HAITOTOKEA: Msimu Pekee Ambao Yanga SC Ilikubali Kupoteza Ubingwa Ili Simba SC Asishuke Daraja

Hizi timu haziwezi kushuka daraja kwani nje ya burudani ya soka, zinasaidia sana kuweka amani na utulivu,
Na pia kuimarisha umoja wetu, unaweza kukuta watu hawajuani hata majina lkn
Wanafurahi na kutaniana kisa Simba na Yanga,
 
Achana na stori za Kahawa ile mechi mtani alipigwa kihalali hakuna cha nini wala nini..
 
Maumba ana uhusiano gn na mechi hyo?

Huyo maumba alikuwa mlawiti watoto wa kiume.
 
Utopolo Msijifiche kwenye kichaka cha huruma.

Hii gemu mlifungwa kihalali na Simba na wala hamkuwa na suala lolote la kuisaidia Simba isishuke daraja.

Nakumbuka Yanga walikuja na Ngoma pamoja na kinyago aliyejipaka masizi uso mzima,
Pia walishaandaa t-shirts za yanga bingwa -1988..

Yote hayo yalikuwa ni maandalizi ya kusheherekea ubingwa ..

Matokeo yake kinyago alisubiri Giza liingie ndy aweze kuondoka.,na Ngoma zilifuatwa siku ya pili.
Hyo ni baada ya lile genge zima la kikundi cha mdundiko wa maleft kusambaratika,na kutelekeza vifaa vyao na kukimbia kusikojulikana.

Hizo t-shirts zao za ubingwa walizivaa nyumbani kama night dress..

Nakumbuka kama sio John makelele( zig zag)
Au Edo boy ndy aliyepeleka kilio kwa utopolo.

Yanga alifungwa sababu ya kujiamini kwake..

Simba waliondoka kishujaa huku mashabiki wao wakisukuma bus la wachezaji hadi Msimbazi ,
Makao makuu ya Simba sports club.

Sasa hebu fafanua vizuri,
Ilikuwaje timu iliyopanga kuiokoa Simba ijiandae na mambo yote hayo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…