Pre GE2025 Godbless Lema: Namuomba Mbowe apumzike, amuachie Lissu afanye kazi ya Uenyekiti CHADEMA

Pre GE2025 Godbless Lema: Namuomba Mbowe apumzike, amuachie Lissu afanye kazi ya Uenyekiti CHADEMA

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Ili uwe Katibu Mkuu sio!
Wewe ni mkimbizi- Canada( Katibu Mkuu)
TAL ni Mkimbizi - Belgium ( Mwenyekiti)
Heche ni Mjaluo wa Kenya ( Makamu Mwenyekiti)
Ndio utakuwa muundo mpya wa chadema🥺😳😳😳😳😳🥺
Haya yote mnayajua baada ya Lisu kutaka Uenyekiti?

Mlimpa Umakamu akiwa wapi?

Ni hasara sana kwa wazazi waliowazaa na kuwasomesheni.
 
Tatizo la Lisu kichwa chake hakijatulia.

Mbowe naye kachoka kwakweli sina tatizo naye apumzike tu.

Chadema inahitaji damu mpya ila wahusika walikosea kutoandaa warithi mapema.

Viongozi wetu wapunguze ubinafsi, nchi ni yetu sote.

Mtu huwezi kaa sehemu moja milele, kupeana nafasi iwe utamaduni wetu wa kudumu.

Hakuna mtu anaweza jimilikishia kitu milele.
 
Wakuu,

Siku ya jana aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA kanda ya Kaskazini kupitia akaunti yake ya X aliahidi kwamba siku ya leo Tarehe 14 January 2024 atakuwa anazungumza na wanahabari.

Wengi wameshuku kuwa huenda Lema atazungumzia kuhusu Uchaguzi wa CHADEMA na kuainisha ni mgombea gani ya Freeman Mbowe au Tundu Lissu anamuunga mkono.

Kaa karibu na Jamii Forums kupata updates zote

======================================================

"Mimi Mbowe ni kaka yangu, tunajuana. Yeye ni Mchaga na mmachame kama mimi, na familia zetu zinafahamiana, ila kwa uchaguzi ujao wa Mwenyekiti namuomba amuachie Tundu Lissu.

Lissu amekuwa Makamu Mwenyekiti, mnadhimu wa Bunge, Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, wanaosema hawezi kuwa Mwenyekiti wanataka nani awe?

Kuna watu wanasema Lissu asiwe Mwenyekiti kwasababu hana pesa, sasa niwaambie katika wakati ambao chama kinapaswa kupata kiongozi asiye na hela ni sasa ili wajumbe wajue kuwa chama hakipaswi kuendeshwa kwa pesa za mtu mmoja bali mobilization kutoka kwa watu. CHADEMA inabidi kitafute namba ya ku-rise fund. Kuna watu waliingia kwenye uongozi bila kuwa na pesa"



View: https://www.youtube.com/live/n4jGmCXtOsc?si=QELvyU3Ewhqvx9gA




Hawajamaliza hii script?
 
Ili uwe Katibu Mkuu sio!
Wewe ni mkimbizi- Canada( Katibu Mkuu)
TAL ni Mkimbizi - Belgium ( Mwenyekiti)
Heche ni Mjaluo wa Kenya ( Makamu Mwenyekiti)
Ndio utakuwa muundo mpya wa chadema🥺😳😳😳😳😳🥺
Wewe Mnywaranda mbona sisi tumepiga kimya...

Wakati kikosi kazi kinajipanga kuwa mtulivu mkuu
 
Kwani si watampumzisha kwenye uchaguzi au? Mbona kelele za apumzike ziko nyingi? Mtu wao hawezi kushinda ama? 😂😂
Mimi hicho ndio sielewi. Kwa vile wameona hastahili kuendelea kuwa Mwenyekiti wafanye kampeni ili wapiga kura wasimchague. Haya ya kumtaka apumzike, oh ni ndugu yangu, oh kabila yangu n.k. halina nafasi hapa. Lema hakuwa na haja ya kuweka press conference kutoa taarifa ya kitu ambacho wote tunakijua. Au anaogopa kuwa Mbowe nae atasema " et tu Lema?"

Mimi ningewashauri kuwa pamoja na kumshauri apumzike wangemwambia pia kuwa apumzike katika kuchangia chama kifedha kupita kiasi. Wanachama watakibeba chama chao.

Amandla...
 
Kadiri Mbowe anakavyokuwa mgumu kuachia kabla ya sanduku la kura...

Matamko yanazidi kuwa mengi....kumsihi aachie ngazi kabla ya uchaguzi, fedheha ya kuachia kabla ni ya muda mfupi kuliko la sanduku la kura, atashindwa hata kumshauri Lissu kwenye mambo ya Msingi
 
Nje ya siasa.
Huu uchaguzi wa chadema umenipa funzo kubwa sana kuhusu binadamu.

Binadamu ni kiumbe Cha ajabu sana! Nimefunza pa kubwa!

Najaribu kuwaza, FAM akishinda Hali itakuwaje katika chama?
 
Ili uwe Katibu Mkuu sio!
Wewe ni mkimbizi- Canada( Katibu Mkuu)
TAL ni Mkimbizi - Belgium ( Mwenyekiti)
Heche ni Mjaluo wa Kenya ( Makamu Mwenyekiti)
Ndio utakuwa muundo mpya wa chadema🥺😳😳😳😳😳🥺
Aisee umeongea ujinga wa kiwango cha juu sana. No wonder hata huko ccm hawakufahamu. Kauli kama hizo ilipaswa waongee wenye ccm yao kina Makala na Ridwan Kikwete siyo kima kama wewe. Chunga sana huu ujinga wako husije ukawarithisha watoto wako!
 
Uchaguzi ukiisha, lissu na nabii wake wapewe mkono wa kwaheli. Maana naona sasa hawamuheshimu menyekiti chama.
Uchaguzi ukiisha yeye na Lisu wanahama Chadema na makelele hay
yao

Mbowe bigwa walitaka kumpindua akiwa gerezani sasa kawaibukia sanduku.la kura kuwa njooni tupambane sanduku la kura

Wanapiga miyowe kibao wanajua Mbowe anaenda kuwabwaga sanduku la kura
 
20250108_180246.jpg
 
Jacob Zuma alimshinda Thabo Mbeki kwenye Urais wa ANC.

Wanaoamini Lisu ndio anakubalika wafunge midomo wawaache wajumbe wamchaguwe wanayemtaka.

Haya mambo ya kuachiana madaraka mngeyafanya mapema kwenye vikao vya kamati kuu na siyo unachukuwa fomu halafu unasema uachiwe ebo!
 
Tatizo la Lisu kichwa chake hakijatulia.

Mbowe naye kachoka kwakweli sina tatizo naye apumzike tu.

Chadema inahitaji damu mpya ila wahusika walikosea kutoandaa warithi mapema.

Viongozi wetu wapunguze ubinafsi, nchi ni yetu sote.

Mtu huwezi kaa sehemu moja milele, kupeana nafasi iwe utamaduni wetu wa kudumu.

Hakuna mtu anaweza jimilikishia kitu milele.
Hebu nipe faida za ACT Wazalendo kwa Zitto Kabwe kukaa pembeni na hiyo damu mpya kuingia kuna tija yoyote? Unamjuwa hata kwa jina aliyemrithi Zitto Kabwe?
 
Back
Top Bottom