Habari mbaya: Uwanja wa Uhuru Dar, Watu 45 wapoteza maisha kutoka na msongamano

Habari mbaya: Uwanja wa Uhuru Dar, Watu 45 wapoteza maisha kutoka na msongamano

Kuna mmoja jana alikuwa na kichanga kama cha miezi miwili, walimkandamiza, yaan ni aliminywa firigisi na utumbo mi nilijua anakufaa haloo usiombe [emoji848][emoji848] mi na rafiki yangu tukamnyang'anya mtoto..alivyochoropoka hapo tukamnasa vibao vitatu tukamrudishia mtoto wake, alikuwa anatafuta upenyo wa kurudi home, maana si kwa ukunga ule kwa mminyo wa kufa mtu
Wakati mwingine wanawake tuna matatizo ... mtoto wa miezi miwili unaenda nae wapi zaidi ya clinic?
Na baba mtoto anamuangalia tu, au mtoto hana baba ila dah ni upuuzi mtu Kama huyo unashindwa kumuonea huruma.
.
.
Hlf unafika pale kuaga unajidondosha chini ubebwe juu juu. Sijawahi waelewa wanaozimia msibani na ni msiba wa mtu ambae sio ndugu yako. Ukilia kwa ustaarabu utapungukiwa nini?

Sent from my Infinix X5515 using JamiiForums mobile app
 
Jamani ila watu.Mimi nimeangalia nyumbani tu. Ya nini kwenda kwenye msongamano wote huo?Sasa wamefuata vifo vyao. Inasikitisha.
Kila mtu angebaki nyumbani nani angeenda? Ni sawa kwenda ila uangalie na mazingira ukikuta hayafai unajiondokea taratibu, na wale wamama walioenda na watoto wadogo kama sio upumbavu ni nini

Sent from my Infinix X5515 using JamiiForums mobile app
 
Sasa wewe tukio kama lile linawekwa jirani na Buza kwa mpalange unategemea nini? Nasikia wameenda hadi wanataka kuvamia ndege iliyobeba maiti waingie ndani wasepe nayo Dodoma. Watu wa Buza banah!
 
Hivi umewahi kufiwa kweli?
Mleta mada tuwekee vyeti vyao vya vifo tuamini taarifa zako kama vinasomeka wamekufa kwa msongamano.

Si vizuri kutangaza kifo cha mtu bila kuambatanisha death certificate
 
Mleta mada tuwekee vyeti vyao vya vifo tuamini taarifa zako kama vinasomeka wamekufa kwa msongamano.

Si vizuri kutangaza kifo cha mtu bila kuambatanisha death certificate
kmmmk
 
Duuuuh! Ila watu walikuwa wengi mno, hiv kwann wasinge peleka hiyo shughuli uwanja wa mkapa?
Mkuu viongozi wote huwaga wanaagwa uwanja wa uhuru kama ilivyofanyika kwa Magu.

Sasa serikali ilikuwa imefanyia kazi ushauri wa chadema kuwa Magu hapendwi na watu,Magu katili hivyo watu watakaoenda ni makatili wenzie wa CCM tu ambao pia ni wachachetu, hivyo hawakujiandaa kihivyoo.

sasa kwa kilichotokea kwa kweli walaumiwe chadema kwa kudanganya serikali na mataifa ya nje.
 
TANZIA
Habari za jioni Mates mwenzetu Mbasa Mtua amepata msiba mkubwa sana kwa kumpoteza mwanae mmoja watoto wa mdogo wake watatu na mtoto wa kaka yake mmoja baada ya kukanyagwa uwanja wa Taifa walipokwenda kumuaga JPM,na hadi sasa hawajui house girl yuko wapi,watoto waliongozana na mke wa mdogo wake,msiba uko kimara nyumbani kwao,tuwaombee wako kwenye wakati mgumu sana,mwenyezi mungu awapumzishe kwa Amani[emoji120]
Hawa ujinga ndio umesababisha msiba wao
 
Kwa hiyo ajali zikitokea barabarani polisi wakitoa taarifa huwa na death certifacate?

Watu walioko eneo la tukio au ndugu zao wasiseme neno mpaka death certificate?
Acha nao hao Mataga wamepaniki. Tulilishwa woga mno. Mwisho umefika tutaelewana tu
 
Jeshi,TPDF,wangeachiwa waendelee kuratibu utaratibu wa kuaga mwili wa Rais( kimsingi ndo wahusika), lakini kimbelembele cha Gondwe na RPC wake, na CCM ya Polepole ndo haya yakatokea.
Msiba wa Nyerere hatukusikia haya,ingawa umati ulikuwa mkubwa sana kuliko wa JPM wa kulazimisha vilio
Wanataka kuvunja rekodi na kuaminisha Rais mpya kuwa jamaa alipendwa hivyo aendeleze alipoachia
 
Kila Mtu atakufa. Tumuhimidi Bwana wa Majeshi
 
Back
Top Bottom