Goba, Dar: Wanne wafariki dunia, 17 wajeruhiwa baada ya jengo kuangukia nyumba za jirani

Mmiliki ni mtu toka mkoa gani?
Isije ikawa Ni wale wanaoamini kamati za ufundi ......zaidi
Mwakifulefule kabila lakohalihusiki
 
Wafuatao ndo wakulaumiwa either mmoja wao, wawili au wote kwa pamoja.

1. Msanifu jengo husika (Arch/Engineer); kwa kushindwa kuandaa na kuproduce structure analysis za hilo jengo ambazo ndio miongozo ya kipi fundi anatakiwa ajenge na kuzingatia.

2. Mmiliki wa jengo; Kama mmiliki alikuwa bahili, akataka dezo kujenga structure sensitive Kama ghorofa kwa kutumia mafundi tu bila wataalam wa usanifu Majengo, Basi matunda ya ubahili huo ndo hayo. Na hili ni tatizo kwa watanzania wengi, wanapenda Sana cheap na kurash mambo kuliko kufuata procedures zinazotakiwa.

3. Mafundi; hapa Kuna mawili,
Mosi, Yawezekana mafundi hawakuwa na uzoefu au ujuzi wa kujenga high structural building, ikiwemo kushindwa kutafsiri lugha ya kihandisi iliyopo kwenye sheets za raman, hasa structural plans ambazo huitaji akili nyingi kidogo kuzielewa specifications zake.

Pili; Wizi wa materials site, mafundi baadhi siyo waaminifu, unakuta sehemu inayotakiwa atumie ratio ya mortar 1:4 yeye anatumia 1:6 ili tu mifuko ya siment kadhaa apite nayo,
Au unakuta sehemu inayotakiwa kuwekwa zege la Grade 25 yeye anaweka 20 ili tu nondo na siment zitakazo baki ziwe faida yake. Au unakuta anatumia nondo 3 badala ya nne kwenye column au beam kama ilivyoshauriwa na mtaalam.

Ifikie mahali Sasa tuache uswahili kwenye mambo ya mhimu Kama haya ya ujenzi wa maghorofa, mambo ya kupeleka mambo kimazoea matokeo yake ndo hayo yaliyo tokea kwenye huo mpolomoko.
 
Natoa pole kwa wafiwa na wananchi wa kata ya #Goba kufuatia vifo vya watu wanne vilivyosababishwa na kuanguka kwa ghorofa lililokuwa linaendelea kujengwa katika kata hiyo.

Uchunguzi wa tukio hili zisiachiwe mamlaka za #WilayaYaUbungo bali uhusishe CRB, ERB, IET, AQRB na TISS.
 
Kwa kawaida mamlaka ziko makini Sana na ujenzi wa ghorofa yoyote. Sijui ilikuwaje wakaacha huu ujenzi wa kuungaunga ukaendelea. Makosa ya wengi hapo
1.Mmiliki
2.Mafundi
3. Mamlaka husika
 
Hamna hata picha mkuu?
 
Amejenga kwa kumtumia fundi Maiko, hata Serikali inamtumia fundi Maiko kwa Fosi Akaunti.
 

Inasikitisha sana.
 
Back to Basics...
View attachment 2035336

Ukiona hayo ni maleluweluwe basi hiki kifuata...

View attachment 2035337

View attachment 2035333
Mkuu acha kuwachanganya watu.
Pale collapse imetaokana na poor or no design, naunder reinforcement .
Uzito mkubwa umewekwa kwa nguzo ambazo haziwezi kubeba mzigo wa ghorofa mbili.
Hiyo clip inayoonyesha swaying ground au hata seismic activity ni misleading, pengine ulikuwa unataka kuonyesha kitu kingine.

Hapo ni poor or no engineering design.
 
Inasikitisha, Mungu awapumzishe salama wapendwa wetu. Pole kwa familia zilizofikwa na maafa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…