Hadi Mama Dangote amekuja Mbao Tanzania, sijui anajenga ghorofa!

Hadi Mama Dangote amekuja Mbao Tanzania, sijui anajenga ghorofa!

Habari zetu kupitia JF zinafika mbali sana.

Ishukuriwe platform hii kwa kutusaidia kuonekana kupitia mijadala yenye tija hasa kwa sisi eneo letu la ujenzi na hamasa tunazopeana humu.

Tunapenda kuwajuza tu kuwa Mama Dangote ni miongoni mwa wateja wetu waliofika #MbaoTanzania kuchukua mzigo wa kutosha hivi karibuni. Tunaamini bila shaka taarifa zetu alikutana nazo humu na kuamua kutufungia safari. Siku akirudi tutamuuliza zaidi.

UMBEA KIDOGO

Sasa, kama inavyofahamika si kawaida kumdadisi mteja na ni vyema kutunza siri za wateja (na tunazitunza), lakini kiukweli imetufurahisha kuona Mama huyu amechukua mzigo wa kutosha kiasi cha kujiuliza anajenga ghorofa?

Yes, tunajua mama ni bosslady hapa mjini na tulishawahi kutambulishwa ni moja wa MDs wa Kampuni ya Wasafi. Je, kwa mzigo huu unadhani atakuwa anashusha mjengo wa aina gani, maeneo yapi?

JF ni jungu kuu. Tunasubiri ukoko!

Nilifikiri hujui wajibu wa mfanyabiashara kutunza habari za wateja kwa faragha.

Kumbe unajua, umeamua kuvunja faragha ya mteja kwa makusudi tu.
 
Nilifikiri hujui wajibu wa mfanyabiashara kutunza habari za wateja kwa faragha.

Kumbe unajua, umeamua kuvunja faragha ya mteja kwa makusudi tu.

Hapa kuna faragha gani imevunjwa? Hakuna taarifa nyeti tulizotoa. Isitoshe uzi kama huu ungeweza kuanzishwa na yeyote ambaye amemuona hapo barabarani kwa sababu huyu ni celeb.
 
Hapa kuna faragha gani imevunjwa? Hakuna taarifa nyeti tulizotoa. Isitoshe uzi kama huu ungeweza kuanzishwa na yeyote ambaye amemuona hapo barabarani kwa sababu huyu ni celeb.
Taarifa kwamba Mama Dangote anajenga na kaja kununua mbao kwako ni nyeti. Hata wewe umejua hilo, ndiyo maana ukajihami kuongelea habari za siri za wateja.

Habari ya kujitetea kwa kusema "uzi kama huu ungeweza kuanzishwa na yeyote" ni sawa na mwizi aliyeiba, halafu anajitetea kwa kusema "mtu yeyote angeweza kuiba".

Huo si utetezi, hapo umekubali umefanya kitu.

Hujui kama huyo mama, ambaye ni mwingi wa habari, anajenga hiyo nyumba kinyemela hataki watu fulani wajue. Umemuanikia habari zake hapa umma ushajua. Kama kuna watu wanamdai washajua, kama kuna wezi wanatafuta mtu wa kumuibia washajua, kama kuna ndugu kupe wanapanga kufuata watu kuwa ombaomba washajua. Ushamuharibia.

Ni hivi, kwa mfanyabiashara wa level yako, ile list tu ya nani ni mteja wako ni list inayotakiwa kulindwa.

Siyo kwa kulinda faragha ya mteja tu. Hata kwa kuilinda biashara yako.

Kwa sababu mpinzani wako wa kibiashara anaweza kuisoma thread hii, akamtafuta huyo mama, akamtongoza kibiashara, akamchukua asiwe mteja wako tena.
 
Kwa hii familia ilivyo wala sitostaajabu wakienda buguruni na kupiga picha pale wauza mbao wanapashusha mizigo yao na kuja kuaminisha watu vinginevyo.
Na haitokuwa ajabu pia uzi huu ukawa umeandikwa na mmoja wa machawa wao. Maana upande mmoja mtu anakwambia anatunza siri ya mteja, upande mwingine anamuanika bibi wa watu na bahama yake.
 
Taarifa kwamba Mama Dangote anajenga na kaja kununua mbao kwako ni nyeti. Hata wewe umejua hilo, ndiyo maana ukajihami kuongelea habari za siri za wateja.

Habari ya kujitetea kwa kusema "uzi kama huu ungeweza kuanzishwa na yeyote" ni sawa na mwizi aliyeiba, halafu anajitetea kwa kusema "mtu yeyote angeweza kuiba".

Huo si utetezi, hapo umekubali umefanya kitu.

Hujui kama huyo mama, ambaye ni mwingi wa habari, anajenga hiyo nyumba kinyemela hataki watu fulani wajue. Umemuanikia habari zake hapa umma ushajua. Kama kuna watu wanamdai washajua, kama kuna wezi wanatafuta mtu wa kumuibia washajua, kama kuna ndugu kupe wanapanga kufuata watu kuwa ombaomba washajua. Ushamuharibia.

Ni hivi, kwa mfanyabiashara wa level yako, ile list tu ya nani ni mteja wako ni list inayotakiwa kulindwa.

Siyo kwa kulinda faragha ya mteja tu. Hata kwa kuilinda biashara yako.

Kwa sababu mpinzani wako wa kibiashara anaweza kuisoma thread hii, akamtafuta huyo mama, akamtongoza kibiashara, akamchukua asiwe mteja wako tena.

Huu mtazamo hatukubaliani nao, japo tunauheshimu.

1. Mantiki ya kusema uzi ungeweza kuanzishwa na yeyote ni kutokana na muktadha wa mteja, hadhi yake na jambo lenyewe. Isitoshe, kuja kununua mbao hakufanya siri ndio maana unaona hata video imerekodiwa akiwa comfortable hivyo kwake si tatizo.

2. Sera yetu haina uoga na washindani, sana sana tunashirikiana nao japo kwa tahadhari. Hivyo kutaja orodha ya wateja au mtu mwenye ushawishi kama Mama Dangote kwetu ni fahari kwa sababu inadhihirisha kuwa tunaaminika na hatuna ubabaishaji kama wauza mbao wengine.

Mwisho kabisa, tunaamini kwenye kutangaza mazuri ya wateja badala ya mabaya yao. Hatuoni tatizo wala athari ya kibiashara kwetu wala kwa mteja wetu kwa kuonesha kufurahia mafanikio yake.

Karibu Ujenge Nasi. Mbao zipo za kutosha.
 
Kwa hii familia ilivyo wala sitostaajabu wakienda buguruni na kupiga picha pale wauza mbao wanapashusha mizigo yao na kuja kuaminisha watu vinginevyo.
Na haitokuwa ajabu pia uzi huu ukawa umeandikwa na mmoja wa machawa wao. Maana upande mmoja mtu anakwambia anatunza siri ya mteja, upande mwingine anamuanika bibi wa watu na bahama yake.

Kwa vile tunaheshimu faragha, hatutachapisha risiti za malipo/manunuzi. Lakini hiki ulichokiandika si kweli, ukweli wake ni kinyume chake.
 
Ni kutangaza indirect coz huyo Mama ni maarufu,mbona wateja wengine huleti habari zao?

Basi hilo si lengo letu, tulitaka kuhamasisha wengine kufanya mambo yenye tija kama alilolifanya. Umaarufu wake unasaidia kufikisha ujumbe kwa haraka.

Pitia nyuzi zetu uone kazi ambayo tumekuwa tukifanya kuhamasisha.
 
Huu mtazamo hatukubaliani nao, japo tunauheshimu.

1. Mantiki ya kusema uzi ungeweza kuanzishwa na yeyote ni kutokana na muktadha wa mteja, hadhi yake na jambo lenyewe. Isitoshe, kuja kununua mbao hakufanya siri ndio maana unaona hata video imerekodiwa akiwa comfortable hivyo kwake si tatizo.

2. Sera yetu haina uoga na washindani, sana sana tunashirikiana nao japo kwa tahadhari. Hivyo kutaja orodha ya wateja au mtu mwenye ushawishi kama Mama Dangote kwetu ni fahari kwa sababu inadhihirisha kuwa tunaaminika na hatuna ubabaishaji kama wauza mbao wengine.

Mwisho kabisa, tunaamini kwenye kutangaza mazuri ya wateja badala ya mabaya yao. Hatuoni tatizo wala athari ya kibiashara kwetu wala kwa mteja wetu kwa kuonesha kufurahia mafanikio yake.

Karibu Ujenge Nasi. Mbao zipo za kutosha.
Tuna tofauti kubwa ya kifalsafa na hatuwezi kuelewana. Labda makosa yangu nakupa kanuni katika ulimwengu wako usio na kanuni.

A million flies eat shit, they can't be wrong. Who am I to tell them otherwise?

Stage ya kujenga nyumba nilishamaliza miaka mingi sana.

Kutoka nyumbani Dar es salaam mpaka kimataifa New York City.
 
Back
Top Bottom