Pre GE2025 Godbless Lema: Namuomba Mbowe apumzike, amuachie Lissu afanye kazi ya Uenyekiti CHADEMA

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Ili uwe Katibu Mkuu sio!
Wewe ni mkimbizi- Canada( Katibu Mkuu)
TAL ni Mkimbizi - Belgium ( Mwenyekiti)
Heche ni Mjaluo wa Kenya ( Makamu Mwenyekiti)
Ndio utakuwa muundo mpya wa chadema🥺😳😳😳😳😳🥺
Haya yote mnayajua baada ya Lisu kutaka Uenyekiti?

Mlimpa Umakamu akiwa wapi?

Ni hasara sana kwa wazazi waliowazaa na kuwasomesheni.
 
Tatizo la Lisu kichwa chake hakijatulia.

Mbowe naye kachoka kwakweli sina tatizo naye apumzike tu.

Chadema inahitaji damu mpya ila wahusika walikosea kutoandaa warithi mapema.

Viongozi wetu wapunguze ubinafsi, nchi ni yetu sote.

Mtu huwezi kaa sehemu moja milele, kupeana nafasi iwe utamaduni wetu wa kudumu.

Hakuna mtu anaweza jimilikishia kitu milele.
 
Hawajamaliza hii script?
 
Kwani si watampumzisha kwenye uchaguzi au? Mbona kelele za apumzike ziko nyingi? Mtu wao hawezi kushinda ama? 😂😂
Mimi hicho ndio sielewi. Kwa vile wameona hastahili kuendelea kuwa Mwenyekiti wafanye kampeni ili wapiga kura wasimchague. Haya ya kumtaka apumzike, oh ni ndugu yangu, oh kabila yangu n.k. halina nafasi hapa. Lema hakuwa na haja ya kuweka press conference kutoa taarifa ya kitu ambacho wote tunakijua. Au anaogopa kuwa Mbowe nae atasema " et tu Lema?"

Mimi ningewashauri kuwa pamoja na kumshauri apumzike wangemwambia pia kuwa apumzike katika kuchangia chama kifedha kupita kiasi. Wanachama watakibeba chama chao.

Amandla...
 
Kadiri Mbowe anakavyokuwa mgumu kuachia kabla ya sanduku la kura...

Matamko yanazidi kuwa mengi....kumsihi aachie ngazi kabla ya uchaguzi, fedheha ya kuachia kabla ni ya muda mfupi kuliko la sanduku la kura, atashindwa hata kumshauri Lissu kwenye mambo ya Msingi
 
Nje ya siasa.
Huu uchaguzi wa chadema umenipa funzo kubwa sana kuhusu binadamu.

Binadamu ni kiumbe Cha ajabu sana! Nimefunza pa kubwa!

Najaribu kuwaza, FAM akishinda Hali itakuwaje katika chama?
 
Ili uwe Katibu Mkuu sio!
Wewe ni mkimbizi- Canada( Katibu Mkuu)
TAL ni Mkimbizi - Belgium ( Mwenyekiti)
Heche ni Mjaluo wa Kenya ( Makamu Mwenyekiti)
Ndio utakuwa muundo mpya wa chadema🥺😳😳😳😳😳🥺
Aisee umeongea ujinga wa kiwango cha juu sana. No wonder hata huko ccm hawakufahamu. Kauli kama hizo ilipaswa waongee wenye ccm yao kina Makala na Ridwan Kikwete siyo kima kama wewe. Chunga sana huu ujinga wako husije ukawarithisha watoto wako!
 
Uchaguzi ukiisha, lissu na nabii wake wapewe mkono wa kwaheli. Maana naona sasa hawamuheshimu menyekiti chama.
Uchaguzi ukiisha yeye na Lisu wanahama Chadema na makelele hay
yao

Mbowe bigwa walitaka kumpindua akiwa gerezani sasa kawaibukia sanduku.la kura kuwa njooni tupambane sanduku la kura

Wanapiga miyowe kibao wanajua Mbowe anaenda kuwabwaga sanduku la kura
 
Jacob Zuma alimshinda Thabo Mbeki kwenye Urais wa ANC.

Wanaoamini Lisu ndio anakubalika wafunge midomo wawaache wajumbe wamchaguwe wanayemtaka.

Haya mambo ya kuachiana madaraka mngeyafanya mapema kwenye vikao vya kamati kuu na siyo unachukuwa fomu halafu unasema uachiwe ebo!
 
Hebu nipe faida za ACT Wazalendo kwa Zitto Kabwe kukaa pembeni na hiyo damu mpya kuingia kuna tija yoyote? Unamjuwa hata kwa jina aliyemrithi Zitto Kabwe?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…