Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kuna tukio nataka nifanye Sasa hizi mbinu ni muhimu Sanaa saanUnataka uiuze ndugu dalali!!
Bado bhana🤣🤣🤣
Mzee Mnyoka anaweza kujikuta anaingia tena matatizoni kama atamkaribisha huyo mgeniKESI YA MZEE MNYOKA 35
Bwana Johnson aliandaliwa Gari maalum ambalo angepanda pamoja na Tito na walinzi wake wawili, huku Gari nyingine ikiwa na walinzi waliobaki pamoja na Oscar
Na Kisha wageni wengine walifuata kwenye magari mengine, kwa hivyo ilitengeneza msururu mdogo hivi uliokua na magari Kama nane ,
Kutoka uwanja wa Ndege , msururu ulinyoosha Kati Kati ya mji ambapo kulikua na hotel ya Twiga ambapo ndipo Mr Johnson pamoja na watu wake walikua wametafutiwa
Oscar alitulia nyuma kabisa akiwa na walinzi Hawa kadhaa ambao wote hawakujishughulisha nae kila mmoja alikua na hamsini zake, Kuna wakati Gari ilipunguza mwendo kidogo au kusimama kidogo Basi wale walinzi wangehamaki na kuweka silaha zao, kwa hivi wakati mwingine Oscar alitamani kucheka,
Lakini yeye alifahamu kuwa kanuni ya kwanza ya Mambo ya ulinzi Ni kutilia Shaka kila kitu,
Waliendelea na Safari na kufika Hoteli ya Twiga salama.
Tito alimsindikiza mgeni wake mpaka kwenye chumba chake Kisha akarudi nyumbani kwake kupumzika.
************
Bwana Bill nae alikua anapanga mipango yake, akili yake ilimuambia kuwa baada ya kazi hiyo nzito Kwisha anaweza akasahaulika, lakini si kusahaulika tu Bali hata kupotezwa kabisa,
Na hivyo alihakikisha kazi hii anaifanya kwa uwezo mkubwa, asingeweza kutoa jasho lake kwa miaka yote Ile halafu faida wapate wengine,
Sasa mkakati wake uliiva kichwani mwake,
Bwana Bill au Kama walivyokuwa wanamuita "Carlos" wakaimfananisha na jambazi hatari na mlanguzi wa madawa ya kulevya,
Unaweza kusema tofauti yao ilikua rangi tu!
Lakini akili zao zilikua karibu kabisa kufanana,
Mkakati wake aliokua ameundaa aliamini lazima utaawacha mabosi zake Hawa mikono kichwani,
Sasa alikumbuka zoezi ambalo aliambiwa alifanye wiki moja iliyopita alipokutana na Tito,
Zoezi lenyewe ilikuwa kuandaa magari mawili yanayofanana kwa ajili ya kuondoka na mzigo nyumbani kwa Tito kupeleka uwanja wa Ndege,
Ndipo sasa yeye akandaa Magari matatu, huku moja akilificha mahali anapojua yeye,
Kisha magari mawili akayaleta mpaka mgodini Kinjeki kusubiri siku ya tukio,
Tayari mabox ambayo yalitakiwa kupeleka mzigo mpaka nyumbani kwa Tito yalishaandaliwa,
Mzigo huu ulitakiwa kuondoka na Bwana Bill siku chache zijazo mpaka nyumbani kwa Tito ambapo angeunganisha na mizigo mingine Kisha kupakia kwenye ndege,
Kwanza kabisa Bwana Johnson alifanya mazungumzo Rasmi na waziri wa nishati Bwana Tito,
Maongezi haya yalikua mubashara kabisa kupitia vyombo vya habari na Tito alisema kwa niaba ya serikali kuwa baada ya Bwana Johnson kumaliza ziara yake wataalamu wake watatoa taarifa Rasmi kuhusu kupatikana kwa urenium ama la,
Waziri Tito alisisitiza kuwa serikali iko bega kwa bega na kampuni hiyo ili kufanikisha mipango yote kwa ajili ya manufaa ya taifa,
"Kwahiyo Kama nilivyosema, mradi huu utakuwa na mafanikio makubwa endapo kiasi urenium kidogo kitagunduliwa, Dunia inabadilika siku hizi tutapata nishati ya uhakika ya umeme, tutapata mapato , tutapata wawekezaji wengi na mambo mengine kwahiyo Mimi niseme watanzania tuwe watu wa kuvuta subra Mambo mengi mazuri yanakuja"
Alimaliza hotuba yake Bwana Tito huku akipeana mikono na Bwana Johnson kwa ajili ya kumaliza kipindi.
***************
Kati Kati ya jiji la Dar es salaam
Oscar alikua na rafiki yake George wakimalizia kupanga mipango yao ,
Walikubaliana George atangulie kijijini akaandae mazingira ili kwamba Oscar akienda na Tito kazi iwe nyepesi,
Alimpa maelezo yote muhimu na watu wa kufanya nao kazi kwa siku zote atakazokuwa pale Kijijini,
"Tumalize hii inshu Kaka na Bila Shaka baada ya hapa sasa naweza kutulia angalau niangalie maisha mengine"
Alisema Oscar
"Kaka hujawahi kusema hivyo kabisa, tumefanya kazi ngumu, lakini daima hujawahi kutamani kupumzika!"
Alisema George
"Unajua nimewaza Sana na sisi Ni Binadamu pia lazima tuishi Kama wengine , we nenda naamini tutamaliza salama"
Alisema Oscar wakati huo alitoa Simu yake baada ya kutingishika kuashiria ujumbe mfupi uliingia,
Aliifungua na ilikua Ni ujumbe kupitia WhatsApp
"Kesho nakuja bongo"
Ujumbe huo ukitoka kwa Joyce,
Sasa kwa Mara ya kwanza Oscar akahisi kukosa amani,
Bila kujielewa akajikuta anaanza kumfikiria Joyce,
Aliwaza sekunde kadhaa Kisha akamjibu,
"Kwanini? Bado hujamaliza hata mwezi?"
"It's an emergency, we will talk"
Alijibu Joyce akimaanisha Ni dharula, wataongea akija,
"Huyu mtoto anakuja kufanya nini?"
Aliwaza Oscar akiingia kwenye Gari lake na kurudi nyumbani kwa Tito.
*******************
Mzee Mnyoka akiwa ofisini kwake , sasa wiki hii alipokea wageni wa kutosha, kuanzia waandishi wa redio, magazeti na hata wageni mbali mbali wa serikali,
Hivyo wakati anaelezwa Kuna mgeni mwingine yupo nyumbani kwake anamsubiri, Mzee Mnyoka hakuwa na haraka ya kurudi nyumbani,
Hata hivyo alishapokea wageni wengi nyumbani na ofisini, na tayari cheo Cha mwenyekiti kilianza kumkaa vizuri,
Mzee Mnyoka alirudi nyumbani kwake na kumkuta mgeni wake,
Tofauti na wageni wote mgeni huyu aliomba sehemu ya kujihifadhi kwa muda wa siku tano,
Yeye alidai alitoka shirika lisilo la kiserikali na alikua anafanya shughuli kwa kujitolea na alikua mafunzoni na kazi yake ya kwanza ilikuwa Ni kuripoti matukio hayo ya ziara ya Bwana Johnson na hivyo anaomba msaada wa Kijiji kwa mwenyekiti,
Mzee Mnyoka alitoka kuongea na mkewe Kisha wakakubaliana wampe chumba Cha James kwani hata hivyo siku tano zisingekuwa nyingi.....
Maliza MkuuTunakaribia mwisho wadau!!
Nipo apa kipenzi
BAADA YA SIKU CHACHE>>>>>>>>>>>>>