God's Conscience vs Free Will: Je, Mungu anajua hatima ya wanadamu itakuwaje?

God's Conscience vs Free Will: Je, Mungu anajua hatima ya wanadamu itakuwaje?

Muda ni kiumbe cha Mungu...Mungu ameumba muda/nyakati. Yeye hawi governed na Muda yaani hana jana, hana leo wala hana kesho ila ametuumbia usiku na mchana ziwe kama ishara za kutambua uwepo wake na pia zitusaidie kujua hesabu za siku, miezi na miaka. Hivyo ukimuwaza Mungu usimtazame ktk muda.

Ametuumba akiwa anajua jana yetu, leo yetu na kesho yetu...ameipa nafsi uhuru imuabudu au imkatae. Hana sifa ya kuwadhulumu waja wake kabisa, infact amejiharamishia dhulma. Anajua nafsi nn zitachagua na ameweka reward /malipo kwa kila chaguzi litakalofanywa na nafsi iwe ni baya au zuri.
Upo vizuri sana, hivyo ndivyo ilivyo
 
Imani kwa ilivyotumika ni muunganiko wa uhalisia kuhusu ukweli wa jambo/mambo ulivyo kama mtu binafsi anavyoona mwenyewe. Imani ni binafsi unaijua mwenyewe imani yako.

Kama ndicho unachokitaka basi amini kwamba ulimwengu huu uliopo ndio huo unaoutamani, ni suala la muda tu.

Ulimwengu tulionao unayo mazuri yote yanayompendeza kila mtu kwa namna yake katika dunia/[uhalisia] wake, hakuna uwezekano wa watu kukosoa chochote katika uhalisia wao. Bali watakosoa vitu vingine tu katika uhalisia wa wenzao walio katika dunia nyingine.

Natumai sasa nimejibu tena, najua nishajibu zaidi ya mara moja.
Imani ingekuwa uhalisia basi leo kungekuwa na imani moja

Since kuna buch la imani tena zinazopingana huo ni uthibitisho imani ni ujinga tu

Hata wewe hukubaliani na imani nyingi, kwanini usikubaliane nazo kama imani ni uhalisia?

Tuna record nyingi za watu kuamini uwongo na mwisho wa siku imani hizo leo hii zinatambulika kama ni ujinga baada ya kuwa debunked
 
Kuumwa tumbo ni kusudi jema kwa hiyo being nzima, kuanzia mtu [kama consciousness ya mtu], mtu kama mwili wa mtu, na hizo seli za tumbo na hata seli zote za mwili wa huyo mtu......... in fact ni chema kwa mke/mme wa huyo mtu, familia ya huyo mtu, jamii na taifa na dunia kwa ujumla. WHY? Tumbo linapouma tunakuwa na taarifa wote kwamba kuna kitu hakiko sawa na juhudi zinafanyika tunarudisha AFYA kwa mtu husika ambaye uwepo wake ni faida kwa wote.

Sisi ni finite, I mean miili yetu ina mwisho na hata hilo jambo la miili yetu kuisha ina kusudi jema pia🤭. Purely materialist kuelewa hilo labda chukulia metamofosisi za kipepeo. Kutoka lifunza [caterpillar] kula majani, na kutembelea tumbo ardhini na mtini tu[kuelekea kushoto au kulia tu] kufa kuwekwa kwenye jeneza[buu] hadi kuwa kakipepeo kufyonza nekta tamu na kupaa angani[kuelekea kushoto, kulia, juu, chini, kujongea kushoto-chini, kushoto-juu, kulia-chini na kulia juu au ku hover palepale maybe!] kuvuka mito na kuishi popote na kuvinjari almost msitu wote. There is season and purpose thereof.

Tuna shida moja tu hapa: Mungu inafahamika ni hana mwisho[infinity] na vyote tulivyonavyo duniani vina mwisho [finite] hivyo hakuna mfano hata mmoja utakaoshibisha picha kamili ya Mungu. Hilo wote tunakubaliana. Mifano tunayotoa inajaribu kugusia sifa chache za ukuu wake, ni analojia zisizo kamili. Mfano wa mwili na seli zake umetumika kuonesha kuwa kuna kusudi jema katika maumivu yetu na umeelezea vizuri hilo, that is all.
Kuumwa tumbo ni jambo jema kwa nani?
 
Imani ingekuwa uhalisia basi leo kungekuwa na imani moja

Since kuna buch la imani tena zinazopingana huo ni uthibitisho imani ni ujinga tu

Hata wewe hukubaliani na imani nyingi, kwanini usikubaliane nazo kama imani ni uhalisia?

Tuna record nyingi za watu kuamini uwongo na mwisho wa siku imani hizo leo hii zinatambulika kama ni ujinga baada ya kuwa debunked
Imani ni kitu binafsi hatuwezi kuwa na imani moja kwa sababu ni watu tofauti.

Uzuri au ubaya wa imani ni kuwa yule anayeamini anaishi na au kufa humo akifaidi mambo yoooote ya hiyo imani yake binafsi. Wewe ukija leo ukasema yule wa zamani alikoseaga tambua kuwa haimuathiri yeye kama hiyo feeling inavyokuathiri wewe.

Kila mtu anaishi dunia yake/ uhalisia wake hatupangiani
 
Upo vizuri sana, hivyo ndivyo ilivyo
Watu wengi hawaelewi kuhusu haya mambo, katika nguzo sita za imani ya kiislam, kuna nguzo ya mwisho inaitwa kuamini Qadar (makadirio ya ALLAH) kuwa heri na shari vyote vinatokana na Qadar yake ALLAH (Mungu).

Mtume Muhammad aliripotiwa akisema kuwa "ALLAH anasema kuwa " mwana wa Adam anamtukana Yeye, Anautukana Muda(nyakati) na YEYE (ALLAH) ndio Muda, kwa hakika katika mkono wake ndipo kuna usiku na mchana" ~bukhar

Abu Huraira reported: The Messenger of Allah, peace and blessings be upon him, said, “Allah Almighty said: The son of Adam abuses me. He curses time and I am time, for in my hand are the night and day.” ~bukhar

Miongoni mwa majina matukufu ya Mungu ni wa "MWANZO" na wa "MWISHO" . Kabla yake hakuna mwanzo na mwisho wake hakuna mwisho" , Kwahiyo Mungu hana Jana wala kesho.

Hizi nyakati ameziumba kwa ajili yetu sisi wanaadamu tupate kujua hesabu za siku na miaka. MUNGU ni wa milele, hafi, hachoki ,hasinzii wala hapumziki.

Tatizo wanaadamu tunamtizama MUNGU ktk mtazamo wa kibinadamu.

Na hata tuwaze vipi bado hatuwezi kumuwaza Mungu katika ukubwa na utukufu wake. Akili zetu zina ukomo wa kufikiri na kuwaza. Ametakasika mola mlezi wa walimwengu wote.
 
We live in the universe of 'duality'

Good|bad, juu|chini, kulia|kushoto, ukweli|uongo
MUNGU | SHETANI

Ili ulimwengu uwe balanced ilibidi MUNGU amuumbe shetani

Kosa kubwa watu hufanya kwenye majadiliano yahusuyo Imani ni kuuliza swali la MUNGU ni Nani badala ya MUNGU ni nini? Na ndicho kinachojadiliwa hapa

Kwanza kabisa tujiulize MUNGU ni nini?

Nikupe mfano huu,
MUNGU katika kusudi lake la milele kabla hajamuumba binadamu aliuliza HAKI,KWELI NA HURUMA endapo ni vema wamuumbe binadamu au lah

Haki akajibu "usimuumbe binadamu Kwa kuwa atazivunja Sheria na kanuni zako zote"

Kweli akajibu "usimuumbe Kwa kuwa binadamu atakuwa mbaya na daima atatafuta uwongo na hila( udanganyifu)

Huruma akajibu "ninajua mwanadamu atakuwa mbaya Sana lakini Mimi nitamuhifandhi na kutembea naye katika njia zake za Giza mpaka mwishowe nitamrejesha kwako"

Umejifunza nini hapa mkuu kuhusu free will mkuu?

Kuna tofauti Kati ya dhambi na nakosa.Ukifanya dhambi MUNGU hawezi kukuona maana ni mtakatikfu ,ndy maana Adam alipokula tunda, MUNGU hakumuona Adam ndy maana akauliza "Adam uko wapi"
Mkuu nikusahihishe tu kuwa hakuna kinachofichikana kwa MUNGU.Iwe ni mdudu mdogo aliye ndani ya udongo au hata ndege aliyepo angani ..vyote ana viona. Moja ya jina ktk majina yake Mwenyezi Mungu linaitwa "MWENYE KUONA" anaona kila kitu kiwe kikubwa ama kidogo hakuna kinachofichikana kwake.

Kitendo cha Adam na Mkewe ,bi Hawa kula tunda la mti waliokatazwa ,tayari Mungu alishajua na infact alishajua kabla hawajala kuwa watakuja tu kula. Alilitambua hili na aliwaonya mapema kuwa wasile maana wakila watavuna matokeo yake.

Kitendo cha Mungu kusema upo wapi ewe Adam hakikuwa na maana kuwa hakujua Adam alipojificha laa hasha . Ni sawa na pale alipomuuliza Musa umeshika nini mkononi mwako ewe Musa .Musa akamjibu kuwa nimeshika fimbo. Sio kwamba alikuwa hajui au hamuoni Musa kuwa ameshika fimbo. Kilugha tunaita ni rhetoric question! Ni swali unauliza ukiwa huna lengo la kupata jibu lake, kwani tayari wewe muulizaji unajua jibu lake.
 
Synonym alishalimaliza hili suala, alisema kuna matendo ambayo mtu atahukumiwa nayo na mengine hatahukumiwa nayo. Nakubali uwepo wa hizo 'ajali' mda mwingine lakini siwezi kuuweka mustakabali wa maisha yote chini ya mambo tusiyoyaendesha sisi kama sisi. Zipo chaguzi nyingi tu za kuitikia hizo unazoziita 'ajali' na zipo chini ya utashihuru wako -FREEWILL

Kaka zipo hatua za kun'gamua na kubeba majukumu na kadri unavyokuwa na majukumu zaidi ndio unazidi kuwa na uwezo zaidi. Na uwezo ni simply uamrishaji wa will yako, hivyo ni uhuru zaidi:View attachment 2252383
Naamini sasa utakuwa umenielewa kwa nini nilijiuliza lile swali lililokuvunja mbavu

Nakazia: Watu eidha hawajui tofauti au wanashindwa kuoanisha kwa usahihi au wanachanganya;

1. Prescience 'Foreknowledge'

2. Devine will and decree 'Mipango/Matakwa na Makadirio'' na

3. Free will

Ndo maana unaona mtu anauliza kwa nini hakupewa nafasi ya kuchagua kuwepo au kutokuwepo duniani hata kabla hajaumbwa?

"And your Lord creates whatsoever/whomsoever He wills and chooses" Al-Qasas, verse no. 68

Au mtu ahoji nafasi ya kijusi katika kuchagua kuzaliwa au kutokuzaliwa? [emoji23]

Hivi kijusi kina akili tambuzi? Hivi kijusi kinaweza kutofautisha kati ya jema na zuri? Hivi kijusi kinaweza kutenda kwa kutaka kwa mfano: kula au kutokula? Kwa minajili hiyo kijusi kina utashi huru? Kwa werevu mtakuwa mmeshang'amua

"It is He who shapes/forms you in the wombs of your mothers however/as He wills" Al-Imraan, verse no. 6

Hivyo, asome na ajifunze kutofautisha kati ya hivi

1. Vitendo vya mja na vitendo vya Mungu

2. Vitendo vya hiari au kutaka na vitendo visivyo vya hiari au kutokutaka
 
Naamini sasa utakuwa umenielewa kwa nini nilijiuliza lile swali lililokuvunja mbavu

Nakazia: Watu eidha hawajui tofauti au wanashindwa kuoanisha kwa usahihi au wanachanganya;

1. Prescience 'Foreknowledge'

2. Devine will and decree 'Mipango/Matakwa na Makadirio'' na

3. Free will

Ndo maana unaona mtu anauliza kwa nini hakupewa nafasi ya kuchagua kuwepo au kutokuwepo duniani hata kabla hajaumbwa?

"And your Lord creates whatsoever/whomsoever He wills and chooses" Al-Qasas, verse no. 68

Au mtu ahoji nafasi ya kijusi katika kuchagua kuzaliwa au kutokuzaliwa? [emoji23]

Hivi kijusi kina akili tambuzi? Hivi kijusi kinaweza kutofautisha kati ya jema na zuri? Hivi kijusi kinaweza kutenda kwa kutaka kwa mfano: kula au kutokula? Kwa minajili hiyo kijusi kina utashi huru? Kwa werevu mtakuwa mmeshang'amua

"It is He who shapes/forms you in the wombs of your mothers however/as He wills" Al-Imraan, verse no. 6

Hivyo, asome na ajifunze kutofautisha kati ya hivi

1. Vitendo vya mja na vitendo vya Mungu

2. Vitendo vya hiari au kutaka na vitendo visivyo vya hiari au kutokutaka
Ewaaaah! kumbe sasa umenielewesha vizuri zaidi. Inaonesha kuwa walio kinyume na free-will in essence hawataki tu kuyakabili majukumu ya kiutu, au ya kiutu-uzima.

Kwa nini wajifananishe na katoto ambako bado hakana utashi huru? Helpless

Ndio maana wanataka hadi wapewe maarifa yote bila kuyatafuta, watatuliwe matatizo yao yote na Mungu bila wao kufanya chochote. Eti ndio wamuamini

Wanajiona watoto wasio na maamuzi wala majukumu badala ya kujiona ni wana wenye majukumu na maamuzi pia.
 
Naamini sasa utakuwa umenielewa kwa nini nilijiuliza lile swali lililokuvunja mbavu

Nakazia: Watu eidha hawajui tofauti au wanashindwa kuoanisha kwa usahihi au wanachanganya;

1. Prescience 'Foreknowledge'

2. Devine will and decree 'Mipango/Matakwa na Makadirio'' na

3. Free will

Ndo maana unaona mtu anauliza kwa nini hakupewa nafasi ya kuchagua kuwepo au kutokuwepo duniani hata kabla hajaumbwa?

"And your Lord creates whatsoever/whomsoever He wills and chooses" Al-Qasas, verse no. 68

Au mtu ahoji nafasi ya kijusi katika kuchagua kuzaliwa au kutokuzaliwa? [emoji23]

Hivi kijusi kina akili tambuzi? Hivi kijusi kinaweza kutofautisha kati ya jema na zuri? Hivi kijusi kinaweza kutenda kwa kutaka kwa mfano: kula au kutokula? Kwa minajili hiyo kijusi kina utashi huru? Kwa werevu mtakuwa mmeshang'amua

"It is He who shapes/forms you in the wombs of your mothers however/as He wills" Al-Imraan, verse no. 6

Hivyo, asome na ajifunze kutofautisha kati ya hivi

1. Vitendo vya mja na vitendo vya Mungu

2. Vitendo vya hiari au kutaka na vitendo visivyo vya hiari au kutokutaka
Nijazie nyama kidogo ndugu yangu ni kuwa kila unaemuona ni binadamu awe alishaishi ktk dunia hii,anaishi ktk dunia hii au atakuja kuishi ktk dunia hii jua kuwa alikubali kuumbwa kuwa binadamu na alikubali kuibeba amana ya Mola wake.

ALLAH anaelezea katika Quran kuwa
Quran 33:72


Indeed, we offered the Trust to the heavens and the earth and the mountains, and they declined to bear it and feared it; but man [undertook to] bear it. Indeed, he was unjust and ignorant.


Kwa hakika Sisi tulikadimisha amana kwa mbingu na ardhi na milima; na vyote hivyo vikakataa kuichukua na vikaogopa. Lakini mwanaadamu akaichukua. Hakika yeye amekuwa dhaalimu mjinga."

Na kila nafsi ya mwanadamu ilikiri mbele ya MUNGU kuwa hapana mola apasae kuabudiwa ila Mwenyezi Mungu. Kisha Mungu ndio akaamua kuzileta nafsi hizi huku duniani kwa nyakati tofauti. Nafsi inaletwa katika ulimwengu huu ktk hali ya umbile la mtoto mchanga kabisa ikiwa ktk fitrah ile ile ya kumjua MUNGU mmoja ila wazazi wa mtoto ndio humtoa mtoto katika hali ile ya kumjua MUNGU mmoja na kuanza kumfundisha kuhusu imani aamini mungu(miungu) asiyekuwa ALLAH
 
Ewaaaah! kumbe sasa umenielewesha vizuri zaidi. Inaonesha kuwa walio kinyume na free-will in essence hawataki tu kuyakabili majukumu ya kiutu, au ya kiutu-uzima.

Kwa nini wajifananishe na katoto ambako bado hakana utashi huru? Helpless

Ndio maana wanataka hadi wapewe maarifa yote bila kuyatafuta, watatuliwe matatizo yao yote na Mungu bila wao kufanya chochote. Eti ndio wamuamini

Wanajiona watoto wasio na maamuzi wala majukumu badala ya kujiona ni wana wenye majukumu na maamuzi pia.
Tatizo wanaadamu tunajisahaulisha kwa makusudi kuwa hatukukubali kuibeba amanah ya MUNGU. Wanaadamu tulikubali wenyewe kuwa tutafata maamrisho ya Mungu hapa duniani na kuyaacha makatazo yake na tulikubali kuwa atakayefata aliyoyaamrisha Mungu atapewa malipo mazuri na atakayeyaacha ataadhibiwa vikali. Haya tuliyakubali kwa mikono yetu miwili kuyabeba licha ya sisi kuwa ni dhaifu na ni wenye kujidhulumu nafsi zetu.

Mbingu, Ardhi na milima, wanyama ,wadudu ,ndege wote walikataa kuibeba hiyo amanah ila sisi na majini tulikubali kuibeba!!! Na ndio hapo tukapewa FREE WILL (to do or not to do). Ila hivyo viumbe vingine vyote havikupewa huu upendeleo wa free will.
 
Kuhusu suala la fact vs imani unajidanganya. Hata fact tunavyoiona inatofautiana kutokana na 'imani' ya anayeitazama hiyo fact.

Fact inaweza kuwa ni homa au maumivu lakini kwenye kusema ni kitu kiovu au ni kitu chema itategemea na imani zetu. Mimi nikipata homa labda naamini ni mwili wangu unanisaidia kupambana na virusi hivyo ninaishi - Purpose is good.

Hapa nimetumia neno imani kama namna tunavyochukulia kuwa ukweli wa mambo ndivyo ulivyo yaani uhalisia. Kwa kusema hivyo the problem of evil ni sababu moja zaidi ya kumuondoa Mungu mwenye upendo katika dunia yako, wakati ni sababu moja zaidi ya kumuona Mungu mwenye upendo katika dunia yangu. Inatokana na imani/uhalisia wetu binafsi.

Katika dunia isiyo na kusudi everything can be evil, lakini katika dunia yenye kusudi EVERYTHING IS GOOD. We are surrounded with overabundance of goodness which we will keep realizing over time. Chooing to be the side of evil or good is your choice to make. FREEWILL
Nilishalitolea analojia ya mwili hili. #637
Unapostulate mambo bila ushahidi wala kuonesha mambo logically, kwa wishful thinking tu.
 
Kwangu mimi nitatumia yote ninayoyajua hadi hivi sasa na nitaamini katika yale ambayo bado sijayathibitisha nitatumia trust na faith kukamilisha ambacho knowledge imebakiza. Kama nikipata data ikathibitisha kinyume labda ntaacha, ila siachi nisikudanganye kwa ninachokijua hadi sasa hivi sisi ni wa Mungu tu bro hamna namna🤦‍♂️. Ndo maana walokole wanasemaga NIMEOKOKAA

Kwa suala la ukatibu mkuu wa UN siwezi kuendelea nalo maana hakuna knowledge inayosapoti hivyo, na kuna vitu tayari vinaniprovia kwamba hicho kitu ni wrong. Mfano:sijawahi hata kupanda ndege[labda hii chukulia ni prerequiste]
Mungu wako, dhana ya kuwapo kwake na kuwapo kwa ulimwengu huu ina logical inconsistency.

Sawasawa na pembetatu ambayo hapohapo ni duara kwenye Euclidean geometry.

Unaruhusiwa kuamini kwamba pembetatu duara ipo, lakini hilo halifanyi pembetatu duara hiyo iwepo.
 
Mkuu nikusahihishe tu kuwa hakuna kinachofichikana kwa MUNGU.Iwe ni mdudu mdogo aliye ndani ya udongo au hata ndege aliyepo angani ..vyote ana viona.
Anaviona.... Kuona ni tendo lenye mchakato/hatua, JE, KWANINI MUNGU ALAZIMIKE KUCHAKATA KATIKA NYENDO ZAKE?
Moja ya jina ktk majina yake Mwenyezi Mungu linaitwa "MWENYE KUONA" anaona kila kitu kiwe kikubwa ama kidogo hakuna kinachofichikana kwake.
Kwanini isiwe CHENYE/PENYE/LENYE/YENYE nk.... Kwanini Dhana Mungu iko personalised? Je, hamuoni kuwa hilo ndilo linalokaribisha Udhaifu na mapungufu mengi juu ya Mungu?
Kitendo cha Adam na Mkewe ,bi Hawa kula tunda la mti waliokatazwa ,tayari Mungu alishajua na infact alishajua kabla hawajala kuwa watakuja tu kula.
Hivyo kuwaonya alikuwa anajua kuwa nibkupoteza muda tu, na bado akafanya?
Alilitambua hili na aliwaonya mapema kuwa wasile maana wakila watavuna matokeo yake.
Hata Leo hii, huwezi kutoa vitisho vya kinyago kinachotisha kwa mtoto kipofu, ilikuwaje atishie watu ambao alikuwa anajua 100% hawatamsikiliza?

Kosa ni kupersonalize Mungu.
Kitendo cha Mungu kusema upo wapi ewe Adam hakikuwa na maana kuwa hakujua Adam alipojificha laa hasha . Ni sawa na pale alipomuuliza Musa umeshika nini mkononi mwako ewe Musa .Musa akamjibu kuwa nimeshika fimbo. Sio kwamba alikuwa hajui au hamuoni Musa kuwa ameshika fimbo. Kilugha tunaita ni rhetoric question! Ni swali unauliza ukiwa huna lengo la kupata jibu lake, kwani tayari wewe muulizaji unajua jibu lake.
Unapaswa usemee hiyo maana sasa, Kwanini atumie Tashititi, ili iwe nini?
 
Tatizo wanaadamu tunajisahaulisha kwa makusudi kuwa hatukukubali kuibeba amanah ya MUNGU.
Tulikubalije? Hiyo amanah nini hasa? Na kwanini tuwajibike kumbebea Mungu, kwanini asibebe mwenyewe?
Wanaadamu tulikubali wenyewe kuwa tutafata maamrisho ya Mungu hapa duniani na kuyaacha makatazo yake na tulikubali kuwa atakayefata aliyoyaamrisha Mungu atapewa malipo mazuri na atakayeyaacha ataadhibiwa vikali. Haya tuliyakubali kwa mikono yetu miwili kuyabeba licha ya sisi kuwa ni dhaifu na ni wenye kujidhulumu nafsi zetu.
Makubaliano hayo yalifanyikaje?
Mbingu, Ardhi na milima, wanyama ,wadudu ,ndege wote walikataa kuibeba hiyo amanah ila sisi na majini tulikubali kuibeba!!!
Usibebe kila dhana uzisikiazo kwenye Hekaya na Masimulizi ya Kiimani.
Na ndio hapo tukapewa FREE WILL (to do or not to do). Ila hivyo viumbe vingine vyote havikupewa huu upendeleo wa free will.
FreeWill ni Kiini Macho, hakijawahi kuwepo kokote.
 
Mungu wako umemtengeneza mwenyewe kichwani halafu umemrusha vikwazo vyote in "a priori" way.

Ama unakubali logic, ama hukubali.

Ukikubali logic, Mungu wako hayupo, kwa sababu dhana ya kuwapo kwake ina logical inconsistency.

Ukikataa logic, Mungu wako hayupo, kwa sababu ulimwengu usiofuata logic haumuhitaji Mungu.

Popote utakapokwenda, unakuta Mungu hayupo.

Kwa sababu, Mungu huyo hayupo.
Aje kama hicho kiitwacho kuwa LOGIC ndio hichohicho kiitwacho kuwa MUNGU?

JE, BADO HAKITAKUWEPO?

Mungu ni Ukamilifu wa Hesabu wa Uwepo ama Kutokuwepo kwa jambo au kitu chochote. Nayo ndiyo Logic.
 
Kwa nini hutamini?
Knowledge, mambo ninayofahamu na sheria za kuaminika zimeonesha hicho kitu hakipo pembetatu ni pembetatu na duara ni duara sijaonaga hata hint ya kuwepo pembetatuduara katika ujuzi wangu ninaoufahamu kwa maumbo bapa hadi sasa. Na sina haja ya kutegemea maajabu maana naamini hiyo eucledian geometry unayoisema ina mipaka ya bapa tu.

Ikiwa tutatengeneza dimensions zaidi basi hiyo pembetatuduara inawezekana kuwepo. Tukiuongeza uwanda wetu wa uhalisia mambo yaliyoonekana hayawezekani yanaanza kuonekana yanawezekana na ndio kawaida kabisa! Pembetatu duara ipo hata kwa 3d ukinipa maplastiki nitakuchongea. Itahitaji tu kuiweka kuitazama upande fulani utaiona pembetatu na ukiigeuza kwingine utaiona duara. Ukiweza kupanda dimension za zaidi pia haikatai utaweza kuziona zote pembetatu na duara kwa wakati mmoja!

Itoshe sasa kutuchosha na swali lako la pembetatu duara - Jibu ni ongeza uwanda wa uhalisia, panua sheria na hiyo pembetatu duara utaiona bila wasi
 
Aje kama hicho kiitwacho kuwa LOGIC ndio hichohicho kiitwacho kuwa MUNGU?

JE, BADO HAKITAKUWEPO?

Mungu ni Ukamilifu wa Hesabu wa Uwepo ama Kutokuwepo kwa jambo au kitu chochote. Nayo ndiyo Logic.
Safi sana kwa kukazia hili, hata mimi nilionelea labda tujaribu kutumia kile kitu anakikubali zaidi. LOGIC, LOGOS, NENO.

Inaonekana alilitambua hilo akaamua kuja na literm la 'deus ex machina' mi nikawa absorbed na hilo li term tukaendelea na mambo mengine.

Ilifanya kazi kwa wagiriki labda na kwake itamsaidia. Akibadilika huyu mwamba atakuwa kama Paulo. Tumuombee tu asije akamdistort Mungu kuwa logic pekee [au na we ndio unavyoamini nini- nimeona dalili].

Kiranga ee angalizo, logic ni moja ya sifa ya Mungu, ni Mungu pia ukitazama kwa jicho la kiroho. Kama unaamini logic unapataje tabu sasa kumuamini Mungu. Kama ambavyo tunasema Mungu ni Upendo vivyo hivyo tunaweza kusema Mungu ni NENO/LOGOS/LOGIC. Je baada ya hapo utakubali?
 
Kosa ni kupersonalize Mungu.
Anhaa kumbe wewe unaposema ni LOGIC unataka kuiacha kama tu entity fulani hewani.

Hapana. Kumpersonalize Mungu ni jambo jema labda kumuanthropormorphize ndio haifai.

Mungu ni personal katika uhusiano wake na uumbaji wake kabisa japo sio anthropormorphic.
 
Back
Top Bottom