CK Allan
JF-Expert Member
- Aug 14, 2013
- 2,781
- 6,139
- Thread starter
- #41
MZAHA WA DAMU 03
By CK Allan
Baada ya kuichaji na kuweka sawa sasa niliingia kwenye mtandao wa facebook na kuanza kutafuta jina Ephraim, nilipitia akaunti zenye majina ya Ephraim kwamba angalau ningepata yenye picha yangu au picha ya mtu ambaye ningeweza kumfahamu
Nilipitia akaunti nyingi lakini sikuweza kuona yenye picha yangu hata hivyo nilitengeneza akaunti kwa jina la Ephraim Tito kisha nikaendelea kutafuta akaunti ya Ephraim, nakumbuka nilitafuta hadi simu ikaisha chaji nikaiweka kwenye chaji kisha nikarudi kupumzika ndani, nilijikuta nikipitiwa na usingizi na ghafla ndoto ikanijia nikajiona nimeshika ile simu na kuingia kwenye mtandao wa facebook kisha nikaenda kwenye sehemu ya kuingia na kuweka taarifa zangu
Jina la kwanza: Ephraim
Jina la pili : Tito
Jina la mwisho: Kikulwe
Tarehe ya kuzaliwa : 25/9/1987
Jinsia :me
Nilijikuta najaza hizo taarifa kwenye ile simu kisha nikatengeneza neno la siri na wakati naingia nikajikuta nastuka tena huku nikitweta
Haraka sana nilichukua kalamu na kuandika zile taarifa kisha nikachomoa ile simu haraka kwenye chaji na kuingia kwenye mtandao wa facebook, nilienda sehemu ya kutafuta marafiki na kuandika Ephraim Kikulwe, zikatokea akaunti nyingi tu nikaanza kupitia moja baada ya nyingine mara ghafla macho yangu yakatua kwenye akaunti moja hivi iliandikwa jina la Kikulwe Ephraim, nilibaki kuduwaa kwenye picha ya mtumiaji niliona picha ya mtu aliyefanana na mimi akiwa katika kiti cha ofisini hivi, sasa nilianza kutafuta kupekua na kupekua picha mbali mbali katika akaunti hiyo, niliona mara ya mwisho kutumiwa akaunti hiyo ilikua oktoba 10/2019
Huku picha ya mwisho ikiwa imepigwa nje ya jengo lilionekana kama ukumbi hivi ukiwa umepambwa huku kukiwa na maneno yalisomekana
“karibu Waziri mkuu Kongwa tunakusubiri”
Sasa sikuweza kuvumilia nilitoka nje na kwenda kuwaonyesha mzee Tito na mkewe kuhusu yale yote niliyoyaona,
“hakuna shaka huyu ni wewe na mwaka Jana mheshimiwa waziri Mkuu mama Zawadi Macha alitembelea wilaya zote kukagua miradi ya maendeleo sasa bila shaka hii ilikua mojawapo ya ziara zake” alisema mzee Tito
“kwahiyo huyu ni Mimi na kwenye hii picha hapa naona kuna watu wengine hebu subiri ..” nilisema huku nikishusha zile picha kuelekea chini
Mara niliona picha yangu tena lakini safari hii ilikua kuna mwanamke kaiweka kwenye ukurasa wake kisha akahusisha na akaunti yangu ambapo kwa lugha ya mtandao waliita “kutag” picha hii aliituma wiki chache zilizokua zimepita
“ni mwaka mmoja umepita bila uwepo wako, Nimekumis, Ofisini tumekumis, SITAACHA kukuombea Pumziko la milele akupe yeye Bwana na Mwanga wa Mbinguni akuangazie tutaonana Mbinguni”
Nilijikuta nguvu zikiniishia na kisha nikaona giza likinifunika mboni za macho yangu baadae sikuelewa tena kilichoendelea.
Nilikuja kuzinduka baadae sana huku nikiwa kitandani kwangu, niliangalia saa ilikua saa 11 jioni
Nilitoka nje na kumkuta mama Tito akiwa anapasua kuni, nilienda kumsaidia huku akiwa haamini kuniona tena nikiwa na afya njema
“mzee yuko wapi?” nilimuuliza sasa nikiwa nachukua ile shoka
“ah itakuwa yupo chumbani kwake” alisema na kabla sijajibu mzee Tito alitokea akiwa na uso wa bashasha
“Ephraim umeamka, ooh afadhali” alisema huku akichukua zile kuni zilizokwisha kupasuliwa na kuingiza ndani
Baada ya muda tulimaliza sasa na kurudi ndani,
“wakati umelala ulikua unamtaja sana Josephine , je ni nani huyu?” mzee Tito aliongea akiwa sasa ananitazama usoni
“nani Josephine? Oooh simu , simu iko wapi ile simu?” nilikimbia chumbani tena na kuchukua ile simu pale kitandani
Kisha nikaingia tena kwenye ule mtandao wa facebook
Nilitafuta ile akaunti tena na sasa wote watatu tukawa tumeduwaa
“ndio huyu, anaitwa Josephine Mpanji, namjuaaaa!” nilijikuta napiga kelele za furaha!
“huyu ni mchumba wangu, angalia hapa, sasa nilishusha chini zaidi na kuangalia picha zake mbali mbali na kulikua na picha ambayo nilikua namvalisha pete ya uchumba katika kanisa la st Gasper Dodoma, haraka nilirudi kwenye ukurasa wake na kutafuta namba ya simu kisha nikaihifadhi na sasa tukashauriana na Mzee Tito kupiga ile namba!
“kwasasa huwezi kuongea nae moja kwa moja kwakuwa huwezi kujua wale watu waliokudhuru pengine bado wanaendelea kukufuatilia hivyo tutaweka sauti ya juu kisha niongee nae mimi lakini kwanza tuandae mazingira ya namna ya kuongea nae bila kuleta taharuki” alisema mzee Tito,
tuliandaa mzingira yote ya maswali anayoweza kuuliza kisha simu ikapigwa
“halo habari ya jioni”
Ilisikika sauti ya mwanamke upande wa pili na sasa nilisikia moyo wangu ukipiga paa baada ya kusikia sauti hiyo
“ndio mimi naitwa mzee Tito Nipo Moro goro”
‘ndio mzee Tito ,sidhani kama nakufahamu” sauti ya upande wa pili ilisikika
“ni kweli , hunifahamu, nimekupigia simu kunisaidia jambo moja” alisema Tito
“ndio mzee Tito nakusikiliza” alisema
“nina kijana wangu ambapo wakati Ephraim anapata matatizo hakuwepo nchini sasa alikua na baadhi ya mizigo ambayo ametoka nayo nje ya nchi yeye anasema kuwa ameagizwa na Ephraim, sasa kwa bahati mbaya kutokana na changamoto ya Corona amewahi kuondoka na akaniachia namba hii alisema nikutafute” alisema mzee Tito huku nikimuonyeshea alama ya “dole” kuwa ameongea vizuri
“sawa mzee Tito ni mizigo gani?” aliuliza
”kwakweli hata mimi sijui, imefungwa tu kwenye boksi” alijibu mzee Tito
“sasa ulitakaje mzee Tito” aliuliza
“kwani uko wapi sasa hivi?” aliuliza mzeee Tito
“kwakweli nipo nyumbani Mbeya, baada ya Ephraim kupotea na unajua ilikua bado wiki moja tufunge ndoa, sikuwa sawa, kwahiyo nikashindwa kabisa kufanya kazi nikaomba likizo nipo tu kwakweli sielewi” sauti ilisikika upende wa pili na sasa nilishindwa kuvumilia na kujikuta nataka kumnyang’anya simu mzee Tito
“sasa mama naomba unisikilize vizuri, naomba kwanza kama hapo ulipo upo na watu usogee sehemu ambayo unaweza kuongea ukiwa mwenyewe bila kusikika
Sawa nitakupigia baada ya dakika chache
‘sasa tufanyaje?” alisema mzee Tito
“nadhani tumuamini tu hakuna namna nyingine sema usimwambie moja kwa moja maana…”
Tulikatishwa na sauti ya simu sasa Josephine alikuwa anapiga simu
“haya niambie mzee Tito” ilisikika upande wa pili
“kuna jambo inabidi ujue nadhani najua alipo Ephraim hakufa kama ambavyo unajua” alianza mzee Tito kwa upole
“unsemaje wewe mzee?, walimuua Ephraim, walimpoteza, tena kwa kisa ambacho sio cha kweli? Hakufanya Ephraim aiiiiii, aiiiiii!” alianza kulia Josephine
“ndio maana nikakupigia Josephine, ni wewe pekee ambaye unaweza kumrudisha tena katika hali yake ya kawaida,” alisema mzee Tito
“unanidanganya najua unanidanganya!’ alisema tena
“muda sio mrefu utaamini lakini nataka unihakikishie jambo moja!” alisema mzee Tito
“ndio jambo gani!”
“kwanza unihakikishie kuwa hutamwambia mtu kuhusu jambo hili halafu tutaongea zaidi juu ya nini cha kufanya” alisema Mzee Tito
“na mimi naomba unihakikishie jambo moja kwanza kabla hatujaendelea” alisema Josephine
“jambo gani?” mzee Tito aliuliza sasa akiweka simu karibu ili tusikie wote
“nataka kujua kama kweli Ephraim yuko hai”
“sawa, hii namba iko whatsap?” aliuliza mzee Tito
“ndio” alijibu
Mzee Tito alikata simu yake kisha akanigeukia,
Sawa ngoja nilichukua ile simu nakuingia chumbani na kuwasha taa kisha nikavua shati, na kurekodi video fupi nikihakikisha Josephine anaona baadhi ya makovu na alama mbali mbali mwilini mwangu ili aweze kuhakikisha kuwa mimi ni mzima wa afya kabisa lakini niliyepitia katika changamoto mbali mbali
Tulimtumia ile video kwa njia ya whatsap na baada ya muda akapiga simu
By CK Allan
Baada ya kuichaji na kuweka sawa sasa niliingia kwenye mtandao wa facebook na kuanza kutafuta jina Ephraim, nilipitia akaunti zenye majina ya Ephraim kwamba angalau ningepata yenye picha yangu au picha ya mtu ambaye ningeweza kumfahamu
Nilipitia akaunti nyingi lakini sikuweza kuona yenye picha yangu hata hivyo nilitengeneza akaunti kwa jina la Ephraim Tito kisha nikaendelea kutafuta akaunti ya Ephraim, nakumbuka nilitafuta hadi simu ikaisha chaji nikaiweka kwenye chaji kisha nikarudi kupumzika ndani, nilijikuta nikipitiwa na usingizi na ghafla ndoto ikanijia nikajiona nimeshika ile simu na kuingia kwenye mtandao wa facebook kisha nikaenda kwenye sehemu ya kuingia na kuweka taarifa zangu
Jina la kwanza: Ephraim
Jina la pili : Tito
Jina la mwisho: Kikulwe
Tarehe ya kuzaliwa : 25/9/1987
Jinsia :me
Nilijikuta najaza hizo taarifa kwenye ile simu kisha nikatengeneza neno la siri na wakati naingia nikajikuta nastuka tena huku nikitweta
Haraka sana nilichukua kalamu na kuandika zile taarifa kisha nikachomoa ile simu haraka kwenye chaji na kuingia kwenye mtandao wa facebook, nilienda sehemu ya kutafuta marafiki na kuandika Ephraim Kikulwe, zikatokea akaunti nyingi tu nikaanza kupitia moja baada ya nyingine mara ghafla macho yangu yakatua kwenye akaunti moja hivi iliandikwa jina la Kikulwe Ephraim, nilibaki kuduwaa kwenye picha ya mtumiaji niliona picha ya mtu aliyefanana na mimi akiwa katika kiti cha ofisini hivi, sasa nilianza kutafuta kupekua na kupekua picha mbali mbali katika akaunti hiyo, niliona mara ya mwisho kutumiwa akaunti hiyo ilikua oktoba 10/2019
Huku picha ya mwisho ikiwa imepigwa nje ya jengo lilionekana kama ukumbi hivi ukiwa umepambwa huku kukiwa na maneno yalisomekana
“karibu Waziri mkuu Kongwa tunakusubiri”
Sasa sikuweza kuvumilia nilitoka nje na kwenda kuwaonyesha mzee Tito na mkewe kuhusu yale yote niliyoyaona,
“hakuna shaka huyu ni wewe na mwaka Jana mheshimiwa waziri Mkuu mama Zawadi Macha alitembelea wilaya zote kukagua miradi ya maendeleo sasa bila shaka hii ilikua mojawapo ya ziara zake” alisema mzee Tito
“kwahiyo huyu ni Mimi na kwenye hii picha hapa naona kuna watu wengine hebu subiri ..” nilisema huku nikishusha zile picha kuelekea chini
Mara niliona picha yangu tena lakini safari hii ilikua kuna mwanamke kaiweka kwenye ukurasa wake kisha akahusisha na akaunti yangu ambapo kwa lugha ya mtandao waliita “kutag” picha hii aliituma wiki chache zilizokua zimepita
“ni mwaka mmoja umepita bila uwepo wako, Nimekumis, Ofisini tumekumis, SITAACHA kukuombea Pumziko la milele akupe yeye Bwana na Mwanga wa Mbinguni akuangazie tutaonana Mbinguni”
Nilijikuta nguvu zikiniishia na kisha nikaona giza likinifunika mboni za macho yangu baadae sikuelewa tena kilichoendelea.
Nilikuja kuzinduka baadae sana huku nikiwa kitandani kwangu, niliangalia saa ilikua saa 11 jioni
Nilitoka nje na kumkuta mama Tito akiwa anapasua kuni, nilienda kumsaidia huku akiwa haamini kuniona tena nikiwa na afya njema
“mzee yuko wapi?” nilimuuliza sasa nikiwa nachukua ile shoka
“ah itakuwa yupo chumbani kwake” alisema na kabla sijajibu mzee Tito alitokea akiwa na uso wa bashasha
“Ephraim umeamka, ooh afadhali” alisema huku akichukua zile kuni zilizokwisha kupasuliwa na kuingiza ndani
Baada ya muda tulimaliza sasa na kurudi ndani,
“wakati umelala ulikua unamtaja sana Josephine , je ni nani huyu?” mzee Tito aliongea akiwa sasa ananitazama usoni
“nani Josephine? Oooh simu , simu iko wapi ile simu?” nilikimbia chumbani tena na kuchukua ile simu pale kitandani
Kisha nikaingia tena kwenye ule mtandao wa facebook
Nilitafuta ile akaunti tena na sasa wote watatu tukawa tumeduwaa
“ndio huyu, anaitwa Josephine Mpanji, namjuaaaa!” nilijikuta napiga kelele za furaha!
“huyu ni mchumba wangu, angalia hapa, sasa nilishusha chini zaidi na kuangalia picha zake mbali mbali na kulikua na picha ambayo nilikua namvalisha pete ya uchumba katika kanisa la st Gasper Dodoma, haraka nilirudi kwenye ukurasa wake na kutafuta namba ya simu kisha nikaihifadhi na sasa tukashauriana na Mzee Tito kupiga ile namba!
“kwasasa huwezi kuongea nae moja kwa moja kwakuwa huwezi kujua wale watu waliokudhuru pengine bado wanaendelea kukufuatilia hivyo tutaweka sauti ya juu kisha niongee nae mimi lakini kwanza tuandae mazingira ya namna ya kuongea nae bila kuleta taharuki” alisema mzee Tito,
tuliandaa mzingira yote ya maswali anayoweza kuuliza kisha simu ikapigwa
“halo habari ya jioni”
Ilisikika sauti ya mwanamke upande wa pili na sasa nilisikia moyo wangu ukipiga paa baada ya kusikia sauti hiyo
“ndio mimi naitwa mzee Tito Nipo Moro goro”
‘ndio mzee Tito ,sidhani kama nakufahamu” sauti ya upande wa pili ilisikika
“ni kweli , hunifahamu, nimekupigia simu kunisaidia jambo moja” alisema Tito
“ndio mzee Tito nakusikiliza” alisema
“nina kijana wangu ambapo wakati Ephraim anapata matatizo hakuwepo nchini sasa alikua na baadhi ya mizigo ambayo ametoka nayo nje ya nchi yeye anasema kuwa ameagizwa na Ephraim, sasa kwa bahati mbaya kutokana na changamoto ya Corona amewahi kuondoka na akaniachia namba hii alisema nikutafute” alisema mzee Tito huku nikimuonyeshea alama ya “dole” kuwa ameongea vizuri
“sawa mzee Tito ni mizigo gani?” aliuliza
”kwakweli hata mimi sijui, imefungwa tu kwenye boksi” alijibu mzee Tito
“sasa ulitakaje mzee Tito” aliuliza
“kwani uko wapi sasa hivi?” aliuliza mzeee Tito
“kwakweli nipo nyumbani Mbeya, baada ya Ephraim kupotea na unajua ilikua bado wiki moja tufunge ndoa, sikuwa sawa, kwahiyo nikashindwa kabisa kufanya kazi nikaomba likizo nipo tu kwakweli sielewi” sauti ilisikika upende wa pili na sasa nilishindwa kuvumilia na kujikuta nataka kumnyang’anya simu mzee Tito
“sasa mama naomba unisikilize vizuri, naomba kwanza kama hapo ulipo upo na watu usogee sehemu ambayo unaweza kuongea ukiwa mwenyewe bila kusikika
Sawa nitakupigia baada ya dakika chache
‘sasa tufanyaje?” alisema mzee Tito
“nadhani tumuamini tu hakuna namna nyingine sema usimwambie moja kwa moja maana…”
Tulikatishwa na sauti ya simu sasa Josephine alikuwa anapiga simu
“haya niambie mzee Tito” ilisikika upande wa pili
“kuna jambo inabidi ujue nadhani najua alipo Ephraim hakufa kama ambavyo unajua” alianza mzee Tito kwa upole
“unsemaje wewe mzee?, walimuua Ephraim, walimpoteza, tena kwa kisa ambacho sio cha kweli? Hakufanya Ephraim aiiiiii, aiiiiii!” alianza kulia Josephine
“ndio maana nikakupigia Josephine, ni wewe pekee ambaye unaweza kumrudisha tena katika hali yake ya kawaida,” alisema mzee Tito
“unanidanganya najua unanidanganya!’ alisema tena
“muda sio mrefu utaamini lakini nataka unihakikishie jambo moja!” alisema mzee Tito
“ndio jambo gani!”
“kwanza unihakikishie kuwa hutamwambia mtu kuhusu jambo hili halafu tutaongea zaidi juu ya nini cha kufanya” alisema Mzee Tito
“na mimi naomba unihakikishie jambo moja kwanza kabla hatujaendelea” alisema Josephine
“jambo gani?” mzee Tito aliuliza sasa akiweka simu karibu ili tusikie wote
“nataka kujua kama kweli Ephraim yuko hai”
“sawa, hii namba iko whatsap?” aliuliza mzee Tito
“ndio” alijibu
Mzee Tito alikata simu yake kisha akanigeukia,
Sawa ngoja nilichukua ile simu nakuingia chumbani na kuwasha taa kisha nikavua shati, na kurekodi video fupi nikihakikisha Josephine anaona baadhi ya makovu na alama mbali mbali mwilini mwangu ili aweze kuhakikisha kuwa mimi ni mzima wa afya kabisa lakini niliyepitia katika changamoto mbali mbali
Tulimtumia ile video kwa njia ya whatsap na baada ya muda akapiga simu