Hajia Manara aonekana Mwanachi Day japo adhabu yake inaendelea

Hajia Manara aonekana Mwanachi Day japo adhabu yake inaendelea

Mbona ni rahisi tu kujitetea! Atasema amealikwa tu kama MC wa kutambulisha wachezaji.

Sasa TFF watasema kama huyo Manara haruhusiwi hata kufanya shughuli zake za kumhingizia kipato, kisa kafungiwa.
Zisihusishe mpira.
Hivyo hapo kibano kitawafata wote Yanga na Manara
 
Yanga sio wajinga na hio event haihusiani na ligi na wala TFF haiwahusu.

Ni sawa na kutaka kumfungia mtu kushiriki hata mambo binafsi ya kifamilia kama birthday ya watoto wake, n.k
Yanga ni mwanachama wa TFF, hivyo lazima wafate utaratibu wa TFF
 
Ni hivi mkuu, huyu Manara last press aliyoitisha alisema yeye bado msemaji halali
Wa Yanga… na leo kupanda jukwaani na kuwatambulisha wachezaji wa yanga ni kwamba anauthibitishia umma kwamba yeye bado msemaji wa Yanga.Ni dharau ya hali ya juu

Mbaya zaidi hapo uwanjani kuna mawaziri na viongozi wakuu wa chama,Yanga kumtumia Manara wanataka kuonesha kama vile wanaungwa mkono na viongozi wa chama na serikali
Alisema yeye bado ni msemaji wa yanga kwa sababu kamati imegoma kumpa nakala ya hukumu. Sasa swali ni je, kamati wamemkabidhi nakala ya hukumu .?
 
Safari hii hawamwachi. TFF wataogogopa wakimwacha clubs nyingine za football hazitaiheshimu TFF sababu ya dharau za kilabu cha yanga.
 
Hapo fine inahitajika kwa timu ya YANGA ndio imempa mualiko kwa ajili ya kuwa MC wakati wanajuwa muhusika yupo ban kwa kujishughulisha na mpira Tz.
 
Katika Hali isiyo ya kawaida yule msemaji wa utopolo aliyepigwa marufuku kujihusisha na mambo ya mpira ndani na nje ya nchi Kwa muda wa miaka miwili, Leo ameonekana ndani ya uwanja wa mkapa akiwa na lundo la walinzi.. kwenu TFF
A8E17F38-931E-4D02-8BC7-CDF7D1C591B7.jpeg
 
Kosa lake liko wapi? Yuko hapo kama MC wa kutambulisha wachezaji! Hivyo kwa mtazamo wangu naona hana kosa.

Angeitishia Press na kuongelea habari za klabu, hapo ungesema kweli amekiuka masharti ya adhabu yake.
... kutambulisha wachezaji ni suala la kisoka au halihusiani na soka mzee baba?
 
Mbona ni rahisi tu kujitetea! Atasema amealikwa tu kama MC wa kutambulisha wachezaji.

Sasa TFF watasema kama huyo Manara haruhusiwi hata kufanya shughuli zake za kumhingizia kipato, kisa kafungiwa.
Hatakiwi hata kusikiliza Kipindi cha michezo radioni kama huo mchezo utakuwa wa miguu.😁

Adhabu kali ielekezwe hadi kwa Yanga na Manara mwenyewe.
 
Mimi ni bush lawyer tu. Ila sioni kosa eti!!!
... adhabu yake ilikuwa kutojihusisha na na soka for 2 yrs. u-MC wake leo ilikuwa kuwatambulisha WACHEZAJI (wa soka) wa KLABU YA YANGA (ya soka), Uwanja wa Taifa kwenye MECHI (ya soka) kati ya YANGA (ya soka) na Vipers (ya soka).

Matukio yote yaliyofanyika Taifa leo keyword ni SOKA. Haihitaji hata kujua sheria, simple logic tu inatosha kufikia conclusion.
 
Back
Top Bottom