Jackal
JF-Expert Member
- Apr 10, 2012
- 9,971
- 13,608
- Thread starter
- #41
NITAKUPATA TU
SEHEMU YA 034
******
CHIEF ndio jina lililosomeka juu ya kioo cha simu yake. Hakuipokea kwa wakati ule. Macho yake yaliwatizama wenzake kisha kuitizama tena simu. Sio kwamba alikuwa akiogopa kuipokea simu bali hakuwa na la kumwambia mkuu wake. Akaiacha simu iendelee kuita mpaka ilipokata. Baada ya simu kukatika, kachero yule akauandika ujumbe kwa lugha ya mafumbo na kuutuma kwa Chief. Baada ya kumaliza hilo akamgeukia dereva wa tax. "Utaendelea kuishi hapa kwa Usalama wako mpaka pale hili jambo litakapokwisha." Baada ya kusema hilo makachero wale wakatoka mle ndani tayari kwa safari ya kwenda kuwatafuta Jimmy na Suresh.
*****
Ilikuwa yapata majira ya saa tatu na nusu usiku pale teddy aliposhuka kwenye bajaj pembezoni mwa ufukwe maarufu jijini dar es salaam, ufukwe wa coco beach. Baada ya kushuka hapo akaongoza taratibu mpaka sehemu mmoja iliyojitenga pekee akakaa na kutulia. Hakuwa hapo kwa sababu ya burudani bali alikuwa pale kwa minajili ya kuipa akili yake utulivu. Mambo yaliokuwa yakiendelea yalizidi kumchanganya na kuifanya akili yake ishindwe kufanya maamuzi. Ni mara tatu amenusurika kufa kwa kupigwa risasi, mara ya nne amenusurika kufa baada ya kugeukwa na wenzake kisha kumpoteza fahamu. Mpaka muda ule hakuwa akijua ni vipi ameokolewa katika kisanga kile. Hakujua ni vipi masimba amemtoa katika kifo ambacho kilipangwa kufanywa juu yake. Ni masimba huyu huyu alijitolea kila kitu na uwezo wake kuhakikisha yeye anarudi kwenye uhai. Hakumuacha pale alipowekwa matatani. Hata pale aliposhiriki kuua familia ya Asteria, bado masimba alimpa nafasi ya kubadilika. Licha ya hayo yote bado moyo wake ulikuwa katika mtihani mzito. Aliihitaji pesa na aliuhitaji mzigo wa madawa ya kulevya alionao Masimba. Aliutaka kwa njia yoyote. Hakuhitaji mzigo ule uingie mikononi mwa serikali. Aliutaka na aliuhitaji. Licha ya kuuhitaji huko, lakini hakujua angeweza kuutoaje mikononi mwa mwanaume yule. Hilo ndio lililomfanya afike usiku ule katika fukwe zile za coco beach kujaribu kuwaza hili na lile ili kupata majibu. Kichwa chake alikiinamisha chini huku mikono yake ikiuchezea mchanga. Mawazo yalikuwa yakipishana kichwani. Kuna kipindi katika akili yake alikuwa anawaza na kujilaumu kwa nini akutane na Masimba. Pesa zikaiteka akili yake, pesa zilimfanya aisahau nafasi ya masimba moyoni mwake. Aliihitaji pesa na aliuhitaji mzigo kwa gharama yoyote. Kwa mara ya kwanza akalikumbuka jina la mtu, mtu ambaye angeweza kupanga naye na kupata majibu. Lakini hakujua angewezaje kumpata huyu mtu. Kwani ulipita muda mrefu sana pasipokuonana. Akaichomoa simu yake mfukoni na kubonyeza namba fulani. Baadae simu upande wa pili ikasikika ikiita. Sekunde tatu baadae sauti nzito ikasikika upande wa pili. " Beni Bomphe naonge."
"Teddy killer hapa naongea, nakuhitaji kwenye fukwe za coco beach muda huu kama upo hapa Mjini." Akaingea teddy kisha kukata simu bila kusubiri jibu kutoka upande wa pili. Uso wake ulikuwa kwenye tabasamu matata sana, sasa uhakika wa kuupata mzigo alikuwa nao. Akaendelea kuwaza na kuwazua, baada ya dakika kumi na tano akamuona mtu akitembea taratibu katika fukwe zile. Kijana mweupe mwenye mwili uliojengeka kimazoezi alikuwa akiangaza huku na huko kama mwenye kutafuta mtu. Teddy akainuka na kumsogelea kijana yule. Muda mfupi baadae walikuwa wamesimama wakitizamana. "Habari za masiku Beni?" Akasabahi teddy.
"Nzuri mkuu, naona nchi imetingishwa." Akajibu beni huku akiongeza na maneno kadhaa. "Yeah! Ukiwa mshenzi lazima upate malipo ya kishenzi. Akajibu teddy huku uso wake ukionyesha kujua kila kitu.
"Usiniambie unamjua alietenda hili? Akaongeza ben huku akishindwa kuuficha mshangao.
"Yeah! Namjua! Alijibu kwa kifupi kisha akamuomba Ben waongee kile ambacho amemuitia.
Kwa shingo upande ben akakubali na kufuatana na teddy mpaka sehemu waliokuwa wamekaa mwanzo. "Nipe dili mama nitoweke hapa, watu kama sisi hatuonekani ovyo." Ben akatamka akimuangalia teddy. Teddy akamueleza ben kila kitu huku akificha vichache sana. Ni maelezo ambayo yalichukua dakika kama sita hivi. Baada ya maelezo yote kutoka kwa teddy, beni akatulia huku akimuangalia Ted usoni. Baadhi ya maneno kutoka kwa teddy hayakumuingia akilini. Aliujua uhusiano wao na masimba tokea ndio kwanza wanajiunga na idara ya ujasusi. Lakini haya ambayo yanatoka kinywani kwa teddy yalimuacha na kigugumizi. "Lazima tumuondoe masimba? Hata ikibidi hata familia yake tuitumie katika kuupata huu mzigo? Ni baadhi ya kauli ambazo zilimuacha Ben akiwaza.
"Kwahiyo unataka masimba asafirishwe? Hatimaye akauliza tena.
"Yeah nahitaji kuupata mzigo, kwahiyo ni lazima tumsafirishe. Pakitokea ugumu familia yake itahusika katika kutupa huu mzigo. Sina huruma wala mapenzi katika hili." Akajibu teddy huku kila kitu kikionyesha kuwa hakuwa akitania. Hilo pia halikutegemewa na ben. Lakini kwa kuwa aliitaka pesa Aliamua kukubaliana na teddy kuifanya kazi ile ambayo ilikuwa hatari. Alimjua masimba na aliujua ugumu wake. Kitendo tu cha kusikia kile alichokifanya kwa waziri mkuu ilimthibitishia ni kiasi gani ameingia kwenye vita nzito. Akamuangalia teddy kwa sekunde kadhaa kisha kwa sauti ya kujiamini akasema. "Nitaifanya hii kazi kwa moyo wangu wote. Ikiwa nitamuua masimba ama familia yake, basi damu yao itakuwa juu yako. Ikiwa ataniwahi mimi basi nadhani damu yangu pia itakuwa juu yako." Baada ya kuongea hilo akainuka na kuanza kuondoka huku hofu ikiwa imeutanda moyo wake. Hakupenda kupambana na mtu kama masimba, sio kwa kuogopa lakini alikuwa akimheshimu kama mtu aliyemfanikishia naye kufika pale.
*******
Alikuwa mfano wa simba aliyejeruhiwa, hakutaka kuwapa nafasi maafisa usalama kumtambua kama yeye ndiye aliyehusika na mauaji ya Waziri mkuu. Hilo likimlazimu masimba kutokulala kabisa kabisa akiwasaka Suresh, Jimmy na Mwamvita. Walikuwa watu pekee waliokuwa wakilifahamu hili. Alitaka kumalizana nao kwanza kabla ya kuangalia nini anatakiwa kukifanya. Usiku huu alikuwa maeneo ya sinza afrika sana akitizama kama anaweza kuwaona wabaya wake. Alikuwa ametulia akiendelea kunywa taratibu bia yake. Macho yake yalikuwa yakimtizama kila mmoja ambaye alikuwa akiingia ndani ya bar ile. Muda mwingi alitumia kuitazama saa yake. Muda ulikuwa ukisonga bila kumuona mtu wala kupata chochote kutoka kwa Dee plus. Kazi aliyompa ya kumfuatilia teddy bado haikuzaa matunda. Bado hakumuamini tena teddy. Aliutambua utamani wa teddy na hata mabadiliko yake. Licha ya kumtoa mkononi mwa kifo bado alijua ama kuhisi teddy anaweza kubadilika tena. Hilo likamfanya Masimba mpe dee plus kazi hiyo, kazi ya kuijua mienendo ya teddy. Hilo likampa ugumu wa kuamini kama hakuna chochote. Akauvuta muda akisubiri chochote. Punde mlio wa sms kwenye simu yake ukamgutusha kutoka mawazoni. Mkono ukazama mfukoni na kuibuka na simu. Sekunde moja iliitosha kuufungua ujumbe ule na kuusoma. "Wadudu wawili wamekaa ufukweni wakidonoa chini." Ulisomeka ujumbe. Ilikuwa lugha aliyoielewa, lugha ambayo ilimpa hamu ya kuwajua hao wadudu wawili na kile wanacho kidonoa.
"Ustawi" alijibu kwa neno hilo huku akiirudisha simu mfukoni. Lakini hazikupita hata dakika moja simu yake ikaita. Akaitoa tena mfukoni na kuangalia namba ya mpigaji. "CHIEF" ndio jina lililosomeka. Roho ikapaaa na damu kumsisika. Akapeleka kidole kwenye kitufe cha kijani kisha kuipeleka simu sikioni.
"Nakuhitaji nyumbani muda huu." Baada neno hilo simu ikakatwa. Masimba akaduwaa.hakuamini kupigiwa simu na mkuu wake wa kazi hasa ukiangalia jinsi alivyokuwa akisakwa. Niende? Lilikuwa swali pekee alilojiuliza. Lakini kabla hajapata jibu la swali lake akamuona Dee plus akiingia. Akampa ishara ya kumtaka asogee.. Dee Plus akasogea kisha bila kuongea kitu mfano wa picha na kumkabidhi Masimba

SEHEMU YA 034
******
CHIEF ndio jina lililosomeka juu ya kioo cha simu yake. Hakuipokea kwa wakati ule. Macho yake yaliwatizama wenzake kisha kuitizama tena simu. Sio kwamba alikuwa akiogopa kuipokea simu bali hakuwa na la kumwambia mkuu wake. Akaiacha simu iendelee kuita mpaka ilipokata. Baada ya simu kukatika, kachero yule akauandika ujumbe kwa lugha ya mafumbo na kuutuma kwa Chief. Baada ya kumaliza hilo akamgeukia dereva wa tax. "Utaendelea kuishi hapa kwa Usalama wako mpaka pale hili jambo litakapokwisha." Baada ya kusema hilo makachero wale wakatoka mle ndani tayari kwa safari ya kwenda kuwatafuta Jimmy na Suresh.
*****
Ilikuwa yapata majira ya saa tatu na nusu usiku pale teddy aliposhuka kwenye bajaj pembezoni mwa ufukwe maarufu jijini dar es salaam, ufukwe wa coco beach. Baada ya kushuka hapo akaongoza taratibu mpaka sehemu mmoja iliyojitenga pekee akakaa na kutulia. Hakuwa hapo kwa sababu ya burudani bali alikuwa pale kwa minajili ya kuipa akili yake utulivu. Mambo yaliokuwa yakiendelea yalizidi kumchanganya na kuifanya akili yake ishindwe kufanya maamuzi. Ni mara tatu amenusurika kufa kwa kupigwa risasi, mara ya nne amenusurika kufa baada ya kugeukwa na wenzake kisha kumpoteza fahamu. Mpaka muda ule hakuwa akijua ni vipi ameokolewa katika kisanga kile. Hakujua ni vipi masimba amemtoa katika kifo ambacho kilipangwa kufanywa juu yake. Ni masimba huyu huyu alijitolea kila kitu na uwezo wake kuhakikisha yeye anarudi kwenye uhai. Hakumuacha pale alipowekwa matatani. Hata pale aliposhiriki kuua familia ya Asteria, bado masimba alimpa nafasi ya kubadilika. Licha ya hayo yote bado moyo wake ulikuwa katika mtihani mzito. Aliihitaji pesa na aliuhitaji mzigo wa madawa ya kulevya alionao Masimba. Aliutaka kwa njia yoyote. Hakuhitaji mzigo ule uingie mikononi mwa serikali. Aliutaka na aliuhitaji. Licha ya kuuhitaji huko, lakini hakujua angeweza kuutoaje mikononi mwa mwanaume yule. Hilo ndio lililomfanya afike usiku ule katika fukwe zile za coco beach kujaribu kuwaza hili na lile ili kupata majibu. Kichwa chake alikiinamisha chini huku mikono yake ikiuchezea mchanga. Mawazo yalikuwa yakipishana kichwani. Kuna kipindi katika akili yake alikuwa anawaza na kujilaumu kwa nini akutane na Masimba. Pesa zikaiteka akili yake, pesa zilimfanya aisahau nafasi ya masimba moyoni mwake. Aliihitaji pesa na aliuhitaji mzigo kwa gharama yoyote. Kwa mara ya kwanza akalikumbuka jina la mtu, mtu ambaye angeweza kupanga naye na kupata majibu. Lakini hakujua angewezaje kumpata huyu mtu. Kwani ulipita muda mrefu sana pasipokuonana. Akaichomoa simu yake mfukoni na kubonyeza namba fulani. Baadae simu upande wa pili ikasikika ikiita. Sekunde tatu baadae sauti nzito ikasikika upande wa pili. " Beni Bomphe naonge."
"Teddy killer hapa naongea, nakuhitaji kwenye fukwe za coco beach muda huu kama upo hapa Mjini." Akaingea teddy kisha kukata simu bila kusubiri jibu kutoka upande wa pili. Uso wake ulikuwa kwenye tabasamu matata sana, sasa uhakika wa kuupata mzigo alikuwa nao. Akaendelea kuwaza na kuwazua, baada ya dakika kumi na tano akamuona mtu akitembea taratibu katika fukwe zile. Kijana mweupe mwenye mwili uliojengeka kimazoezi alikuwa akiangaza huku na huko kama mwenye kutafuta mtu. Teddy akainuka na kumsogelea kijana yule. Muda mfupi baadae walikuwa wamesimama wakitizamana. "Habari za masiku Beni?" Akasabahi teddy.
"Nzuri mkuu, naona nchi imetingishwa." Akajibu beni huku akiongeza na maneno kadhaa. "Yeah! Ukiwa mshenzi lazima upate malipo ya kishenzi. Akajibu teddy huku uso wake ukionyesha kujua kila kitu.
"Usiniambie unamjua alietenda hili? Akaongeza ben huku akishindwa kuuficha mshangao.
"Yeah! Namjua! Alijibu kwa kifupi kisha akamuomba Ben waongee kile ambacho amemuitia.
Kwa shingo upande ben akakubali na kufuatana na teddy mpaka sehemu waliokuwa wamekaa mwanzo. "Nipe dili mama nitoweke hapa, watu kama sisi hatuonekani ovyo." Ben akatamka akimuangalia teddy. Teddy akamueleza ben kila kitu huku akificha vichache sana. Ni maelezo ambayo yalichukua dakika kama sita hivi. Baada ya maelezo yote kutoka kwa teddy, beni akatulia huku akimuangalia Ted usoni. Baadhi ya maneno kutoka kwa teddy hayakumuingia akilini. Aliujua uhusiano wao na masimba tokea ndio kwanza wanajiunga na idara ya ujasusi. Lakini haya ambayo yanatoka kinywani kwa teddy yalimuacha na kigugumizi. "Lazima tumuondoe masimba? Hata ikibidi hata familia yake tuitumie katika kuupata huu mzigo? Ni baadhi ya kauli ambazo zilimuacha Ben akiwaza.
"Kwahiyo unataka masimba asafirishwe? Hatimaye akauliza tena.
"Yeah nahitaji kuupata mzigo, kwahiyo ni lazima tumsafirishe. Pakitokea ugumu familia yake itahusika katika kutupa huu mzigo. Sina huruma wala mapenzi katika hili." Akajibu teddy huku kila kitu kikionyesha kuwa hakuwa akitania. Hilo pia halikutegemewa na ben. Lakini kwa kuwa aliitaka pesa Aliamua kukubaliana na teddy kuifanya kazi ile ambayo ilikuwa hatari. Alimjua masimba na aliujua ugumu wake. Kitendo tu cha kusikia kile alichokifanya kwa waziri mkuu ilimthibitishia ni kiasi gani ameingia kwenye vita nzito. Akamuangalia teddy kwa sekunde kadhaa kisha kwa sauti ya kujiamini akasema. "Nitaifanya hii kazi kwa moyo wangu wote. Ikiwa nitamuua masimba ama familia yake, basi damu yao itakuwa juu yako. Ikiwa ataniwahi mimi basi nadhani damu yangu pia itakuwa juu yako." Baada ya kuongea hilo akainuka na kuanza kuondoka huku hofu ikiwa imeutanda moyo wake. Hakupenda kupambana na mtu kama masimba, sio kwa kuogopa lakini alikuwa akimheshimu kama mtu aliyemfanikishia naye kufika pale.
*******
Alikuwa mfano wa simba aliyejeruhiwa, hakutaka kuwapa nafasi maafisa usalama kumtambua kama yeye ndiye aliyehusika na mauaji ya Waziri mkuu. Hilo likimlazimu masimba kutokulala kabisa kabisa akiwasaka Suresh, Jimmy na Mwamvita. Walikuwa watu pekee waliokuwa wakilifahamu hili. Alitaka kumalizana nao kwanza kabla ya kuangalia nini anatakiwa kukifanya. Usiku huu alikuwa maeneo ya sinza afrika sana akitizama kama anaweza kuwaona wabaya wake. Alikuwa ametulia akiendelea kunywa taratibu bia yake. Macho yake yalikuwa yakimtizama kila mmoja ambaye alikuwa akiingia ndani ya bar ile. Muda mwingi alitumia kuitazama saa yake. Muda ulikuwa ukisonga bila kumuona mtu wala kupata chochote kutoka kwa Dee plus. Kazi aliyompa ya kumfuatilia teddy bado haikuzaa matunda. Bado hakumuamini tena teddy. Aliutambua utamani wa teddy na hata mabadiliko yake. Licha ya kumtoa mkononi mwa kifo bado alijua ama kuhisi teddy anaweza kubadilika tena. Hilo likamfanya Masimba mpe dee plus kazi hiyo, kazi ya kuijua mienendo ya teddy. Hilo likampa ugumu wa kuamini kama hakuna chochote. Akauvuta muda akisubiri chochote. Punde mlio wa sms kwenye simu yake ukamgutusha kutoka mawazoni. Mkono ukazama mfukoni na kuibuka na simu. Sekunde moja iliitosha kuufungua ujumbe ule na kuusoma. "Wadudu wawili wamekaa ufukweni wakidonoa chini." Ulisomeka ujumbe. Ilikuwa lugha aliyoielewa, lugha ambayo ilimpa hamu ya kuwajua hao wadudu wawili na kile wanacho kidonoa.
"Ustawi" alijibu kwa neno hilo huku akiirudisha simu mfukoni. Lakini hazikupita hata dakika moja simu yake ikaita. Akaitoa tena mfukoni na kuangalia namba ya mpigaji. "CHIEF" ndio jina lililosomeka. Roho ikapaaa na damu kumsisika. Akapeleka kidole kwenye kitufe cha kijani kisha kuipeleka simu sikioni.
"Nakuhitaji nyumbani muda huu." Baada neno hilo simu ikakatwa. Masimba akaduwaa.hakuamini kupigiwa simu na mkuu wake wa kazi hasa ukiangalia jinsi alivyokuwa akisakwa. Niende? Lilikuwa swali pekee alilojiuliza. Lakini kabla hajapata jibu la swali lake akamuona Dee plus akiingia. Akampa ishara ya kumtaka asogee.. Dee Plus akasogea kisha bila kuongea kitu mfano wa picha na kumkabidhi Masimba










