Hadithi ya mashimo ya mfalme Sulemani

Hadithi ya mashimo ya mfalme Sulemani

Skraga akapunga mkuki wake mara moja, mara ya pili, akapiga. Aah! Umempiga, umetoka upande wa pili kadiri ya futi moja.

Akanyosha mikono yake juu akaanguka, akafa. Basi yamekwisha; pale maiti amelala, nasi bado hatujatambua vema mambo yaliyotokea. Bwana Henry akaruka juu na kupiga ‘Lahaula,’ lakini mara alikaa tena, maana kila mtu alikaa kimya.

Mfalme akasema, ‘Lilikuwa pigo zuri sana. Haya, mwondoe.’ Na watu wanne wakatoka katika kikosi wakamwinua Yule mtu aliyeuawa wakamchukua. Hapo tulisikia ile sauti ndogo tena ya Yule kama nyani, ‘Futeni alama ya damu, futeni. Amri ya mfalme imetekelezwa.’

Mwanamwali mmoja akatoka amechukua chokaa katika kapu akainyunyiza juu ya alama ya damu. Huku nyuma Bwana Henry alishikwa na ghadhabu kuu; nikamzuia kwa shida asisimame, nikamnong’oneza, ‘Kaa, kaa usisimame au tutapoteza maisha yetu.’ Akakubali akakaa.

Twala alikaa kimya mpaka alama zile za damu zimekwisha futwa, ndipo aliposema, ‘Watu weupe mmetoka wapi, mmekuja kutafuta nini?’ Nikajibu, ‘Tumetoka katika nyota, usituulize kwa namna gani, Tumekuja kutazama nchi hii.’

Akasema, ‘Mmesafiri kutoka mbali ili kuja kutazama kitu kidogo. Je, na Yule ametoka katika nyota vile vile?’ (akamwonyesha Umbopa.) Nikamjibu, ‘Hakika hata watu wa rangi uliyonayo wewe wapo mbinguni; lakini Mfalme Twala haifai kuuliza mambo ambayo huwezi kuyafahamu.’

Akajibu, na sauti yake iliyochukiza sana, ‘Nyinyi watu wa nyota mnasema kwa sauti na maneno ya kiburi sana, afadhali mkumbuke kuwa nyota ziko mbali, na nyinyi mpo hapa. Je, itakuwaje nikikufanyeni kama Yule waliye mchukua?’

Nikacheka sana, lakini katika moyo wangu sikuwa na kicheko, nikajibu, ‘Ee Mfalme, tahadhari sana, nenda pole pole juu ya mawe ya moto usije ukaunguza nyayo zako; uushike mkuki kwenye mpini usije ukakukata mkono.

Ukigusa hata unywele mmoja wa vichwa vyetu utaangamia papo hapo. Je, huyu Infadus na Skraga hawajakwambia sisi ni watu gani? Umepata kuwaona watu kama sisi?’ (Nikamwonyesha Bwana Good, maana nilijua hakika kuwa hajaona mtu kama yeye.) Mfalme akamtazama Bwana Good akasema, ‘Ni kweli, sijaona.’


Basi nikaendelea nikasema, ‘Hawajakwambia namna tunavyoweza kuwaua watu kwa mbali?’ Mfalme akajibu, ‘Wameniambia, lakini sisadiki. Nataka nione kwa macho yangu ukimuua mtu. Muue mtu Yule anayepita kule, nami nitasadiki.’ Akaonyesha mtu aliyekuwa akipita upande mwingine wa mji.

Nikajibu, ‘La, sisi hatumwagi damu ya watu wasio na hatia lakini ukitaka kuona, basi amuru mtu alete ng’ombe, na kabla hajaenda hatua ishirini nitamuua Yule ng’ombe.’ Mfalme akacheka, akasema, ‘Hapana, ukimuua mtu ndipo nitakapo sadiki.’

Nikajibu, ‘Vema’ wewe nenda upite uwanjani na kabla hujafika mlangoni utakuwa maiti; au kama hupendi kwenda wewe mwenyewe, basi mpeleke mwanao Skraga.’ Basi kusikia hayo tu, Skraga akalia sana akaondoka akakimbilia nyumbani. Twala akakunja uso akasema, ‘Leteni ng’ombe.’


Mara watu wawili walikwenda mbio kuleta ng’ombe, nikamwambia Bwana Henry, ‘Sasa Bwana Henry ni juu yako kumpiga ng’ombe, maana nataka mfalme ajue kuwa si mimi tu ninayeweza kupiga bunduki.’

Basi tukakaa kimya kidogo, halafu tukaona ng’ombe anakuja mbio, na mara alipoona wale watu wengi, akasimama.

Nikamwambia Bwana Henry. ‘Haya sasa piga.’ Na pale pale akaelekeza bunduki akapiga. Mara ile ile ng’ombe alilala kafa. Basi hapo watu wote walishangaa wakazuia pumzi; nikageuka nikamwambia mfalme, ‘Je, mfalme nimesema kweli?’
Mfalme akajibu, na sauti yake ilikuwa ya mtu anayeogopa sana, ‘Ndiyo, mtu mweupe, umesema kweli.’

Basi nikaendelea nikasema, ‘Sikiliza, Twala. Umeona sasa unaweza kusadiki kuwa sisi tumekuja kwa amani wala si kwa vita. Tazama.’ Nikamwonyesha ile bunduki tuliyomletea.
‘Huu ndio mwanzi utakaokupa nguvu kuua kama sisi tunavyoua, lakini naweka sharti hii, usimuue mtu. Ukiielekeza kumpiga mtu, utajiua wewe mwenyewe.

Ngoja, nitakuonyesha. Mwambie mtu mmoja apime hatua arubaini kisha achomeke mkuki katika ardhi na bamba lake lituelekee sisi.’

Akaamuru ikafanywa, nikasema, ‘Sasa tazama utaona kuwa nitalivunja nikapiga bunduki.

Risasi ikalipiga lile bamba la mkuki likavunjika vunjika vipande. Tena watu wote walizuia pumzi kwa kushangaa, nikasema, ‘Sasa Twala, twakupa mwanzi huu, na baadaye nitakufundisha namna ya kuutumia, lakini uangalie sana usiutumie uchawi huu wa nyota kumdhuru mtu wa duniani.’


Nikampa ile bunduki. Mfalme akaitwaa kwa kuiogopa akailaza miguuni pake. Alipokuwa akiiweka, Yule kama nyani akatamani kutoka kivulini mwa nyumba. Alitambaa kwa miguu na mikono, lakini alipofika mahali alipokuwa kakaa mfalme, akasimama, akafunua uso wake ambao ulikuwa wa kutisha mno.

Alikuwa mwanamke kizee sana sana, na uso wake umekunjika mno kwa uzee hata kuwa kama uso wa mtoto mchanga wenye mikunjo mingi.

Kinywa chake kilikuwa kama ufa katika mikunjo hiyo, na chini ya ufa, kidevu chake kilitokeza kama ncha. Alikuwa na pua ndogo na kama macho yake yasingelioneka , uso wake ungalikuwa kama uso wa maiti iliyokauka kwa kuwekwa juani.


Lakini macho yake yaling’aa kama mwenye akili nyingi. Kichwa chake kilikuwa kipara, hana nywele kabisa, na ngozi ya utosini iliyokunjana ikimeta kama ngozi ya nyoka.
Mtu huyu alitufanya kutetemeka kwa hofu.

Alisimama kimya kidogo, kisha akaweka mkono wake uliokuwa na makucha marefu sana, juu ya bega la mfalme Twala, akasema kwa sauti nyembamba na kali, ‘Sikiliza, Ee Mfalme! Sikilizeni, Ee Mashujaa!


Sikilizeni, Ee milima na nyanda na mito, na nchi ya Wakukuana! Sikilizeni, Ee mbingu na jua, Ee mvua na dhoruba na ukungu! Sikilizeni, Ee wanaume na wanawake, Ee vijana na wanawali, na nyinyi watoto msiozaliwa bado! Sikilizeni, vitu vyote vyenye uhai vitakavyokufa! Sikilizeni, vitu vyote vilivyokufa vitakavyofufuka na kufa tena! Sikilizeni, nami nitabashiri. Sasa nabashiri, nabashiri!’

Sauti yake ilififia na watu wote walishikwa na hofu kuu. Kizee huyu alitisha mno. Akaendelea. ‘Damu! Damu! Damu! Mito ya damu; damu pote pote. Naiona, naisikia, naionja ina chumvi! Ni nyekundu juu ya nchi! Inanyesha kutoka mawinguni. Nyayo! Nyayo! Nyayo! Nyayo za watu weupe watokao mbali. Zinatikisa nchi; nchi inatetemeka mbele ya bwana wake.


Damu ni njema, damu nyekundu hung’aa; hakuna harufu kama harufu ya damu iliyomwagwa kwa kiasi. Simba watailamba na kunguruma, tai wataoshea mbawa zao ndani yake na watalia kwa furaha.


Mimi ni mzee! Mimi ni mzee! Nimeona damu nyingi; ha,ha.! Lakini nitaona nyingi zaidi kabla sijafa, nitafurahi. Baba zenu walinijua, na baba zao walinijua, na baba za baba zao. Nimeona watu weupe, ninajua tama zao. Mimi mzee, lakini milima hii imenipita kwa uzee. Nani aliyetengeneza Njia Kuu, niambieni?’


Nani aliyechora sanamu zile juu ya miamba, niambieni? Nani aliyeumba wale Watatu walio kimya wanaotazama shimo, niambieni?’

Akaelekeza mkono wake kuonyesha kwenye milima ile mirefu. Akaendelea, ‘Hamjui, lakini mimi najua. Walikuwa watu weupe waliowatangulieni nao watakuja hapo nyinyi mtakapokwisha kutoweka, watawaleni na kuwaaharibuni.


Ndiyo! Ndiyo! Ndiyo! Na hao watu weupe walijia nini? Wenye kutisha, Wenye elimu ya uchawi na maarifa yote, wenye nguvu wasiochelea! Ee Mfalme, lile jiwe linalong’aa katika kipaji chako ni nini? Mikono ya nani ilifuma nguo hizo za minyororo unazovaa kifuani, Ee mfalme?

Hujui!, ila mimi najua. Mimi, mzee, mimi mwenye busara, mimi Isanusi, Kichawi.’ Akatugeukia akasema, ‘Nyinyi watu weupe wa Nyota mnatafuta nini? Mnatafuta mmoja wenu aliyepotea?


Hayupo. Hapana mguu mweupe uliokanyaga nchi hii tangu vizazi na vizazi vilivyopita ila mara moja tu, naye alipoondoka hapa aliondoka kwenda kufa tu.

Mmekuja kuchuma mawe yanayong’aa; najua, najua; damu itakapokwisha kukauka mtayaona; lakini je, mtarudi mtokako au mtakaa na mimi?


Ha!ha!ha! Na wewe, wewe mwenye ngozi nyeusi, mwenye udaha, nani wewe, unatafuta nini? Wewe hutafuti mawe yanayong’aa wala chuma cha dhahabu, hayo unawaachia watu weupe watokao kwenye Nyota.

Nadhani nakujua; nadhani naweza kusikia harufu ya damu iliyo katika moyo wako. Haya uvue mkanda ..

Basi hapo Yule kizee akawa amepandwa na pepo akaanguka chini na povu likamtoka kinywani, akachukuliwa ndani ya nyumba.

Mafalme akasimama anatetemeka, akapunga mikono. Mara moja vikosi vyote vikaanza kutoka kwa taratibu, na baada ya dakika kumi hapakuwa na mtu ila sisi na Mfalme na watumishi wachache.

Mfalme akasema, ‘Watu weupe, ‘ninayo nia ya kuwauweni, Gagula amesema maneno ya ajabu juu yenu. Mnasemaje?’ Nikacheka nikasema, ‘Angalia, Ee Mfalme, sisi si wepesi wa kuuawa.

Umeona kufa kwa Yule ng’ombe; wataka kuwa kama alivyo Yule ng’ombe?’
Mfalme akakunja uso akasema, ‘Si busara kujaribu kumtisha mfalme.’
Nikasema, ‘Hatujaribu kukutisha, tunayoyasema ni ya kweli.

Ukijaribu kutuua basi utatutambua’ Yule mfalme akaweka mkono kichwani akafikiri, kisha akasema, ‘Nendeni kwa amani.


Usiku wa leo kuna ngoma kuu. Mtayiona. Msiogope na kudhani labda nitajaribu kuwanasa. Kesho nitafikiri juu ya habari zenu.’ Nikajibu, ‘Vema, Ee mfalme.’ Kisha tukaondoka, tukafuatana na Infadus tukaenda nyumbani kwetu.
Safi Mkuu ikiwezekana tupia kama zote
 
Bwana Henry akaniuliza, ‘Je, imekuwaje sasa?’ nikatikisa kichwa tu. Bwana Good akasema, ‘Mimi najua.

Nadhani njia ilipita huku lakini mchanga umepeperusha na kuifunika, na huko juu nadhani imefunikwa kwa mawe yaliyotoka juu mlimani.’ Basi tukaona kuwa labda maneno yake ni ya kweli, tukaanza kuteremka mlimani.

Sasa safari yetu ilikuwa nyepesi wala si kama ile ya kupanda mlima tulipokuwa tunaona njaa kali. Kama tungaliweza kuwasahau masikini Ventvogel na Yule mzee pangoni nadhani tunaliona furaha kabisa, ingawa hatukujua hatari inayoweza kutokea kwa mbele. Kila tukiteremka tuliona hewa inazidi kuwa nzuri, na nchi yenyewe ilikuwa nzuri kabisa.

Njia ilikuwa ya ajabu mno, pengine ilivuka misingi mirefu juu ya daraja yenye matao, na pengine ilipanda mlima kwa kuzunguka zunguka, na pengine ilipenya ndani yam lima wenyewe. Ukuta wa tundu lile lililopenya mlima ulichorwa picha.

Bwana Henry akazitazama akasema, ‘Watu wanaita njia hii njia ya Sulemani lakini mimi nafikiri kama ni kazi ya watu wa Misri walipofika hapa kabla ya watu wa Sulemani. Maana, kazi hii kama si kazi ya Wamisri, nadhani imefanana sana nayo.’

Ilipopata saa sita tulikuwa tumekwisha teremka na kufika mahali penye miti mingi. Mara Bwana Good akasema, ‘Ah! Hapa tunaweza kupata kuni; na tukae hapa kidogo tuchome nyama iliyobaki; maini yale mabichi yamekwisha shuka tumboni.’

Basi tuliacha njia tukaenda kwenye mto wa maji safi tukakaa, na upesi tuliwasha moto. Sasa tulikata nyama ya Inko tuliyoleta tukaioka. Tulipokwisha shiba, tukavuta tumbako tukaaa tumefurahi, na raha yetu tulipoilinganisha na taabu iliyotupata ilikuwa kama ni raha ya peponi.

Baadaye kidogo sikumwona Bwana Good, nikatazama kuona umekwenda wapi. Nikamwona amekaa karibu na mto amekwisha oga. Sasa amevaa shati lake tu na tabia yake ya umaridadi ikadhihirika; maana amekunja suruwali na koti, naye anatikisa kichwa kwa kuona namna zilivyoraruka kwa miiba ya njiani. Kisha akatwaa viatu vyake akavisugua kwa majani, kisha akatwaa kipande cha mafuta ya nyama akaanza kuvisugua kwa mafuta.

Kisha akavitazama kwa miwani yake, maana alivaa siku zote miwani yenye kioo kimoja tu, akavivaa. Sasa alitoa kioo kidogo na kitana akajitazama uso na tena akatikisa kichwa, akachana nywele zake, lakini hakuwa radhi.

Akapapasa ndevu zake, maana hakuweza kunyoa kwa muda wa siku kumi, akatwa kile kipande cha mafuta akakiosha katika maji, kisha akasugua ndevu zake kwa mafuta, akatwaa wembe katika mfuko wake akaanza kunyoa ndevu zake.

Lakini niliona akiumia sana, maana niliweza kumsikia akiguna, nikacheka sana. Maana niliona kuwa ni ajabu kuwa mtu anakubali kuvumilia maumivu ya kunyoa kwa mafuta katika mahali tulipo sisi, yaani porini pasipo na watu. Basi alizinyoa ndevu zilizokuwa nyingi sana, kwa upande wa kulia wa uso wake, na mara nilishtuka sana nikaona mshale wa nuru unampitia kichwani.
Aisee[emoji39] [emoji39]
 
Bwana Good akaruka ameshtuka sana, na mimi vile vile nikaruka nikatazama, na haya ndiyo niliyoona.

Pale yapata hatua ishirini kutoka nilipokuwa nimesimama mimi, na hatua kumi kutoka alipokuwako Bwana Good, niliona watu wamesimama. Wote walikuwa warefu na weusi, lakini wekundu kidogo kama rangi ya shaba nyekundu, na wengine walivaa manyoya marefu meusi na ngozi za chui; basi haya ndiyo niliyoona kwanza.

Mbele niliona kijana mwenye umri wa miaka kumi na saba amesimama kama ndiyo kwanza autupe mkuki. Mshale ule wa nuru niliouona ulikuwa mwangaza uliomulikwa na mkuki alioutupa.

Nilipokuwa nikitazama, mzee mmoja aliyekuwa kama askari akaja mbele akamshika mkono Yule kijana akasema naye, kisha wote wakatujia.
Bwana Henry na Bwana Good na Umbopa wote walishika bunduki zao wakaelekeza. Lakini wale watu wakazidi kutujia.

Basi niliona kuwa hawa kujua bunduki ni kitu gani, maana wangalijua wasingezi dharau hivyo. Basi nikawaambia waweke bunduki zao chini, maana watambue kuwa usalama wetu u katika kutafuta suluhu.


Wakafanya nilivyotaka, kisha nikaenda mbele kuonana na wale watu, nikamwambia Yule mzee kwa Kizulu. Maana nilibaatisha tu, lakini nilipoona kuwa wanafahamu maneno yangu nilistaajabu.

Yule mzee akaitikia, lakini maneno yake yaliachana kidogo na maneno ya Kizulu ila si sana, na mimi na Umbopa tuliweza kuyafahamu mara. Yule mzee akauliza, ‘Mmetoka wapi? Nyinyi ni nani? Kwa nini sura za nyinyi watatu ni nyeupe na huyu wanne ni kama sura zetu?’


Akapeleka mkono kumwonyesha Umboka. Nikamtazama Umbopa na nikajua kuwa anasema kweli. Sura yake ilikuwa kama sura za watu wale waliokuwa wamesimama mbele yetu, na maungo vile vile yalifanana nao. Nikamjibu, ‘sisi ni wageni tumekuja kwa amani, na mtu huyu ni mtumishi wetu.’
Akasema, ‘’Unasema uwongo, wageni hawawezi kuvuka ile milima.

Lakini uwongo wenu utafaa nini? Ikiwa nyinyi ni wageni lazima mtakufa, maana wageni wowote hawana ruhusa kuishi katika nchi hii ya Wakukuana. Hii ndiyo amri ya Mfalme. Basi mjiwekeni tayari kufa, e nyinyi wageni’’ Niliposikia maneno hayo nilifadhaika, na hasa nilipoona mikono ya wale watu inashuka na kushika visu vikubwa vilivyofungwa viunoni mwao. Bwana Good akauliza, ‘Je, mtu huyu anasema nini?’ Nikamjibu, ‘Anasema kuwa tutauawa .’

Bwana Good akaghumia, na kama ilivyokuwa desturi yake anapokuwa kwenye shida yeyote, alitia vidole kinywani akashika meno yake akayavuta chini, kisha akayaacha yarudi juu tena kwa kishindo. (Maana alikuwa ametiwa meno yaliyotengenezwa, kwa kuwa meno yake yameng’olewa).

Jambo hilo lilituokoa, maana mara walipoona hivyo, wale watu wakashtuka wakapiga kelele kwa hofu, wakaruka nyuma hatua mbili tatu. Nikasema, ‘Je, kuna nini?’ Bwana Henry akaninong’oneza akasema, ‘Ni meno ya Bwana Good nadhani alipoyavuta chini; wale watu wameona ni ajabu.

Haya, Bwana Good, yatoe kabisa.’ Basi akayatoa akayaficha upesi katika mkono wa shati lake.

Basi wale watu sasa walishikwa na udadisi wakasahau hofu yao kidogo, wakaja mbele, sasa ile habari ya kutuua waliisahau.

Yule mzee akaelekeza mkono wake kumwonyesha Bwana Good, naye amesimama amevaa shati na viatu tu, na tena amenyoa upande mmoja tu wa uso wake, akasema, ‘Ee nyinyi wageni, imekuwaje kuwa huyu mnene amevaa nguo maungoni ila miguu ni mitupu, na pia ndevu zaota kwa upande mmoja tu wa uso wake, naye, analo jicho moja ambalo linapenya nuru? Imekuwaje anaweza kuyatoa meno yake nakuyarudisha apendavyo?’


Nikamwambia Bwana Good, ‘Funua kinywa chako.’ Akafunua midomo yake kama mbwa mkali, wakaona kuwa hana meno kabisa, waliouona ni ufizi tu. Basi wale watu wakashtuka sana, wakasema, ‘Meno yake yako wapi sasa? Tulioyaona kwa macho yetu sasa hivi!’

Basi Bwana Good akageuza kichwa chake kidogo akainua mkono wake akayaweka meno ndani kwa siri, kisha akacheka. Kumbe! Kinywa chake kimejaa meno tena. Basi walipoona hivyo, Yule kijana alijiangusha chini akalia kwa hofu; na magoti ya Yule mzee yaligongana kwa kuogopa, akasema, na sauti yake ilitetemeka.

‘Naona kuwa nyinyi ni mizuka, maana hapana mtu aliyezaliwa na mwanamke mwenye ndevu upande mmoja tu wa uso, wala jicho moja linalopenya nuru, wala meno yanayotoweka na kuonekana tena. Ee mabwana, mtuwie radhi.’

Basi nikaona kama ni bahati yetu tena, nikamjibu kwa sauti kali, ‘Basi, msiogope; nitawataarifu habari za kweli. Sisi ni wanaume kama nyinyi lakini tumetoka katika ile nyota kubwa inayozidi kung’aa usiku.

Tumekuja kukaa pamoja nanyi kwa muda kidogo na kuwaleteeni neema. Mnaona rafiki zangu, nimejifunza lugha yenu ili niwe tayari.’

Wakaitika, ‘Ni kweli, ni kweli.’ Nikaendelea nikasema, ‘Na sasa, rafiki zangu, labda mnaogopa, mnafikiri kuwa tutamuua Yule kijana aliyemtupia mkuki huyu mwenzetu mwenye meno yanayotoka na kurudi tena. Maana mmetupokea vibaya baada ya safari ndefu tuliyoifanya ili kufika hapa.’

Yule mzee akasema, ‘Mabwana, mtusameheni nawasihi, maana yeye ni mwana wa mfalme na mimi ni mjomba wake. Akidhurika lazima mimi nitauawa.’ Yule kijana akaitikia, akasema, ‘Ndiyo, hayo ni kweli kabisa.’

Nikasema, ‘Labda mnafikiri kuwa hatuna nguvu za kujilipiza kisasi, lakini nitakuonyesheni. Haya wewe (nikamwita Umbopa kwa ukali sana) nipe mwanzi wangu wa uchawi unaosema.’ (Nikamwashiria anipe bunduki yangu).

Umbopa alitambua mara moja niliyotaka, akanipa bunduki yangu huku akiinamisha kichwa, na akasema, ‘Ni huu, bwana wa mabwana.’ Basi kabla sijamwambia anipe bunduki niliona swala amesimama juu ya mwamba kadiri ya mwendo wa hatua mia moja, nikanuia kumpiga.

Basi niliwaonyesha huyo swala, nikasema, ‘Niambieni kama yupo mtu aliyezaliwa na mwanamke anayeweza kumuua Yule mnyama kwa mshindo tu!
Yule mzee akajibu, ‘Hapana mtu, wala haiwezekani kabisa.’ Nikajibu, ‘Lakini mimi nitamuua.

Nikaelekeza bunduki yangu, Yule mnyama alikuwa mdogo lakini nilijua kuwa ni lazima nimpige. Nikavuta pumzi nikakaza mtambo wa bunduki kwa taratibu. Yule swala alisimama kimya kabisa. Bunduki ikalia, na mara Yule swala akaruka juu, akaanguka juu ya mwamba amekwisha kufa.


Basi, hapo wale watu waliguna kwa hofu, nikasema, ‘Haya, mkitaka mnyama nendeni mkamchukue huyo.’ Yule mzee akamwashiria mtu mmoja, na akaenda akamleta mnyama, wakamzungukia wakatazama tundu iliyoingia risasi.

Nikasema, ‘Kama hamsadiki hata sasa, basi mtu mmoja asimame mwambani nimfanye kama nilivyomfanya huyo swala. Hapo mtafahamu kuwa mimi sisemi maneno ya bure.’
Hapana aliyetaka kufanya hivyo mpaka Yule mwana wa mfalme aliposema, ‘Umesema vema. Wewe, mjomba wangu, nenda ukasimame mwambani, Uchawi ule umeua mnyama tu, hauwezi kumuua mtu.’

Lakini Yule mzee hakupenda shauri lile, akaudhika, akasema, ‘Hapana! Hapana! Macho yangu ya kizee yameona mambo ya kutosha. Watu hawa ni wachawi wa kweli kweli. Tuwachukue kwa mfalme.

Lakini ikiwa mmoja wenu anataka ushuhuda zaidi, basi na yeye asimame mwambani na ule mwanzi wa uchawi utasema naye.’

Hapo wote wakaanza kukataa. Na mmoja akasema, ‘Hapana, uchawi wa namna hiyo usipotee bure kwa ajili yetu. Sisi tumeridhika. Uchawi wote wa watu wetu hauwezi kufanya jambo kama hilo.’

Yule mzee akasema, ‘Ni kweli. Bila shaka ni kweli. Na sasa nyinyi watoto wa nyota, sikilizeni, nyinyi watoto wenye macho yanayong’aa, meno yanayotoweka, nyinyi mnaonguruma kwa ngurumo inayoweza kuua kwa mbali. Mimi ni Infadus, mwana wa Kafa, aliyekuwa mfalme wa watu wa Kukuana.


Huyu kijana ni Skraga, mwana wa Twala aliye mfalme mkuu wa Kukuana, Mlinzi wa Njia Kuu, Mtishaji wa adui zake, Mwenye elimu ya uchawi, Jemedari wa askari mia elfu, Twala mwenye chongo, Mweusi, Mtishaji.’

Nikasema kwa maneno ya dharau, ‘Mn, basi na tuongoze kwa Twala. Sisi hatutaki kusema na watu wanyonge na wadogo.’

Yule mzee akajibu, ‘Vema, mabwana wangu. Sisi tunawinda muda wa siku tatu kutoka mji wa mfalme, lakini mabwana muwe na subira na sisi tutawaongozeni.’ Nikajibu, ‘Vema, wakati wote upo mikononi mwetu, maana sisi hatufi.

Tu tayari mtuongoze. Lakini wewe Infadus, na wewe Skraga, angalieni! Msitudanganye, msijaribu kututega, maana tutatambua fikra zenu duni kabla hazijaingia katika akili zenu, na hatutakosa kujilipiza kisasi.

Nuru ile inayotoka katika jicho la Yule mwenye miguu mitupu na ndevu upande mmoja tu wa uso, itakuaribuni, itapita katika nchi yenu. Meno yake yanayotoweka yatajibana mikononi mwenu na yatakuleni nyinyi na wake zenu na watoto wenu; mianzi ya ajabu itasema nanyi kwa sauti na itawafanyeni kuwa kama takataka.

Angalieni.’ Basi maneno yangu yaliwatisha sana, na yule mzee alijibu, ‘Koom! Koom!’
Baadaye nilipata kufahamu ya kuwa yale maneno ndiyo wanayoyatumia kwa kumwamkia mfalme.

Akageuka akawaamuru watu wake, na mara upesi wakashika vitu vyetu ili wavichukukue, ila bunduki hawakushika, maana waliziogopa. Hata na nguo za Bwana Good wakazishik, naye alipoona hivi akataka kuzitwaa, ‘Ee, Bwana mwenye jicho linalong’aa na meno yanayoyeyuka, usitwae nguo, maana watumishi wako watazichukua.’

Bwana Good akasema kwa Kiingereza, ‘Ndiyo, lakini nataka kuziva.’ Umbopa akatafsiri maneno yake, na Infadus akajibu, ‘Hapana Bwana, usifiche miguu yako mizuri iliyo meupe tusiione tena? Tokea sasa lazima uvae shati na viatu na miwani yako tu basi.’

Na mimi nikaongeza, ‘Ndiyo, na tena lazima uache ndevu upande mmoja tu wa uso wako. Ukijibadili kwa namna yoyote watu hawa watafikiri kuwa tunawadanganya. Nakusikitikia, lakini kweli, lazima ufanye hivyo. Kama wakishuku habari hizi si za kweli, basi maisha yetu yatapotea kabisa.’

Bwana Good akasema, ‘Je, unasema kweli?’ Nikamjibu, ‘Ndiyo, nasema kweli kabisa, maana miguu yako meupe mizuri na miwani yako imekuwa ni umbo lako na lazima uvumilie tu.’ Akavumilia lakini hakuzoea, mpaka baada ya kadiri ya siku kumi, kwenda akivaa nguo chache hivi.
Hii kitu ni tama wakuu

Pamoja sana mkuu blackstarline
 
Skraga akapunga mkuki wake mara moja, mara ya pili, akapiga. Aah! Umempiga, umetoka upande wa pili kadiri ya futi moja.

Akanyosha mikono yake juu akaanguka, akafa. Basi yamekwisha; pale maiti amelala, nasi bado hatujatambua vema mambo yaliyotokea. Bwana Henry akaruka juu na kupiga ‘Lahaula,’ lakini mara alikaa tena, maana kila mtu alikaa kimya.

Mfalme akasema, ‘Lilikuwa pigo zuri sana. Haya, mwondoe.’ Na watu wanne wakatoka katika kikosi wakamwinua Yule mtu aliyeuawa wakamchukua. Hapo tulisikia ile sauti ndogo tena ya Yule kama nyani, ‘Futeni alama ya damu, futeni. Amri ya mfalme imetekelezwa.’

Mwanamwali mmoja akatoka amechukua chokaa katika kapu akainyunyiza juu ya alama ya damu. Huku nyuma Bwana Henry alishikwa na ghadhabu kuu; nikamzuia kwa shida asisimame, nikamnong’oneza, ‘Kaa, kaa usisimame au tutapoteza maisha yetu.’ Akakubali akakaa.

Twala alikaa kimya mpaka alama zile za damu zimekwisha futwa, ndipo aliposema, ‘Watu weupe mmetoka wapi, mmekuja kutafuta nini?’ Nikajibu, ‘Tumetoka katika nyota, usituulize kwa namna gani, Tumekuja kutazama nchi hii.’

Akasema, ‘Mmesafiri kutoka mbali ili kuja kutazama kitu kidogo. Je, na Yule ametoka katika nyota vile vile?’ (akamwonyesha Umbopa.) Nikamjibu, ‘Hakika hata watu wa rangi uliyonayo wewe wapo mbinguni; lakini Mfalme Twala haifai kuuliza mambo ambayo huwezi kuyafahamu.’

Akajibu, na sauti yake iliyochukiza sana, ‘Nyinyi watu wa nyota mnasema kwa sauti na maneno ya kiburi sana, afadhali mkumbuke kuwa nyota ziko mbali, na nyinyi mpo hapa. Je, itakuwaje nikikufanyeni kama Yule waliye mchukua?’

Nikacheka sana, lakini katika moyo wangu sikuwa na kicheko, nikajibu, ‘Ee Mfalme, tahadhari sana, nenda pole pole juu ya mawe ya moto usije ukaunguza nyayo zako; uushike mkuki kwenye mpini usije ukakukata mkono.

Ukigusa hata unywele mmoja wa vichwa vyetu utaangamia papo hapo. Je, huyu Infadus na Skraga hawajakwambia sisi ni watu gani? Umepata kuwaona watu kama sisi?’ (Nikamwonyesha Bwana Good, maana nilijua hakika kuwa hajaona mtu kama yeye.) Mfalme akamtazama Bwana Good akasema, ‘Ni kweli, sijaona.’


Basi nikaendelea nikasema, ‘Hawajakwambia namna tunavyoweza kuwaua watu kwa mbali?’ Mfalme akajibu, ‘Wameniambia, lakini sisadiki. Nataka nione kwa macho yangu ukimuua mtu. Muue mtu Yule anayepita kule, nami nitasadiki.’ Akaonyesha mtu aliyekuwa akipita upande mwingine wa mji.

Nikajibu, ‘La, sisi hatumwagi damu ya watu wasio na hatia lakini ukitaka kuona, basi amuru mtu alete ng’ombe, na kabla hajaenda hatua ishirini nitamuua Yule ng’ombe.’ Mfalme akacheka, akasema, ‘Hapana, ukimuua mtu ndipo nitakapo sadiki.’

Nikajibu, ‘Vema’ wewe nenda upite uwanjani na kabla hujafika mlangoni utakuwa maiti; au kama hupendi kwenda wewe mwenyewe, basi mpeleke mwanao Skraga.’ Basi kusikia hayo tu, Skraga akalia sana akaondoka akakimbilia nyumbani. Twala akakunja uso akasema, ‘Leteni ng’ombe.’


Mara watu wawili walikwenda mbio kuleta ng’ombe, nikamwambia Bwana Henry, ‘Sasa Bwana Henry ni juu yako kumpiga ng’ombe, maana nataka mfalme ajue kuwa si mimi tu ninayeweza kupiga bunduki.’

Basi tukakaa kimya kidogo, halafu tukaona ng’ombe anakuja mbio, na mara alipoona wale watu wengi, akasimama.

Nikamwambia Bwana Henry. ‘Haya sasa piga.’ Na pale pale akaelekeza bunduki akapiga. Mara ile ile ng’ombe alilala kafa. Basi hapo watu wote walishangaa wakazuia pumzi; nikageuka nikamwambia mfalme, ‘Je, mfalme nimesema kweli?’
Mfalme akajibu, na sauti yake ilikuwa ya mtu anayeogopa sana, ‘Ndiyo, mtu mweupe, umesema kweli.’

Basi nikaendelea nikasema, ‘Sikiliza, Twala. Umeona sasa unaweza kusadiki kuwa sisi tumekuja kwa amani wala si kwa vita. Tazama.’ Nikamwonyesha ile bunduki tuliyomletea.
‘Huu ndio mwanzi utakaokupa nguvu kuua kama sisi tunavyoua, lakini naweka sharti hii, usimuue mtu. Ukiielekeza kumpiga mtu, utajiua wewe mwenyewe.

Ngoja, nitakuonyesha. Mwambie mtu mmoja apime hatua arubaini kisha achomeke mkuki katika ardhi na bamba lake lituelekee sisi.’

Akaamuru ikafanywa, nikasema, ‘Sasa tazama utaona kuwa nitalivunja nikapiga bunduki.

Risasi ikalipiga lile bamba la mkuki likavunjika vunjika vipande. Tena watu wote walizuia pumzi kwa kushangaa, nikasema, ‘Sasa Twala, twakupa mwanzi huu, na baadaye nitakufundisha namna ya kuutumia, lakini uangalie sana usiutumie uchawi huu wa nyota kumdhuru mtu wa duniani.’


Nikampa ile bunduki. Mfalme akaitwaa kwa kuiogopa akailaza miguuni pake. Alipokuwa akiiweka, Yule kama nyani akatamani kutoka kivulini mwa nyumba. Alitambaa kwa miguu na mikono, lakini alipofika mahali alipokuwa kakaa mfalme, akasimama, akafunua uso wake ambao ulikuwa wa kutisha mno.

Alikuwa mwanamke kizee sana sana, na uso wake umekunjika mno kwa uzee hata kuwa kama uso wa mtoto mchanga wenye mikunjo mingi.

Kinywa chake kilikuwa kama ufa katika mikunjo hiyo, na chini ya ufa, kidevu chake kilitokeza kama ncha. Alikuwa na pua ndogo na kama macho yake yasingelioneka , uso wake ungalikuwa kama uso wa maiti iliyokauka kwa kuwekwa juani.


Lakini macho yake yaling’aa kama mwenye akili nyingi. Kichwa chake kilikuwa kipara, hana nywele kabisa, na ngozi ya utosini iliyokunjana ikimeta kama ngozi ya nyoka.
Mtu huyu alitufanya kutetemeka kwa hofu.

Alisimama kimya kidogo, kisha akaweka mkono wake uliokuwa na makucha marefu sana, juu ya bega la mfalme Twala, akasema kwa sauti nyembamba na kali, ‘Sikiliza, Ee Mfalme! Sikilizeni, Ee Mashujaa!


Sikilizeni, Ee milima na nyanda na mito, na nchi ya Wakukuana! Sikilizeni, Ee mbingu na jua, Ee mvua na dhoruba na ukungu! Sikilizeni, Ee wanaume na wanawake, Ee vijana na wanawali, na nyinyi watoto msiozaliwa bado! Sikilizeni, vitu vyote vyenye uhai vitakavyokufa! Sikilizeni, vitu vyote vilivyokufa vitakavyofufuka na kufa tena! Sikilizeni, nami nitabashiri. Sasa nabashiri, nabashiri!’

Sauti yake ilififia na watu wote walishikwa na hofu kuu. Kizee huyu alitisha mno. Akaendelea. ‘Damu! Damu! Damu! Mito ya damu; damu pote pote. Naiona, naisikia, naionja ina chumvi! Ni nyekundu juu ya nchi! Inanyesha kutoka mawinguni. Nyayo! Nyayo! Nyayo! Nyayo za watu weupe watokao mbali. Zinatikisa nchi; nchi inatetemeka mbele ya bwana wake.


Damu ni njema, damu nyekundu hung’aa; hakuna harufu kama harufu ya damu iliyomwagwa kwa kiasi. Simba watailamba na kunguruma, tai wataoshea mbawa zao ndani yake na watalia kwa furaha.


Mimi ni mzee! Mimi ni mzee! Nimeona damu nyingi; ha,ha.! Lakini nitaona nyingi zaidi kabla sijafa, nitafurahi. Baba zenu walinijua, na baba zao walinijua, na baba za baba zao. Nimeona watu weupe, ninajua tama zao. Mimi mzee, lakini milima hii imenipita kwa uzee. Nani aliyetengeneza Njia Kuu, niambieni?’


Nani aliyechora sanamu zile juu ya miamba, niambieni? Nani aliyeumba wale Watatu walio kimya wanaotazama shimo, niambieni?’

Akaelekeza mkono wake kuonyesha kwenye milima ile mirefu. Akaendelea, ‘Hamjui, lakini mimi najua. Walikuwa watu weupe waliowatangulieni nao watakuja hapo nyinyi mtakapokwisha kutoweka, watawaleni na kuwaaharibuni.


Ndiyo! Ndiyo! Ndiyo! Na hao watu weupe walijia nini? Wenye kutisha, Wenye elimu ya uchawi na maarifa yote, wenye nguvu wasiochelea! Ee Mfalme, lile jiwe linalong’aa katika kipaji chako ni nini? Mikono ya nani ilifuma nguo hizo za minyororo unazovaa kifuani, Ee mfalme?

Hujui!, ila mimi najua. Mimi, mzee, mimi mwenye busara, mimi Isanusi, Kichawi.’ Akatugeukia akasema, ‘Nyinyi watu weupe wa Nyota mnatafuta nini? Mnatafuta mmoja wenu aliyepotea?


Hayupo. Hapana mguu mweupe uliokanyaga nchi hii tangu vizazi na vizazi vilivyopita ila mara moja tu, naye alipoondoka hapa aliondoka kwenda kufa tu.

Mmekuja kuchuma mawe yanayong’aa; najua, najua; damu itakapokwisha kukauka mtayaona; lakini je, mtarudi mtokako au mtakaa na mimi?


Ha!ha!ha! Na wewe, wewe mwenye ngozi nyeusi, mwenye udaha, nani wewe, unatafuta nini? Wewe hutafuti mawe yanayong’aa wala chuma cha dhahabu, hayo unawaachia watu weupe watokao kwenye Nyota.

Nadhani nakujua; nadhani naweza kusikia harufu ya damu iliyo katika moyo wako. Haya uvue mkanda ..

Basi hapo Yule kizee akawa amepandwa na pepo akaanguka chini na povu likamtoka kinywani, akachukuliwa ndani ya nyumba.

Mafalme akasimama anatetemeka, akapunga mikono. Mara moja vikosi vyote vikaanza kutoka kwa taratibu, na baada ya dakika kumi hapakuwa na mtu ila sisi na Mfalme na watumishi wachache.

Mfalme akasema, ‘Watu weupe, ‘ninayo nia ya kuwauweni, Gagula amesema maneno ya ajabu juu yenu. Mnasemaje?’ Nikacheka nikasema, ‘Angalia, Ee Mfalme, sisi si wepesi wa kuuawa.

Umeona kufa kwa Yule ng’ombe; wataka kuwa kama alivyo Yule ng’ombe?’
Mfalme akakunja uso akasema, ‘Si busara kujaribu kumtisha mfalme.’
Nikasema, ‘Hatujaribu kukutisha, tunayoyasema ni ya kweli.

Ukijaribu kutuua basi utatutambua’ Yule mfalme akaweka mkono kichwani akafikiri, kisha akasema, ‘Nendeni kwa amani.


Usiku wa leo kuna ngoma kuu. Mtayiona. Msiogope na kudhani labda nitajaribu kuwanasa. Kesho nitafikiri juu ya habari zenu.’ Nikajibu, ‘Vema, Ee mfalme.’ Kisha tukaondoka, tukafuatana na Infadus tukaenda nyumbani kwetu.
[emoji119] [emoji119] hii kitu ni kali wakuu
 
Hainichoshi kuisoma riwaya hii ingawa nimekuwa nikiisoma tangu ningali kijana mdogo hadi salsa!
Hakika ni riwaya nzuri na yenye milima na mabonde yenye kusisimua moyo na akili pia bila kusahau kuongeza imani juu ya uwepo wa Mungu, Muumba mbingu,ardhi na vyote vilivyomo humo (vilivyo bayana na vya siri)
Ahsante sana mtoa Uzi wenye mtiririko huu! Umenipa mapumziko mazuri ya mwishoni mwa juma hili!
Ningefarijika pia iwapo ungeweza kunikumbusha namna ninavyoweza kuipata riwaya ya Kiswahili iliyoitwa "USO WA MAUTI"
Ni riwaya niliyotokea kuipenda sana tangu nikiwa mdogo ingawa kwa bahati mbaya sana jina la mtunzi limenitoka,ingawa nakumbuka ilikuwa na mandhari ya Tanzania Visiwani hivi (Zanziba) ingawa sina hakika sana juu ya hili!
 
Hainichoshi kuisoma riwaya hii ingawa nimekuwa nikiisoma tangu ningali kijana mdogo hadi salsa!
Hakika ni riwaya nzuri na yenye milima na mabonde yenye kusisimua moyo na akili pia bila kusahau kuongeza imani juu ya uwepo wa Mungu, Muumba mbingu,ardhi na vyote vilivyomo humo (vilivyo bayana na vya siri)
Ahsante sana mtoa Uzi wenye mtiririko huu! Umenipa mapumziko mazuri ya mwishoni mwa juma hili!
Ningefarijika pia iwapo ungeweza kunikumbusha namna ninavyoweza kuipata riwaya ya Kiswahili iliyoitwa "USO WA MAUTI"
Ni riwaya niliyotokea kuipenda sana tangu nikiwa mdogo ingawa kwa bahati mbaya sana jina la mtunzi limenitoka,ingawa nakumbuka ilikuwa na mandhari ya Tanzania Visiwani hivi (Zanziba) ingawa sina hakika sana juu ya hili!
Kweli kabisa hii riwaya inafundisha sana, pia mafanikio ya mtu yanaweza kuja kwa njia tofauti.Riwaya “USO WA MAUTI” sijawahi kuisoma! Pengine siku nitakutana nayo ikitoke nitakujulisha mkuu.
 
Kweli kabisa hii riwaya inafundisha sana, pia mafanikio ya mtu yanaweza kuja kwa njia tofauti.Riwaya “USO WA MAUTI” sijawahi kuisoma! Pengine siku nitakutana nayo ikitoke nitakujulisha mkuu.
Pamoja sana chief tupe muendelezo umetuweka sana Mkuu wikiend hii wengine ndo starehe zetu hizi mkuu
 
Mkuu mwaga madude, galula anasema ukweli , kuna mwanawali mmoja atahitajika kuuwawa kwenye ngoma ya usiku ila watamwokoa .bila kusahau wataponea chupuchupu kuuwawa katika mashimo ya suleman.mkuu dondosha vitu jumapili hii
 
SURA YA KUMI

Tulipofika nyumbani nilimwashiria Infadus aingie pamoja nasi, nikamwambia, ‘Infadus, tunataka kusema nawe.’ Akajibu, ‘Semeni, mabwana zangu.’ Nikasema, ‘Tumeona kuwa huyu Mfalme Twala ni mtu katili.’ Akajibu, ‘Ni kweli, mabwana zangu.

Nchi yote inalalamika kwa sababu ya ukatili wake. Usiku huu mtaona. Itakuwapo ngoma kuu ya kutambulisha wachawi na wengi watatambuliwa kuwa ni wachawi na kuuawa. Hapana mtu anayeweza kusema kuwa maisha yake yapo salama.

Mafalme akiwatamani ng’ombe wa mtu, au mke wa mtu, au akishuku kuwa atawashawishi watu kumwasi basi Yule Gagula mliyemwona au wanawake wengine katika wanawake wanaotambulisha wachawi, watamchagua usiku huu naye atauawa. Wengi watakufa kabla ya mwezi kufifia usiku huu.


Kila mara ni hivyo. Labda hata na mimi nitauawa. Mpaka sasa nimeokoka kwa kuwa ni hodari katika vita, nami napendwa sana na askari; lakini sijui hesabu ya siku zangu za uhai.

Nchi inaugua kwa ajili ya ukatili na maovu ya Mfalme Twala; imechoka naye na mambo yake ya kumwaga damu.’

Nikamuuliza, ‘Infadus, kwa nini watu hawamwondoi? Akajibu, ‘Mabwana zangu, yeye ndiye mfalme, na akiuawa, Skraga atatawala mahali pake na moyo wa Skraga akitawa nira itakayowekwa shingoni mwetu itakuwa nzito kuliko ile ya Twala.


Ingalikuwa Imotu hakuuawa, au Ignosi mwana wake angalikuwepo, ingalikuwa bora; lakini wote wawili wamekufa.’ Hapo tukasikia sauti; tukageuka tukaona kuwa ni Umbopa, akasema, ‘Unajuaje kuwa Ignosi alikufa?’ Yule Infadus akasema, ‘Je, namna gani we mtoto? Nani aliyekupa ruhusa ya kusema?’


Akajibu, ‘Sikiliza, Infadus, nami nitakwambia hadithi. Zamani, wakati alipouawa Mfalme Imotu katika nchi hii, mke wake alikimbia pamoja na mtoto Ignosi, sivyo?’ Akajibu, ‘Ndiyo.’
Umbopa akasema, ‘Ilisemwa kuwa mwanamke huyo na mtoto wake walikufa katika milima, sivyo?’ Infadus akasema, ‘Ndiyo.’


Umbopa akaendelea, ‘Basi ilivyo ni kuwa Yule mama na mtoto Ignosi hawakufa. Walivuka milima wakaongozwa na kabila la watu wanaotembea tembea jangwani mpaka kufika katika nchi yenye maji na majani na miti.’

Infadus akauliza, ‘Je, unajuaje hayo?’ Umbopa akajibu; ‘Sikiliza. Walisafiri mbali kwa muda wa miezi mingi mpaka kufika nchi ya watu waitwao Amazulu, nao ni ukoo mmoja na Wakukuana.

Watu hawa kazi yao ni vita, Wakakaa nao miaka mingi mpaka mama mtu akafa. Basi alipokufa, Yule mtoto Ignosi akawa msafiri tu, akasafiri katika nchi za ajabu wanapokaa watu weupe, akakaa nao miaka mingi, akajifunza maarifa yao.’


Yule Infadus akasema kwa sauti ya kutosadiki, ‘Ni ‘hadithi nzuri, lakini ya nini?’ Basi Umbopa akaendelea, akasema, ‘Miaka mingi alikaa akifanya kazi ya utumishi na uaskari, lakini katika moyo wake alikumbuka yote aliyoambiwa na mama yake juu ya nchi yake, alitamani sana namna ya kufika tena katika ile nchi, ili apate kuwaona watu wake na nyumba ya baba yake, kabla hajafa.


Miaka mingi alikaa akingoja, na halafu alipata nafasi, maana alionana na watu weupe waliokusudia kutafuta nchi ile isiyojulikana, akafuatana nao. Wale watu weupe walisafiri wakaenda mbele tu wakimtafuta mtu mmoja tu aliyepotea.


Walivuka jangwa lenye joto, wakavuka milima yenye theluji, wakafika nchi ya Wakukuana, na pale ndipo walipokuona wewe, Ee Infadus.’

Yule Infadus akashangaa, akasema, ‘Kweli, wewe, una wazimu kusema hivyo.’ Umbopa akasema, ‘Unafikiri tu hivyo; tazama nitakalokuonyesha, Ee wewe mjomba wangu. Mimi ni Ignosi, Mfalme wa haki wa Wakukuana!’

Basi hapo alifungua nguo yake akasimama uchi mbele yetu, akasema, ‘Tazameni, hii ni nini?’ Akaonyesha kiunoni mwake amechanjwa alama ya nyoka anayezunguka kiuno. Infadus akatazama, na macho aliyakodoa kwa kushangaa, kisha akampigia magoti akasema, ‘Koom!Koom!

Ndiye mtoto wa ndugu yangu; ndiye mfalme.’ Umbopa akasema.’ Umbopa akasema, ‘Ee mjomba wangu, sikukwambia hayo? Inuka; mimi sijawa mfalme, lakini kwa msaada wako pamoja na msaada wa hawa watu weupe mashujaa walio rafiki zangu, nitakuwa mfalme.


Lakini Yule kichawi Gagula alisema kweli, yaani nchi italowa kwa damu kwanza, naye damu yake italowesha nchi pia, yaani ikiwa anayo damu, kwani ndiye aliyemuua baba yangu kwa maneno yake, ndiye aliyemfukuza mama yangu. Na sasa wewe Infadus, imekupasa uchague. Utakubali kuweka mikono yako katika mikono yangu uwe mtu wangu?


Wewe utakubali kushirikiana nami katika hatari zilizo mbele yangu, na’ kunisaidia nimwangushe huyo jeuri na muuaji, au huwezi kukubali? Chagua.’


Yule mzee alikamata kichwa akafikiri, kisha akaondoka akamjia Umbopa, yaani Ignosi, akapiga magoti mbele yake akamshika mkono, akasema, ‘Ignosi, mfalme wa haki wa Wakukuana, naweka mikono yangu katika mikono yako, nami ni mtu wako mpaka kufa.


Ulipokuwa mtoto nilikupakata nakakulea, na sasa mkono wangu ulio dhaifu utapigana kwa ajili yako na uhuru.’


Umbopa akajibu, ‘Vema, ewe Infadus. Nikishinda wewe utakuwa mtu mkubwa katika ufalme wangu chini ya mfalme mwenyewe.

Nikishindwa, hapana ila kifo, na wewe tangu hapo si mbali na kufa sasa. Simama, mjomba wangu. Na nyinyi watu weupe, mtanisaidia? Je yale mawe meupe sitaweza kuwapa? Hakika nikishinda yale mawe meupe mtayaona na kuchukua kwa kadiri ya nguvu zenu. Je, mtakubali?

Nikatafsiri maneno yake, na Bwana Henry akajibu, ‘Mwambie kuwa hafahamu tabia ya Mwingereza. Mali ni njema, nayo ikitujia tutaiokota; lakini mungwana hajiuzi kwa mali. Lakini mimi binafsi nasema haya:

Tokea mwanzo nilimpenda Umbopa, na kwa kadiri ya nguvu zangu nitamsaidia. Nitafurahi sana kujaribu kumtia adabu Yule shetani mwovu Twala.
 
Je, nyinyi Bwana Good na Quatermain, mwasemaje?’
Bwana Good akasema, ‘Waweza kumwambia ya kuwa mimi nipo tayari kabisa kumsaidia, lakini neno moja nalitaka, nalo ni kuruhusiwa kuvaa suruali zangu.’


Basi nikatafsiri maneno hayo yote, na Ignosi ambaye ndiye Umbopa akasema, ‘Vema rafiki zangu, nawe Makumazahn wewe utakuwa pamoja nami? Maana wewe ni mwindaji wa zamani mwenye uerevu kupita ule wa nyati aliyejeruhiwa.’


Nilifikiri kwanza nikajikuna kichwa, kisha nikasema, ‘Umbopa au Ignosi, mimi sipendi vita, ni mtu wa amani na tena ni mwoga kidogo (na hapo Umbopa akacheka) lakini napenda kuambatana na rafiki zangu.


Wewe ulitusaidia sisi, nami nitakusaidia wewe. Lakini mimi ni mfanyabiashara na kwa hiyo, ikiwa tutapata almasi, basi nakubali ahadi yako. Na tena, kama ujuavyo, sisi tulikuja kumtafuta ndugu yake Bwana Henry aliyepotea; lazima utusaidie kumtafuta.’

Basi Ignosi akajibu, ‘Nemekubali, lakini wewe, Infadus, apa kwa alama hii ya nyoka iliyochanjwa kiunoni mwangu kisha uniambie kweli. Mtu mweupe yeyeto ameingia katika nchi hii?

Akajibu, ‘Hapana, Ignosi.’
Ignosi akasema, ‘Mtu mweupe angalionekana au habari za mtu mweupe zingalivuma, wewe ungalipata habari?’ Akajibu, ‘Hakika ningalipata habari.’


Akamwambia Bwana Henry, ‘Umesikia, Inkubu, hakufika katika nchi hii.’ Bwana Henry akasikitika akasema, ‘Basi, basi, ni hivyo. Naona hakufika hata hapa, masikini, masikini! Tumefanya safari ya bure. Lakini ndiyo Mungu alivyo panga.’


Basi nikaona afadhali kumtoa katika fikira za huzuni, nakasema, ‘Haya, sasa tufanye kazi.

Ni vizuri kuwa mfalme wa haki, Ignosi, lakini utafanya nini upate kuwa mfalme kweli?’ Akajibu, ‘Hayo mimi sijui; je, Infadus unalo shauri linalofaa?’

Mjomba wake akajibu, ‘Ignosi, Mwana wa Umeme, usiku wa leo itakuwapo ngoma kuu ya kutambulisha wachawi. Wengi watatambuliwa na kuuawa, na wengi zaidi watajaa huzuni na masikitiko na hasira juu ya mfalme Twala.


Ngoma itakapokwisha nitasema na wakubwa, na ikiwa nitaweza, wao watasema na watu walio faraghani, nami nitawaleta kwako wapate kushuhudia kuwa kweli wewe ni mfalme. Nadhani kabla ya jua kuchomoza kesho utakuwa na mikuki ishirini elfu tayari kutii amri zako.

Na sasa lazima niende nikafikiri na kusikiliza na kuweka yote tayari. Baada ya ngoma kwisha ikiwa nita kuwa hai, tukutane hapa hapa, tutaweza kuongea zaidi. Lakini haikosi kutakuwa na vita.’


Basi hapa mazungumzo yetu yalivunjika kwa kuwa matarishi wa mfalme walikuja. Tukakaribia mlangoni na tukawapa ruhusa kuingia, kisha watu watatu waliingia na kila mtu alikuwa kachukua nguo za minyororo ya chuma iliyong’aa na iliyofumwa, na shoka zuri la vita.

Wakasema, ‘Hizi ni zawadi kutoka kwa mfalme, za watu weupe waliotoka katika nyota.’ Nikajibu, ‘Tunamshukuru mfalme.’ Basi wakatoka wakaenda zao nasi tukazitazama nguo zile. Kazi yake ilikuwa nzuri mno kupita zote tulizoona.

Nikamuuliza Infadus, ‘Je, hizi nguo zina tengenezwa hapa kwenye hii nchi?’
Akajibu, ‘Hapana, bwana wangu, tumezirithi kutoka kwa mababu zetu.

Hatujui ni nani aliyezitengeneza, na sasa zimebaki chache tu. Waana wa mfalme tu ndio wanaoruhusiwa kuzivaa. Zina nguvu kama zile za uchawi na mkuki hauwezi kuzipenya. Mtu akivaa nguo hizi katika vita yu salama.


Mfalme amependezwa sana, au ameogopa sana, maana asingewaleteeni nguo hizi. Mabwana zangu, afadhali mzivae usiku wa leo.’

Basi tulipumzika siku ile tukaongea juu ya mambo yaliyotokea. Jua lilipotua tuliona mwangaza wa mioto mingi na katika giza tulisikia vishindo vya nyayo za watu wengi na vya mikuki yao, vikosi vilipokuwa vikipita na kujipanga katika utaratibu wa kujitayarisha kwa ngoma kuu ya usiku.


Baadaye kidogo mwezi ulitoka ukaangaza nchi yote, tukasimama na kutazama mbalamwezi; akaja Infadus amevaa nguo zake nzuri za vita, amefuatana na askari ishirini, kutupeleka kwenye ngoma.

Tulikuwa tumekwisha vaa zile nguo za minyororo ya chuma kama alivyotushauri, na juu yake tukavaa nguo zetu za kila siku.

Tukajifunga bastola zetu, tukachukua mikononi mashoka yale ya vita aliyotupa mfalme, tukaondoka.

Tulipofika kwenye jumba kuu tuliona mahali palipojaa watu kiasi elfu ishirini waliopangwa kwa vikosi.

Vikosi hivyo viligawanywa katika makundi, na katikati ya kila kundi na kundi waliacha njia ili kusudi wale watakaotambulisha wachawi wapate nafasi ya kupita.
 
Back
Top Bottom