MY SOULMATE SEHEMU YA 15.
Produced by : Equatorstory Specials.
############# Tulipo ishia ###########
Nickson amesimama hotelini karibu na geti akimsubiri Bertha atoke uwani. Mbele ya Nickson alipo simama magari mawili yalisamama mbele ya Nickson ambayo ni ya mumewe wake Bertha, Mzee Mandoto alishuka.
****** Twende sasa ***********
Mandoto : "Nickson nakuona!."
Nickson : "Nyie ni kina nani na mnapakije gari mbele yangu hapa sio parking bwana."
Mandoto : "Hahahahaha ina maaana hunijui mimi ni nani?"
Nickson : "We ni nani kwani?".
Wakati Nickson ana bishana nao yule mpelelezi alikuwa akimzunguka kwa nyuma kuelekea mgongoni kwake.
Mandoto : "Usiwe na kiburi wewe." Alisema akimpiga Nickson ngumi ya uso!
Nickson alitaka kupigana amrushie Mandoto ngumi wakati huo mpelelezi yupo nyuma yake akamgusa Nickson shingoni na Nickson alizimia gahfla.
Mpelelezi : "Oya tumuingize kwenye kwenye gari fasta tuondoke."
Mara ghafla Bertha alikuja na walinzi wakikimbilia kwenye eneo la tukio.
Mlinzi : "We mnafanyaje hapo?"
Mandoto : "Achana naye tuondoke sitaki kesi tuta mrudia."
Mandoto alisema huku akijiandaa kupanda gari waondoke lakin akawa ana mtizama Bertha . Mpelelezi na huyo mtu wa watatu wakao panda kwenye gari mbio mbio. Wakaondoka wakati walinzi wanafika hilo tukio walisha anza kuondoka wakimwacha Nickson akiwa amezimia.
Bertha : "Nickson Nickson..."
Bertha ali ita bila mafanikio aki jaribu kumuamsha. Walinzi walimchukua Nickson na kwenda kumpa huduma ya kwanza na baada ya masaa kama mawili Nickson alizinduka akiwa na maumivu makali ya shingo na kichwani alitaka kulala tu. Bertha alitafuta usafiri akampeleka mpaka chumbani kwake Bertha ili aweze kumuhudumia.
******************
Ni asubuhi ya siku inayo fuata. Boss Sambeke anaenda kukutana na Rita wa chuo cha kina Nickson kwa ajili ya maongezi.
Rita : "Habari za asubui Boss nakuona ume nenepa kidogo."
Boss : "Hhaaha ata mi enyewe naona wazidi kungara.". Walisema hayo wakikumbatiana.
Rita : "Asante Boss."
Boss : "Haina shida kabisa eeenh bhana au una mtu nini?"
Rita : ''Hapana niambie Boss unajua nime ji iba ety?"
Boss : "Sasa Binti nataka tuongee swala moja bhana"
Rita : "Ndio nakusikiliza.."
Wakati Boss haja anza kuoongea alikuja waiter waka agiza kifungua kinywa.
Boss : "Kuna huu mradi bhana nataka ni pate hiyo 'tenda' hapo"
Rita : "Tenda gani hiyo?". Alisema aki sogeza kichwa mbele kidogo asikie kwa makini.
Boss : "Ya kutengeneza aplikesheni ya kuhifadhi notes."
Rita : "Ah mbona umechelewa."
Boss : "Kivipi?"
Rita : "Kuna vijana walikuja na kitu kama hicho hicho.."
Boss : "Weweee embu nielezeee."
Rita : "Wakaka flani hivi walikua wanaitwa ....... Nickson na Eric."
Boss : "Enhee ikawaje?". Boss aliuliza kana kwamba hajui kinachoendelea.
Rita : "Ndio tena Dr Massoud ali ipenda sana wakakubaliana millioni 150 nafikiri watakua na kikao week ijayo."
Boss : "Wewe!!"
Rita : "Ndio kwa hiyo ume chelewa Boss tafuta nyingine tuna haja ya mifumo mingi sana!"
Boss : "Sasa hapo ndo nataka niongee na wewe ramani."
Rita : "Niambie mkuu."
Boss : "Mimi nataka niichukue hiyo nafasi hiyo nataka kui iba!"
Rita : "Kivipi mimi sijakwelewa"
Boss : "Yani nataka huyo asiuze huo mfumo hapo chuoni".
Rita :"Utafanyaje wakati mfumo aliuleta na unafanya kazi tayari wewe muda wa kwenda kuunda upya una pata wapi au unao tayari?"
Boss : "Hehehh hilo lisikupe shaka jambo dogo sana!"
Rita : "Eti eeh?".
Boss : "Ninao vijana wa tano wamekuwa waki unda huu mfumo karibumi mwezi sasa na wanafanya kazi vyema sana!"
Rita : "Sasa una dhani hapo mimi nina mchango gani?"
Boss : "Nataka ukawa vurugie mambo sema hata huo mfumo ali uiba alipo kuwa ana fanya kazi kwangu."
Rita :"Weweeee. Sio vizuri bhana mimi nikigundulika nitafutwa kazi."
Boss : "We shida yako nini utakosa hela?"
Rita : "Ndio una dhani nitaishije huku?. Hizi nguo sitoeza kumudu wala hata hivi viatu siwezi kuvaa tena!."
Boss : "Najua we mdada upo hali ya juu unasemaje ukifanikisha nkakupa zawadi?"
Rita : "Zawadi gani nayo weza kuiweka kazi yangu kwenye mashaka hiyo."
Boss : "Ntakunulia gari la millioni kumi alafu nakupa na zako kumi!."
Rita : "Mhhh we utanitapeli."
Boss : "Sasa pale ofisin si una toa cheki wewe?. Ukipewa wote tuna enda benki tunatoa hela nakupa hela yako kesi imeisha!."
Rita : "Wewe mi sikuamini!."
Boss : "We una taka hela au unataka ukweli eti we binti?"
Rita : "Mimi hela zinaongea sijaja huku kuremba macho!"
Boss : "Sawa we fanya hivyo tafuta akili."
Rita : "Hahah iyo kazi ndogo huyo rafiki yake Eric anapenda wanawake!."
Boss : "Kwa hiyo tuna fanyaje?."
Rita : "Hiyo niache anayo namba yangu namuona anajileta leta tu kwangu."
Boss : "Ah wapi wewe sema umemuelewa!"
Rita : "Kiasi ni mtanashati kwa hiyo nita pata faida mbili ntampata yeye ntapata na hela . Weweeeee chezea mimi?."
Boss : "Safi wewe mwanamke una akili nafikiri tuishie hapa ngoja niende kazini."
Rita : "Haya ngoja na mimi niende."
Boss : "Sawa kwaheri mamilo."Rita aliamka akaondoka huku Boss amekaaa akimtazama anavyo ondoka.
Rita aliondoka akiwa na mawazo je afanye hili swala kweli anajua ata muumiza Nickson lakini bila ya hivyo hatoweza kupata hizo millioni 20 labda afanye kazi miezi 24 ndo atafikisha hiyo hela . Lakini kwani Nickson ana muhusu nini?. Wakati akiwa ofisini anawaza hili swala mara ghafla Eric alipiga simu.
Rita :"Haloo". Alisema kwa sauti ya upole inayovutia kweli.
Eric : "Poa mambo mermbo?"
Rita : "Mi mzima bhaba." . Rita alisema akiwa anasokota nywele zake kana kwamba Eric yupo hapo.
Eric : "Mh mama hiyo sauti duh."
Rita : "Kwani ina nini?".Rita aliongeza maringo kwenye simu na alivyo kuwa amekaa.
Eric : "Hamna ume amkaje wewe mdada?".Eric alianza kuongea kwa sauti ya chini na ya utulivu kidogo.
Rita : "Salama tu sijui wewe jamani."
Eric : "Mi nipo salama kwanza unajua nini?"
Rita : "Nini niambie basii."
Eric : "Nimekuota mwenzio."
Rita : "Jamani umeota nini afu na mimi nitakwambia niliota nini."
Eric : "Nimeota umekuja kwangu kunisalimia wakati naenda kukufuatia soda mgeni wangu nikateleza nika anguka mpaka nilishtuka usingizini. Saivi nimeamka tu kwenda kukua angalia sebleni nikakukosa."
Rita : "Jamani usijali nitakuja jamani pole. Usihofu nitakuja!"
Eric : "Kweli?. Unajua nimemiss kukuona nitumie basi picha yako."
Rita : "Yani ume ni miss afu unataka picha tu? Wewe hujanimis wewe."
Eric : "Jamani sasa nitafanyaje?"
Rita : "Kama umeniss kweli mi sikutumii picha nataka tukutane."
Eric : "Unasema?". Eric alijikuta aki inuka ghafla kwa mshangao akipaza na sauti.
Rita : "Hutaki au?."
Eric : "Hapana nataka nataka. Saaa ngapi tuna kutana?". Eric alijua hapa asha daka mtu mwingine wa kumchezea.
Rita : "Saa moja jioni nitakwambia badae hoteli gani nataka kwenda au unaogopa hela?"
Eric : "Ivi una nionaje? Mimi nina hela ety umesahau kwamba nakaribia kupata mamillioni hapo? ".
Rita : "Sawa baadae."
Eric baada ya kukata simu alisamama na aka anza kushangilia ushindi wake kwa kucheza akiwa na kaptula yake ya kulalia.
Nickson aliamka baada ya kulala masaa kadhaa kwa sababu ya dawa pia alizopewa yamkini yalimuongezea usingizi. Aliamka akajikuta yupo chumbani kwa bertha aka angalia huku na huku na hakumwona Bertha popote alipo . Alikuta ujumbe kwenye simu yake kutoka kwa Bertha. "Samahani imenibidi niondoke.". Nickson hakuamini mach yake kama Bertha ameondoka aka anagalia ujumbe mwingine akakuta bertha amemwandikia. "Nime enda sokoni kuongeza vitu kuna chai na mikate niliokwandalia kula hiyo nafikiri ntakua nisharudi."
Nickson alishuha pumzi alidhania kuwa Bertha ameondoka kweli lakini aka dhani kua yamkini ni kweli ameondoka?.
Nickson akanywa chai na akatoka kwenda kuoga ili kujiweka vizuri . Alipo toka kuoga alikuta Bertha amerudi kutoka alipokuwa amekwenda.Bertha alimkubatia akilia kwa uchungu.
Bertha :"Jamani pole nisamehe jamani mkaka wa watu nikuweka majaribuni na huna hatia."
Nickson : "Mambo madogo sio kosa lako."
Bertha : "Jamani pole ".Bertha aliendelea kulia akiwa amemkumbatia Nickson aliekuwa akimbembeleza taaratibu.
Nickson : "Kaa hapo tuongee!."
Bertha alipunguza kulia aka keti na kufuta machozi .
Nickson : "Usilie bhana."
Bertha : "Sawa sawa. " Bertha alikuwa aki jikaza asiendelee kulia.
Nickson : "Yule ndo mume wako ulio niambia?"
Bertha :"Ndio na sijui amenipataje yule shetani."
Nickson : "Labda katumia mtandao."
Bertha : "Hapana mimi simu yangu nili iacha kwake na wala sija wasiliana na mtu. Wa kwetu ambaye anaeza kumwambia niko wapi itakuwa ametumia wapelelezi na sijui wame nipataje huku kote."
Nickson : "Inaonekana ana hela ? Mpaka kuajiri wapelelezi na wamekupata?"
Bertha : "Yule mbaba ana hela yule lakin simpendi kabisa."
Nickson :"Yani hata hela zake hutaki?."
Bertha : "Hapana Nickson tuhame hapa twende sehemu nyingine twende hata kenya nina marafiki zangu huko huko sio rahisi atupate tuta enda kujificha kijiji cha mbali ambako hamna hata umeme."
Nickson :"Usimwogope huyo hana matisho."
Bertha : "Wapi wewe umepigwa mpaka umezimia Nickson acha utani bhana."
Nickson : "Hamna sikuzimia alinipiga ngumi nikajifanya nimezimia kujitetea ."
Bertha : "Hahahahha ahahaha jamani Nickson unanifanya nicheke wewe mkaka Mungu akubariki jamani una roho nzuri sana."
Nickson : "We mwache akuje tena nitapambana nae we usimwogope bhana."
Bertha : "Nickson wacha zako yule anaeza kukua mara moja isingekua kukuwahi angeku beba Mungu ndo anajua alitaka kwenda kukufanyia nini yule Shetani."
Nickson : "Labda alitaka kwenda kuniuliza ushauri juu ya wanawake maana anaona mimi na wewe tunaelewana".
Bertha : "Hahahahahahahahaha ahahahahah ahahahaha"
Nickson : "Au alitaka kwenda kunipa hela nije nimwombee msamaha kwako huezi jua."
Bertha : "Hahahahaha bhana wewe una mambo jamani. "
Nickson : "Kawaida!."
Bertha : "Vipi umekula?."
Nickson : "Nimekunywa chai saa zile lakini pika basi maana nataka kwenda jimu nijiandae na Mr Mandoto na Mimi raundi ya pili."
Bertha : "Yani wewe. Haya ngoja nipike tule ushibe bhana."
Ilifika jioni Rita na Eric wanakutana kwa ajili ya chakula kama walivyo kubaliana. Eric amekuja amependeza kama ilivyo kawaida yake lakini Rita amechelewa kidogo. Eric yupo ana rusha macho huku na kule aki angalia amuone Rita.
Rita : "Mambo?"
Eric : "Poa umependeza!."
Rita : "Kawaida na uzuri unachangia."
Eric : "Hata mimi naona karibu nisha shika meza pale twende tukakae."
Eric aliongoza kueilekea meza na kumsogezea Rita kiti akae ndipo na yeye akaenda kukaa .
Walikaa waka piga stori hapa na pale walicheka walitumia muda kujuana na Rita ndipo alipo mwambia Eric alichokuwa ana muitia siku ya leo.
Rita : "Eric nataka nikwambie kitu .."
Eric : "Jisikie huru niambie niko hapa."
Rita : "Sijui utakubali."Alisema huku akiweka mkono wake juu ya mkono wa Eric.
Eric : "Sema mama nakupa masikio yangu yote."
Rita : "Nataka tuongee biashara."
Eric : "Enhee."
Rita : "Nataka nikwambie huku mjini akili."
Eric : "Najua."
Rita : "Sasa mimi nataka umgeuke huyo rafiki yako."
Eric : "Una sema.....????"
Rita : "Nisikilize kuna tajiri nimeongea nae anataka auzie hiyo aplikesheni chuo."
Eric : "Sasa mimi nakuablianaje wakati napata kama millioni 75 huoni kama ntakua nafanya ujinga ?"
Rita : "Sawa yule Boss amesema ataiuza kwa millioni 200 alafu mia zote ni zako."
Eric : "Enhee unataka nikubaliane na huo uongo?"
Rita : "Hapana sio uongo huyu mtu ni mashuhuri. Hana mambo ya kupinda alafu ukuibali."
Eric : "Enhee inakuaje?". Eric aliuliza akiwa ana dalili ya kuchukia kidogo.
Rita : "Tuliza jazba wangu."
Eric : "Inakuwaje?"
Rita : "Naku kubaliana na achana na mtu wangu wa aliepo Uganda nakubali niwe wako."
Eric : "Mhhhhh".
Rita : "Hiii yote itakua yako Eric."Rita ali simama aka zunguka akijionesha kwa Eric.
Eric alibaki akishangaa huku Rita akiondoka kwa madoido yote kama miss Tanzania vile. Eric hakuamini alichosikia yote yalimjia kwenye chake ghafla alibaki akiwaza millioni mia zinakuwa zake na atakuwa na RIta. Eric aliondoka na kwenda nyumbani akawaza na kuwaza akitafuta kitu cha kufanya kweli amgeuke rafiki yake kwa ajili ya hela na mwanamke?.
Itaendelea............