Gone Too Soon: RIP JF Member.....Chetuntu!!!

Gone Too Soon: RIP JF Member.....Chetuntu!!!

Aaaaaaish, jamani why?? nilikuwa nachati nae sana kwa PM na nilijua ni mjamzito maskini chentutu, ni rafiki yangu sana humu, mara nyingi akiingia tuna pm hapa na pale,mara ya mwisho ni mwanzoni mwa august maskini angejua linalokuja labda angefanya cha ziada, napenda kujua alijifungulia hospital gani, Mungu ailaze roho ya marehemu chentutu mahala pema peponi.....naunga mkono pia kuchangia kwani sie humu ni binadamu na tunaweza kabisa kufanya jambo kuonyeshwa tumeguswa, nami naungana na wanaohitaji kutoa rambirambi zikasaidie familia yake
 
Pole soulmate, ndio dunia kila mtu hiiyo njia atapita, pole sana kimey ni mipango ya Mungu, still njisikia vibaya coz nimejua leo hii habari, unajua humu JF kuna kitu unachati na mtu mpaka unampicture labda yuko hivi au vile na mimi pia nahisi kama nimepotelewa na mtu ambae tulikuwa wote mara kwa mara, nakumbuka mara nyingi nikionekana natoa comment ya huzuni lazima ani pm kuniuliza kwa undani, jamani kwa kweli nitamkumbuka sana chentutu...babu tengeza fuko la rambirambi, naona na next level pia ana wazo hilo embu fanyeni fasta aisee...nazidi kumuombea marehemu apumzishwe mahala pema peponi
 
...inawezekana ni makosa ya kibinadamu tu, nashauri ui report thread hiyo ili ifanyiwe kazi/marekebisho.
tuwe wastahmilivu katika kipindi hiki kizito kwa misiba ya taifa hao wahanga wa ajali ya meli, na
mwenzetu chetentu.
...mzee mwenzangu asante sana kwa kuniona, marekebisho yamefanyika....tunasubiri michango ya wadau tu hapa!
 
Tumeumbwa kwa udongo na tutarudi kwa udogo.
R.I.P Chetuntu.
 
R.I.P mpiganaji mwenzetu..dada yetu..Mzazi mwenzetu... Mungu ampe nguvu Kijana wake aliyemwacha!
 
RIP dear!! We will miss you! I hate Eclampsia, a disease that kills a lot of women but with no clear/known cause, full of complications and very difficult to prevent
 
Mungu awape faraja ndugu , marafiki na wana jamii wote. Ampumzishe kwa Amani.
 
Mara kadhaa nimekuwa nikitafakari maisha yetu hapa jamvini....
Niliwahi kujiuliza kuwa "hivi hapa jamvini mwenzetu akitutoka inakuwaje??"
Hilo ni swali gumu kumuuliza mtu kwenye nyakati za "heri"...
Mungu anatenda kwa usiri.... leo nimepata jibu!
Thread hii ya "Asprin" imenipata hapa.... saa hii..
Sina namna katika kueleza kinachotokea katika mwili na akili yangu...
Katika namna ambapo tumejitengenezea nafsi mpya katika JAMVI hili...
Tumepata ndugu, marafiki, wachumba, majirani, watu wanaokufurahisha...MAISHA KATIKA JF..
Na uhakika hamna kitu cha hivyo kwenye mtandao wowote wa kijamii.......
Hivi ninavyoandika haya ni ngumu hata kukumbuka kuwa kuna machozi yananitiririka kwenye kibanda hichi cha "internet cafe"
"Chentu".... Tulikupenda.....Bado tunakupenda.... Daima kwenye kumbukumbu zetu hapa JAMVINI na MOYONI
 
dah...yaani dada mzuri hivi amekufa jamani....rest in peace my sister ..we will always miss you
 
RIP...Bwana alitoa, na Bwana ametwaa, jina la Bwana libarikiwe.
 
Pole kwa mwanae,wazazi, ndugu ,jamaa na marafiki. Mungu amevuna shambani mwake. Alazwe pema peponi ameen.
 
Back
Top Bottom