Kwanza serikali haiwez ikakupa mtaji kizembe namna hiyo...yaan maisha haya bora uchanwe live tu... maisha magumu kweli lakini napinga kbs serikali kuja kukupa mtaji...umekaa tu eti unasubirinkushikwa mkono..lol
Kupewa mtaji na serikali ni kujiendekeza, na wengi watapewa lkn hawatafanyia kitu zaidi ya kula na kunywa ..tatizo litabaki pale pale.
Siku hizi jamani kuna biashara za kila Aina..hata kwa 20,000 mtu anaanza biashara..ukipambana unapata mtaji ambao unataka. Vijana mjini wameamka yaani kila biashara inafanywa Ili mradi maisha yaende.
Binafsi sijafikia ninapotaka ila namshukuru Mungu naiona mbele yangu. Nilishalia mtaji weee Lkn nikaona ni kazi bure..hatakuja tokea mtu akupe mtaji hata ndugu yako hakupi.
So nikupambana kuanzia chini kabisa.
Walemavu ninaowaonea huruma ni wale wasioona. Ila mlemavu alie na mikono inayofanya kazi tena msomi mwenye degree yake kulilia kupewa mtaji kwa kigezo cha ulemavu sio sahihi. Apambane Kama sisi..
Ukute alikuwa anapata mkopo..angeweza kutoa hapo 200,000 ya mtaji. Ila ndo hivyo vijana tunawaza kupata mtaji mamilioni ili tufungue makampuni makubwa. Kwa maisha ya sasa haitatokea...pesa imekuwa ngumu kupita maelezo.
Tuache kulialia kila siku..tumesharahisishiwa biashara kitambulisho Cha mjasiriamali 20,000 kwa mwaka. Tufanye chochote kile ila ndo hivyo sie tunaojiita wasomi tunaona aibu.
** Wengi wanaolalamika (hata wasio walemavu) ni wale tunaojiita wasomi. Tunawaza mambo makubwa ingawa kiuhalisia hayapo hivyo.
**Kuna shughuli kibao za kutengeneza vitu...YouTube imejaa madini kibao yaani ukiwa mtu wa kupenda kutengeneza vitu Kama mimi hukosi cha kufanya. Kinachobakia ni kutafuta wateja tu..na Kama kazi yako nzuri hukosi wateja ingawa changamoto hazikosekani pia, kikubwa ni kujaribu na sio kulialia.
Ajira hakuna watu wajiongeze