Goba ni uswazi iliyochangamka ni Manzese ama Tandale ya miaka 30 ijayo

Kuna umuhimu sana kununua kiwanja kilichopimwa na survey plan yake ni approved tayari wizarani

Kuna kampuni iliniuzia kiwanja kigamboni ambacho kina ukubwa wa 960sq, ila kumbe katika upimaji wao walikosea barabara walizibana sana nafkiri ni katika kutafuta faida kubwa zaidi

Sasa kimbembe kikaja walivyokua wanataka kuanza ku process hati walivyopeleka survey plan yao ikakataliwa ...ikabidi watumie surveyor mwingine kuja kupima tena

Walivyopima tena kiwanja changu kikapungua kutoka 960sq mpaka 835sq kutokana na kutanuliwa kwa barabara za mitaa. Ndo survey plan yao ikawa approved wizarani

Hivi viwanja vya siku hizi wauzaji wamekua wanapima kiholela bila kufuata taratibu zilizopitishwa wizarani , mwisho wa siku mtu ukija ku process hati unatumia gharama kubwa sana kutokana na makosa ya waliokuuzia kiwanja

Note:

Tuwe makini sana tunapotaka kununua viwanja hasa sehemu za miji
 
Ni wakati sasa Serikali inapaswa kuingilia hii biashara ya upimaji na uuzaji ardhi. Hua najiuliza hivi viongozi wetu wakienda huko ulaya hawaoni wenzetu miji yao ilivyopangwa? Mbona huku kwetu wanaacha mambo yanakua hovyo hivi?

Mkuu sisi wa Afrika kwenye suala la kupanga "planning", hatuwezi...si kwenye ujenzi pekee hata kwenye uzazi wa watoto tushafeli
 
Goba ni ya wale wasioweza kuishi Mbezi beach ila wana maisha ya juu kidogo. Kiwanja goba saiv sio mchezo mkuu.
N kweli ila fikilia ardhi ya goba ilivyo mabonde na miinuko, alafu ujenzi wake kila kujipangia, Sijui wenyewe mnaita Squatter.
Sasa vuta picha miaka 30 ijayo miundo ya maji machafu itakua imejaa, na gari taka halitakuwa na uwezo wa kuifikia nyumba C, nini kitatokea.
 
Naunga mkono hoja 👍👏
 
wanaona lakini si ukitaka kula na kipofu usimsumbue ata kidogo
 
Kwa maana hiyo bhas viwanja vingi vya goba sio surveyed plots, watu wameuziana ile kwenda serikali ya mtaa?

Watu wa mipango mji walikua wapi mda wote huo?

After 20 years mnataka kusema goba itageuka kuwa scansca (tegeta) ?
Zamani tulipokuwa tunaenda goba huko kote palikuwa mashamba tu ya watu
Mtu anakuambia nakwenda shambani anarudi na mihogo nk
Goba haikupimwa kabisa

Ova
 
Nilibahatika kwenda kwenye nyumba ya jamaa mmoja zambia,lusaka panaitwa Kingsland aise ujenzi na maeneo yote yamekaa kimpangilio mbweni yenyewe,sjui osterbay haifikii

Ova
 
Zamani tulipokuwa tunaenda goba huko kote palikuwa mashamba tu ya watu
Mtu anakuambia nakwenda shambani anarudi na mihogo nk
Goba haikupimwa kabisa

Ova
Ni hatari sana hiyo....Watu wanapachukia kigamboni kutokana na geographical area yake lakini kule viwanja vimepangika sana kuanzia mji mwema kwenda huko kimbiji, mwasonga n.k
 

Njooni Dodoma nyinyi
 
Kwa maana hiyo bhas viwanja vingi vya goba sio surveyed plots, watu wameuziana ile kwenda serikali ya mtaa?

Watu wa mipango mji walikua wapi mda wote huo?

After 20 years mnataka kusema goba itageuka kuwa scansca (tegeta) ?
Tatizo la Tanzania ni kutofuatwa sheria na ushamba mwingi
 
Nyie mnapaita sahvi goba Centre
Wakati zamani hapo palikuwa panaitwa goba mwembe madole
Enzi hizo unaenda usafiri huko landrover na iko moja tu
Na wakati ule watu wengi huko walijipatia maeneo wakatiwa vijiji vya ujamaa,nguvu kazi kwenye kusafisha maeneo na wao wakawa wanajikatia maeneo

ila serikali yetu walichelewa sana
Kupapanga ndomana nyumba zimejengwa vululuvululu

Ova
 
Jumlisha ile milima mabonde sasa itakuwa zaidi ya Tandale.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…