KING MIDAS
JF-Expert Member
- Dec 1, 2010
- 8,589
- 16,936
Brilliant moveNa huyu machinga hakuwa mwingine Bali alikua Ni rafiki yake George..
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Brilliant moveNa huyu machinga hakuwa mwingine Bali alikua Ni rafiki yake George..
Well uko vizuriKESI YA MZEE MNYOKA 22
Mnyoka Sasa alirudi nyumbani huku akiamini ule utetezi wake kidogo ungesaidia kuwatia Hamasa viongozi ya kuweza kumpa haki yake, kutokana na Hali ngumu ya maisha Mzee Mnyoka Sasa aliamua kuuza baadhi ya vitu vyake pale Ndani ili apate hela ya kujikimu, aliuza baskeli yake Phoenix kwa shilingi elfu 75,
Alimpa mkewe mama Monica elfu 35 na nyingine akabaki nazo,
Mzee Mnyoka Sasa aliacha kabisa kwenda kanisani hata Ile siku moja kwa mwezi, hakuona umuhimu Tena wa kukutana na Padri John,
Mtoto wake James nae aliamua kumsaidia baba yake kwa kufanya vibarua pale mgodini, James Sasa aliweza kurudi na shilingi elfu 15 au 10 kila siku, ambapo alimpa mama yake ahifadhi,
Mzee Mnyoka hakupenda mwanae afanye kazi pale Mgodini, lakini Sasa hakuwa na namna yoyote Ile,
Alijisikia vibaya kuona badala mwanae angekuwa twisheni huko , Sasa yupo na wavuta bangi, na majambazi pale mgodini,...
Hakuwa na namna zaidi ya kumsisitiza tu kuwa Makini,
"Mambo haya yataisha tu,"
Mzee Mnyoka alikua akimwambia mwanae
************
Oscar yeye aliwahi mapema kabisa akajichanganya na wanafunzi pale getini, alijua kuwa lazima Kuna watu watakuja kumchukua Swalehe hivyo alikua makini kutazama mtu ambaye angetoka na Swalehe,
Wakati Pablo na mwenzake wanaingia,
Huku wamevaa vizibao vya Pilika Online TV, Oscar aliwapiga jicho,
Kama mpelelezi mzoefu alihisi Jambo kwenye muonekano wa Pablo, jinsi alivyoongea na jinsi alivyokua Oscar alikataa kuwa huyu Ni mwandishi tu,
Na wakati Pablo anainama kutoa vifaa vyake kwenye begi, ndipo Oscar alifanikiwa kuona bastola kiunoni mwa Pablo,
"Kumbe Ndio wewe!"
Oscar alijisemea Sasa akirudi nyuma Hadi kwenye piki piki yake, aliyokuja nayo,
Alishajua hawawezi kufanya tukio pale, Ni kweli baada ya muda Pablo alitoka na mtu wake kazi ikawa ndogo tu kwa Oscar kuwafuatilia,
Gari haikuelekea ubungo badala yake walinyoosha Kama wanaelekea mwenge, na ilipofika barabara ya shekilango wakasimama kwenye mataa,
Oscar alikua karibu nao kabisa, na kutokana na msongamano jioni idadi ya piki piki na magari ilikua kubwa hivyo Pablo asingeweza kufikiri kufuatiliwa ,
Gari iliendelea ilipofika sinza madukani, wakachukua barabara ya Uzuri
Halafu walipofika kwamtogole Gari wakaingia kulia,
Mwendo wa dakika 6 hivi wakatokea kwenye nyumba moja, Oscar akajifanya kuwapita kidogo Kisha akasimama kwa mbali kidogo, ilishakua saa moja na dakika kadhaa na giza lilikuwepo kwenye sehemu ambazo Hakuna taa, Oscar alijibanza na Kunyata pole pole, hakukua na geti , Oscar alinyata tu kuelekea kwenye Ile nyumba Kisha akatega sikio,
"Ngoja nimpigie, kuwa tushampata dogo"
Alisema Pablo.
"Ndio tunae hapa tunakusikiliza,
Ehh,
Ndio,
Sawa"
Pablo alikua anaongea na Tito,
"Anasema tumalize kazi halafu tuhakikishe Hakuna anayegundua , "
Pablo alimwambia mwezake,
Sasa sikia tunamaliza kazi halafu tutajua pa kumuweka,
Ni wakati huo Sasa Oscar alishusha Kofia yake inayofunika uso Kisha akafungua mlango pole pole,
Kwa kasi ya ajabu aliwatokea na hakuwapa muda wa kutafakari aliachia risasi mbili na sekunde kadhaa Pablo na mwenzake wakawa maiti pale pale,
Sasa alijaribu kumuamsha Swalehe lakini bado alikua amepoteza fahamu, alimbeba na kutoka nae nje begani Kisha akakumbuka kumsachi, alitoa simu yake na bahati mbaya ilikua na nywilla, hivyo akatoa line moja na kuweka kwenye simu yake Kisha akajaribu kukadiria namba moja wapo ya mtu wa karibu Ni wakati anajaribu kupiga Mara simu ikaita,
"Oya Kipanya vipi mbona hurudi Mwana? Si unajua tuna assignment kesho..."
Oscar alimkatisha,
"Sikiliza njooni hapa kwa mtogole mwenye simu Yuko hapa amezimia, njooni mtakuta karibu na mnara hapa kushoto nje ya nyumba,
Yeah, ukishuka sinza madukani unachukua uzuri road, kwamtogole unaingia barabara ya kulia Kama mita 200 hivi kwenye mnara wa simu kushoto Kuna nyumba ya vigae haina geti hapo nje mtamkuta"
Oscar alirudi kwenye piki piki yake akasubiri baada ya nusu saa Sasa zilizifika piki piki zaidi ya 4 wakamchukua Swalehe,.
Kesho yake Tito alimuita Oscar
"Yule dogo ameshindikana, Pablo na mwenzake wamekutwa wameuwawa na dogo Yuko hospitali, Sasa sijajua kitu gani kimetokea Ila Sasa nakupa kazi hiyo wewe,
Kammalize huyo mpuuzi pengine akawa amejua kitu fulani "
Alisema Tito
"Yuko hospitali gani kwani"
Oscar alimuuliza Tito
"Sijajua bado lakini tutajua muda si mrefu, shida ni kuwa tayari wanasiasa wameshalichukulia Hili suala tayari, hebu ona,"
Tito aliongea akimkabidhi "tablet" yake aangalie video
"Sisi Kama upinzani tutasimama na Swalehe, tunajua wapo viongozi hawataki kukosolewa, Sasa Bwana mdogo aliuliza swali dogo tu lile tayari wanataka kumuua, tayari nishaongea na Kamanda wa mkoa atoe majibu kuhusu jaribio Hili la mauaji ya mwanafunzi"
Alisema Mheshimiwa Farida, mbunge wa Kawe, wa chama Cha upinzani, huku akiwa amezunguukwa na wanahabari
"Duh Sasa hapa Mzee itakua ngumu kidogo kwa siku hizi maana chochote kibaya kikimtokea dogo itaonekana Kuna mkono wa mtu hebu tufikirie njia nzuri zaidi"
Alisema Oscar akimrudishia simu yake,
"Ngoja nimpigie kamanda Niongee nae"
Alisema Tito Kisha akabonyeza simu yake Tena,
Aliongea kwa dakika tano Kisha akatabasamu,
"Imeisha hii twende zetu Oscar"
Alisema Tito huku wakielekea kwenye Gari
Simu ya Oscar ilitikisika kidogo kuashiria ujumbe mfupi umeingia,
"Leo ni uingereza vs Panama mechi ya kirafiki usikose mechi hii kwenye screen kubwa pale kinondoni Pub saa 1 usiku "
Oscar aliangalia namba iliyotuma iyo sms Kisha akatabasamu!
***********
Iliundwa kamati ndogo ya watu watatu kuchunguza kesi ya Mzee Mnyoka,
Walifika nyumbani kwake asubuh na mapema, walianza kumhoji mkewe Kisha wakahoji na majirani kuhusu tabia na mwenendo wa Mzee Mnyoka, Kisha wakamaliza na Mzee Mnyoka mwenyewe,
"Kiukweli sisi hatujui Kama uliiba au la , sisi tunachuguza tu kujua ukweli, Kisha tutapeleka taarifa yetu kwenye Ofisi ya Kijiji, usijali Mzee Mnyoka kamati itatenda haki, Kama hukuiba Basi usiwe na wasi wasi, Ila tu uelewe itachukua muda sana"
Alisema mwenyekiti wa kamati,
Mzee Mnyoka Sasa aliona huu Ni "uzwazwa" kusubiri kesi isiyo na macho Wala masikio halafu imsubirishe huku watoto wake wakishindwa kwenda shule!
Aliamua Sasa liwalo na liwe aliingia chumbani kwake na kujifungia Kisha akatoa simu yake Ile aliyokua ameificha Kisha akapiga namba fulani aliyoelekezwa,
Namba haikupatikana,
Ni wakati anataka kuirudisha ndipo ikaita,
"Mzee Mnyoka Kuna jipya? "
Ilisikika sauti ya upande wa pili,
Mzee Mnyoka alitambua sauti ya Oscar alimueleza kwa ufupi kuhusu zuio la kuuza kahawa yake kwa kesi ambayo alikua hahusiki nayo
"Nitajie majina ya hao viongozi wa Kijiji"
Alisema Oscar ,
Mzee Mnyoka alimtajia
"Okay Sasa Mzee Niko bize kidogo hawa wote watahusika baadae kwasasa kwa ajili ya mahitaji yako na watoto wako kwenda shule, tutafanya namna, nakushauri jifanye mjinga wasikilize wanachokuambia ili tusiwakurupushe kwa ajili ya Ile inshu yetu, niamini Mzee serikali inatambua mchango wako, sema lazima Kuna Mambo ya kiitifaki yanachelewesha , kesho kutwa utapata msaada wa Pesa unaohitaji
Alisema Oscar Kisha akakata simu,
Mzee Mnyoka aliirudishia sehemu yake Kisha akatoka kwa bahati mkewe hakuwepo,
********
Oscar Sasa alikua amemaliza kuongea na Mzee Mnyoka Kisha akapiga simu mahali fulani huku akitaja jina la Mzee Mnyoka na Kijiji alicho na baadhi ya vitu Kisha akaingia kwenye Gari kwenda Kinondoni Pub,
Alifika Kama saa moja kasoro hivi Kisha akatafuta kiti na kukaa,
Ni baada ya dakika tano alikuja machinga akiwa anauza mikanda ya suruali, na viatu vya kiume, Alikua akipita meza moja baada ya nyingine mpaka alipokua Oscar ,
Alitoa Ile mikanda na viatu na Kisha akatoa kiatu kimoja kumpa Oscar ajaribishe,
Oscar alichukua kile kiatu na kukitazama,.
"Nipe mwenzake"
Alisema Kisha akapewa mwenzake
Na akapeana mkono na yule "muuzaji"
"Asante broo"
"Boya wewe, muone Sasa"
Alijibu Oscar,
Kwani ndani ya viatu vile kulikua na ujumbe ambao Oscar alikua ameomba aletewe kuhusu zile nyaraka alizokua ameiba kwa Tito
Na huyu machinga hakuwa mwingine Bali alikua Ni rafiki yake George..
Sawa namba mbona siioni ?Asante mkuu,
Nitakutafuta chukua namba yangu hapo
Oukey asante.Post namba #92
Asante mumie
Thanks maa