vn_warehouse
JF-Expert Member
- Apr 13, 2023
- 648
- 854
Kigamboni watu wa mipango mji wamejitahidi sana
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Dalili za umasikini
Si yote
Nyerere ndo sababu ya matatizo yote TanzaniaGoba na milima yake kuanzia Kayuni mpaka huko tegeta A. Kama ingepangiliwa vizuri ikapimwa ingekuwa kama Beverly hills, Capetown RSA, Lavington Nairobi, Cite El nasr Au Menzah VI Tunis au Cairo New city Egypt, Cocody Abidjan Ivorycoast.
Hakuna raha kama mitaa inaelekea milimani halafu nyumba zimepangana. Sijui Nyerere alisahau wapi kuongoza upimaji ardhi na makazi maana yeye peke yake ndio alikuwa na akili za kuona miaka 100 mbele.
Ukitaka kujua nyerere alikuwa na akili angalia ardhi aliyowapimia na kuwapa TPA, Tazara, TRC wangekuwa hawa viongozi wa sasa wasingekuwa na akili ya kuacha ardhi kubwa leo gsm anafaidi eneo la tazara, azam anafaidi eneo la TPA, TRC. Hii kambi ya Lugalo enzi za mwalimu ilikuwa inaanzia mwenge mpaka mto mbezi bondeni kawe yote haikuwepo.
Hahahah ndioo. Ni gharamaa. Ila pia madalali wamezidi. Wakiambiwa wauze mil 10 wao wanakuuzia mil 50. Very stuppidGoba ni ya wale wasioweza kuishi Mbezi beach ila wana maisha ya juu kidogo. Kiwanja goba saivi sio mchezo mkuu.
Goba nilisikia kuna hadi fisi huwa wanatembea tembea kama mbuzi wa buguruni.Kwanini muende uswahilini Goba, mpeleke ushuani Mbweni kuna viwanja vipo vizuri na hakuna uswahili hata wa kuombana maji ya kunywa.
Hakuna sehemu Goba utapata kiwanja cha 10m mkuu, labda kama kipo njia ya maji. Kuna sehemu naifaham inaitwa Kulangwa, vidume peke yao ndio wanapamudu..sio poa!Hahahah ndioo. Ni gharamaa. Ila pia madalali wamezidi. Wakiambiwa wauze mil 10 wao wanakuuzia mil 50. Very stuppid
Aaah wapi, Tegeta A pako na uzuri gani mkuu, kote huko ni shanty tu.Tegeta A mbona pako vizuri,mpka goba mpakan
Mbagala ya Kaskazini MagharibiWikiendi iliyopita, Jumamosi na Jumapili nilipata wasaa wa kutembea Goba kwa sehemu kubwa kwa sababu nilikua na ndugu yangu ambae katoka huko mkoani anataka kiwanja na kujenga Dar.
Ndugu yangu kafika hapa tayari alishachagua eneo analolitaka kua ni Goba, basi tukatafta madalali na kuanza kuzungukia viwanja, kuanzia makongo, Goba Senta, Goba Kulagwa, Goba Kilalata kwa awadhi, ostabei na sehemu nyingine nyingi.
Baada ya mizunguko ya siku 2 ndio nikagundua kwamba Goba ni Uswahilini kwenye nyumba za kisasa.
Kwa maana kwamba Goba haijapangiliwa kabisa. Goba kuna nyumba kali na za kisasa sana ila hakujapangwa, nyumba nzuri ila zimejegwa zigzaga, hakuna mitaa iliyonyooka.
Miaka 30 ijayo Goba itakua kama Manzese ya sasa ama Tandale, itakua uswazi.
Ni wakati sasa Serikali inapaswa kuingilia hii biashara ya upimaji na uuzaji ardhi. Hua najiuliza hivi viongozi wetu wakienda huko ulaya hawaoni wenzetu miji yao ilivyopangwa? Mbona huku kwetu wanaacha mambo yanakua hovyo hivi?
Ni hayo tu wakuu.
Hakuna sehemu Goba utapata kiwanja cha 10m mkuu, labda kama kipo njia ya maji. Kuna sehemu naifaham inaitwa Kulangwa, vidume peke yao ndio wanapamudu..sio poa!
Unaonesha ww ni dalaliHakuna sehemu Goba utapata kiwanja cha 10m mkuu, labda kama kipo njia ya maji. Kuna sehemu naifaham inaitwa Kulangwa, vidume peke yao ndio wanapamudu..sio poa!
Sijawahi hata kuwaza mkuu, ila Goba naifaham kidogo, hasa maeneo ya kuanzia Mageti, njia nne, njia ya madale....huko hakushikiki chief, kama umefika mitaa wanaita kwa madokta(madr wa muhimbili wana vichuguu huko), hupanunui hata kwa 20m.
Hapo nimetolea mfano mkuu. Madalali wanazinhia sanaHakuna sehemu Goba utapata kiwanja cha 10m mkuu, labda kama kipo njia ya maji. Kuna sehemu naifaham inaitwa Kulangwa, vidume peke yao ndio wanapamudu..sio poa!
Nina eneo kubwa kidogo hapo flamingo madale ila kwakweli sipendi. Sifurahii jinsi majirani walivyojipangiliaSijawahi hata kuwaza mkuu, ila Goba naifaham kidogo, hasa maeneo ya kuanzia Mageti, njia nne, njia ya madale....huko hakushikiki chief, kama umefika mitaa wanaita kwa madokta(madr wa muhimbili wana vichuguu huko), hupanunui hata kwa 20m.
Umbali gani toka barabara kuu?Nina eneo kubwa kidogo hapo flamingo madale ila kwakweli sipendi. Sifurahii jinsi majirani walivyojipangilia
Kama dakika 7 hivi. Sema nadhani pia kwakua tulipita shortcut. Hako kamtaa kangu kamejificha kidogo.Umbali gani toka barabara kuu?
Mbona flamingo, huko mkoroshini ni pazuri tu(japo sipafaham sana)
Dk7 walking distance au bodaboda? Bado ni karibu mno, kama huna mpango napo subiri kidogo utauza bei nzuri hadi ufurahi.Kama dakika 7 hivi. Sema nadhani pia kwakua tulipita shortcut. Hako kamtaa kangu kamejificha kidogo.