenye nyumba.

Au unaweza kuepuka kabisa ujenzi wa mitaro kwa kuacha wazi upande wa nyuma ambao ndio maji yataelekezwa huko, na hii ni nzuiri zaidi maana pia itakupunguzia idadi ya tofali ambazo zingehitajika upande wa nyuma huku pia ukiepuka materials kwaajili ya ujenzi wa gutter ambalo lingehitaji zege la nondo.

Na kwakuongeza tu namna hii ya kuacha wazi upande wa nyuma iatakusaidia kupunguza risk ya nyumba kuvuja endapo hukutumia fundi mwenye uzoefu/ujuzi wa nyumba hizi, so risk ya kuvuja itabaki kuwa kwenye maungio ya bati na ukuta (kama fundi ni kimeo).
Kwa maelekezo zaidi juu ya masuala yote yahusuyo ujenzi unaweza kutucheki whatsapp 0717682856.

Unaweza kuona mfano wa hako ka ramani hapo chini (kalichorwa kwa lengo la kusave space na gharama). Kana vyumba vitatu (1master), kiStudy room kidogo, kitchen, dining na public toilet.

View attachment 1745814

View attachment 1745815

View attachment 1745816
Inaelekeaaa mkuu unaauzoefu mzur na hz nyumbaaa
 
Basi shida ipo hapo kwenye utaalamu, swala la kuvuja limekua kawaida kwa hizo nyumba....
Ila kwakweli kwa kutizama zinavutia ni nzuri
Shida inaanzia mbali.... Boss mwenye mjengo ana opt kupaua hivyo ili ku save cost, fundi-mchundo anaekutana nae pia anamuaminisha kuwa hiyo ita save costs sana. Mimi kuna fundi alinishauri mapema kabisa kuwa kama lengo lako ni kusave costs, achana na upauaji wa aina hiyo kabisa. Ila kama unachagua style hiyo kwa kuwa unaipenda na unapenda vitu vizuri, na suala la gharama sio shida kwako, go for it.
Evelyn Salt
 
Nyumba hii nimeikuta ddm fundi alinipa mpk garam lkn nasikia sinatatizo la kufujaView attachment 1763805View attachment 1763807View attachment 1763806View attachment 1763808View attachment 1763809View attachment 1763810View attachment 1763811View attachment 1763812
IMG_20200906_122227_0.jpg
 
Back
Top Bottom