Githeri Man awaunganisha Wakenya wakati wa taharuki kwenye mtandao

Githeri Man awaunganisha Wakenya wakati wa taharuki kwenye mtandao

1cfa7fb2a003da77774cf2f520800f8a.jpg
0143a86cc15897d37e3fc78bd6563e9b.jpg
e08391455bbf3ef3642ec042630f83a0.jpg
2f750f8ecf58e2b412b710765e86e4c7.jpg
46666d1ef2e632e3a3ca41743faf4289.jpg
f5312ce1734935de393d4f7cb05e8b62.jpg
0cff47516e4a7cc76cb014f298c98285.jpg
993a73fe83d121a20e26cd5ac61904f1.jpg
6ab3219329b80fac78dd3527b1878157.jpg


sent from iPhone 7
 
Githeri sio makande as such, kwa wadau wa kanda ya kaskazini mnajua makukuru, wachaga wanaita ngararum.. Ni mahindi ambayo hayajakobolewa yanachangwanywa na maharage kisha yanatiwa magadi kiaina.. Tofauti na makande ambayo mahindi yamekobolewa na hayawekwi magadi
 
Githeriman tibim! Kweli, kila mtu na siku yake! Britania wanamtaka, KWS wanataka kufanya kazi naye, KCB bank na Safaricom pia. Maina Kageni amesema yeyote atakayemfikisha kwa studio za CapitalFm anapewa 20,000 mara that that! KissFm wanamngoja pia. Yote hayo kwasababu jamaa alihisi njaa wakati akingoja kupiga kura! Wanaosema Mungu hayupo ni mambumbumbu tu.
 
b8f06ee17465b6fed9718f353ead67cd.jpg
e590dd1e8790ef25065561e883f20fc6.jpg
26ad7c734e88f107e2e735482f491fa0.jpg
Licha ya kuwepo miongoni mwa wananchi kuhusu matokeo ya kura ya urais, Wakenya kwenye mitandao ya kijamii Jumatano na Alhamisi waliunganishwa na picha ya mwanamume mmoja aliyekuwa akifurahia mlo wa Githeri kwenye foleni ya kupiga kura hapo Jumanne.

Mwanamume huyo ambaye amebandikwa jina 'Githeri Man' alinaswa na kamera ya mmoja wa wapiga kura akila mchanganyiko wake wa mahindi na maharage alioutia ndani ya karatasi ya plastiki katika kijibaridi cha asubuhi ya Jumanne.

Hadi wakati wa kuchapishwa kwa habari hii, jina lake halikuwa limetambulika wala anapoishi, kituo ambapo alipiga kura yake na aliyeipiga.

Kwenye Twitter Githeriman picha ya mwanamume huyo ilihaririwa na kuwekwa katika hali ambazo ziliibua msisimko mkubwa na utani usio na kifani.

Mojawapo ya picha hizo ilionyesha mwanamume huyo akiwa katikati ya Rais Kenyatta, Naibu Rais William Ruto na vinara wa NASA Raila Odinga na Kalonzo Musyoka.

Katika picha nyingine, alionyeshwa akifika Canaan. Msisimko wa safari ya Canaan ulianzishwa na Bw. Raila Odinga aliyasema atakuwa 'Yoshua' na kuwaongoza wakenya kutoka 'Misri'.

Alionekana pia akiwa kondakta, huku pia akitokea katika studio za Runinga za NTV na Citizen. Kwenye Spoti haikuachwa nyuma kwenye uchangamfu huo, mwanamume huyo alionekana kwenye picha mbalimbali.

Daniel Ndambuki wa Churchill Show anamsaka amhoji katika kipindi chake. Mimi niko tayari kumchangia pesa. Kubeba kwake githeri kunaonyesha alikuwa amejitolea kupiga kura. Amewaunganisha wakenya wote katika wakati wa taharuki. Tusherehekee maisha yake.

Ni kuhaririwa kwa picha hiyo ambako kulichangia wakenya mtandaoni kupunguza jumbe za chuki baada ya mwaniaji urais wa NASA, Raila Odinga kudai kwamba mfumo wa KIEMS wa IEBC ulidukuliwa usiku wa kuamkia Jumatano na kuweka matokeo ya uwongo.
 
huyo jamaa yaan kawa man of ze match ghafla
Kweli, ya mungu ni mengi aisee! Britania kampuni ya biskuti na kadhalika wametumia katuni ikila githeri kwa tangazo lao. Sasa hivi wanamtafuta ili wamlipe kwa kutumia katuni inayofanana naye! Dah! KWS, Safaricom na KCB bank wote wanamtaka! Jamaa anafanyia Nairobi County kazi ya kufagia!
 
He looks like Nigerian film star "Usihofu"
Hahahahahahaha
 
Kweli, ya mungu ni mengi aisee! Britania kampuni ya biskuti na kadhalika wametumia katuni ikila githeri kwa tangazo lao. Sasa hivi wanamtafuta ili wamlipe kwa kutumia katuni inayofanana naye! Dah! KWS, Safaricom na KCB bank wote wanamtaka! Jamaa anafanyia Nairobi County kazi ya kufagia!
ndiyo maisha yalivyo.........supu imemuangukia mdomoni

ila katisha kawa man of ze match zaidi ya uhuru aiseee inaelekea jamaa anaucomedy kwa mbali[emoji15] [emoji23] [emoji23]
 
Zinachekesha sana daaaaah [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Sent from my Android phone
 
Back
Top Bottom