Hadithi ya mashimo ya mfalme Sulemani

mkuu hongera sana na shukrani kwa kutuletea hii simulizi ya kale nilikuwa nipita kimya kimya lakini leo nikaona nikupe heshima yako hongera sana
 
Ahsante mkuu blackstarline

Tunakupata kwa uzuri
 
SURA YA KUMI NA TATU

Pole pole bila haraka, majeshi yale matatu yalitambaa kutujia.

Walipofika karibu kadiri ya mwendo wa hatua mia sita, jeshi lile la katikati lilisimama chini ya kilima kungojea majeshi yale mawili mengine yatuzunguke mfano wa duara. Yaani walikusudia kutushambulia kutoka mahali patatu kwa mara moja.


Bwana Good akasema, ‘Laiti ningekuwa na bomu ningelifuta eneo lote hili katika muda wa dakika ishirini.’ Bwana Henry akajibu, ‘Kweli, lakini hatuna bomu, basi ya nini kulililia!

Wewe, Quatermain, afadhali ujaribu kumpiga Yule mtu mrefu, nadhani ndiye mkubwa wao.’

Basi nilitwa bunduki yangu, nikangoja hata Yule mtu amejitenga na watu wake akawa pamoja na mtumishi wake tu; nikalala nikaegemeza bunduki juu ya mwamba nikapiga, nikitumai kumpiga kifuani.


Lakini moshi ulipo inuka nilimwona amesimama salama ila mtumishi wake amelala amekwisha kufa. Basi Yule mkubwa mara akastuka akawakimbilia wenzake. Bwana Good akasema,’Una shabaha, bwana! Umewatisha sana.’


Basi nilichukizwa, maana sipendi kukosa shabaha mbele za watu, nikainua bunduki tena, nikaelekeza kwa Yule mkubwa tena, nikapiga. Mara akatupa juu mikono yake akaanguka kifudifudi.

Askari wetu walivyo ona hivyo walipiga makelele ya furaha, maana walifanya kama ni ishara njema kubashiri kwamba tutashinda, na jeshi lile la mkubwa Yule aliyeuawa wakarudi nyuma wamefadhaika.

Sasa Bwana Henry na Bwana Good wakatwaa bunduki zao wakaanza kupiga na kwa kadiri tulivyoona nadhani tuliua askari sita au wanane kabla hawajatoka katika eneo la bunduki zetu.

Mara tulipoacha kupiga tulisikia makelele makubwa yanatoka upande wa kushoto, na mara tukasikia makelele yanatoka upande wa kulia vile vile, tukajua kuwa majeshi yale mawili mengine yanatushambulia.

Wale adui waliokuwa mbele yetu walitawanyika kidogo waliposikia makelele hayo wakashika njia ya kuja kilimani, wakienda mbio kidogo na huku wakiimba kwa sauti ya kiume naya mkazo.

Tulipiga bunduki zetu kwa taratibu wakati walipokuwa wakija, na Ignosi vile vile akapiga bunduki mara kwa mara, tukawaua wengine.

Lakini hatukuweza kuwazuiya, ikawa kama; mtu apigaye bahari kujaribu kuzuia mawimbi.

Walizidi kuja na huku wanapiga kelele na kufanya vishindo kwa mikuki yao; sasa walikuwa wakiwafukuza watu wetu tuliowaweka mbele katika miamba chini ya kilima huku wakipanda pole pole wasije wakachoka.

Safu ya kwanza ya watu wetu wa mbele iliwekwa katikati ya kilima, na safu ya pili ilikuwa nyuma yao kadiri ya hatua sitini, na safu ya tatu ilikuwa katika ukingo wa kilima kwa juu.

Wakazidi kuja mbele wakiitana kilio chao cha vita, ‘Twala!Twala!Twala! Pigeni! Pigeni!’
Na watu wetu wakaitika, Ignosi!Ignosi! Pigeni! Pigeni!’

Wakawa karibu sasa, wakaanza kutupiana visu, vikameremeta nyuma na mbele, na mara kwa kelele kubwa, wakakutana.

Huku na huku mashujaa walipambana wakapigana, na watu wakaanguka kama majani ya miti wakati wa kiangazi; lakini kwa haraka nguvu za wale adui waliokuwa wakitushambulia zilisukuma nyuma safu yetu ya kwanza mpaka walikutana na safu ya pili.
 
Hapo vita vilikuwa vikali sana, lakini tena watu wetu walisukumwa nyuma, mpaka baada ya dakika ishirini tu toka mwanzo wa vita, safu yetu ya tatu ilikuwa katika vita.

Lakini sasa adui zetu walikuwa wamechoka, na tena wamepata hasara kubwa ya watu waliouawa na waliopata majeraha, nao hawakuweza kuvunja ukuta ule wa mikuki ya safu yetu ya tatu. Kwa muda kidogo askari wote wakapambana huku na huko katika vita, na mwisho wake hautambulikana.
Bwana Henry akatazama vita huku macho yake yaking’aa, ndipo alipojitosa katikati ya vita bila kusema neno, na Bwana Good akamfuata.

Mimi nilikaa pale pale . Askari walimwona Bwana Henry akiingia vitani wakaanza kuitana, ‘Ndovu ameingia! Pigeni!Pigeni!’

Kutoka hapo mwisho wa vita ulijulikana. Wale waliokuwa wakishambulia walisukumwa nyuma hatua kwa hatua kushuka kilima mpaka wakawakimbilia wale waliowekwa nyuma kuwasaidia, huku wamefadhaika sana.

Na mara tarishi alifika kutuarifu kuwa jeshi lile lililoshambulia kwa upande wa kushoto vile vile limesukumwa nyuma.

Nilianza kufurahi na kufikiri kuwa tumeshinda, kumbe, tukaona watu wetu wa upande wa kulia wanafukuzwa, nao wanatujia kwa kasi wakisukumwa nyuma na adui, ikawa kama maadui wameshinda upande huo.

Ignosi aliyekuwa kasimama karibu nami, alitambaua hali ya mambo ilivyo mara moja, akatoa amri upesi sana.

Mara vikosi vya Wajivu, waliokuwa wamewekwa kama akiba, vikajipanga. Ignosi akatoa amri nyingine na mara nikajiona nimo katikati ya vita vikali kuwashambulia maadui wanaotujia.nilijificha nyuma ya mwili mkubwa wa Ignosi kadiri nilivyoweza, nikafuata.

Katika muda kidogo tulikuwa tukipita kwa nguvu katikati ya askari wetu waliokuwa wakikimbia, nao mara walijipa moyo wakajipanga tena nyuma yetu, na hapo sijui nini kilichotokea.

Ninachoweza kukumbuka ni kusikia kelele kubwa na kuona jitu kubwa sana mbele ya macho yangu, linanijia na mkuki wake juu umetapakaa damu.

Lakini nilikuwa tayari, maana nilitambua kuwa nikisimama tu lazima nitauawa, basi nilijitupa chini kwa ghafla, na kwa kuwa alikuwa akija kwa nguvu hakuweza kujizuiya, akajikwaa akaanguka.

Kabla hajaweza kuondoka tena nilikuwa nimekwisha nyanyuka na nikampiga kwa bastola yangu.

Baada ya kitambo kidogo niliangushwa na mtu nikawa sina habari tena ya shambulio hilo. Nilipoteza fahamu tena nilijiona nimelala kilimani tena na Bwanab Good ameniinamia akininyunyuzia maji, akaniuliza, ‘Je, rafiki, sasa waonaje?’ Nikanyanyuka nikajipapasa kabla ya kumjibu, nikasema, ‘Sasa naona nafuu.’

Akasema, ‘Alhamdulilahi! Nilipoona wanakuchukua nilijiskia uchungu sana; nilifikiri kuwa umekwisha kufa.’ Nikamuuliza vita vimekwendaje, akaniambia, ‘Maadui wamesukumwa nyuma kila mahali.

Lakini hasara ni kubwa mno. Watu wa upande wetu waliokufa na kujeruhiwa wapata elfu mbili, na kwa upande wao nadhani hawapungui elfu tatu. Tazama huko!

Nikatazama nikaona mistari mirefu ya watu wanakuja wanne pamoja. Nikaona kuwa wale waliojeruhiwa wamechukuliwa katika machela.
 
Basi tuliondoka hapo kwa haraka tukapita upande wa pili wa kilima, tukamwona Bwana Henry ameshika shoka lake la vita mkononi, na Ignosi na Infadus na wakubwa wachache wengine wanasemezana na kushauriana.


Bwana Henry akasema, ‘Ah, nimefurahi umekuja. Ignosi anataka kufanya mambo nami sifahamu maneno yake.

Nadhani kuwa ingawa tumekwisha kuwashinda maadui kwa sasa, lakini askari wengine wengi wanaletwa kumsaidia Twala, naye anadhani anawaweka watuzunguke ili tusipate chakula, na Infadus anasema kuwa maji yetu yapo karibuni kuisha.’


Infadus akasema, ‘Ndiyo, kweli. Chemchem haitoki maji ya kutosha watu wengi, na sasa yanapungua. Kabla ya kuingia usiku, wote tutaona kiu. Sikiliza, Makumazahn, wewe ndiye mwenye akili, pengine umeona vita vingi katika nchi nyingine, yaani ikiwa wanafanya vita katika nyota.

Twambie tufanye nini? Twala ameleta watu wengi kuchukua mahali pa wale waliokufa. Twala amekwisha pata akili.

Mwewe hakufikiri kukuta kuku tayari! Lakini tumekwisha muuma kifua; ana hofu kutupiga tena. Lakini hata na sisi tumejeruhiwa naye atangoja hapo mpaka tufe; atatuzunguka kama anavyofanya chatu anapokamata swala. Naye atapigana vita vya kusubiri tu.’
Nikasema, ‘Vema nimekusikia.’


Basi akaendelea, akasema, ‘Basi Makumazahn, waona sisi hapa hatuna maji, na chakula tulichonacho ni kidogo tu, nasi lazima tuchague kukaa na kufa kama simba anayekufa katika pango lake kwa njaa, au kujaribu kutoka kwa njia ya kaskazini au tumrukie Twala na kumshambulia kwa nguvu zetu zote.


Ndovu (yaani Bwana Henry ) ni shujaa, maana leo amepigana kama nyati aliyetegwa, na askari wa Twala walianguka mbele yake kama mtama mchanga unaopigwa na mvua yam awe; yeye asema ni afadhali tuwarukie; lakini ni desturi ya ndovu kushambulia.


Je, wewe Makumazahn, wasemaje? Wewe sungura mwerevu aliyekwisha ona mambo mengi na kupenda kumumiza adui kutoka kwa nyuma. Shauri la mwisho ni Ignosi aliye mfalme, maana ni hiari ya mfalme kupigana vita, lakini na tusikilize shauri lako, Ee Makumazahn.

Na vile tusikilize shauri la Bougwan, yeye mwenye jicho linalong’aa’. (Maana hilo ni jina walilomwita Bwana Good.)

Nikamuuliza Ignosi, ‘Je, Ignosi, wasemaje?’ lakini yeye, ambaye alikuwa mtumishi wetu lakini sasa amevaa kiaskari na kuonekana kuwa mfalme kabisa, akajibu, ‘Hapana, tafadhali wewe sema, nami niliye mtoto tu kwako kwa akili zangu, nitasikiliza maneno yako.’


Basi kuombwa hivyo, nikashauriana na Bwana Henry na Bwana Good, kisha nikawapa kauli yangu. Ikawa ya kuwa sisi tumekwisha tiwa mtegoni, na tena maji yanatupungukia, ni afadhali tuwashambulie askari wa Twala.


Tena nikashauri kuwa yafaa kuanza shambulio mara moja kabla ya kukauka majeraha yetu, na tena kabla askari wetu hawajakata tamaa kwa kuona wingi wa askari wa Twala.

Nikasema kuwa tukingoja, huenda wakubwa wengine wa upande wetu wakaghairi na kwenda kufanya suluhu na Twala, na hata kututia katika mikono yake.

Basi kauli yangu ikapokewa kwa furaha; na Wakukuana walipendezwa sana na shauri langu. Lakini neno la mwisho likawa kwa Ignosi aliye mfalme, tukamgeukia tusikilize asemavyo.

Baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu kidogo akifikiri , alisema, ‘Rafiki zangu watu weupe; na Infadus mjomba wangu, na wakubwa wangu; nimekaza moyo wangu. Nitampiga Twala leo hivi na kubahatisha nguvu zetu.


Sikilizeni, hivi ndivyo namna nitakavyowapiga. Sasa ni saa sita na watu wote wanakula na kupumzika baada ya vita. Baadaye kidogo jua linapoanza kushuka, wewe mjomba wangu pamoja na jeshi lako uende pamoja na jeshi lingine hata pale penye mteremko, na mara Twala atakapowaoneni ataleta jeshi lake kupigana.


Lakini njia hii nyembamba na kwa hivyo jeshi linaweza kuja kikosi kikosi; na kwa hivyo wataangamizwa kikosi kikosi, na macho ya askari wote wa Twala yatakuwa yanatazama vita hivi vikali.

Na rafiki yangu Ndovu (yaani Bwana Henry) atafuatana nawe, na Twala akiona shoka lake kubwa linang’aa na kumeremeta katika safu ya kwanza ya Wajivu, moyo wake utafifia.


Mimi nitafuatana na jeshi la pili litakalokufuata wewe, yaani, ikiwa wewe utaangamizwa , basi mfalme atabaki, na watu watapigana kwa ajili yake. Na Makumazahn ataandamana pamoja na mimi.’

Infadus akasema, ‘Vema, Ewe Mfalme.’ Ignosi akaendelea tena akasema, ‘Na hapo askari wote wa Twala wanapotazama vita vikali, nataka jeshi la tatu lililobaki ligawanyike sehemu tatu.

Sehemu moja itatambaa kwenda kwa upande wa kushoto wa adui na kuwarukia, na sehemu ya pili watatambaa kwenda upande wa kulia, nami nikiona kuwa askari wa pande zote mbili wako tayari kuwarukia watu wa Twala, basi mimi nitashambulia kwa katikati, na tukiwa na bahati, tutashinda.


Nasi kabla jua halijashuka kabisa tutakuwa tumekaa kwa amani na raha katika mji wa Loo.

Na sasa tule tujiweke tayari, na wewe, Infadus, utengeneze mambo yote tusije tukasahau hata kitu kimoja, na Bougwan (yaani Bwana Good) yeye na aandamane na wale watakaokwenda kwa upande wa kulia apate kuwatia wakubwa nguvu kwa jicho lake linalong’aa.’

Basi matengenezo hayo yote yakafuatwa kwa upesi sana, yakaonyesha ustadi wa uaskari wa Wakukuana. Katika muda wa saa moja, watu wote walikuwa wamekwisha kula na majeshi yaligawanyika tayari.

Baadaye kidogo Bwana Good akatujia mimi na Bwana Henry akasema, ‘Kwaherini, rafiki zangu. Mimi nakwenda kwa upande wa kulia, na sasa nimekuja ili tupeane mikono maana labda hatutaonana tena.’ Basi tukapeana mikono kwa kimya sana na uzuni.
 
Mambo ni moto[emoji39]
 
SURA YA KUMI NA NNE

Baada ya kupita muda kidogo zile sehemu mbili zilizoamrishwa kwenda pande za kushoto na kulia za kilima zilikuwa zimekwisha kwenda kwa hadhari sana zisije kuonekana na wapelelezi wa Twala. Tukakaa kwa muda wa nusu saa ili kuwapa nafasi ya kufika mahali pao.


Ndipo jeshi lile liitwalo Wajivu na jeshi lile lingine lililoamrishwa kuandamana nalo, yaani lililoitwa Wanyati, yakaondoka.

Watu wa majeshi yote mawili walikuwa wazima kabisa na wenye nguvu, maana Wajivu hawakuingia katika vita mpaka mwisho walipowafukuza maadui, na wale Wanyati vile vile walikuwa wamewekwa nyuma katika vita asubuhi, na kwa hivyo hawakuingia katika vita.


Infadus alikuwa mkubwa wa askari wa zamani sana, naye alitambua sana faida ya kuwatia moyo watu wake, wakati wa shida; basi akatoa hotuba kwa maneno mazuri ya mashahiri ya vita, aka waeleza namna walivyopewa heshima kwa kuwekwa wa kwanza katika vita, na kwa kupewa Yule mtu weupe aliyetoka katika nyota afuatane nao.


Akaahidi kuwapa zawadi kubwa ya ng’ombe na kuwapandisha vyeo wote watakaotoka salama katika vita, ikiwa majeshi ya Ignosi yatashinda .


Kazi ya jeshi hili ilikuwa kupigana na kikosi baada ya kikosi cha askari wa Twala katika ile njia nyembamba chini mpaka waishe kuangamizwa kabisa, au mpaka wale waliozunguka wapate nafasi ya kuwarukia maadui.


Lakini hawakufadhaika hata kidogo wala sikuona dalili ya hofu katika sura zao. Walikuwa wakienda kukutana na mauti kwa hakika, walikuwa wakitoka katika nuru ya mchana kwa milele, nao walikuwa na nguvu za kwenda bila kutetemeka.


Basi Infadus alimaliza hotuba yake akasema, ‘Tazameni mfalme wenu! Nendeni mkapigane na kufa kwa ajili yake, maana huu ndio wajibu wa mashujaa wanaume, na yeye atakayeogoba kufa kwa ajili ya mfalme wake, na yeye atakayempa kisogo adui yake, na alaniwe na kufedheheshwa.


Nyinyi wakubwa na askari tazameni mfalme wenu! Sasa nyenyekeeni mbele ya nyoka mtukufu, mnifuate mimi na Ndovu (yaani Bwana Henry), nitawaonyesha njia mpaka tufike katika moyo wa majeshi ya Twala.’

Kwanza ikawa kimya kabisa kwa kiasi cha dakika moja, kisha sauti ikatoka askari waliposongana mbele yetu, ikawa kama sauti ya mawimbi ya bahari yakivuma kwa mbali, na ilikuwa sauti ya vishindo vya mikuki ikigongana na ngao.


Pole pole sauti ikazidi na kuzidi mpaka ikawa kama ngurumo inayozunguka katika milima, ikajaza hewa yote kwa mawimbi makubwa ya sauti.

Kisha ikapungua pole pole tena, ikapungua mpaka ikafa, ndipo wakapaaza sauti kuu ya kumwamkia mfalme.


Ignosi akapokea kuamkia kwao kwa kuinua juu shoka lake la vita, na Wajivu wakajipanga wakatoka kwa taratibu ya watatu watatu, na kila mstari ulikuwa na askari elfu moja, wakubwa wao mbali.

Walipokuwa wamekwisha kwenda hatua mia sita, Ignosi akajiweka mbele ya Wanyati nao wakajipanga hivyo hivyo wakatoka, nami niliandamana nao.


Tulipofika ukingo wa kilima, Wajivu walikuwa wamekwisha teremka nusu ya kilima, nao wanakaribia ile njia nyembamba. Watu wa kambi la Twala sasa wakaanza kushughulika sana, na kikosi baada ya kikosi wakaja mbio wapate kufikia ile njia kabla Wajivu hawajawahi.


Wajivu walipokwisha kufika kwenye mahali palipokuwa papana kidogo, wakasimama kimya, nasi, yaani Wanyati, tulisimama nyuma yao kadiri ya hatua mia moja tuwe tayari kuwasaidia.


Sasa tulipata nafasi kutazama jeshi la Twala, tukaona kuwa hawajapata wengine wa kuwasaidia tangu vita vya asubuhi.


Askari wa Twala walipofika karibu na kupanda kwenye njia ile nyembamba, wakasita, maana waliona kuwa kikosi kimoja tu kinaweza kupita kwa mara moja, na tena waliona Wajivu mashujaa na watukufu wa majeshi yote ya Wakukuana wamesimama juu ya miamba isiyopitika wanangoja tayari kuwazuia.


Kwanza walisita, kisha wakasimama; hawakuwa na moyo wa kuonana na kupigana na Wajivu waliosimama thabiti hivi.

Lakini mkubwa mmoja akatoka amevaa manyoya marefu ya mavazi ya mkubwa wa jeshi, amefuatana na wakubwa wengine na watumishi, nikamdhania kuwa ndiye Twala mwenyewe.
 
Akatoa amri, na kikosi cha kwanza wakatoa sauti kubwa wakawashambulia Wajivu, na wao walisimama kimya tayari kuwapokea mpaka walipofika karibu kadiri ya hatua arobaini wakaanza kutupiana visu vyao vikubwa.


Ndipo wakawarukia kwa kishindo kikubwa huku mikuki juu, na majeshi wakaonana na kupigana vita vya kufa, Mara kishindo cha ngao zikigongana kilikuwa kama ngurumo , na uwanda wote ukameremeta kwa mianga ya nuru iliyotoka mikuki iliyong’aa.

Huku na huku wakapambana, wakachomana chomana mikuki yao, lakini si kwa muda mrefu.

Pole pole ikawa kama wale wanaoshambulia wanapungua, ndipo kwa jitihada kuu Wajivu wakawakanyaga kama wimbi kubwa linavyopanda juu ya mwamba baharini.

Kikosi kile kiliangamizwa kabisa, lakini katika Wajivu, mistari miwili tu ilibaki, mmoja umekwisha, yaani theluthi ya kikosi iliangamizwa.


Basi wakajipanga tena wakasongana pamoja, na tena walisimama kimya wakangojea adui kushambulia. Huku nyuma sisi tulijongea mbele tukasimama juu ya mahali walipokuwa wamekwisha pigana, ikawa pamefunikwa kwa watu elfu nne, wengine maiti, wengine wanakufa, na wengine wamejeruhiwa, na ardhi ikawa nyekufundu kwa damu.


Igosi akatoa amri kuwa wale maadui waliojeruhiwa wasiuawe kabisa, na kwa kadiri nilivyoona, watu wakafuatana amri hiyo. Lakini sasa kikosi kingine kikaja, na watu wake walivaa manyoya meupe na ngozi nyeupe, wakawa na ngao nyeupe.


Wakaja kushambulia wale Wajivu elfu mbili waliosalia, nao wakasimama kimya kabisa mpaka maadui walipofika karibu kadiri ya hatua arobaini, ndipo walipojitupa kwa nguvu zisisowezekana kuzuiwa.

Tukasikia tena kishindo kile cha ngao zao, na tena tukaona mambo yale yale. Lakini sasa mambo hayakuisha upesi sana, maana wale adui walikuwa vijana, wakapigana kwa ukali mno, na kwanza ikawa kama watashinda na kuwasukuma nyuma Wajivu.

Mauaji yalikuwa mengi mno, na mamia walianguka kila dakika, na katika vilio na kuugua kwa wale wanaokufa na waliojeruhiwa na vishindo vya mikuki kugongana na ngao, tulisikia sauti ya ‘S’gee!S’gee!’ Hii ndiyo sauti aliyofanya kila mtu alipomchoma mkuki adui yake.

Lakini utii mkamilifu na ushujaa usiobadilika huleta miujiza, maana tulipodhani kuwa Wajivu tayari wameshindwa sisi tukajiweka tayari kuingia katika mahali pao, nikasikia sauti kubwa ya Bwana Henry akiita katika vita, nikaona shoka lake juu.

Ndipo tulipoona mambo yanabadilika. Wajivu wakaacha kurudi nyuma, wakasimama imara kama mwamba, na mawimbi ya maadui yakawarukia tena na tena wasiweze kuwavunja ila walirudishwa nyuma kila mara.

Sasa Wajivu wakaanza kujongea tena, lakini sasa wakijongea mbele; na kwa kuwa hawana bunduki hapakuwa na moshi, kwa hivyo tuliweza kuona kila kitendo katika vita. Baada ya dakika moja, vita vikaanza kufifia tena.

Ignosi akaita, ‘Ah!Kweli hawa ndio wanaume; watashinda tena, tazama vita vimekwisha!
Mara adui walioshambulia walikimbia kama moshi kutoka kinywa cha mzinga, na manyoya meupe yao yalipeperuka katika upepo, wakawaacha Wajivu wameshinda kabisa.

Lakini hawakuwa jeshi tena. Katika mashujaa elfu tatu walioingia katika vita, mia sita tu walibaki, wametapakaa damu; wengine wameanguka chini.


Lakini hata hivyo wakapiga makelele kwa furaha na badala ya kurudi nyuma kama tulivyofikiri kuwa watafanya, waliaanza kuwafukuza adui wale wanaokimbi, na tena, Alhamdu-lilahil nilimwona Bwana Henry yu salama amesimama pamoja na rafiki yetu Infadus.

Tena majeshi ya Twala wakashambulia, na tena wakawa katikati ya vita. Sasa kwa mara ya kwanza katika maisha yangu niliona moyo wangu unatamani vita.

Nikageuka nikamuuliza Ignosi, ‘Je, tusimame hapa mpaka tuote mizizi? Mpaka Twala awameze ndugu zetu wote huko?’ Ignosi akajibu, ‘Hapana, Makumazahn, tazama, sasa wakati umewadia, twendeni!’


Alipokuwa akisema, jeshi lingine lilitoka kwa upande likaanza kushambulia kundi lile dogo, basi Ignosi akainua shoka lake la vita akatoa amri, na mara moja Wanyati waliruka mbele kama wimbi la bahari.

Yaliofuata mimi siweze kusimulia. Ninayo ya kumbuka ni haya: shambulio la nguvu lililotikisa nchi, kisha kishindo kikubwa, na makelele mengi ya watu, na mifululizo ya mikuki niliyoona katika ukungu uliokuwa mwekundu kamadamu.
 
Nilipopata fahamu tena nikajiona nimo katikati ya wale Wajivu waliobaki nimesimama nyuma ya Bwana Henry mwenyewe.

Sijui namna nilivyofika huko lakini baadaye Bwana Henry akanieleza kuwa nilichukuliwa kwa nguvu za shambulio la kwanza la Wanyati, nikaachiliwa huku waliporudiswa nyuma tena, naye akaruka, akanishika, akanivuta ndani.


Nani anaweza kusimulia habari za vita vilivyofuata? Adui walitushambulia tena na tena kama mawimbi ya bahari, na tena tuliwasukuma nyuma.

Lakini mara tulisikia mlio, ‘Twala, ni Twala!’ Na katika msongamano Twala akaruka amechukua mkuki na shoka, akaita, ‘Upo wapi.

Wewe Ndovu, wewe mtu mweupe uliyemuua mwanangu Skraga, njoo ujaribu kuniua mimi!

Na hapo alimtupia Bwana Henry kisu kikubwa, naye akakiona kinakuja akakikinga kwa ngao yake.

Basi ndipo Twala akapika ukelele mkuu akamrukia akampiga shoka kwa nguvu hata nguvu ya pigo ilimwangusha Bwana Henry, akaangukia magoti, ingawa alikuwa mtu mwenye jiramu na nguvu .

Lakini sasa jambo hilo halikuendelea, maana tulisikia sauti ya mshangao, tukatazama tukaona sababu yake. Kwa mkono wa kulia na wa kushoto vile vile uwanda ulikuwa kama u hai kwa jinsi walivyokuja askari wenye kupambwa na manyoya.


Walikuwa ni askari wetu waliokwenda kuzunguka, na sasa wamefika hapa.

Tena wamefika kwa wakati unaofaa sana, maana kama alivyobashiri Ignosi, askari wote wa Twala walikuwa wamekodoa macho yao kutazama vita vikali vilivyoshika baina ya Wajivu na Wanyati, wala hawakuona askari wetu waliotokea pembezoni mpaka wamekaribia sana kuwashambulia.


Na sasa kabla hawajawahi kujipanga, askari wetu wamewarukia kama mbwa anavyorukia windo lake.

Katika muda wa dakika tano, mwisho wa vita ukatambulikana, maana wale askari wa Twala walishambuliwa kwa pande zote mbili, nao wali fadhaika kwa mauaji waliyofanya Wajivu na Wanyati, walianza kukimbia, na kwa upesi uwanda wote katikati ya mahali tulipo na mji wa Loo ulitapakaa makundi madogo madogo ya askari wakijaribu kujiokoa.


Na wale askari waliokuwa wakiwashambulia Wajivu na Wanyati nao wakayeyuka kama wemeyeyushwa kwa uchawi, na sisi tuliachiliwa tumekaa kama mwamba ulioachiliwa na bahari iliyokupwa.


Lakini tuliachiliwa jinsi gani! Kote kote wamelala wale waliokufa, na wale wanaokufa, na wale wenye majeraha, na katika Wajivu, waliobaki ni tisini na tano tu.


Zaidi ya elfu tatu na mia nne wameanguka katika jeshi hilo, na wengi wao wameanguka wala hawaamki tena. Infadus akawa anajifunga jeraha mkononi mwake, akawaambia watu wake, ‘Watu wangu, leo hivi mmethibitisha kabisa sifa ile ambayo watu waliwapeni tangu zamani.

Habari za vita vya leo zitasimuliwa na watoto wa watoto wenu.’

Kisha akageuka akamtazama Bwana Henry akampa mkono akasema, ‘Wewe Ndovu, wewe ni shujaa kweli kweli, nimeishi maisha marefu yangu katikati ya askari na mashujaa, nami nimemwona mashujaa wengi, lakini sijaona mtu kama wewe.’

Basi hapo Wanyati waliobaki walikuwa wakipita kwenda mji wa Loo, na walipokuwa wakipita tukapata habari ya kuwa Ignosi alitaka Infadus na Bwana Henry na mimi tukaonane naye.

Basi tukawaamuru Wajivu waliobaki wakusanye wenye majeraha nasi tukaenda kumtafuta Ignosi.

Tulipomwona alitwambia kuwa anatangulia Loo kwenda kujaribu kumkamata Twala, maana ndipo vita vitakapokwisha kabisa.

Kabla hatujaenda mbali tulimwona Bwana Good ameegemea kisiki cha mti mbali kidogo, na karibu naye tulimwona maiti tuliyedhani ni Mkukuana.
 
Bwana Henry akafadhaika akasema, ‘Nafikiri amejeruhiwa.’

Na hapo aliposema hayo, Yule tuliyefikiri kuwa ni maiti Mkukuana akaruka akampiga Bwana Good kichwani akamwangusha chini, akaanza kumchoma mikuki, Tulimkimbilia Bwana Good, na tulipomkaribia tulimwona Yule Mkukuana anampiga na kumpiga tena kwa mkuki, na kila alipopiga mikono na miguu ya Bwana Good ikaruka juu.


Yule Mkukuana alipotuona tunakuja, akazidi kumpiga kwa nguvu, akapiga kelele, ‘Haya, wewe mchawi nimekuua.’ Akakimbia. Bwana Good akalala kimya wala hakuweza kujimudu hata kidogo, tukafikiri kuwa rafiki yetu tayari amekufa.


Tulimkaribia kwa huzuni, tukashangaa tulipoona anacheka ingawa amegeuka rangi kwa maumivu, akacheka na miwani bado ipo katika jicho lake, akasema, ‘Hizi nguo za chuma ni nzuri sana, naona kuwa Yule Mkukuana amestaajabu.’

Na mara akazimia. Tulipomtazama tuliona kuwa amejeruhiwa vibaya mguu mmoja kwa pigo la kisu kikubwa, lakini nguo zile za chuma zimemlinda asiumizwe zaidi na Yule Mkukuana. Ikawa ameokoka kwa rehema ya Mungu.

Hatukuweza kumtibu wakati ule basi tukamweka juu ya ngao akachukuliwa pamoja nasi. Tulipofika penye lango la Loo tukaona kikosi cha askari wa upande wetu wamesimama kulinda zamu kwa amri za Ignosi.

Vikosi vingine viliwekwa penye milango mingine ya mji.
Yule mkubwa wa kikosi alipomwona Ignosi, alimwamkia kwa amkio la kifalme, akamwambia kuwa askari wa Twala wamejificha katika mji, na Twala mwenyewe vile vile yumo mjini, lakini alifikiri kuwa watu watajitoa, maana wame fadhaika kabisa.


Basi aliposikia hayo Ignosi alituma tarishi kwa kila mlango wa mji kuwaamuru walio ndani wafungue milango, naye aliahidi kuwa wote watakaojitoa na kutoa silaha zao watapata msamaha.

Basi habari hii ikapokewa, na mara tulisikia makelele na milango ikafunguliwa. Tukaingia katika mji, lakini tuliangalia sana tusije tukaghafilika.

Katika njia zote tulikuta askari wamesimama na vichwa kuinamia chini, na silala na ngao zao zimewekwa chini miguuni pao, na Ignosi alipokuwa akipita walimwamkia kwa amkio la kifalme.

Tukaenda mbele mpaka jumba la Twala, Tulipofika kwenye kiwanja kile tulichokwenda juzi juzi kutazama ngoma, tulikiona kipo wazi kabisa, lakini si wazi, maana pale mbele ya mlango wa jumba lake, Twala mwenyewe alikaa, pamoja na mtu mmoja tu, naye alikuwa Gagula.

Ilisikitisha kumwona vile alivyokaa, na shoka lake na ngao yake vimewekwa chini ubavuni pake, na kichwa chake kainamisha kifuani, na mtu mmoja tu amekaa kumfariji.


Na ingawa tulikumbuka ukatili wake, hatukuweza kujizuia kuto kumsikitikia.

Hapana hata askari mmoja katika maelfu ya askari wake; hapana hata mfuasi mmoja katika wale wengi walionyenyekea mbele yake, hapana hata mke mmoja aliyesalia kumfariji katika uchungu wa yaliyomfika. Masikini!

Tulipita mlango wa kiwanja tukaenda mpaka mbele ya Twala, na huku Gagula anatutukana vibaya.

Tulipokaribia, Twala akafanya kutuona, akainua kichwa chake kilichovikwa manyoya marefu, akamtazama Ignosi kwa jicho moja lake, likang’aa kama ile almasi iliyofungwa katika kipaji chake cha uso, akasema kwa sauti yenye uchungu na dharau, ‘Hujambo, Ewe mfalme, wewe uliyekula chakula changu, na sasa kwa msaada wa uchawi wa watu weupe umewashawishi askari wangu kuniasi!

Niambie, ajali yangu ni nini, Ewe mfalme?’

Ignosi akajibu kwa ukali, ‘Ajali yako ni ile ile uliyompa baba yangu, ambaye kiti chake umekikalia kwa miaka hii yote.’ Twala akasema, ‘Vema, nimekubali. Nitakuonyesha njia ya kufia, ili nawe ukumbuke wakati wako utakapowadia.

Tazama, jua linazama, ni vizuri na jua langu lizame pamoja nalo. Na sasa, ewe mfalme, mimi tayari kufa, lakini nataka haki ya mfalme wa Wakukuana, yaani nife nikipigana. Huwezi kunikatalia; ukikataa hata wale waoga waliokimbia leo, hata na wao watakwita mwoga.’

Ignosi akajibu , ‘Nimekubali. Chagua, utapigana na nani? Mimi mwenyewe siwezi kupigana nawe, maana mfalme hupigana katika vita tu.’


Jicho la Twala likatutazama, na kwa dakika moja nilimwona ananitaza mimi tu, na baadaye akasema, ‘Ndovu, wasemaje, tumalize yale tuliyoanza leo, au nikwite kwa jina la mwoga?’

Ignosi akasema kwa haraka, ‘La, huna ruhusa kupigana na Ndovu.’ Twala akajibu, ‘Vema, kama anaogopa, sipigani naye.’ Basi Bwana Henry alifahamu maneno hayo, na uso ulimwiiva akasema, ‘Nitapigana naye, naye ataona kuwa siogopi.’


Nikamsihi, ‘Nakuomba usipigane naye, usijitie katika hatari ya bure, maana huyu anajua lazima afe. Kila mtu aliyekuona leo anajua kuwa wewe ni shujaa, si muoga.’

Akajibu, ‘Lazima nipigane naye. Hapana mtu atakayeniita muoga na kuishi. Sasa mimi ni tayari.’ Akashika shoka lake akasimama mbele. Nilipoona kuwa amekwisha azimia, wasiwasi uliniingia, lakini sikuweza kumzuia asipigane.

Ignosi akaweka mkono juu ya bega lake kwa upole, akamwambia, ‘Rafiki, ndugu yangu mweupe, usipigane naye. Vita uliyopigana leo inatosha kabisa, na ukidhurika, moyo wangu utakuwa mzito sana.’

Bwana Henry akasema, ‘Ignosi, lazima nitapigana naye .’ Akaijibu, ‘vema, Ndovu, wewe ni shujaa kweli kweli. Tazama, Twala, Ndovu yu tayari kupigana nawe.’

Twala akacheka kicheko kikubwa, akasimama akamtazama Bwana Henry. Kwa muda kidogo wakasimama hivi na mwangaza wa jua lililokuwa likishuka ukawaangaza ukaonyesha maungo yao namna yalivyokuwa mazuri.

Kisha wakaangaza kuzungukiana, na mashoka yao juu.

Mara Bwana Henry akaruka mbele akajaribu kumpiga Twala kwa nguvu zake zote, lakini Twala aliepa.

Nguvu za pigo zilikuwa nyingi hata alitaka kuanguka, basi adui yake akawa tayari akapungu shoka lake kichwani, akapiga kwa nguvu nyingi kabisa. Moyo wangu ulisita, nikafikiri kuwa yamekwisha. Lakini sivyo;

Bwana Henry akaweka mkono wake juu kwa upesi akalikinga shoka. Mara Bwana Henry akapata nafasi kupiga mara ya pili, lakini Twala akakinga kwa ngao yake.

Basi ikaendelea hivyo, pigo kwa pigo, na kila pigo lilikingwa. Sasa watu wote waliokuwako wakaanza kusongana katika mshangao wao, wakapiga kelele au kuguna kwa kila pigo.

Hapo Bwana Good aliye kuwa amezimia, akapata fahamu tena, na mara akasimama akaanza kurukaruka huku akimtia moyo Bwana Henry.

Basi hivyo hivyo wakapigana, hata kwa bahati mbaya Twala akapata nafasi ya kulipiga shoga la Bwana Henry likamtoka mkononi, likaanguka chini.

Sasa wote waliugua kwa mashaka na huzuni, na Twala akainua shoka lake juu akamrukia huku akipiga kelele. Nikafumba macho.

Nilipofumbua macho tena, niliona ngao ya Bwana Henry imelala chini, naye amemkumbatia Twala kiunoni.

Huku na huku waliminyana, huku wamekamatana kwa nguvu zao zote. Twala akajitahidi sana, akamwinua Bwana Henry juu, wakaanguka chini wote pamoja, na Twala alijaribu kumpiga shoka la kichwa, na Bwana Henry akajaribu kumpiga Twala kisu.


Ikawa shindano kuu kabisa, na hapo Bwana Good alipiga ukulele, ‘Shika shoka lake!’ Na labda Bwana Henry alisikia, maana alitupa kisu chake akashika shoka la Twala wakaanza kupinduana chini wakipigana kama paka wa mwitu wanavyopigana, huku wakitweta kwa nguvu.

Mara tuliona kuwa ngozi iliyofungiwa shoka kwenye mkono wa Twala imekatika, na Bwana Henry ametengwa naye na amepata shoka hilo. Mara akaruka juu, na damu inamtoka usoni pale alipojeruhiwa na Twala, na mara ile Twala naye akaruka juu.


Basi sasa ikawa kupigana tena, mpaka Bwana Henry akajitahidi akapiga shoka kwa nguvu zote, akampiga la shingo.

Hapo watu waliokuwapo waliguna kwa pamoja maana kichwa cha Twala kikaanguka kikabiringika mpaka kikafika kwenye mguu wa Ignosi kikasita.


Kwa dakika hivi kiwiliwili chake kilisimama wima, kisha kikaanguka kwa kishindo, na pale pale Bwana Henry alizimia, naye akaanguka juu ya maiti ya Twala.


Basi tulimwinua tukammwagia maji akafumbua macho yake. Hakufa, nami, jua lilipokuwa likishuka, nikasimama mbele, nikafungua ile almasi iliyofungwa juu ya kipaji cha uso wa Twala, nikampa Ignosi, nikasema, ‘Itwae Ignosi, mfalme wa haki wa Wakukuana, mfalme kwa ‘kuzaliwa, na mfalme kwa kushinda.’

Ignosi akaifunga juu ya kipaji chake, akaja mbele akaweka mguu wake juu ya kiwiliwili cha Twala, akaanza kuimba wimbo wa ushindi, hivi:

Sasa uasi wetu umemezwa katika ushindi, na vitendo vyetu viovu vimegeuka kuwa haki kwa nguvu. Asubuhi wadhalimu waliamka wakajitikisa; walijifungia manyoya wakajiweka tayari kwa vita. Waliamka wakashika mikuki yao: askari waliwaita wakubwa wao, ‘Njooni mtuongoze.’

Na wakubwa walimwita mfalme, ‘Utuongoze vitani.’ Wakaondoka na kiburi chao, watu ishirini elfu na tena ishirini elfu.

Manyoya yao yalifunika nchi kama manyoya ya ndege yanavyofunika tundu lake; walitikisa mikuki yao kwa vigelegele.

Ndiyo, walirusha mikuki yao katika mwangaza wa jua; wakatamani vita wakafurahi.
Wakanishambulia; wenye nguvu wao eakanijia mbio waniue, wakipiga kelele,’ Hal Ha! Ni kama aliyekwisha kufa.’ Ndipo nilipovuma juu yao, na pumzi zangu zikawa kama upepo wa tufani, na tazama! Wakatawanyika .



Umeme wangu uliwachoma; nililamba nguvu zao kwa umeme wa mikuki yangu; niliwapeperusha kwa ngurumo ya kulia kwangu.

Walivunjika, walitawanyika, walitoweka kama ukungu wa asubuhi.
Sasa wamekuwa chakula cha kunguru na fisi, na mahali pa vita pamenona kwa damu yao.


Wa wapi wale walioamka asubuhi na nguvu zao?
Wa wapi wale wenye kiburi waliotikisa manyoya yao wakasema ‘Ni kama aliyekwisha kufa:’


Wameinamisha vichwa lakini si katika kusinzia; wamejinyosha, lakini si katika usingizi.
Wamesahauliwa; wametoweka gizani nao hawatarudi; ndiyo, watu wengine watawachukua wake zao, na watoto wao hawatawakumbuka tena.



Na mimi, mimi? Mimi ni mfalme. Kama tai nimeona tundu langu.

Tazama! Nilitembea mbali wakati wa usiku, lakini nimewarudika makinda yangu wakati wa mapambazuko.

Ingieni nyinyi kwenye kivuli cha mabawa yangu, ee nyinyi watu, nami nitawafariji, nanyi hamtafadhaika tena.

Huu ndiyo wakati wa neema, huu ndio wakati wa kuteka. Ng’ombe walio bondeni ni wangu, wanawali pia walio mjumbani ni wangu.

Taabu imepita, neema imefika. Sasa uovo utafunikwa uso wake, na Huruma na Furaha watakaa katika nchi.

Furahini, furahini, watu wangu!

Dunia yote ifurahi kwa kuwa jeuri imekanyagwa, na mimi ndiye mfalme.

Ignosi akanyamaza, na kutoka katika giza lililokuwa limeingia, jibu likaja kama ngurumo kutoka milimani, ‘Wewe ndiye mfalme!’

Hivyo yale niliyombashiria Yule tarishi yalitimia, na katika muda wa saa arubaini na nane, kiwiliwili cha Twala kimelala kikavu mbele ya mlango wa jumba lake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…