Haamini Macho Yake Kuona Shule Ikijengwa Kwenye Kitongoji Chao

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

MZEE KIUNYA ANAOMBA KUMUONA MHE RAIS: HAAMINI MACHO YAKE KUONA SHULE MPYA IKIJENGWA KWENYE KITONGOJI CHAO

Kijiji cha Kigera cha Musoma Vijijini kimepokea Tsh 348,500,000 (Tsh 348.5m) kutoka Serikalini kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Msingi mpya (Mradi wa BOOST) ambayo itakuwa ya pili, na inajengwa kwenye Kitongoji cha Kusenyi

Mzee Kiunya, mzaliwa na mkazi wa Kitongoji cha Kusenyi, kwa furaha tele ya kupata shule kwenye Kitongoji chao, amemtuma Mbunge Prof Muhongo "ampelekee hapo Kitongojini Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan" akafungue shule hiyo inayokamilishwa ujenzi. Mzee huyo ameongea kwa lugha ya "Kikwaya."

Tafadhali sikiliza CLIP/VIDEO iliyoambatanishwa hapa yenye taarifa za shukrani nyingi, ikiwemo ya Mzee Kiunya, kutoka Kijijini Kigera, Kata ya Nyakatende, Musoma Vijijini.

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

Tarehe:
Jumatano, 23.8.2023
 

Attachments

  • WhatsApp Video 2023-08-22 at 23.51.28.mp4
    21.6 MB
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…