Green card lottery ni Umanamba mamboleo

Green card lottery ni Umanamba mamboleo

Wakoloni walitusafirisha kwa majahazi kama watumwa kwenda kwao kuwafanyia kazi bure (manamba) kwenye mashamba, viwanda na majumbani kwao, history mbaya sana hii kukumbukwa, maana sio tu kwenda kuwafanyia kazi wazungu bure lakini wengi wao walikufa njiani wakati wakisafirishwa kwa kutoswa majini, msongamano mkubwa, njaa na ugonjwa njiani.

LEO hii sababu zilezile na manamba ndio hizihizi sa Green card lottery, Jamani hali hii ni mpaka lini? what are you looking for?

Hii ni kujitafutia balaa wewe mwenyewe na familia yako kwa matumaini feki kabisa huku ukijua kuwa utakwenda kule kufanyakazi kubwa na nyingi sana ili upate chochote kitu wakti nguvu, juhudi na akili hizo ungeweza kuziwekeza hapahapa nchini kwako na kupata mafanikio makubwa sana ya ajabu.

Si shauri uombe hiyo nyambafu
Waweza uita utumwa Mambo Leo.
 
Wakoloni walitusafirisha kwa majahazi kama watumwa kwenda kwao kuwafanyia kazi bure (manamba) kwenye mashamba, viwanda na majumbani kwao, history mbaya sana hii kukumbukwa, maana sio tu kwenda kuwafanyia kazi wazungu bure lakini wengi wao walikufa njiani wakati wakisafirishwa kwa kutoswa majini, msongamano mkubwa, njaa na ugonjwa njiani.

LEO hii sababu zilezile na manamba ndio hizihizi sa Green card lottery, Jamani hali hii ni mpaka lini? what are you looking for?

Hii ni kujitafutia balaa wewe mwenyewe na familia yako kwa matumaini feki kabisa huku ukijua kuwa utakwenda kule kufanyakazi kubwa na nyingi sana ili upate chochote kitu wakti nguvu, juhudi na akili hizo ungeweza kuziwekeza hapahapa nchini kwako na kupata mafanikio makubwa sana ya ajabu.

Si shauri uombe hiyo nyambafu
Watz tuna akili dumazi sana. Mi ingekuwa ni uwezo wangu ningewatoa watanzania waende huko mbele angalau mwaka mmoja watz wanatakiwa wapate exposure ni wajinga mno huwez kuendelea bila kutoka ukajifunze mapya.
 
Kavulata: Unajua unachokisema au umekaririshwa? Niko Marekani, sikuja kwa kufungwa mnyororo,na hata nikitaka kuondoka hakuna kamba iliyonifunga.
Ushauri kila siku kwa vijana wa kitanzania, kama unaona opportunities zimebana Tanzania jaribu popote, nina mifano mingi mno, na nimeona kwa watu toka mataifa mbali mbali niliokutana nao US!
Ukiwa na focus, na documents halali na yote unayoyasikia kuhusu Marekani, ni mahali unaweza kufikisha ndoto zako, sisemi ni rahisi, lakini kuna nyenzo ambazo hupati katika nchi nyingi za Kiafrica.
Sijahonga au kumuona yoyote watoto wangu kupata mikopo ya vyuo vyao, sikuwa na connection zozote zile watoto wangu kupata white color jobs! In short mtoto wangu alikuwa recruited akiwa bado chuoni, na leo akiwa na miaka24 is making almost $ 85,000/ Wenzake aliowaacha bongo waliomaliza chuo wanasaka ajira!
Sasa sijui ni utumwa wa aina gani huo!
Ni kweli Marekani/ Canada zinataka nguvu kazi, lakini ukiingia huku ni juhudi zako na akili yako! Wengine wataenda juu, na wengine chini, sawasawa na wazawa! Anayenifyekea majani nyumbani kwangu ni mzungu! Maana sina muda! Na kila baada ya wiki mbili au tatu ananipigia simu kama yameota aje kufyeka! Na ameniambia ni fundi katika serikali yetu ya mtaa anatafuta pesa ya ziada! Hii ndio Marekani, simdharau najua anachotafuta!
Hivyo usikaririshwe na akina Lumumba.
Hulazimishwi ni akili yako tu! Wengine wanatumia hapo bongo wanatoka! Wengine mambo yanakataa! Maisha popote pale!
Infact always I have an American dream.

There is no success like American success.

Nimejipanga nijaribu bahati yangu mwakani nicheze lottery ya Green Card natafuta nyezo tu muhimu mwakani must be.

Nina kazi but I ain't satisfied with my current position. And if kama nitaaendelea kubaki hapa I will die poor all red lights nimeshaziona.

So am seeking new challenges and new environment.

U never know may be something good will happen there.
 
Kwenye akili yako wewe unadhani kule Marekani hakuna watu maskini, ombaomba, unadhani kuwa hakuna watoto wanaokaa chini darasani, hakuna wamachinga, hakuna malaya, hakuna wadokozi hakuna wanaume wanaoshikishwa ukuta wapate chochote, wanaodeki na kuosha mbwa. Akili na mawazo kama hayo ndiyo yanayowafanya watu wapande boti wafie kwenye maji na wewe umdharau huyo mama. Toka huko kaka, tembea uone.
Ushaambiwa kwa nyenzo za kukufanya ufanikiwe marekani ni rahisi zaidi tofauti na Africa kama kweli unataka kutusua na akili ya maisha unayo.

Africa tabu tubu sera mbovu, serikali zisizo na vipaumbele, wanasiasa njaa kujaza matumbo yao, uvunjifu wa katiba waziwazi, vyombo corrupt vya USALAMA , husda, wivu , vijino pembe vya watu weusi wenzetu, uchawi na ushirikina uliopitiliza kwenye mambo ya maendeleo, afya, biashara nakadhalika.

America the land of opportunities, the land of free and brave. GOD BLESS AMERICA.

Haters gonna hate[emoji1787]
 
Aliye ibiwa na aliye iba nani zuzu?
Nyie ndio mazuzu mnao ibiwa mnabaki mkilalamika tu!

Acha waendelee kuiba tena ikibidi waibe hata mkeo!
IQ yako ni ndogo sana, Ukraine imenyang'anywa na Urusi mikoa 4, kwahiyo unataka kusema Ukraine ni mazuzu?

DR Congo wanaporwa mali zao kwa mtutu wa bunduki na wazungu kwa mgongo wa Rwanda na Uganda. Msumbiji wanataka kunyang'anywa gesi yao, Sudan Kusini wamenyang'anywa mafuta yao na wazungu kwa mgongo wa vita ya wenyewe kwa wenyewe wanaopatiwa silaha na wazungu. Nani kakwambia kuwa M23 wana uwezo wa kupigana na serikali DRC?
 
Ushaambiwa kwa nyenzo za kukufanya ufanikiwe marekani ni rahisi zaidi tofauti na Africa kama kweli unataka kutusua na akili ya maisha unayo.

Africa tabu tubu sera mbovu, serikali zisizo na vipaumbele, wanasiasa njaa kujaza matumbo yao, uvunjifu wa katiba waziwazi, vyombo corrupt vya USALAMA , husda, wivu , vijino pembe vya watu weusi wenzetu, uchawi na ushirikina uliopitiliza kwenye mambo ya maendeleo, afya, biashara nakadhalika.

America the land of opportunities, the land of free and brave. GOD BLESS AMERICA.

Haters gonna hate[emoji1787]
Unachosema wewe ni sawa na house girl ambae anafanyakazi kwa boss wake kuanzia alfajiri na kulala saa 5 usiku baada ya kumalizia kumfungulia na kumlisha mbwa kutoka bandani kwa ujira wa TZS 60,000 kwa mwezi. Lakini msichana huyu alipokuwa kwao alikuwa anaamka saa 2 asubuhi, kuzurura, kuangalia TV na kwenda kulala saa 2 usiku.

Nguvu, juhudi na muda anaotumia kufanyakazi kwa boss kama angetumia nusu tu ya nguvu,juhudi na muda kufanyakazi akiwa nyumbani kwao hata kwa kuchoma vitumbua na maandazi na kuyauza angepata pesa nyingi zaidi hukohuko kwao kuliko hizi 60,000 za boss.

Fursa ziko hapahapa nyumbani Tz ni kuacha uvivu. Nilimkuta kijana mmoja Marekani anaona aibu kurudi Tz kwakuwa wenzake aliowaacha TZ walikuwa na maendeleo makubwa sana kuliko yeye. Wenzake wameoa, wana mashamba ya miti Iringa, wamejenga kule Goba, shamba kubwa la kuku, wana magari na ardhi kubwakubwa tu. Visa yake na passport vimekwisha lakini anashindwa kurudi kurudi kwa kuogopa kuwa atadakwa kwa makosa hayo pia.

Hebu waambieni ukweli vijana wenu.
 
Ushaambiwa kwa nyenzo za kukufanya ufanikiwe marekani ni rahisi zaidi tofauti na Africa kama kweli unataka kutusua na akili ya maisha unayo.

Africa tabu tubu sera mbovu, serikali zisizo na vipaumbele, wanasiasa njaa kujaza matumbo yao, uvunjifu wa katiba waziwazi, vyombo corrupt vya USALAMA , husda, wivu , vijino pembe vya watu weusi wenzetu, uchawi na ushirikina uliopitiliza kwenye mambo ya maendeleo, afya, biashara nakadhalika.

America the land of opportunities, the land of free and brave. GOD BLESS AMERICA.

Haters gonna hate[emoji1787]
Nchi ambayo hata wanaume wanaolewa, ndio hizo fursa unazozisema? Nenda ukaangalie kule kwenye magereza yao ukaone ni akina nani wamefungwa humo?
 
Daah! umenena, nini nafahamu kuwa furahi ya mtu haitokani na kuwa na pesa nyingi tu bali mjumuiko wa mambo mengi na hela ikiwemo. Nimekutana na kijana ambae huko majuu ambae analala kwenye gari yake maisha, nilipomuuliza kwanini kwanini huna chumba chako aliniambia ninafanya kazi shift 3 kwa siku hivyo muda wa kulala sina, hata hiyo nyumba naona nitapoteza pesa zangu bure wakati silali humo. Akanambia ana madeni mengi yanayohitaji ku service (kulipa) hivyo lazima afanye kazi zaidi ya 1 ili apate ziada. kaka kijana huyu hajawahi kula chakula cha nyumbani kwake zaidi ya kule fast foods mitaani, makato mengi na anashindwa kutuma pesa nyumbani maana wafyeka hela nyingi sana. kaka kuna mitaa/maduka/malls ukiingia mwenye ngozi nyeusi wanadhani huna pesa ya kuingia hapo bali unataka kuiba, ubaguzi bado haujakwisha tunalazimisha tu.

Nguvu, muda, juhudi, maarifa na akili mnazozitumia kumudu kuishi huko hata zingewekezwa japo nusu tu kwenye jangwa zingetoa matunda. Vijana wetu huku ni wavivu sana ni wavivu sana na ni wavivu sana ndio maana wanapata tamaa ya green card wakidhani huko US pesa ziko kwenye viroba tu ni za kuzoa na kutumia.

Kama asili na chanzo kikuu cha ushoga huko ni maisha magumu, watu wanaunganisha nguvu ili kumudu maisha bila kulazimika kuwa na watoto wa kutunza, yaani kuona mwanamke ni kuongeza ugumu kwenye ugumu. bahati mbaya mimi nimeishi huko sana tena vijijini kabisa ambako maisha ni kama haya hapa ya tandika na kwamtogole, kuchafu na idadi kubwa ya ombaomba wazungu mitaani ambao wanapatiwa nguo kule salvation army na kwingineko kwenye malls kama vile Walmart zenye madirisha ya watu maskini (wazungu) kupatiwa misaada.

kaka usiwadanganye watu ukawapa hope na kuja kuishia kuolewa na wanaume wenzao, wanaofanikiwa ni watu kidogo sana kati ya hao wahamianji. Wengi wao wanaishia kwenye vyombo vya usalama kufungwa na
 
Ndugu yangu Kapulata, naogopa sana generalization au sweeping statements! Ambazo hata Marekani kwa Wamarekani ambao hawajatoka nje! ukikutana nao na mtu anakuuliza nasikia huko kwenu Albino wanachinjwa hovyo hovyo! au Bado kuna kuna baadhi ya Wamarekani huku wanaamini bado tunaishi kwenye miti!

Nashangaa mtu kama wewe ambaye una smart phone, una uwezo kupata information nyingi, credible from different sources ukaandika hivyo!

Nashindwa nianzie wapi kukujibu, na wala sijui uwewahi kutoka nje ya Tanzania au la! Lakini hiyo sio hoja!
Mara nyingi ukifuatuilizia mada zangu sina Ushauri kabisa mtu aje Marekani kama kama ana opportunities au anaona kila anachokipata anaweza kukipata nyumbani ( lakini kila mtu katika maisha anajua ni hasa anataka maishani mwake) .

Nawafahamu watu ambao walikuwa wanafanya BOT wakaja kusoma huku Finance, Information technology etc, wakaamua kubaki, unadhani ni wanafanya kazi unazozisema wewe? Najua hata watu kama hao wanaofanya Silicon Valley, kwa hiyo ungekaa kimya kama hujui!

Marekani inataka Kibali halali cha kufanya kazi, inataka upate elimu ya hapa, inataka nidhani ya maisha, KAMWE hutafanya kazi tatu kwa ku survive labda uwe na malengo fulani ya kutaka fedha za ziada!
Naandika nachokifafamu! Na bado nashauri kwa kijana wa Kitanzania, kama unaona mlango wa unachokitaka Tanzani umefungwa, jaribu Marekani, ingia KIHALALI Unaweza kupata unachotafuta, sana kielimu hata mjaji wa kuwekeza nyumbani. na kuwapatia watoto maisha bora!

Sina kabisa ushauri kwa mtu ambaye anataka kuja Marekani kuishi vila vibali halali!

Sikukatazi kabisa jamaa yangu kuwa na mtazamo wako! Nimeona wengi Watanzania wenye elimu, nidhamu ya maisha, vibali halali vya kuwa Marekani wakifanikiwa!
 
Ndugu yangu Kapulata, naogopa sana generalization au sweeping statements! Ambazo hata Marekani kwa Wamarekani ambao hawajatoka nje! ukikutana nao na mtu anakuuliza nasikia huko kwenu Albino wanachinjwa hovyo hovyo! au Bado kuna kuna baadhi ya Wamarekani huku wanaamini bado tunaishi kwenye miti!

Nashangaa mtu kama wewe ambaye una smart phone, una uwezo kupata information nyingi, credible from different sources ukaandika hivyo!

Nashindwa nianzie wapi kukujibu, na wala sijui uwewahi kutoka nje ya Tanzania au la! Lakini hiyo sio hoja!
Mara nyingi ukifuatuilizia mada zangu sina Ushauri kabisa mtu aje Marekani kama kama ana opportunities au anaona kila anachokipata anaweza kukipata nyumbani ( lakini kila mtu katika maisha anajua ni hasa anataka maishani mwake) .

Nawafahamu watu ambao walikuwa wanafanya BOT wakaja kusoma huku Finance, Information technology etc, wakaamua kubaki, unadhani ni wanafanya kazi unazozisema wewe? Najua hata watu kama hao wanaofanya Silicon Valley, kwa hiyo ungekaa kimya kama hujui!

Marekani inataka Kibali halali cha kufanya kazi, inataka upate elimu ya hapa, inataka nidhani ya maisha, KAMWE hutafanya kazi tatu kwa ku survive labda uwe na malengo fulani ya kutaka fedha za ziada!
Naandika nachokifafamu! Na bado nashauri kwa kijana wa Kitanzania, kama unaona mlango wa unachokitaka Tanzani umefungwa, jaribu Marekani, ingia KIHALALI Unaweza kupata unachotafuta, sana kielimu hata mjaji wa kuwekeza nyumbani. na kuwapatia watoto maisha bora!

Sina kabisa ushauri kwa mtu ambaye anataka kuja Marekani kuishi vila vibali halali!

Sikukatazi kabisa jamaa yangu kuwa na mtazamo wako! Nimeona wengi Watanzania wenye elimu, nidhamu ya maisha, vibali halali vya kuwa Marekani wakifanikiwa!
Unapoonhelea maisha ya Marekani unaongelea kufanya kazi kufa na kupona la sivyo uta perish. Hata tz ukifanyakazi zako vizuri ambazo sio za kuajiliwa lazima utatoka kimaisha. Kila kitu kipo Huku, Mimi binafsi nasikia vizuri sana kama nikiwa sehemu ya watu wanaowahudumia watanzania wenzangu. Sipendi kuishi kwa hofu na kubaguliwa.
 
wewe unafikiri kwanini huko marekani mtoto anaweza kuingia darasani na bunduki na kuua kila mtu humo? unafikiri hawana akili? hujiulizi mara mbilimbili? Upweke (loneliness) na stresses zimejaa huko. Wewe hujiulizi hata akina Kelly wako jela na wana mihela mingi? sio hela tu bali fikiria na mambo mengine kaka.
Kavulata, nadhani kidogo umesema , tunaangalia mambo mengi tunapotaka nje ya nchi, wewe huangalii mambo mengi kama unavyoonyesha, nikiangalia kwa mtazamo wako huo Afrika hapakaliki pia! Sina haja ya kusema wewe unajua wazi!
Napoangalia shule za msingi, madarasa ya vijijni. kukosa maji. umeme, huduma za afya, ukosefu wa ajiri ambao unaleta burden ya extended family, kwani kila anayejaribu kujikwamua kwenda juu, unaanza kazi ukoo mzima kukuvuta chini, kibinadamu unahitajika kutoa msaada, wewe mwenyewe unataka kusonga mbele, ni tatizo linalomkabili kila mwafrika, lakini bado watu wanaishi.

Kwa kifupi adha za maendeleo na kero zake zipo, lakini faida yake ni kubwa kuliko adha za umaskini, na watu wanaishi! Niko Marekani sioni tabu kabisa na hiyo unayosema loneliness! Siwajui majirani zangu, na wao hawanijui, tunapungiana mikono tunapokutana nje tukiingia kwenye magari yetu kila mtu akienda kwenye shughuli yake! Kuna sehemu nyingi mno Marekani za kuondoa hiyo unaita loneliness! Kuna community functions ukitaka! Unapenda kusoma, library ziko kila kona za bure utapata kitabu unachotaka, CDs za Movies za kuazima kwa kadri yako, Gyms, parks za kutembea na kupumzika nk!

Hivyo Mkuu tunapokuja huku tunafikiri mambo mengi pia! Kama na mimi nikitaka kurudi Tanzania inabidi niangalia mambo mengi pia! Mgao wa umeme/Maji, unreliable internet, siwezi kutaka kitu Amazon nikakipata kwa siku mbili! Na ningekuwa na watoto wadogo ningehangaika kuhusu elimu yao! Marekani hilo halina shina kabisa! Kusaidia ndugu zangu, ambao karibu kila Mtanzania ana msururu mrefu wa kusaidia! Dola zangu 400- 500 nazotuma Tanzania kusadia ndugu zangu kwa mwezi, ingekuwa ni ngumu mno kuwasaidia nikiwa bongo! labda ningekuwa Waziri!

Hivyo naomba uwe na broader perspective ya kuangalia mambo! Halafu inanisikitisha mno kuona mtu wa leo unataka kuua spirit ya adventure kwa wale ambao wanataka kujaribu! ! Nawaheshimu wazungu kwa hilo, wanatoka, wanatembea, wanajaribu, ni risk takers! Wengi wetu hata hapo Tanzania ni mikoa michache umefika, tena kikazi, sio kutembea, kuona maisha mbali mbali.

Kwa kifupi sikuja Marekani nikitokea bongo! Nimekatisha West Africa, Far East na nikatua Marekani! Bado nataka kutembea na kuona! Is part of my DNA!

Waacha wanaotaka kujaribu wajaribu! Usiwe mwoga! Maisha ni popote pale, hata bongo kwa upande wako!
 
Unapoonhelea maisha ya Marekani unaongelea kufanya kazi kufa na kupona la sivyo uta perish. Hata tz ukifanyakazi zako vizuri ambazo sio za kuajiliwa lazima utatoka kimaisha. Kila kitu kipo Huku, Mimi binafsi nasikia vizuri sana kama nikiwa sehemu ya watu wanaowahudumia watanzania wenzangu. Sipendi kuishi kwa hofu na kubaguliwa.
Nimeishi Marekani kama miaka kumi sasa, sijawahi kubaguliwa kazini, barabarani au kupata huduma! Watoto wangu walianza kwenda private shule zenye 98% Wazungu, baadaye Public School, kisha Universities, hawajawahi kabisa kabisa kulalamika ubaguzi!

Kijana wangu mmoja yuko kwenye Financial institution kubwa tu, hajawahi kunilalamikia ubaguzi! Mtaani kwangu wote ni wazungu na Mkenya mmoja! Gari zangu hazijapigwa mawe, au takataka kutupwa kwenye yard yangu!
Nimekamatwa kwa makosa halali ya barabarani na askari wa kizungu, si mara moja au mbili, nilipata ticket, nililipa mambo yakaisha!

Angalia sana media, hata za Marekani zina agenda! hiyo ndio experience yangu!

Na unaposema kufanya kazi kufa na kupona maana nini! Una promote uvivu? Hebu fikiria Tanzania kungefanya kazi kufa na kupona tungekuwa wapi!
Nadhani ufahamu wako wa Marekani ni finyu! Marekani kuna kazi mbali mbali! Kama unafanya kazi let say bank, mwalimu nk si kuna masaa mkuu! Saa za kufanya kazi Marekani zinajulikana! Hivyo inategemea aina ya kazi mkuu! Una a lot of generalization!
Tembelea basi ili uwe na uelewa wa Marekani.

Sijakwambia Tanzania hutatoka kimaisha! Na kutoka kimaisha maana yake nini? Kila mtu ana definition yake! Kama kutoka kimaisha ni kuwa nyumba na gari, basi niliingia Marekani nikiwa nimetoka kimaisha kwa mtazamo wa wengi! Maana sikua na nyumba na gari moja tu! Nilikuwa na miradi pia! Lakini kwangu mimi bado nilikuwa natafuta maisha mengine kwa ajili yangu na watoto wangu!

Panua definition yako ya kutoka kimaisha ndugu yangu!
 
Watz tuna akili dumazi sana. Mi ingekuwa ni uwezo wangu ningewatoa watanzania waende huko mbele angalau mwaka mmoja watz wanatakiwa wapate exposure ni wajinga mno huwez kuendelea bila kutoka ukajifunze mapya.
Kichwani ni fikra za kitumwa, unafikiria kuwa wazungu walianza kwa magorofa marefu kama ya pale Chicago, Hebu niambie namna ushoga ulivyoanza hapo. Niambie ni watu wangapi wanashindwa kwenda gym kwa kukosa fedha
Nimeishi Marekani kama miaka kumi sasa, sijawahi kubaguliwa kazini, barabarani au kupata huduma! Watoto wangu walianza kwenda private shule zenye 98% Wazungu, baadaye Public School, kisha Universities, hawajawahi kabisa kabisa kulalamika ubaguzi!

Kijana wangu mmoja yuko kwenye Financial institution kubwa tu, hajawahi kunilalamikia ubaguzi! Mtaani kwangu wote ni wazungu na Mkenya mmoja! Gari zangu hazijapigwa mawe, au takataka kutupwa kwenye yard yangu!
Nimekamatwa kwa makosa halali ya barabarani na askari wa kizungu, si mara moja au mbili, nilipata ticket, nililipa mambo yakaisha!

Angalia sana media, hata za Marekani zina agenda! hiyo ndio experience yangu!

Na unaposema kufanya kazi kufa na kupona maana nini! Una promote uvivu? Hebu fikiria Tanzania kungefanya kazi kufa na kupona tungekuwa wapi!
Nadhani ufahamu wako wa Marekani ni finyu! Marekani kuna kazi mbali mbali! Kama unafanya kazi let say bank, mwalimu nk si kuna masaa mkuu! Saa za kufanya kazi Marekani zinajulikana! Hivyo inategemea aina ya kazi mkuu! Una a lot of generalization!
Tembelea basi ili uwe na uelewa wa Marekani.

Sijakwambia Tanzania hutatoka kimaisha! Na kutoka kimaisha maana yake nini? Kila mtu ana definition yake! Kama kutoka kimaisha ni kuwa nyumba na gari, basi niliingia Marekani nikiwa nimetoka kimaisha kwa mtazamo wa wengi! Maana sikua na nyumba na gari moja tu! Nilikuwa na miradi pia! Lakini kwangu mimi bado nilikuwa natafuta maisha mengine kwa ajili yangu na watoto wangu!

Panua definition yako ya kutoka kimaisha ndugu yangu!
Nina wasiwasi wewe nilishakuona pale Detroit kwenye majumba ya bei rahisi yaliyohamwa baada ya viwanda kufa na vingine kuhamishiwa Asia na wazungu wengi kukimbia. Mji mchafu na wenye vibaka wengi kama kwamtogole. Kaka acha kuwaamisha vijana kwamba Marekani hakuna maskini, hakuna wanaoshindwa kumsomesha mtoto wake, hakuna anashindwa gharama za matibabu, hakuna ombaomba, hakuna wanaolala kwenye magari yao au night club kwa kukosa nyumba, hakuna Malaya wa kutupwa wanaojiiza. Kaka unaharibu kuchora picha kubwa sana na mbao iliyopakwa dhahabu nje. Sio kweli vijana bakini nyumbani. Marekani ni kuzuri kwa kusoma TU na kurudi nyumbani kwakuwa Kuna shule nyingi zenye walimu wazuri.
 
Kichwani ni fikra za kitumwa, unafikiria kuwa wazungu walianza kwa magorofa marefu kama ya pale Chicago, Hebu niambie namna ushoga ulivyoanza hapo. Niambie ni watu wangapi wanashindwa kwenda gym kwa kukosa fedha

Nina wasiwasi wewe nilishakuona pale Detroit kwenye majumba ya bei rahisi yaliyohamwa baada ya viwanda kufa na vingine kuhamishiwa Asia na wazungu wengi kukimbia. Mji mchafu na wenye vibaka wengi kama kwamtogole. Kaka acha kuwaamisha vijana kwamba Marekani hakuna maskini, hakuna wanaoshindwa kumsomesha mtoto wake, hakuna anashindwa gharama za matibabu, hakuna ombaomba, hakuna wanaolala kwenye magari yao au night club kwa kukosa nyumba, hakuna Malaya wa kutupwa wanaojiiza. Kaka unaharibu kuchora picha kubwa sana na mbao iliyopakwa dhahabu nje. Sio kweli vijana bakini nyumbani. Marekani ni kuzuri kwa kusoma TU na kurudi nyumbani kwakuwa Kuna shule nyingi zenye walimu wazuri.
Mkuu sasa naona ni ubishi wa kitoto, na sioni hata chembe ya kuhabarishana, naishi Texas, siku ukipata nafasi karibu, nimekupa experience yangu! Nimetembelewa na ndugu zangu na marafiki zangu, sio mara moja wala mbili,wako wanaotaka kurudi,lakini kila leo nawaambia Marekani inataka legal papers, focus na determination! Kwaheri mkuu.
 
Mkuu sasa naona ni ubishi wa kitoto, na sioni hata chembe ya kuhabarishana, naishi Texas, siku ukipata nafasi karibu, nimekupa experience yangu! Nimetembelewa na ndugu zangu na marafiki zangu, sio mara moja wala mbili,wako wanaotaka kurudi,lakini kila leo nawaambia Marekani inataka legal papers, focus na determination! Kwaheri mkuu.
Labda kwa kuongezea, inaonekana labda umeishi Marekani, maana unazungumzia Detroit na Chicago na experience za malaya, kwa kufupi tu ukiingia ulimwengu huo, uwe Tanzania au popote hutoka, na Marekani panapohitaji kujitambua utakuwa umejimaliza mwenyewe.
Kama Marekani ilikukataa,maana umekiri ina elimu nzuri! Inawezekana hukumaliza kwa kukosa karatasi na ukarudi Tanzania, this is just my assumption,pole sana!, nawafahamu watu wengi wa namna hiyo, walichokosa Marekani kimewafanya kuwa bitter and negative, ni maisha mkuu, nawajua baadhi walikuja Marekani with optimism, wakokosa karatasi, watoto wao waka kosa elimu na kurudi Tanzania frustrated, kama haikua ridhiki kwako, kwa wengine imekuwa,hata hapo Tanzania wako wanaokosa na kupata! Kama una imani ya dini niseme ni mipango ya Mwenyezi Mungu, ndio mtoa ridhiki mkuu!
Kwaheri, karibu Texas!
 
Kavulata: Unajua unachokisema au umekaririshwa? Niko Marekani, sikuja kwa kufungwa mnyororo,na hata nikitaka kuondoka hakuna kamba iliyonifunga.
Ushauri kila siku kwa vijana wa kitanzania, kama unaona opportunities zimebana Tanzania jaribu popote, nina mifano mingi mno, na nimeona kwa watu toka mataifa mbali mbali niliokutana nao US!
Ukiwa na focus, na documents halali na yote unayoyasikia kuhusu Marekani, ni mahali unaweza kufikisha ndoto zako, sisemi ni rahisi, lakini kuna nyenzo ambazo hupati katika nchi nyingi za Kiafrica.
Sijahonga au kumuona yoyote watoto wangu kupata mikopo ya vyuo vyao, sikuwa na connection zozote zile watoto wangu kupata white color jobs! In short mtoto wangu alikuwa recruited akiwa bado chuoni, na leo akiwa na miaka24 is making almost $ 85,000/ Wenzake aliowaacha bongo waliomaliza chuo wanasaka ajira!
Sasa sijui ni utumwa wa aina gani huo!
Ni kweli Marekani/ Canada zinataka nguvu kazi, lakini ukiingia huku ni juhudi zako na akili yako! Wengine wataenda juu, na wengine chini, sawasawa na wazawa! Anayenifyekea majani nyumbani kwangu ni mzungu! Maana sina muda! Na kila baada ya wiki mbili au tatu ananipigia simu kama yameota aje kufyeka! Na ameniambia ni fundi katika serikali yetu ya mtaa anatafuta pesa ya ziada! Hii ndio Marekani, simdharau najua anachotafuta!
Hivyo usikaririshwe na akina Lumumba.
Hulazimishwi ni akili yako tu! Wengine wanatumia hapo bongo wanatoka! Wengine mambo yanakataa! Maisha popote pale!
mkuu samahani ivi kwa ambao awana elimu kipengele cha uzoefu wa kazi miaka 2. ni kazi gani haswa?
 
Mkuu sasa naona ni ubishi wa kitoto, na sioni hata chembe ya kuhabarishana, naishi Texas, siku ukipata nafasi karibu, nimekupa experience yangu! Nimetembelewa na ndugu zangu na marafiki zangu, sio mara moja wala mbili,wako wanaotaka kurudi,lakini kila leo nawaambia Marekani inataka legal papers, focus na determination! Kwaheri mkuu.
Fafanua kuhusu legal papers na zinapatikanaje tujifunzee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom