Godbless Lema: Ningekuwa Rais nchi hii ningeondoa Hotel zote porini

SAsa hapa Chadema ndio wanapobugi, unadhani huu uchumi unaendeshwa kwa sigara na pombe?
Nimemkuta kada mmoja chadema,nikamuuliza mbona hamna plan B kuwezesha vijana,kuleta maendeleo,mnacheza na kupinga tuu,jamaa akanikimbia.
 
Sidhani kama anachosema ni kitu mwafaka. Mbona upande wa Maasai Mara kwa wenzetu Kenya kuna mahoteli ya kitalii zaidi ya 50 na maisha ya wanyama hayako hatarini.
 
Maana hapo kwanza nicheke...

Maajabu ya CHADEMA kumcheka CCM Kwa kuwa na RAIS Bora kama Samia ambae kawapa Ruksa ya kufanya Demokrasia,na wao wakijiskia Proud kuwa na Mwenyekiti au RAIS Form Four Failure kama Freeman Mbowe.

Kama mlivyomuona Jiwe ni MTU wa maana basi hakuna Fala yule hata kidogo kumfanya Samia awe Makamu wake we Bavicha.
 
Huna akili wewe acha kuota ndoto za alinacha wajerumani hawajawahi kualika makaburu
 
Huna akili wewe acha kuota ndoto za alinacha wajerumani hawajawahi kualika makaburu

soma historia vizuri huo ulikuwa ni mpango wa kuleta settlers kuja kusettle arusha kama vile waingereza walivyo settle upande wa pili wa valley kenya na kulima na kufuga leo kenya wanatuzidi kwa kiasi kikubwa kwenye agriculture na dairy products yote inatoka rift valley ya upande wa kenya ambapo kwetu rift valley ambayo the most fertile region in afrika ni hifadhi, kwanza unajua hata kwamba moshi ya leo ilikuwa inaitwa arusha chini? yaani kulikuwa na arusha juu ambayo ni arusha ya leo na moshi ya leo iliitwa arusha chini au upper and lower arusha kama ukipenda, kulikuwa na mipango kabambe na maendeleo ya kufa mtu sema vita iliingilia kati, hawa wazungu wote ni ndugu vita huwa inawazingua tu waonekane ni maadui lkn siyo kiivyo hata wao wanachonganishwa pia…
 
Mimi sijawahi kuwa mwanachama wa CHADEMA hata siku moja. Kusema kibibi Samia hafai kuwa rais siyo lazima uwe upinzani. Ni kutumia akili tu.
 
Hakukuwa na plan ya ku settle ngorongro kreta isopokuwa baadhi ya maeneo kama kando ya Miloma Meru na maeneo ya Oldeani na Mang'ola na hadi leo kuna majengo na mashamba ya settlers na maeneo hayakuwa hifadhi so acha kupotosha kama hauna taarifa. Eneo lingine ni lushoto ambao settlers walipelekwa
 
Sidhani kama anachosema ni kitu mwafaka. Mbona upande wa Maasai Mara kwa wenzetu Kenya kuna mahoteli ya kitalii zaidi ya 50 na maisha ya wanyama hayako hatarini.
Sidhani kama Kenya ndiyo yard stick yetu, wamekosea kwa hiyo sisi tusifanye makosa yale yale.

Hoja ya mji wa Karatu kuendelezwa na kuwa mji wa kitalii lisipuuzwe kwa sababu ni mji ulio karibu sana na hifadhi ya Ngorongoro na Serengeti.
 

ngorongoro imefanywa hifadhi kuanzia mwaka 1959 miaka 2 tu kabla ya uhuru, kabla ya hapo ilikiwa na shamba la mifugo na mpango kuleta settlers kutoka afrika kusini boers ( makaburu) ulisitishwa na vita kuu, ngorongoro kama hifadhi haina hata miaka 100 ilianzishwa mwaka 1959, labda mnasahau kwamba ngorongoro ni sehemu ya rift valley ambapo ni most fertile region in afrika inakwenda mpaka southern afrika, waingereza hawakuitenga rift valley kwenye koloni lao kenya kama hifadhi kwa nini unafikiri? kwa sababu settlers wa kizungu walikuwa huko wanalima na kufuga huku kwetu wakapiga spana …
 
Kwake Lema ulinzi wa IKOLOJIA mintaarafu ya hapo Ngororongo wala si muhimu.....

Hivi madola yasingeweka sheria juu ya kulinda hifadhi za WANYAMAPORI ,hali ingelikuwaje hivi leo ?!!![emoji44][emoji44]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…