Green card lottery ni Umanamba mamboleo

Green card lottery ni Umanamba mamboleo

Wakoloni walitusafirisha kwa majahazi kama watumwa kwenda kwao kuwafanyia kazi bure (manamba) kwenye mashamba, viwanda na majumbani kwao, history mbaya sana hii kukumbukwa, maana sio tu kwenda kuwafanyia kazi wazungu bure lakini wengi wao walikufa njiani wakati wakisafirishwa kwa kutoswa majini, msongamano mkubwa, njaa na ugonjwa njiani.

LEO hii miaka 60 baada ya uhuru sababu zilezile za kusafirisha manamba kwenda Marekani, Ulaya na uarabuni ndio sababu hizihizi za watu kwenda huko kwa Green card lottery, Jamani hali hii ni mpaka lini? what are you looking for? Kilichobadilika tu leo ni kitu kimoja tu kutoka manamba walionunuliwa kwenye masoko ya watumwa hadi kwenda kwa green card na baadhi ya sifa za watu wanaohitajika kusafirishwa na aina ya usafiri. Wakati ule walihitaji watu vijana wenye nguvu za kufanya kazi za wakati ule na sasa hivi kwa kutumia green card wanahitaji watu vijana wenye afya wenye elimu na ujuzi maalum kwaajili ya kufanya kazi za wakati huu.

Hii ni kujitafutia balaa wewe mwenyewe na familia yako kwa matumaini feki kabisa huku ukijua kuwa utakwenda kule kufanyakazi kubwa na nyingi sana ili upate chochote kitu wakati nguvu, juhudi na akili hizo ungeweza hata kuziwekeza hapahapa nchini kwako na kupata mafanikio makubwa sana ya ajabu pamoja na kutoa mchango kwenye ujenzi wa taifa lako kwa njia za kodi, tozo na huduma kwa jamii yako.

Jaamaani, Si shauri uombe hiyo kitu, nyambafu!!!!
Nadhani hata suala la kutafuta maisha nchi za nje nalo limepitwa na wakati. Teknolojia imewezesha kupata vitu vingi sana by proxy
 
Kavulata,

Najua mimi na wewe tulikubaliana kutokubaliana katika mada hiii.....lakini mkuu statistics hazidanganyi.....Unajua mwaka uliopita Walioomba Green Card walikuwa wangapi? Hasa kutoka Africa na nchi nyingine za Ulimwengu! Tanzania tu idadi ya wanaoomba Greencard kuja Marekani inaongezeka kila kukicha! Na maendeleo yote yanayozungumzwa nchi za kiafrica.....
a na vibali halali vya kuwa US.
Elimu yetu tuliyopewa haitoshi. Tumefundishwa kulikimbia tatizo badala ya kulitatua tatizo kwenye mazingira yetu. Kama tatizo ni uongozi haufai wewe utachangiaje katika kutatua changamoto ya uongozi nchini kwako? Kama shida ni neo colonialism wewe ulifanya nini kama kijana. Vijana wetu ukiwemo ww mnaona suluhisho ni kukimbilia kule ambako vijana wenzenu wa mataifa hayo walipambana na mifumo Yao kwa jasho na damu zao kurekebisha mambo.

Vijana kama Ibrahim Traore kule Burkina Faso wanatafuta majibu ya shida zao wakati you cowards majisalimisha kwa watesi wetu kuwa manamba (cheaper labors) kuyajenga mataifa Yao. Narudia tena elimu yetu inawafanya vijana wetu iwe rahisi hata ikibidi kuf*rwa (short cut) ili kutoboa.
 
Kavulata,

Naona mada imerudi sana, hebu angalia hizo Statistics tena........Labda in Summary tu, hizi nchi " Algeria, Egypt, Uzbekistan, Iran and Russia have the highest numbers of selectees for the DV-2023 Program..........Hawa ndio wameongoza kuleta manamba USA.....
Angalia Jedwali..."

EUROPE
ALBANIA 2,001GREECE 28NORTHERN IRELAND 4
ARMENIA 3,525HUNGARY 66NORWAY 4
AUSTRIA 34ICELAND 4POLAND 228
AZERBAIJAN 1,260IRELAND 13PORTUGAL 10
BELARUS 1,535ITALY 154 Macau 7
BELGIUM 32KAZAKHSTAN 1,908ROMANIA 228
BOSNIA AND HERZEGOVINA 47KOSOVO 413RUSSIA 5,505
BULGARIA 161KYRGYZSTAN 2,846SERBIA 134
CROATIA 12LATVIA 48SLOVAKIA 20
CYPRUS 8LITHUANIA 91SLOVENIA 2
CZECH REPUBLIC 19MALTA 8SPAIN 96
DENMARK 12MOLDOVA 670SWEDEN 26
Faroe Islands 1MONTENEGRO 28SWITZERLAND 27
ESTONIA 17NETHERLANDS 19TAJIKISTAN 2,485
FINLAND 14 Aruba 4TURKEY 3,383
FRANCE 209 Curacao 1TURKMENISTAN 555
GEORGIA 2,071 Sint Maarten 3UKRAINE 3,808
GERMANY 512NORTH MACEDONIA 258UZBEKISTAN 5,511
Kwenye jedwali hawa jamaa wapiga mabomu toka kote wanataka kwenda huko wakaimbe habeeb na wanazaa km mchwa.
Ngoja tunywe supu nyama ziko chini
 

DV 2023 Latest Statistics​

Trodvies 5 months ago 10

Latest Statistics​

Latest statistics for the DV 2023 Program indicates that up to last weekend, with a total of 9,619 cases interviewed, 14,956 applicants had been issued visas. In addition, there are 8,224 cases – totaling 17,924 applicants – at various embassies awaiting interview.
According to the latest statistics, the Europe region remains on top of visa issuances with a total of 6,340 so far; followed by the Africa region with 5,307. Asia is in third place with 2,336.

Sasa ndugu yangu Kavulata....hao wanaotoka Europe region kuja US utasemaje? Kila mtu anajua ni nini hasa anachotafuta US....!
Nipe statistics za Waafrika ambao walipelekwa Marekani kama watumwa kutoka west Africa kupitia the Atlantic ocean. Watumwa wanahitajika hadi Leo ila tofauti ni namna wanavyowapata.
 
Nipe statistics za Waafrika ambao walipelekwa Marekani kama watumwa kutoka west Africa kupitia the Atlantic ocean. Watumwa wanahitajika hadi Leo ila tofauti ni namna wanavyowapata.

According to Statistics nazokupa...Warusi ndio wanaongoza kuingia kama Manamba.....!Au Huangalii...
 
According to Statistics nazokupa...Warusi ndio wanaongoza kuingia kama Manamba.....!Au Huangalii...

Na kinachochekesha si Waafrica tu......Tanzania ni 165 tu......Urusi ni 5,505 2023........Nakumbuka Mwaka juzi fundi wa simu aliyekuja ku fix Modem yangu toka kampuni ya simu alikuwa Mrussia......
 
Elimu yetu tuliyopewa haitoshi. Tumefundishwa kulikimbia tatizo badala ya kulitatua tatizo kwenye mazingira yetu. Kama tatizo ni uongozi haufai wewe utachangiaje katika kutatua changamoto ya uongozi nchini kwako? Kama shida ni neo colonialism wewe ulifanya nini kama kijana. Vijana wetu ukiwemo ww mnaona suluhisho ni kukimbilia kule ambako vijana wenzenu wa mataifa hayo walipambana na mifumo Yao kwa jasho na damu zao kurekebisha mambo.

Vijana kama Ibrahim Traore kule Burkina Faso wanatafuta majibu ya shida zao wakati you cowards majisalimisha kwa watesi wetu kuwa manamba (cheaper labors) kuyajenga mataifa Yao. Narudia tena elimu yetu inawafanya vijana wetu iwe rahisi hata ikibidi kuf*rwa (short cut) ili kutoboa.

Upo Africa wewe......nipe Idadi ya Mapinduzi ambayo imeleta matokea chanya Africa...maybe 2%......Je mpaka leo changamoto ngapi zimetatulia.....Kuchimbiwa vyoo....Vyandalua kujikinga na Malaria.......Au Hujui Bajeti zetu zinategemea kiasi gani kutoka Nje.......Sijui uko upande upi wa Bandari....Wengine wanasema imeuzwa.....Wengine wanasema tunawapa Dubai kuzuia wezi....Kwe;i tunajua kupambana na changamoto....!
 
Upo Africa wewe......nipe Idadi ya Mapinduzi ambayo imeleta matokea chanya Africa...maybe 2%......Je mpaka leo changamoto ngapi zimetatulia.....Kuchimbiwa vyoo....Vyandalua kujikinga na Malaria.......Au Hujui Bajeti zetu zinategemea kiasi gani kutoka Nje.......Sijui uko upande upi wa Bandari....Wengine wanasema imeuzwa.....Wengine wanasema tunawapa Dubai kuzuia wezi....Kwe;i tunajua kupambana na changamoto....!

Kavulata......unasema " Elimu yetu tuliyopewa haitoshi" Hiyo mitala ya elimu inatengenezwa na nani......Si na watu kama wewe....Kila tatizo Beberu.....Beberu.....Beberu.....Miaka nenda tunaletewa vyandalua kujikinga na Malaria.....tunaleta wawekezaji toka China kuuza maua karikooo.......Unataka Nani amwelimishe nani.....na elimu kama ipi....? Maana Vijana wana elimu hawana kazi......!The only way ni kuingia siasa....short cut ya kufanikiwa Tanzania!

Tuliimba na kufundishwa Ujamaa......Waliousoma huo Ujamaa vyuo vikuu miaka ya 60-70.....Walipokuja kushika viwanda miaka ya 80 wakavimaliza.....! Au hauko Tanzania....
 
Nadhani hata suala la kutafuta maisha nchi za nje nalo limepitwa na wakati. Teknolojia imewezesha kupata vitu vingi sana by proxy

Extra Miles.....Nakubaliana na wewe Mkuu, hilo halipingiki.....Lakini kuhama Nchi ni zaidi ya kupata vitu......kuna sababu nyingi mno.......sometimes ni pure adventure.....aina ya maisha unayotaka.....ambapo ulipo huwezi kupata kwa urahisi huko uliko...Ndio maana kama umesoma mada huko nyuma. mara nyingi nawauliza watu wanaotaka kuja US, ni kuwa unakuja kufanya nini! Je umeshindwa kupata unachokitaka Tanzania?
 
Extra Miles.....Nakubaliana na wewe Mkuu, hilo halipingiki.....Lakini kuhama Nchi ni zaidi ya kupata vitu......kuna sababu nyingi mno.......sometimes ni pure adventure.....aina ya maisha unayotaka.....ambapo ulipo huwezi kupata kwa urahisi huko uliko...Ndio maana kama umesoma mada huko nyuma. mara nyingi nawauliza watu wanaotaka kuja US, ni kuwa unakuja kufanya nini! Je umeshindwa kupata unachokitaka Tanzania?
Binafsi nadhani kama ni suala la adventure linafanyika kwa njia ya utalii, ila suala la kutafuta maisha linaanza na mtu binafsi kufanikiwa nchini kwake na kisha kwenda nje kama anahitaji kufanya hivyo.
 
Nipe statistics za Waafrika ambao walipelekwa Marekani kama watumwa kutoka west Africa kupitia the Atlantic ocean. Watumwa wanahitajika hadi Leo ila tofauti ni namna wanavyowapata.

Kavulata Statistics za nini...mbona ni mamilioni.....kinachoumiza zaidi ni babu yangu na babu yako walishindwa kabisa kuwazuia wazungu/waaarabu waliposhuka pwani zetu na majahazi yao.....kisha kudanganywa na gololi.....

Na unajua umbali toka Kigoma hadi Dar es Salaam ( Bagamoyo) ni kama Kilometer 1374 Hebu fikiria kundi la Waafrika kama mia mbili limefungishwa mnyororo na waarabu watatu au wanne tu, linatatembea kwa kwa mguu usiku mchana, maybe kwa miezi miwili hadi kufika Bagamoyo......kuingizwa jahazini kama makondoo......There is something wrong with our ancestors laana hii sijui imetoka wapi....! Leo hii tunawapa Bandari kwa kisingio tumeshindwa kuzuia wezi...!

Huwezi kumlaumu mzungu au mwarabu.....unaanza na mababu zetu.....to be specific babu yangu na babu yako.....
 
Elimu yetu tuliyopewa haitoshi. Tumefundishwa kulikimbia tatizo badala ya kulitatua tatizo kwenye mazingira yetu. Kama tatizo ni uongozi haufai wewe utachangiaje katika kutatua changamoto ya uongozi nchini kwako? Kama shida ni neo colonialism wewe ulifanya nini kama kijana. Vijana wetu ukiwemo ww mnaona suluhisho ni kukimbilia kule ambako vijana wenzenu wa mataifa hayo walipambana na mifumo Yao kwa jasho na damu zao kurekebisha mambo.

Vijana kama Ibrahim Traore kule Burkina Faso wanatafuta majibu ya shida zao wakati you cowards majisalimisha kwa watesi wetu kuwa manamba (cheaper labors) kuyajenga mataifa Yao. Narudia tena elimu yetu inawafanya vijana wetu iwe rahisi hata ikibidi kuf*rwa (short cut) ili kutoboa.

Una uhakika gani Ibrahim Traore hatakua kama Sargent Samwel Doe....Mohammed Siad Barre......Mengistu Haile Mariam....Sani Abacha.....Omar AL Bashir........Valentine Strasser..... Mobutu Sesse Seko.....Orodha ni ndefu mno....Hawa wote walitafuta majibu ya shida zao.....unafahamu matokeo.....!1
 
Kavulata Statistics za nini...mbona ni mamilioni.....kinachoumiza zaidi ni babu yangu na babu yako walishindwa kabisa kuwazuia wazungu/waaarabu waliposhuka pwani zetu na majahazi yao.....kisha kudanganywa na gololi.....

Na unajua umbali toka Kigoma hadi Dar es Salaam ( Bagamoyo) ni kama Kilometer 1374 Hebu fikiria kundi la Waafrika kama mia mbili limefungishwa mnyororo na waarabu watatu au wanne tu, linatatembea kwa kwa mguu usiku mchana, maybe kwa miezi miwili hadi kufika Bagamoyo......kuingizwa jahazini kama makondoo......There is something wrong with our ancestors laana hii sijui imetoka wapi....! Leo hii tunawapa Bandari kwa kisingio tumeshindwa kuzuia wezi...!

Huwezi kumlaumu mzungu au mwarabu.....unaanza na mababu zetu.....to be specific babu yangu na babu yako.....
umeshaamua kwa hiari yako kuwa utakuwa mzalishaji cheap wa wazungu na mjenga nchi ya kizungu, lakini unaweza kusema idadi ya wafungwa gerezani inalingana na idadi ya askari gerezani? Idadi y mahabushi kwenye karandinga ni sawa na idadi ya askari kwenye karandika hilo? Babu zetu walikuwa mashujaa sana kuliko wewe ila walizidiwa tu na watu wachache wenye bunduki mikononi, kamba za kunyongea hadharani na kufungwa nyororo miguuni na shingoni, hata ungekuwa wewe ungefanya nini.

Na bahati mbaya sana watu hawa walikuwa wanauzwa na viongozi wao ndani ya jamii, hivyo hata kama ukitoroka msafara na kurudi nyumbani utakutana na kifo kutoka kwa machifu ambao walikuuza utumwani na utakamatwa tena na kusalimishwa kwa tajiri. Nilitembea kituo kimoja cha kumbukumbu ya watumwa pale Detroit, nilikosa usingizi kwa siku 5. Babu zetu walikataa fedheha ya kutumikia whites lakini vijana wao wa sasa wanahamasishana kwenda kuwafanyia kazi whites. Kizazi kimerudi nyuma kwa hatua nyingi sana, aibu ya karne hii. What are you looking for, money?!!!
 
Una uhakika gani Ibrahim Traore hatakua kama Sargent Samwel Doe....Mohammed Siad Barre......Mengistu Haile Mariam....Sani Abacha.....Omar AL Bashir........Valentine Strasser..... Mobutu Sesse Seko.....Orodha ni ndefu mno....Hawa wote walitafuta majibu ya shida zao.....unafahamu matokeo.....!1
Hawa wote unaowasema walisaidiwa na ex wakoloni wetu kupindua kwa faida ya wakoloni, Traore is a deferent case, wananchi wako nyuma yake na wako tayari yawafike mabaya pamoja na traore.
 
We Baki Tanzania unapotafuta fursa, acha wengine pia wakatafute fursa nje ya Nchi.
 
umeshaamua kwa hiari yako kuwa utakuwa mzalishaji cheap wa wazungu na mjenga nchi ya kizungu, lakini unaweza kusema idadi ya wafungwa gerezani inalingana na idadi ya askari gerezani? Idadi y mahabushi kwenye karandinga ni sawa na idadi ya askari kwenye karandika hilo? Babu zetu walikuwa mashujaa sana kuliko wewe ila walizidiwa tu na watu wachache wenye bunduki mikononi, kamba za kunyongea hadharani na kufungwa nyororo miguuni na shingoni, hata ungekuwa wewe ungefanya nini. Na bahati mbaya sana watu hawa walikuwa wanauzwa na viongozi wao ndani ya jamii, hivyo hata kama ukitoroka msafara na kurudi nyumbani utakutana na kifo kutoka kwa machifu ambao walikuuza utumwani na utakamatwa tena na kusalimishwa kwa tajiri. Nilitembea kituo kimoja cha kumbukumbu ya watumwa pale Detroit, nilikosa usingizi kwa siku 5. Babu zetu walikataa fedheha ya kutumikia whites lakini vijana wao wa sasa wanahamasishana kwenda kuwafanyia kazi whites. Kizazi kimerudi nyuma kwa hatua nyingi sana, aibu ya karne hii. What are you looking for, money?!!!

Malizia kabisa.....na Viongozi wetu wanauza Bandari...
 
Malizia kabisa.....na Viongozi wetu wanauza Bandari...
Kama vijana wenye kesho nyngi wameamua kuzikimbia bandari zao na kwenda kuwa manamba ng'ambo kwanini wazee wasiziuze? wacha ziuzwe ili sote twende marekani na ubelgiji tukatafute maisha, kaeni kimya subiri maombi yenu ya Greencard yajibiwe. Isiwe huku mwataka na kule mwataka.
 
Hawa wote unaowasema walisaidiwa na ex wakoloni wetu kupindua kwa faida ya wakoloni, Traore is a deferent case, wananchi wako nyuma yake na wako tayari yawafike mabaya pamoja na traore.

Hata Mwezi haujafika unasema Traore ni different case.....ndugu yangu Kavulata sasa umeakuwa mnajimu? .....Kuna mapinduzi ambayo wananchi wamewahi kuwa kinyume na Wapinduaji.....?Hata Uganda kipindi cha Idi Amin wananchi walitoka na kushangilia...... Kumbuka watu walivyofurahia ujio wa Samueli Doe.....! Mengitsu Haile Mariam....au umesahau historia? Tafadhali tunza maneno yako......tena inawezekana kabisa hao hao wenzake ndio watakao mgeuka.....!Hao wanamapinduzi huwa wanakuja na maneno ya Kimapinduzi.....wape mwaka tu......! Nigeria wamepinduana mpaka wenyewe wakachoka.....
 
Kama vijana wenye kesho nyngi wameamua kuzikimbia bandari zao na kwenda kuwa manamba ng'ambo kwanini wazee wasiziuze? wacha ziuzwe ili sote twende marekani na ubelgiji tukatafute maisha, kaeni kimya subiri maombi yenu ya Greencard yajibiwe. Isiwe huku mwataka na kule mwataka.

Tutakula kote kote.......! Hujasikia uraia pacha...au vibali maalumu viko jikoni........
 
Kama vijana wenye kesho nyngi wameamua kuzikimbia bandari zao na kwenda kuwa manamba ng'ambo kwanini wazee wasiziuze? wacha ziuzwe ili sote twende marekani na ubelgiji tukatafute maisha, kaeni kimya subiri maombi yenu ya Greencard yajibiwe. Isiwe huku mwataka na kule mwataka.

Kavulata, si heri kula jasho langu ughaibuni, kuliko kuwaibia Watanzania.....Jamaa zangu niliowaacha nyumbani, ambao wengi wako kwenye nyazifa za DED/RAS....Wakurugezi mawizarani nk.....wana pesa kufuru.....unajua wamezipata wapi? Wengine pesa za aina hiyo zilitushinda, dhamira zetu ziko hai..... na kama uzalendo ndio huo......basi siuwezi....! Tumewaachia watu kama wewe wenye Uzalendo......!!!
 
Back
Top Bottom