GSM ‘wachomoa betri’ Yanga

Kaka kama hujui mambo uliza aseee.....
Unajiabisha mtu mzima unavyodanganya.
Simbà ni kampuni MO anamiliki asilimia 49 za hiyo kampuni so akiondoka atauza...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aseee....mkuu usiulize maswali yasiyo na vichwà....
Ulichokiongea ww ni sawa mtu aulize TBL...ni kampuni.....inalipa tshs..ngapi TRA?....Ina kiasi gani bank?...maswali yasiyojibika kwa mtu makini kwani...yanahitaji data kamili kutoka bodi ya wakurugenzi..we unauliza huku.
Sawa ndugu yangu Sasa hiyo kampuni kwenye akaunti yake huko benki ina kiasi gani na imelipa kiasi gani huko TRA Kama Kodi ya mapato??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe unafikiri huyo GSM ni nani? Mimi nadhani huyo GSM ni Sponsor...Sasa huyo Mo kule Simba ni mwekezaji kweli? Au ni Sponsor? Au ni owner yaani mmilki? Au ni vyote? Hivi alimteua Makonda akiwa ni mwekezaji au mmiliki au sponsor?
Aseee. Bro kwa Mara nyingine unaboronga.
Mo.ndo mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi...
Nadhani tatizo ni kuwa hujui structure ya SIMBA SPORTS CLUB LIMITED...
Ipo kaisome

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kaka kama hujui mambo uliza aseee.....
Unajiabisha mtu mzima unavyodanganya.
Simbà ni kampuni MO anamiliki asilimia 49 za hiyo kampuni so akiondoka atauza...

Sent using Jamii Forums mobile app
Nadhani kwa kauli hiyo ndugu yangu wewe ndiye unajiabisha ...atauza kampuni au atauza hisa?? Ni wapi Mimi nimedanganya ...Simba ni kampuni kweli?? Au Simba inamiliki kampuni..? Kama Simba ni kampuni tukienda kwa Registrar of companies je tutakuta jina gani pale? Hivi unajua kuwa yanga ndiyo iliyokuwa ya Kwanza kujiandikisha kuwa kampuni ? What happened? Baadaye yanga nayo ikaanzisha kampuni..what happened?!
 
Well said dogo..bila Shaka kutakuwa na mkutano wa wanahisa na itafahamika hahaha
 
Nafikiri Yanga kuna udhaifu mkubwa sana kwenye uongozi. Hebu tujiulize inawezekana kweli GSM walikuwa wanafanya baadhi ya mambo mpaka kupitiliza je uongozi ulishindwa nini kuwaita wakakaa meza moja kuyamaliza mpaka GSM aandike barua kali kiasi hicho? Je hao viongozi timu ikirudi kwenye bakuli wataweza kweli kuiendesha? Kwa kipindi chote GSM anatoa msaada wao viongozi waliharakishaje zoezi la timu kupata mwekezaji sahihi ili GSM asiwe anapitiliza kwenye mkataba wake? Kwa vyote vyote iwavyo naona iwapo viongozi hawatajirudi safari itawakumba wataondoka na GSM atatamalaki Yanga. Viongozi wanajua na hata wapenda soka wote nchini wanajua mpira wa sasa hivi ni pesa na sio blah blah. Wanapojitokeza watu kama GSM wakaingiza pesa zao kwenye mpira tuwaunge mkono badala ya kuwakatisha tamaa. Tanzania hii kuna matajiri wengi sana lakini ni wachache sana wanaoweza kuingiza pesa zao kwenye michezo hususani mpira miguu kwani wanajua wakiwekeza kwenye mpira uwezekano wa wao kurudisha pesa zao ni mdogo na unachukua muda mrefu sana.

Suala la pili ni kuhusu tetesi za Tshishimbi kusajiliwa Simba. Kiukweli nitaushangaa sana uongozi wa Simba iwapo utamsajili kwa sababu kwa sasa Simba wanahitajika wachezaji wenye uwezo zaidi ya huyo Tshishimbi. Ukiangalia umri wake, majeruhi na hata kiwango chake sio sawa na wakati ule anafika Tanzania. Sitaki kuamini kuwa timu kubwa kama Simba haina timu ya "scounting" kwa ajili ya wachezaji wapya halafu inasema inataka kuwa sawa na vilabu vikubwa Afrika kama TP Mazembe, Al Haly, Mamelodi, n.k. Mfano mdogo tu nani alikuwa anamfahamu kuwa kuna bonge la mchezaji anaitwa Morison si mpaka GSM walipomleta Tanznaia. Wachezaji wa aina ya Morison tena wenye umri mdogo wapo wengi Afrika lakini bila kusumbua kichwa kama GSM au kuwa na timu ya "scouting" mtabaki mnawagombea na kubadilishana hawa hawa wakina Niyozima, Tshishimbi na wengineo basi. Na Simba wakifanya mchezo kwenye usajili yatarudi yale yale ya wabrazili.
 
hii corona imeingia yanga, siku zote mashabiki wao walikuwa wanaiombea mabaya simba sasa kibao kimegeuka kwao nafikiri kisa ni milioni 200 gsm zinamfirisi
Ila kama simba wamesajili Tshishimbi wasahau kuingia hata raundi ya pili michuano ya Afrika hana chochote cha ziada
 
Acha ujinga wewe . Simba sasa hivi ipo kwenye mfumo wa kisasa . MO hafanyi hisani Simba . Amewekeza pale . Hawezi kujiondoa kienyeji bila kufuata taratibu za kibiashara au kimkataba . Akitaka kuondoka kama muwekezaji zitaangaliwa terms za makubaliano wakati wa kuwekeza . Ana 49% ya hisa . Kwahiyo pamoja na mambo mengine anatumia brand ya Simba kutangaza products zake . MO anaitumia Simba na Simba inamtumia MO . Ni win win situation .
Sent using Jamii Forums mobile app
 
shishimbi hana thamani ya kulipwa huo mshahara...kwanza umri umekwenda, injury prone...ntashangaa kama yanga au simba watamlipa huo mshahara.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hiyo aliwaambia Utopolo kujikosha tu . Shishimbi Mcongoman . Anataka kula bata mjini kwa kupata mshahara wa uhakika Simba . Atakuwa anapata 5M na 30M za kusaini mkataba basi . Ni mawazo yangu tu .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dahh...hasira za Nini...kwanini unatanguliza neno ujinga...umepanic kwanini??hivi wiki chache zilizopita alipotangaza kuachia ngazi na baadhi wakamuomba asifanye hivyo alitumia taratibu zipi?
 
Mkuu viongozi wengi wa TFF /Simba /Yanga wamezoea ( Walizoea ) kupiga . Anapotokea mtu kuwabana wanampiga zengwe . GSM alikataa kuwapa pesa mkono ktk maeneo ambayo alikuwa anasaidia . Kama ni pesa za usajili , mishahara , bonasi , kambi na viwanja vya mazoezi alikuwa anawapa wahusika direct . Sasa jamaa wameona wanakosa ulaji wakaona bora tu waanzishe harakati za majungu . Sasa viongozi wataimba Alleluia kukabiliana na muziki wa mashabiki na wanachama wa Utopolo a.k.a vyura fc
Sent using Jamii Forums mobile app
 
MO ni mmoja wa wamiliki wa Simba Sports Club Limited . Ana 49%/ ya hisa na pia MO ni Sponsor kupitia baadhi ya products za kampuni zake . Nafikiri unapaswa kuruhusu akili yako kuelewa kuliko kusikiliza hisia zako .
Wewe unafikiri huyo GSM ni nani? Mimi nadhani huyo GSM ni Sponsor...Sasa huyo Mo kule Simba ni mwekezaji kweli? Au ni Sponsor? Au ni owner yaani mmilki? Au ni vyote? Hivi alimteua Makonda akiwa ni mwekezaji au mmiliki au sponsor?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acha comedy basi inamaana hujui kama simba imeuza hisa kwa mo ?
Haya embu nitajie hao watu kama mo kwa upande wa yanga ni nani.hao gsm tu yanawashinda ndo itakua mtu tu atoe hela zake kiholela kuwapa watu wazitafune!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dahh...hasira za Nini...kwanini unatanguliza neno ujinga...umepanic kwanini??hivi wiki chache zilizopita alipotangaza kuachia ngazi na baadhi wakamuomba asifanye hivyo alitumia taratibu zipi?
wewe kiumbe mo aliachia ngazi uenyekiti wa body ya wadhamini simba.akuachia ngazi kwenye udhamini wala hisa alizonunua bali ni uwenyekiti wa body.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwani Manji siyo mtu ....vipi kuhusu GSM...wako wengi mno...ila kwa Sasa mazingira hayaruhusu...
 
wewe kiumbe mo aliachia ngazi uenyekiti wa body ya wadhamini simba.akuachia ngazi kwenye udhamini wala hisa alizonunua bali ni uwenyekiti wa body.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kumbe...unadhani ilikuwa nivhivyo tu...inawezekana Mimi nina taarifa za ndani kuliko wewe maenzangu 'mwanahisa'
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…