Hadi leo najiuliza, ilikuwaje tukajenga SGR kwenda Burundi na kuacha kuboresha TAZARA kuwa SGR ambapo tungefika Congo kirahisi sana

ndiyo maana huwa anatuona mafa.la
 
Kwa upande wa mizigo tungeboresha Tazara kuiwekea umeme na kuwa Kiwango cha SGR hali ingekuwaje?

Kulifanyika hata comparison kulinganisha hayo mambo mawili?

Kwenda Hadi Mpanda naweza kwambia kuwa ni hasara kwa sababu Bado sioni faida za kiuchumi za haraka maana still faida zinategemea effectiveness ya Bandari ya Kalema
 
Waulize mataga na chawa wa Mwendazake 😄😄.

Utasikia itadumu miaka 100 😬😬
 
Reli ya Kati inalenga Congo mashariki,Burundi,rwanda,uganda
 
SGR haiendi Uganda! Inaishia Mwanza!

Kama target ni Congo , kulikuwa na haja gani kuipeleka Burundi na Rwanda tena kwa gharama kubwa sana? Kwa nini tusingeboresha TAZARA na kufika Congo kirahisi sana?
Congo ni kubwa sana,

Tazara inaweza kupokea mizigo ya Lubumbashi, Burundi na Rwanda zinaweza kupokea mizigo ya Bukavu na Kisangani.

Kwahivyo kazi iendelee ya kuifungua nchi
 

..nini hasara za Tazara kuwa Cape Gauge Rail?

..reli zote za nchi za SADC ni Cape Gauge Rail.

..unanichanganya hapo kwenye Standard Gauge vs Cape Gauge.
 
..nini hasara za Tazara kuwa Cape Gauge Rail?

..reli zote za nchi za SADC ni Cape Gauge Rail.

..unanichanganya hapo kwenye Standard Gauge vs Cape Gauge.
Hajui kama Tazara ilishakuwa na project ya ku-update reli yake ilianza kuunganishwa Dar mpaka Zambia miaka ya 90's kama sikosei, kuna jamaa zangu walipata ajira kwenye project hiyo na mpaka sasa bado wapo wanafanyakazi Tazara.

Labda tu kuna kitu hakijui, hapo Tazara sasa hivi kuna treni ya mizigo ya kampuni ya makaburu ambayo inatumia tu miundombinu ya Tazara lakini ina wafanyakazi wake na treni zake.

Washambenga wengi hawana habari hata media zetu nina hakika hawajui kinachoendelea Tazara ya leo.
 
Kitu ambacho huwa sielewi ni ili swala.

Tungeamua kuboresha njia reli ya kati tukajenga depot mfano dodoma na morogoro malori yote yanayofanyw transit yanachukulia mzigo hapo na kusambaza.

Kiasi cha pesa tungeweza kujenga highway zinazosogea hadi mipakani kurahisha usafirishaji wa mizigo na abiria.

Reli ingesaidia kupungua mrundikano wa mizigo bandarini maana ni kutoa na kupeleka depot kwa ajili ya other transit.

Hakuna lori ambalo lingeruhusiwa kufika ukanda wa bandari
 
Si ndio plan ya bandari kavu ya Kwala?
 
Wewe 'Jamaa' huwa sikuelewi kabisa katika 'thought process'yako ikoje?

Sasa kama umesema TAZARA imetelekezwa na nchi hizo mbili, licha ya kuwepo uhitaji wake mkubwa sana, ni kipi kinachokufanya udhani kwamba SGR na yenyewe itapitia matatizo hayo hayo?

Wala huna muda wa kjiuliza ni sababu zipi hasa zinafanya TAZARA isithaminiwe sana na mmojawapo wa hawa washirika wawiwli?

Umejiuliza kama mshirika mmoja anaona anazo njia mbadala za kufikisha mizigo anayotaka, na kutokuwa na haja ya kushughulikia TAZARA?

Au umejiuliza ufanisi wa bandari inayohudumiwa na TAZARA, pengine ndiyo inayochangia TAZARA isiwe na ufanisi?

Na mwisho, hivi unajuwa kusoma ramani kweli ikiwekwa mbele yako, ili kujuwa ni sehemu zipi hasa za DRC ambazo zinahitaji kuhudumiwa zaidi ya hiyo Lubumbashi?

Unajuwa DRC ilivyo kubwa, toka kusini hadi Kaskazini? Hata kama leo sehemu za Kaskazini zitakuwa zina matatizo, wewe unadhani hali itakuwa hivyo hivyo daima?

Ndiyo, TAZARA inahitaji kukarabatiwa ili ifanye kazi zake kwa ufanisi zaidi, na bandari yetu nayo inahitajika kufanya kazi kwa weledi zaidi ili mizigo ya nchi hizo zote iweze kuongezeka; na kama kutakuwepo na ulazima wa kuifanya iwe ya SGR, basi iwe hivyo kwa wakati maalum tukiwa na uwezo wa kufanya hivyo.

Lakini kwa sasa, huwezi kudharau umuhimu wa SGR inayopitia katikati mwa Tanzania, si kwa manufaa ya nchi yetu pekee, bali hata kwa majirani zetu pia, kibiashara.
 
Hizi 'Depot' zimezungumziwa mara nyingi sana, lakini naona kuna maslahi ya watu yanayozuia mpango huo kufanyika.

Ni maswala ya "Kamba ndefu tu" yanayozuia mambo mengi ya maana yasifanyike hapa nchini. Maneno mengi matamu matamu, lakini inapokuja kwenye utendaji, ni tofauti kabisa!
 
Kumbe hata huna ufahamu wa jambo unalolizungumzia; unaweka tu mada mradi umesikia habari ya TAZARA ikizungumziwa?
 
Reli zetu hatujengi kuwanufaisha majirani, tunajenga kwa manufaa yetu wenyewe kwanza, halafu majirani wanapata makombo yetu. SGR haikujengwa kwenda Rwanda, bali ilijengwa kwenda Mwanza, na Kigoma baadaye. Rwanda, Uganda, Burundi na DRC watajiunganisha kwenye SGR yetu kwa kushirikiana nasi siyo kuwa tumawajengea.

TAZARA ilijengwa mwaka 1970 kwa ajili ya kuifanya Zambia isiwe tegemezi kwa nchi za Rhodesia, Mozambique, and South Africa ambazo zilikuwa hazijapata uhuru wakati huo. Baada nchi zote tatu hizxo kupata Uhuru, Zambia imekuwa haiitegemi TAZARA sana kwani inaweza kutumia bandari za Beira, Maputo, Richards Bay na Durban. TAZARA ilikuwa ni ubia kati ya Tanzania na Zambia kwa mkopo kutoka China; kwa hiyo uamuzi wowote wa kuboresha TAZARA siyo wa serikali ya Tanzania tu, ni lazima Serikali ya Zambia ihusike pia. Uamuzi wa kuboresha reli za TRC ni wa serikali ya Tanzania tu; tutaamua kwa wakati tunaoona unatufaa
 
Kiongozi wa watu vs kiongozi wa Mapaka😁😁😁
Your browser is not able to display this video.
 
Muhimu reli zetu ziungane na majirani, mfano reli ya Kilimanjaro Tanga ifike Mombasa, ya Kati ifike Kongo, ya Mwanza ikunje Bukoba hadi Uganda, tutafutiwe Mv Liemba mpya kwenda Congo, Mv Mbeya ifike Malawi. Huko ndio kufungua nchi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…