Goodluck Gozbert unaelekea wapi?

Goodluck Gozbert unaelekea wapi?

So yaani MUNGU apewe vibaya na shetani ndo apewe vizuri?...
Yaan MUNGU apewe nyimbo za hovyo, zisizosikika vizuri alafu shetani apewe melody nzuri?
MUNGU ana wivu pia so anahitaji tumwimbie vizuri na tumchezee pia!
Daudi alimchezea MUNGU hadi nguo zikamvuka unajua alicheza kwa viwango gani?
Tusiaminishane kwamba nyimbo mambo mabaya na madhaifu ndo ya MUNGU na mazuri ndo ya shetani
njili Ya Yesu
Fanuel Sedekia

Dunia ya sasa ni ya mabadiliko
Ya sayansi uchumi na utamaduni
ila nina ujumbe kwalo kanisa
injili ya Yesu haibadiliki ×2
Hata kama dunia ya sasa ndiyo hiii
Bado twakuletea injili ile halisi
Ile ya Yesu mwenyewe nao mitume
Uweza wa Mungu uletao wokovu ×2
Injili yake Yesu nao mitume
ilifungua wagonjwa watu nao waliokoka
tena imetuletea tumaini milele
Nasi twakuletea injili hiyohiyo ×2
Hata kama dunia ya sasa ndiyo hiii
bado twakuletea injili ile halisi
ile ya Yesu mwenyewe nao mitume
Uweza wa Mungu uletao wokovu ×3
 
Nyimbo za vitabuni (HYMNS) ndo nyimbo hizi zingine "viewer/listener discretion is advised")
 
Mavazi,staili za KANYAGA na vingine vingi,jamaa kaweka,happy kwakweli kazingua,hiyo video ni ya kidunia sana.
 
Kwenye biblia ambayo ndio standard guideline ya wakristo hakuna sehemu ilipoandikwa nyimbo ya dini iwe na tune gani..

Hata nyimbo ya Rose Muhando ukienda kuipiga Vatcan itainekana kama nyimbo ya club sababu Vatcan wamezoea nyimbo za kilatini za slow slow...
Acha bongo tuburudike kwa tune yetu ya bongo flavor... cha muhimu Mungu atukuzwe tu
 
Huo wimbo hauna maadili ya kidini, hakuna ubunifu wowote kiufupi ameingia Choo cha kike, hyo ni bongo fleva, achague kusuka au kunyoa kama anaimba dini aimbe kama ni bongo fleva aimbe bongo fleva, kipaji chake kipo kwenye dini ila Moyo wake unatamani bongo fleva, na hapa ndo kajionyesha rangi yake halisi , achague kimoja kuunganisha vyote atajipigiza kwenye Jiwe......

Umeongea ya moyoni mwangu, sina la kuongeza. Ubarikiwe sana
 
Wabongo tuache kukariri....ni wapi na lini Biblia ilieleza kuwa nyimbo za gospel lazima ziwe kama mnavyo fikiri?
Yeye kafikisha ujumbe kwa hadhira iliyokusudiwa.... Angeimba kama wengi walivyo kariri , unahisi mimi kijana wa bongo fleva ningeifuatilia?
Waimbaji wengi wa gospel wanaimbia hadhira ya kizazi kilichopita na sio cha sasa ndio maana mziki wa gospel unaonekana kupitwa na wakati na wengi hawana time nao.
Yanapotokea mabadiliko kama haya ni suala jema kwani hakuna ubaya wowote na hajatukana.
 
Angalia uchezaji ule mavazi na hata muundo wa nyimbo ni wakidunia sana

Nyimbo ya dini ila imekamata watu wa dunia kama imma mbasha sharobaro wachungaji wa leo ni matozi wanapiga vitu kwel na wanawake wa kilokole wanavaa mavazi ya kubana na sketi juu ya magoti kanisani na mtaani ndo ujue dunia inaendelea ignore mavazi mana ni nguo tu sikiliza ujumbe ndo muhimu mkuu
 
Back
Top Bottom