calvin priva
Member
- Jan 24, 2014
- 9
- 3
wewe hupendi?
Hapana ndugu sina kiwanja ila nipo eneo ambalo kuna uhitaji mkubwa wa hostelMkuu tupe kwanza wewe una noni special mpaka wakujengee?
Je unakiwanja kipo karibu na chuo au eneo ambalo watu wanahitaji hizo hostel au?
Hapana, sina kiwanja kariakoo maana sehemu ambapo kuna uhitaji wa hostel hiyo ni maeneo ya sinza na watu wengi sana wanahangaika kutafuta hostelje unakiwanja kariakooo au??? he he he ongeza nyama kumfanya mdhamini akujengee wewe na amuache mwingine
Asante sana ndugu.. Hostel nimeplan iwe sinza kama nitafanikiwa maana hostel nyingi za huku hazikidhi vigezo na husababisha wanafunzi wengi kuzikimbia hivyo kuna uhitaji mkubwa wa hostel, gharama ya chumba kimoja ni elfu sabini kwa mwezi na italipwa kwa awamu tatu yaani laki mbili na themanini kila baada ya miezi minne. Chumba kimoja watakaa wanafunzi wanne.Je hizo hostel utazijenga eneo gani?
Utatoza kodi ya kiasi gani kwa chumba?
Eneo unalo tayari au ni la kununua?
Kupata ufadhili inategemea na project plan yako na ushawishi wako, ila kwa ushauri ni vizuri uwe na mtaji wa kianzia atleast....hakuna mtu anaweza kukupa ela kwa idea ambayo hata wewe umeshindwa kuigharamia kidogo.
All the best.
Asanteni sana kwa ushirikiano.. sina kiwanja ila gharama ya chumba kimoja ni Tsh.70,000 kwa mwezi then watalipia kwa miezi minne (awamu 3 kwa mwaka) that means ni sawa na Tsh.280,000 na kila chumba kimoja watakaa watu wanne. Ukiangalia hesabu ya mwaka mmoja kwa vyumba arobaini vya mdhamini ambavyo vitakuwa na watu 160 (kila chumba kimoja watu 4) na ada ya mtu mmoja kwa mwaka ni Tsh.840,000 that means ada ya mwaka mmoja kwa wanafunzi 160 wa hivyo vyumba arobaini ni sawa na Tsh.33,600,000 hivyo mdhamini atakata kiasi hicho cha pesa kila mwaka hadi kumaliza deni lake na baada ya hapo atanikabidhi umiliki wa jengo.
Ni kweli kaka ila mimi nilikuwa nakaa hostel zilizopo mori na bei zilkuwa juu ya 70 halafu sababu za wanafunzi wengi kukimbia niliziona baadhi ndio maana nimeamua kufanyia tu hukohuko sinza ila nitafuatilia zaidi kutokana na ushauri wako kaka, asante.soko la hostel sio zuri kiasi hicho.. maana kuna wanafunzi wanapanga mitaani pia... mwanafunzi akupe 70 kwa mwezi akae hostel ya kushare wanne wakati hiyo hiyo 70 yake inamruhusu kupanga chumba cha peke yake mtaani?
sinza kuna hostel nyingi sana na hakuna hata moja inayojaa na hapo wanachaji chini ya hiyo bei kwa kitanda....
Wazo lako zuri lakini zingatia haya ili uwe na ushawishi kwa kampuni/mwekezaji wa mradi wakoNimewaza sana kutafuta ufadhili wa kampuni yoyote ili inijengee hostels za kisasa zenye vyumba hamsini lakini nimeona ni vyema nilete wazo langu hapa na baada ya hapo ndo nichukue maamuzi, malipo ya deni la kampuni tutakatana ndani ya miaka kadhaa hadi pesa yao imalizike na haitaniumiza kwasababu katika vyumba hamsini hao watachukua kodi ya vyumba arobaini kila mwaka hadi wamalize deni lao then mimi nitabaki na vyumba kumi kwaajili ya matumizi yangu baada ya kumaliza deni lao nyumba nzima inakuwa yangu.. Je, ufadhili kama huo unawezekana?
Kwahio mtu akujengee hostel, halafu akupe room kumi uwe unakula hela tu. Baada ya investment yake kurudi akuachie hilo jengo bure kabisa. Who are you???
Simuoni mtanzania mwenye roho ya hivyo kwa kweli,,,tafta namna ya kutoka tu!
Eeh man, yani nimesoma uzi wake nikakaa nikatafakari kwa utulivu sana. Its a good idea ila kwa bongo hakuna mtu atafanya kitu cha kijinga hivyo,hakuna mtu duniani mjinga kiasi hicho.. dogo hachangii chochote eti na bado apewe vyumba kumi bure... angalau angekuwa na kiwanja ingesound...