Graduates wengi mkiweka aibu na uoga pembeni, basi mtaani mnaishi

Graduates wengi mkiweka aibu na uoga pembeni, basi mtaani mnaishi

Nilikutana na kimbunga cha uchumi kuyumba 2016 mishe zote zikafa. Nikafungua mgahawa mwananyamala biashara ikagoma ,ikabidi nitengeneze toroli ili iwe mobile kitchen.

Nikawa napika chapati ,nilianzia posta pale kituo kinapakana na usalama wa taifa,tra na mamlaka ya bandari. Baishara ilikua nzuri kweli ila usalama wa taifa wakanitimua. Nikahamia na toroli langu kigamboni nako biashara inawa ngumu Sana,kimara,mbezi kote hola.

Nikaamua kubeba toroli langu mkoani mbeya,nimepambana soweto kama miezi 6 hola. Huku nasikia maneno tu huyu amechanganyikia make amesoma ulaya saizi ilitakiwa awe na kazi nzuri tu.

Baada ya mapambano ya muda mrefu gizani sasa jua limewaka. Waliokua wanasema mbovu wanajificha huku wengine wakijisogeza karibu ili waonje keki ya mafanikio. Maisha ya kutafuta hela inatakiwa kujikana nafsi tu ,usione aibu kwani njaa ni yako na familia yako. Unaemuonea aibu ndiye awe mteja wako wa kwanza.
 
Nilikutana na kimbunga cha uchumi kuyumba 2016 mishe zote zikafa. Nikafungua mgahawa mwananyamala biashara ikagoma ,ikabidi nitengeneze toroli ili iwe mobile kitchen.

Nikawa napika chapati ,nilianzia posta pale kituo kinapakana na usalama wa taifa,tra na mamlaka ya bandari. Baishara ilikua nzuri kweli ila usalama wa taifa wakanitimua. Nikahamia na toroli langu kigamboni nako biashara inawa ngumu Sana,kimara,mbezi kote hola.

Nikaamua kubeba toroli langu mkoani mbeya,nimepambana soweto kama miezi 6 hola. Huku nasikia maneno tu huyu amechanganyikia make amesoma ulaya saizi ilitakiwa awe na kazi nzuri tu.

Baada ya mapambano ya muda mrefu gizani sasa jua limewaka. Waliokua wanasema mbovu wanajificha huku wengine wakijisogeza karibu ili waonje keki ya mafanikio. Maisha ya kutafuta hela inatakiwa kujikana nafsi tu ,usione aibu kwani njaa ni yako na familia yako. Unaemuonea aibu ndiye awe mteja wako wa kwanza.
Daaaaah,maisha ya kujiajiri yana changamoto kubwa sana

Waliokuzunguka wana kushangaa kusoma nje na kufanya hizo kazi au wana shangaa kutokana na elimu uliyo nayo?
 
Umeongea ukweli mtupu sana humu. Ni wazi vijana wengi tunaishi kwa matumaini na hii inatokana na jamii tulizolelewa nazo ambazo nyingi zinaamini ukisoma basi mafanikio yatakufuata nyuma, kitu ambacho kwa miaka ya karibuni kimekuwa hakitekelezeki. Ni wakati sasa vijana tusahau kuwa tuliwahi vaa majoho na kuudhuria mihadhara ambayo ilitupa matumaini makubwa juu ya maisha baada ya chuo.

Vijana tunakwama wapi ? Kwa nini tunakosa ubunifu na kila mmoja kutaka auze nguo, mikoba, mashuka na simu ? Je nani atamsupport mwenzake ?
😂😂😂😂😂🤣🤣🤣🤣🤣
 
Yaaan mimi ndo siwezi kujilipua nina maaibu na mauwoga kama yote[emoji16][emoji1787][emoji1787]
Jitahidi anza hata na kimgahawa kisha uendee catering deals. Utasogea mamii!

Yani inatubidi tufanye mambo wanayofanya hata wasioenda shule ili tusogee tu. Chukulia kama wewe ni inferior tu hujawahi zama class. Chukulia corrola kama landcruiser upite kwenye dimwbi hilo hilo la aibu usogee mbele kwenye mafanikio.
 
Nilikuwa na mentality ya kuwa eti nimesoma mpaka level fulani basi nikawa nachagua kazi na kufungua biashara ndogo nikawa naona aibu

Nilichofanya ni kuhama mtaa na kuanza biashara ndogo baadae nimekuja kupata kazi wakati naendelea na biashara ndogo na ikazaa nyingine.

Kikubwa kama mtaa unaoishi wanakujua vizuri inabidi uhame ufanye kazi zako kwa uhuru na jitahidi kufanya mambo yako kisiri usimwambie kila mtu
Ulianzaje mkuu,nipe somo mkuu.
 
Mkuu umesomeka ila kuna kitu kimoja kumbuka kukaa mbali na marafiki so vizuri hawa ndo wanaoweza kukupa connection za kazi. Mfano me siwez mkazia friend ambae nimetoka nae chuo tulikuw wote kwa shida na raha kwamba nikae mbali nae kisa kapata kazi doesn't make sense
Sikuhizi unahitaji bundle tu hata ukiwa Kibondo au Ndungu mradi upate internet connection unawafikia walioko hata marekani.

Sasa connection ipi unayozungumzia kijana au ile ya kukaa bar kunywa bia za bure kila jioni.🤣🤣🤣
 
Nilikuwa na mentality ya kuwa eti nimesoma mpaka level fulani basi nikawa nachagua kazi na kufungua biashara ndogo nikawa naona aibu

Nilichofanya ni kuhama mtaa na kuanza biashara ndogo baadae nimekuja kupata kazi wakati naendelea na biashara ndogo na ikazaa nyingine.

Kikubwa kama mtaa unaoishi wanakujua vizuri inabidi uhame ufanye kazi zako kwa uhuru na jitahidi kufanya mambo yako kisiri usimwambie kila mtu
Hahah sawa kabisa, na hio ndio mbinu ya kijasusi.
 
Aibu na Uoga ni janga kubwa sana. Asikuambie mtu, mtu asikuambia mimi sina mtaji ila ukweli ni Aibu na Uoga.

Kuna Mtumishi mmoja Baba yake na Mkurugenzi wa Jamiiforums aliwahi tuambia mafanikio huanza pale Uoga na Aibu zinapoondoka

Tuna hivi vitu moyoni.

1.Wazazi watanielewa kweli kijana wao mwenye Degree?

2.Hivi Shemeji yangu akisiki itakuwaje?

3.Hivi Mchumba wangu atanielewa kweli kwamba ni mimi niliyekuwa Chuo?

4.Marafiki zangu watanielewa kweli?

5. Majirani vipi?

Combination ya hivyo vyote humfanya mtu aone bora akae tu kisingizio kiwe sina mtaji

Unaondoaje AIBU na UOGA?

1. Jitoe ufahamu kabisa, weka pamba masikioni hapa na pale ambapo inafikia stage wanakuona kama unerukwa na akili ila wewe na Mungu wako ndio mnajua unacho kifanya.

Hii hatua ni ngumu sana kujitoa ufahamu sio mchezo manake inabidi kweli uwe na roho ya Chuma au Roho ngumu sana.

2. Hama nenda mbali na wanako kujua. Kama home ni Korogwe pale na wanakujua ulikuwa Chuo kikuu basi nenda Karatu Arusha anza makazi pale fanya chochote hata kuuza vocha na sigara na karanga.

Hii ni njia nzuri sana manake unakuwa mbali sana na unakuwa kivyako vyako au na mshikaji wako na mnafanya mambo.

3. Usijaribu kumshirikisha mtu yoyote yule hata Wazazi wako kwamba unataka kufanya nini au unafanya nini bali waje kujua wenyewe baadae sana.

Kitendo cha kuwaambia Wazazi au Ndugu na Jamaa na Marafiki kwamba kwa sasa nataka nifungue kibanda cha kuuza Vocha wengi hawatakuelewa na watakukatisha tamaa balaaa.

Hii inachangiwa na imani kwamba Chuo kikuu ni ni levo tofauti.

4. Jitenge na ma-met zako au Marafiki walio na kazi watakutia Uoga zaidi manake ukiwa unawaona wanatokea kazini utaumia zaidi.

5. Washikaji na ndugu na Jamaa wakiwa wanakupigia pigia simu wewe wajibu in short una kibarua unafanya sehemu. Ili kukata mazungumzo manake wakipiga ukaawambia unauza Vocha Dah, hawatakuelewa kabisa kabisa.

Jitahidi kuwakatisha na wajibu in short tu.

MWISHO
Achana na kwamba una Degree hata ikibidi watu wengi waambie hujaenda shule au uliishia tuu Form four.

Ondoa Aibu na Uoga wacha watu wakuone kama umechanganyikiwa, wacha wakuseme, wacha wakucheke, wacha wakukebehi ila mwisho wa siku unajua unacho kifanya.

Kwa sasa Naishia hapa.

MAFANIKIO HUANZA PALE TU AIBU NA UOGA VINAPO TOWEKA
Ila kwa kweli Leo umeahusha nondo itamsaidi sana waha madogo
 
Hii safi
Naungana na mtoa mada kwenye kukimbia mji au mtaa wa nyumbani ili kufanya yako kwa uhuru maana hata mimi imenisaidia hio [emoji23][emoji23][emoji23] watu hawatakiwi kujua unapambanaje na hata mambo ya kuji expose kwenye mitandao ya kikuda unayaweka kando.
 
Back
Top Bottom