Haiwezekani mtu mmoja kumiliki hisa 49% - Mwakyembe

Haiwezekani mtu mmoja kumiliki hisa 49% - Mwakyembe

Sasa anasemaje haiwezekani Kwani si ni idadi ya hisa zinazouzwa au kama ni sheria inakataza ni sababu gani sheria inakataza kuna ubaya gani au ndo hizo sheria wanazotuka kwa miswada ya dharura. Yaani Waziri ana Phd lakini kama vile haitusaidii kabisa kwenye michezo. Kwenye sanaa nako makatazo tu kwenye michezo nako hivo hivo wakati inafahamika kuwa uwekezaji kwenye michezo ni wa kusuasua angalau Simba inaonekana kupiga hatua naona serikali anataka kuanzisha figisu figisu ili MO ajiondoe timu ianze kuhangaika. Sijui nani aliyetuloga.
Tanzania inakwamishwa na viongozi wetu wenyewe.
 
Mkuu. serikali wanafurahia migogoro ya simba na yanga,

Yote hayo ni kuwadhibiti wenye hela zao

Hapo sawa, coz hisa 49 unataka wawekezaji 3 while ligi yenyewe tu haina mwekezaji sasa huyo mwekezaji wa kuwekeza kwenye timu anatokea wapi? 😂😂 Yanga si hiyo mpaka leo inahangaika mbona hao wawekezaji wasiende kama ni rahisi hivyo?
 
Watoe grants sio wanapanga vitu wao wanatoa maneno tu. Kilomoni ndio maana anapiga domo
 
TFF hajapata mdhamin wa Ligi Kuu
Yanga - haijapata Mdhamin
Bado unataka asilimia 49 zigawanywe kwa watu watatu, Mzee nakuheshimu ila lingentoka tusi hapa...
Kama ni rahisi zile ruzuku za vyama vyao vya siasa zianze kupewa club za soka.
 
Kwa hapo serikali ifikirie Mara mbili, inaenda kuua tena michezo. Sidhani kama magufuli anataka urasimu huu. Mwakembe anahujumu sana michezo. Mara wachezaji wa nje lazima wawe wanacheza timu zao za taifa, why why why. Sekta ya michezo ingeacha kabisa nguvu ya soko itawale. Wangebuni kodi tu wavune mapesa basi.
 
Hizi timu za kkoo zingekuwa zipo mbali sana ila nimali za wanasiasa,zikiwa independent au kumilikiwa na wachache watakufa njaa wengi
 
Sasa naona hujuma za wazi!! Kuna watu wanataka MO ajiondoe ili Simba irudi ilipotoka. Niombe wanasimba na wanamichezo wote tusikubali suala hili. Wasiturudishe nyuma!

Mbona mashirika mengi ya serikali yaliuzwa kwa asilimia 100. Leo kwenye club ambazo serikali haijawekeza hata cent inataka kuweka masharti.

Nimwombe Waziri akasimamie michezo mingine ambayo umekufa..!!

Huyu Waziri anatuvuruga..huyu ndo anamtuma KILOMONI si bure. Kwanani atoe hilo tamko na kesho KILOMONI aitishe press. Hii n hujuma dhidi ya Simba
 
Mo aiache Simba afu tuone kina Kagere watalipwa na nani maana nina 100pc Sport Pesa wakimaliza mkataba hawatarudi tena
 
Nimesononeka sana huu upuuz sijui utaendelewa kukumbatiwa mpaka lini
 
TFF hajapata mdhamin wa Ligi Kuu
Yanga - haijapata Mdhamin
Bado unataka asilimia 49 zigawanywe kwa watu watatu, Mzee nakuheshimu ila lingentoka tusi hapa...
Kama ni rahisi zile ruzuku za vyama vyao vya siasa zianze kupewa club za soka.
Huyu Mwakyembe atakuwa na PhD fake
 
TFF hajapata mdhamin wa Ligi Kuu
Yanga - haijapata Mdhamin
Bado unataka asilimia 49 zigawanywe kwa watu watatu, Mzee nakuheshimu ila lingentoka tusi hapa...
Kama ni rahisi zile ruzuku za vyama vyao vya siasa zianze kupewa club za soka.
Yanga inadhaminiwa na sport pesa mkuu.
 
Inawekana kiongozi.

Ni mambo ya pesa tu.

Hisa ina thamani. Akuuzie?
 
Sasa anasemaje haiwezekani Kwani si ni idadi ya hisa zinazouzwa au kama ni sheria inakataza ni sababu gani sheria inakataza kuna ubaya gani au ndo hizo sheria wanazotuka kwa miswada ya dharura. Yaani Waziri ana Phd lakini kama vile haitusaidii kabisa kwenye michezo. Kwenye sanaa nako makatazo tu kwenye michezo nako hivo hivo wakati inafahamika kuwa uwekezaji kwenye michezo ni wa kusuasua angalau Simba inaonekana kupiga hatua naona serikali anataka kuanzisha figisu figisu ili MO ajiondoe timu ianze kuhangaika. Sijui nani aliyetuloga.
PhD yake haikusaidii kwasabb uelewa wako ni wa darasa la pili ..itakuwa ngumu sana kwako kumuelewa mwenye PHD. Ushauri rudi Shule ukuze ufahamu wako
 
Hii ni taarifa kutoka kwa Mh Waziri wa Michezo Mh Harisson Mwakyembe , ambapo amedai ili kumiliki hisa zinazofikia 49% za club ya soka basi hakuna budi wawekezaji hao kuwa angalau watatu na si mmoja , yaani club itamiliki 51% wawekezaji watamiliki 49 %

Tamko hili limetoka wapi na limelenga nini ?
Ilikuwa zaidi ya 50 hairuhusiwi, ikaonekana jamaa bado mbishi hata 49 poa, wanakomaätena. Hatari sana.
Anatafutwa MO.
 
  • Thanks
Reactions: mmh
Back
Top Bottom