Haki ya kumuona Mtoto baada ya kuachana au kutengana na mzazi mwenzako

Haki ya kumuona Mtoto baada ya kuachana au kutengana na mzazi mwenzako

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Andiko la Wakili Bashir Yakub kuhusu haki ya mzazi kumuona mtoto baada ya kutengana na mwenza au kuachana kabisa.

Sheria Namba 21 ya Mwaka 2009 Kifungu cha 38 cha Sheria ya Mtoto kinatoa haki hiyo na mzazi au mlezi anayekaa na mtoto hapaswi kuipinga, muhimu kusiwe na lengo la kumdhuru au kitu chochote kibaya wakati wa kumuona.

Anayenyimwa haki hiyo anaweza kufungua malalamiko Mahakama ya Mwanzo au ya Wilaya iliyopo ndani ya eneo analoishi mtoto (Awe na chini ya miaka 18).

Sababu za kumtima mzazi haki hiyo kwa madai hatoi matunzo au alimtelekeza Mtoto hazina mashiko kisheria, kwani mzazi au mlezi naye ana haki ya kufikisha malalamiko yake Mahakamani kuhusu madai yake hayo lakini si kumnyima mzazi mwenzake haki ya kumuona mtoto.

1fc01046-ef8a-4936-861f-810f913ec2d9.jpg
 
Hii inawahusu walikuwa wameoana au kuwa kwenye utaratibu rasmi wa mahusiano yanayotambulika sio waliopeana mimba guesthouse na kisha kuingia mitini, ni vizuri anayeweka articles za kisheria akasaidia kuelimisha kikamilifu.
 
Sasa jitu halitoi matunzo, hiyo haki inatoka wapi? Kwanza halioni aibu?
 
Nadhani adhabu nzuri ya mzazi asiyetoa matunzo Kwa mwanae, ni kumpa uhuru na mwanae, amuone waongee wafurahi. Aone kuwa hata bila yeye mwanae atakua.

Lakini pia ni heri mtoto aonane na mzazi wake asiyemtunza, huku akiishi na anayemtunza Kisha mwenyewe akikua itakuwa rahisi kujua mbivu na mbichi.

Kosa la kutokumruhusu mzazi mwenza asionane na mtoto au watoto linaweza kupelekea mtoto baadae kumchukia mzazi aliyekuwa anamhudumia Kwa kudhani huenda ni chuki zake tu ndio zilifanya mtoto akose kuonana na mzazi wake mwingine, na ni rahisi kuambiwa uongo wowote akakubaliana nao pindi akiamua Sasa kumtafuta huyo mzazi wake mwenyewe.
 
Back
Top Bottom