ngaribazezeta
Member
- Dec 11, 2017
- 82
- 47
Kutembelea michoro ya wenzio na ukafanikiwa kushinda ni ujanja ambao wengine hawana.Kwakuwa umeandika kishabiki zaidi na mahaba mazito kwa La liga, naomba nikukumbushe kuwa kuna mzunguko wa pili bado haujaanza, kumbuka msimu uliopita.
Kuhusu ubora wa Guardiola, kwangu mimi ni mtu anayetembelea michoro ya wenzake na kutegemea pesa zaidi. Timu zote alikutwa zimesukwa vyema, ni kama Vicente Del Bosque alipopewa Spain akatwaa ndoo kubwa, kazi yake kubwa ilikuwa nini?
Sitaki kuamini kuwa leo ukimpa Salum Mayanja timu ya Real Madrid afundishe atafanikiwa kutoa vipigo na kuchukua ubingwa eti kwakuwa tu amekuta timu iliyoundwa vizuri sana. Sidhani kama ni sahihi kuamini kuwa kocha yeyote angekifundisha hicho kikosi cha Spain unachokisema angeweza kuchukua ubingwa Hatahivyo,kama man city angelikuwa ndie bingwa wa msimu uliopita chini ya kocha mwingine labda ungetushawishi kuwa guardiola msimu huu anafaidika na timu iliyoundwa na kocha mwingine msimu uliopita.