Gwaride la Watoto lamkosha Rais Samia mpaka kuinuka kwenye kiti na kusimama kwa tabasamu na furaha ya hali ya juu

Gwaride la Watoto lamkosha Rais Samia mpaka kuinuka kwenye kiti na kusimama kwa tabasamu na furaha ya hali ya juu

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
28,722
Reaction score
20,610
Ndugu zangu Watanzania,

Tanzania na watanzania tuna kila sababu ya kujivunia utanzania wetu na utaifa wetu,tuna kila sababu ya kujiona fahari ya kuzaliwa Tanzania,tuna kila sababu ya kuona Taifa letu litaendelea kuwa salama na kisiwa cha Amani na kupigiwa mfano Barani Afrika na Duniani Kwote kwa ujumla wake.

Tuna kila sababu ya kuona Taifa la kesho lipo imara na madhubuti kwelikweli,tuna kila sababu ya kuona kuwa Taifa letu lina nguvu kazi ya kutosha kwa leo na hata kesho,tuna kila sababu ya kuona na kujivunia mipango endelevu ya kujenga uzalendo kuanzia kwa watoto mpaka wanakuwa katika kulilinda,kulitetea na kulipigania Taifa letu mpaka tone la Mwisho.

Leo Mkoani Kilimanjaro katika kilele cha maadhimisho ya miaka 60 ya jeshi la polisi. ambako mgeni Rasmi ni Mama yetu na RAIS wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan kumetokea tukio la kugusa na kuteka mioyo ya mamilioni ya watanzania.ambapo imeshuhudiwa Gwaride la watoto likipita mbele ya Amiri Jeshi Mkuu wetu kwa ukakamavu na umakini wa hali ya juu sana na mkubwa sana Utafikiri makomandoo na askari wa JWTZ au Mossad ya Israel au CIA kutoka Marekani.

Namna watoto hao wakike kwa wakiume walivyopita kishupavu na kikakamavu mbele ya Mama yetu kipenzi na Amiri Jeshi Mkuu imemfanya mpaka ainuke kwenye kiti chake cha heshima akiwa amejaa tabasamu na furaha ya hali ya juu sana. Furaha aliyokuwa nayo Rais wetu ilikuwa ni kubwa mpaka unaona namna akitamani aendelee kusimama kuendelea kuwaangalia watoto hao walioteka ,kukosha na kukonga mioyo ya wengi sana.

Kwa hakika Tanzania yetu ipo imara na itaendelea kuwa imara na salama kwa sababu kila anayezaliwa Tanzania na kupulizwa na upepo anajikuta yupo tayari kulipigania Taifa hili na kuwa na moyo wa uzalendo.ndio sababu huwezi wadanganya watanzania kulibomoa Taifa lao.
Screenshot_20240917-122438_1.jpg
.​

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
 
Najaribu kuunganisha dots Kuna uhusiano Gani kati ya kuadhimisha miaka 60 ya jeshi la polisi na kuwahusisha watoto wa shule kwenye hayo maadhimisho.

Je hao ni watoto wa polisi (kota)?
Au wanasona shule za polisi? Kwa hiyo muda wa shule au kupumzika likizo wao wanautumia kujifunza unnecessary kwata.

Sijaongea lolote kuhusu kumfurahisha rais naomba mniache
 
Najaribu kuunganisha dots Kuna uhusiano Gani kati ya kuadhimisha miaka 60 ya jeshi la polisi na iuwahusisha watoto wa shule kwenye hayo maadhimisho.

Je hao ni watoto wa polisi (kota)?
Au wanaona shule za polisi? Kwa hiyo muda wa shule au kupumzika likizo wao wanautumia kujifunza unnecessary kwata.

Sijaongea lolote kuhusu kumfurahisha rais
Acha wivu wako wewe.Taifa linaanza kujengwa kwenye mioyo ya watoto kwa kuwajengea uzalendo,utii na moyo wa kujitolea angali wakiwa bado wadogo kabisa.hivyo ndicho yafanyavyo Mataifa yote makubwa makubwa na yenye kujitambua kama ilivyo kwa Tanzania.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Tanzania na watanzania tuna kila sababu ya kujivunia utanzania wetu na utaifa wetu,tuna kila sababu ya kujiona fahari ya kuzaliwa Tanzania,tuna kila sababu ya kuona Taifa letu litaendelea kuwa salama na kisiwa cha Amani na kupigiwa mfano Barani Afrika na Duniani Kwote kwa ujumla wake.

Tuna kila sababu ya kuona Taifa la kesho lipo imara na madhubuti kwelikweli,tuna kila sababu ya kuona kuwa Taifa letu lina nguvu kazi ya kutosha kwa leo na hata kesho,tuna kila sababu ya kuona na kujivunia mipango endelevu ya kujenga uzalendo kuanzia kwa watoto mpaka wanakuwa katika kulilinda,kulitetea na kulipigania Taifa letu mpaka tone la Mwisho.

Leo Mkoani Kilimanjaro katika kilele cha maadhimisho ya miaka 60 ya jeshi la polisi. ambako mgeni Rasmi ni Mama yetu na RAIS wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan kumetokea tukio la kugusa na kuteka mioyo ya mamilioni ya watanzania.ambapo imeshuhudiwa Gwaride la watoto likipita mbele ya Amiri Jeshi Mkuu wetu kwa ukakamavu na umakini wa hali ya juu sana na mkubwa sana Utafikiri makomandoo na askari wa JWTZ au Mossad ya Israel au CIA kutoka Marekani.

Namna watoto hao wakike kwa wakiume walivyopita kishupavu na kikakamavu mbele ya Mama yetu kipenzi na Amiri Jeshi Mkuu imemfanya mpaka ainuke kwenye kiti chake cha heshima akiwa amejaa tabasamu na furaha ya hali ya juu sana. Furaha aliyokuwa nayo Rais wetu ilikuwa ni kubwa mpaka unaona namna akitamani aendelee kusimama kuendelea kuwaangalia watoto hao walioteka ,kukosha na kukonga mioyo ya wengi sana.

Kwa hakika Tanzania yetu ipo imara na itaendelea kuwa imara na salama kwa sababu kila anayezaliwa Tanzania na kupulizwa na upepo anajikuta yupo tayari kulipigania Taifa hili na kuwa na moyo wa uzalendo.ndio sababu huwezi wadanganya watanzania kulibomoa Taifa lao.

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Nimebugujikwa na machozi baada ya kuona gwaride
 
Ndio mambo anayoyaweza hayo. Siku nyingine mwanamke kua kiongozi asitokee pwani jamani.
 
nchi yangu ina upuuzi mwingi sana ......

kuna habari kibao za kupost kuhusu nchi mtu anakupostia gwaride la watoto ni nini hiki jamani kama sio uchawa
Hizo habari nani kakuzuia wewe kuzipost hapa? Acha uvivu wa kutumia akili na kukaa muda wote ukilalamika Hovyo hovyo tu.
 
Acha wivu wako wewe.Taifa linaanza kujengwa kwenye mioyo ya watoto kwa kuwajengea uzalendo,utii na moyo wa kujitolea angali wakiwa bado wadogo kabisa.hivyo ndicho yafanyavyo Mataifa yote makubwa makubwa na yenye kujitambua kama ilivyo kwa Tanzania.
Hujajibu hoja. Nimewema sijaona logic ya kuwahusisha watoto wa shule kufanya gwaride kwenye maadhimisho ya miaka 60 ya jeshi la polisi. Unaweza ukanipa logic.? Ndo mana mnakimbiaga midahalo ya live
 
Back
Top Bottom