Haitopita miezi miwili bila Waziri Masauni au IGP Wambura kung'olewa ofisini

Haitopita miezi miwili bila Waziri Masauni au IGP Wambura kung'olewa ofisini

Mr Dudumizi

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2020
Posts
7,799
Reaction score
14,215
Habari zenu wanaJF wenzangu,

Hawa jamaa wawili ni kama vile wamepewa majukumu makubwa wasiyoyaweza. Watu wanatekwa, wanauwawa na wengine kupotezwa kimya kimya wao wanaangalia tu. Sasa sijui jukumu la waziri wa mambo ya ndani na IGP ni nini?

Sikatai kwamba inawezekana polisi au serikali haihusiki na yanayoendelea, sikatai kwamba inawezekana kuna kundi la majambazi na watu wasioitakia mema nchi yetu wanaweza kufanya haya ili zigo liiangukie polisi na serikali, lakn wao kama serikali kupitia vitengo vyao vya upelelezi wamefanya nini kuzuia haya yasiendelee kutokea?

Inashangaza katika nchi tunayosema ni ya amani askari anashindwa hata kuvaa sare kwenda kumkamata mtuhumiwa kweli!! Je sare za polisi zilishonwa kwa ajili ya kina nani?

Unakuta kundi la watu wanne au watatu likiwa limevaa nguo za kawaida, eti linaenda kumkamata mtu mwembe chai, likiulizwa nyinyi ni kina nani linasema sisi ni askari kutoka mwenge tumekuja kumkamata mtuhumiwa.

Sasa unajiuliza inakuaje askari atoke mwenge kuja kumkamata mtuhumiwa mwembechai, je magomeni askari wameisha, kwanini wasitumiwe askari wa magomeni kumkamata mtuhumiwa? Hiyo tisa, kumi je kwanini hawana sare za polisi, RB, barua ya mjumbe au mwenyekiti wa serikali ya mtaa nk.

Sasa kwa style hii ya ukamataji mnafikiri watu wabaya hawatokosa kujipenyeza ni kufanya haya kwa maadui zao wakijua kwamba jumba bovu litawaangukia polisi na mamlaka?

Kwanini hamrudishi utaratibu mzuri wa ukamataji wa kufuata sheria? Au mpaka mtumbuliwe ndo muanze kufikiria ambayo mngefanya. Maana tumeshaanza kusikia mpaka wanafunzi na viongozi wa dini wanapotea na wengine kukutwa wameuwawa.

Kuna uwezekano mkubwa wa Masauni na Wambura kukalia kuti kavu. Very soon time will tell us...
 
Habari zenu wanaJF wenzangu,

Hawa jamaa wawili ni kama vile wamepewa majukumu makubwa wasiyoyaweza. Watu wanatekwa, wanauwawa na wengine kupotezwa kimya kimya wao wanaangalia tu. Sasa sijui jukumu la waziri wa mambo ya ndani na IGP ni nini?

Sikatai kwamba inawezekana polisi au serikali haihusiki na yanayoendelea, sikatai kwamba inawezekana kuna kundi la majambazi na watu wasioitakia mema nchi yetu wanaweza kufanya haya ili zigo liiangukie polisi na serikali, lakn wao kama serikali kupitia vitengo vyao vya upelelezi wamefanya nini kuzuia haya yasiendelee kutokea?

Inashangaza katika nchi tunayosema ni ya amani askari anashindwa hata kuvaa sare kwenda kumkamata mtuhumiwa kweli!! Je sare za polisi zilishonwa kwa ajili ya kina nani?

Unakuta kundi la watu wanne au watatu likiwa limevaa nguo za kawaida, eti linaenda kumkamata mtu mwembe chai, likiulizwa nyinyi ni kina nani linasema sisi ni askari kutoka mwenge tumekuja kumkamata mtuhumiwa.

Sasa unajiuliza inakuaje askari atoke mwenge kuja kumkamata mtuhumiwa mwembechai, je magomeni askari wameisha, kwanini wasitumiwe askari wa magomeni kumkamata mtuhumiwa? Hiyo tisa, kumi je kwanini hawana sare za polisi, RB, barua ya mjumbe au mwenyekiti wa serikali ya mtaa nk.

Sasa kwa style hii ya ukamataji mnafikiri watu wabaya hawatokosa kujipenyeza ni kufanya haya kwa maadui zao wakijua kwamba jumba bovu litawaangukia polisi na mamlaka?

Kwanini hamrudishi utaratibu mzuri wa ukamataji wa kufuata sheria? Au mpaka mtumbuliwe ndo muanze kufikiria ambayo mngefanya. Maana tumeshaanza kusikia mpaka wanafunzi na viongozi wa dini wanapotea na wengine kukutwa wameuwawa.

Kuna uwezekano mkubwa wa Masauni na Wambura kukalia kuti kavu. Very soon time will tell us...
Masauni ni Mkojani mwenzentu na ni ndugu katika imaani, haendi popote labda abadirishwe wizara tu.
 
Hali ya nchi yetu inasikitisha sana ,Wafariji nao kauli zao zinachangamana na watesi wetu ,Mungu ailinde Tanzania yetu
Waathirika wa matukio wanatakiwa wafarijiwe na wasaidiwe. Ndo ubinadamu unavyotakiwa kuwa.
 
Kazi sanaa Mama anamuamini sanaa Wambura alimtafuta mwenyewe rejea clips zake yule kiboko ya majambazi yuko wapi....akajibiwa dodoma....
 
Hawawezi kutumbuliwa Kwa sababu aliyewaweka ndiyo hutoa maagizo ya kuwapoteza waliopotea
 
Shida uko police kumejaa vilaza na mazuzu.katika karne hii namna ya kupata Askari wa police haina tofauti na enzi za Ukoloni.
 
Miezi miwili mingi sana ,watu wengi watauawa...waondolewe haraka sana kuokoa roho za watu.
Masauni kashindwa kujifunza hekma kutoka kwa mzee wa hekma hayati alhaji mzee Ally Hassan Mwinyi ambae yeye alijiuzulu hata kwa makosa ambayo yalitokea bila yeye kuamrisha yatokee.

Yeye anaona bora ang'ang'anie madaraka asioyaweza, huku raia wasiokuwa na hatia wengine wanafunzi wakiendelea kupotea katika mazingira ya kutatanisha, wengine kutekwa na kuuwawa bila sababu za msingi.
 
Back
Top Bottom