Hakika Uhuru Kenyatta ana tofauti Kubwa na Wengine EA

Hakika Uhuru Kenyatta ana tofauti Kubwa na Wengine EA

Huyu anataka mtu ashughulikiwe mbele ya mkutano. Ajabu!
 
Uganda m7 ametokea msituni Rwanda kagame nae wa msituni CCM 2015 waliishiwa kabisa mtu wa kuwawakilisha uchaguzi mkuu ikabidi walifurukunyue hili jiwe kutoka chini ya karavati kwenye mabarabara ndio maana anaua demokrasia anatuonyesha demokaravatia nimesikia IMF wanasema jiwe alifanya ukarabati wa mzunguko wa hela wa shilingi 1.5 tr kwa kuruhusu BOT wachapishe noti ili zirudi kwenye mzunguko huku hajui hela ameificha chini ya makaravati miradi isiyorudisha hela kwa wananchi
 
Ingekuwa Tz mpka sasa angekuwa Segerea! Yani usalimiane na rais umekaa tena rais mwenyewe Magu, tungemsahau!
 
Tofauti ni kubwa mmoja alikulia Ikulu mwingine karibu na zizi la mabeberu harufu mbaya ya ubeberu imemlevya sana ndo maana anachukia mabeberu na akati anaishi kibeberu hii inasadifu ile kauli mafahari wawili hawakai zizi moja hivyo anahofu ya kuonwa ubeberu wake na mabeberu.
 
At ease, relaxed, rais anajiamini hajipendekezi. Simply class.
 
Kenyatta ni mfanyabiashara na ukizijua fitna zilizopo kwenye biashara ni lazma utakuwa na utulivu kama alionao..

Kingine katokea kwenye royal family yaani sio mara yake ya kwanza kukaa ikulu hivyo hana vitu vya kumshtua sana na kingine ni yupo social, Kwa wale watumiaji wa vitu flani vya chugga wanajua jinsi gani "Peace and love" humaanisha [emoji16][emoji16][emoji16]

Kingine anaongoza watu waliopo huru sana pamoja na katiba ambayo haimfanyi kuwa na "FINAL SAY" yaani kiufupi mazingira yanamlazimu kuwa smart..
Yapo mengi ila haya ni machache katika mengi[emoji4][emoji4][emoji4]
Point
 
Au Tanzania ingekuwa ndiyo Marekani!!

Eeenh, Allen umewaza nini mkuu.

Yaani Tanzania hii hii, ingekuwa ndio Marekani ya sasa, halafu umwondoe Bwana Trump.....iwe nani? Yaani watu mna mawazo ya kichokozi kweli!

Nimejitahidi sana kuwa na picha ya Tanzania hiyo kichwani...... Hivi nani angefanya fyokofyoko mbele yetu akasalimika!

Anyway, ndoto hizo tuachane nazo; acha tupambane tu na hali yetu inayotukabili sasa.
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] Machadema mna kazi kweli kweli! Hamieni kwa Kenyata.

Yani mtu kaua watu zaidi ya 1,500 ili tu abaki ikulu alafu wewe unakuja kumsifia hapa?

Hivi machadema akili zenu mmezificha wapi?
Umekimbilia mabaya tu. Usisahau nayako kuyaweka pia
 
"Nchi ya democrasia Ile uwezi linganisha na nchi ya kidicteta"

Wewe utalinganisha mtu wa democrasia na mtu mtu dicteta jinsi wanavyokaa na kuonekana never"

Niliishi na wakikuyu sana Nairobi ni watu wakarimu sana wanaipenda nchi yao sio kwamba wana ukabila kama tunavyoaminishwa na watu wengine makabila mabaya kenya ni yale madogo madogo yanajihisi yanatengwa katika utawala wa kenya kitu ambacho sio kweli leo hii kenya maendeleo yapo mikoa yote.

Sio kama kipindi cha Moi alivyokuwa anawabagua wakikuyu na makabila mengine ndio maana unaona sasa hivi Ruto itakuwa ngumu kwake kwenda Ikulu 2022 kwa sababu ya historia yake kwenye kuwasababisha wakikuyu wengi kauawa mwaka 2007.

Uhuru ni presidential material watamkumbuka sana wakenya siku akiondoka sioni kabisa wa kuja kuziba pengo lake exactly 100%.
Huyu Uhuru Kenyatta yupo mbioni kubadilisha katiba ili aendelee kutawala 2022
 
Kufumba na kufumbua macho Uhuru ameunganisha the two feuding communities. The handshake...the handshake is as solid as a rock.
 
Kila kiongozi anaeneo lake la kusifiwa na eneo la kupewa lawama kwan kiongozi ni binadam si mkamilifu
Naam, hata Idd Ami, Hitler, na akina Mussolin wapo waliowasifia!

Umechambua vizuri kuhusu mambo ya Kenya na Kenyatta. Kenyatta wa sasa; na hasa huyu wa baada ya "Handshake" ni Kenyatta tofauti kabisa na yule Kenyatta wa ICC, na hata yule wa "Wakora" waliotaka kumnyang'anya ushindi.

Nadhani maana ya ile 'handshake' ilikuwa ni kulinda 'legacy' yake. Sasa hivi amebaki kuimba nyimbo za kupambana na rushwa, lakini haendi popote; na hiyo mipango yake ya' Big Fou' muda ndio umekwishamtupa mkono.

Mtu anapozungumzia kutokuwepo ukabila kama alivyoweka mleta mada, nadhani mtu huyo atakuwa ana uelewa tofauti ya ukabila.

Katiba yao sio 'perfect'; lakini wanajitahidi kuiheshimu na kuitekeleza kwa vitendo sio kama hapa kwetu hasa katika awamu hii.

Kwa sasa hivi, ukitaka kumlinganisha Kenyatta na kiongozi yeyote katika eneo hili, utakuwa huwatendei haki hao unaomlinganisha naye, hasa hawa wanaotafuta hata njia za kuondoa roho za watu ili mradi waogopwe.

Zaidi ya yote, nadhani Kenya ni jamii iliyo tofauti sana na jamii ya waTanzania kwa mambo mengi, moja wapo ikiwa ni huo ukabila, na pia hatuwezi kubeza kiwango chao cha elimu. Wamefanikiwa sana katika elimu yao, na mafanikio ndio yanaanza kujitokeza na kuonekana sasa katika mfumo wao wa uchumi, pamoja na kupishana sana kati ya walionacho na wasiokuwa nacho.
Sina hakika sana kama Kenya sasa hivi ukiwawekea kiongozi anayekiuka taratibu zote hadi katiba wale watu watakaa kimya. Sina hakika.
 
Naam, hata Idd Ami, Hitler, na akina Mussolin wapo waliowasifia!

Umechambua vizuri kuhusu mambo ya Kenya na Kenyatta. Kenyatta wa sasa; na hasa huyu wa baada ya "Handshake" ni Kenyatta tofauti kabisa na yule Kenyatta wa ICC, na hata yule wa "Wakora" waliotaka kumnyang'anya ushindi.

Nadhani maana ya ile 'handshake' ilikuwa ni kulinda 'legacy' yake. Sasa hivi amebaki kuimba nyimbo za kupambana na rushwa, lakini haendi popote; na hiyo mipango yake ya' Big Fou' muda ndio umekwishamtupa mkono.

Mtu anapozungumzia kutokuwepo ukabila kama alivyoweka mleta mada, nadhani mtu huyo atakuwa ana uelewa tofauti ya ukabila.

Katiba yao sio 'perfect'; lakini wanajitahidi kuiheshimu na kuitekeleza kwa vitendo sio kama hapa kwetu hasa katika awamu hii.

Kwa sasa hivi, ukitaka kumlinganisha Kenyatta na kiongozi yeyote katika eneo hili, utakuwa huwatendei haki hao unaomlinganisha naye, hasa hawa wanaotafuta hata njia za kuondoa roho za watu ili mradi waogopwe.

Zaidi ya yote, nadhani Kenya ni jamii iliyo tofauti sana na jamii ya waTanzania kwa mambo mengi, moja wapo ikiwa ni huo ukabila, na pia hatuwezi kubeza kiwango chao cha elimu. Wamefanikiwa sana katika elimu yao, na mafanikio ndio yanaanza kujitokeza na kuonekana sasa katika mfumo wao wa uchumi, pamoja na kupishana sana kati ya walionacho na wasiokuwa nacho.
Sina hakika sana kama Kenya sasa hivi ukiwawekea kiongozi anayekiuka taratibu zote hadi katiba wale watu watakaa kimya. Sina hakika.
Mkuu nimekupata vizuri kabisa !!

Umeongea ukweli na kiukweli kenya wako juu kabisa kiuchumi na sababu ya wao kuwa juu ni kwa sababu za kihistoria !! Mojawapo ikiwa ni kuchelewa kupata uhuru ukilinganisha na nchi nyingne za A mashariki ,ikumbukwe pia Kenya kipindi cha mkoloni ndo nchi pekee A mashariki iliyokuwa na ma settlers wengi na waingereza baada ya vita kuu ya kwanza ya dunia walipochukua makoloni baad y mjerumani kuadhibiwa kuna makoloni mengi waliamua kuyaacha kwa maana ya kwamba hawakuwekeza sana ktk hayo makoloni kwa sababu mbali mbali mojawapo ikiwa ni kuwepo kwa upinzani mkali toka kwa wazawa mfano Tanganyika wakat ule ,lakn pia walihitaji ardhi ya kutosha kwa ajili ya kuendeshea shughuli zao za kiuchumi rejea sera zao za Mfumo wa Kipande ( kipande system huko kenya) na nadhani umiliki wa ardhi huko kenya uliathiriwa sana na wazungu maana had leo kule ardhi inamilikiwa tofauti na kwetu huku,

Kingine ikumbukwe pia kwamba kenya walihodhi sana mali zote zilizokuwa za
Mali ya jumuiya ya a mashariki ikiyokuja kuanguka mwaka 1977 napo hapo kuna kwann kenya iko juu,

Kitu kingine ,kenya ukiondoa terrosist scandals za hivi karibuni hasa Al shaabab haijawahi kuwa na rekodi ya kupigana vita kama ilivyokuwa hapa kwetu kwa maana hiyo ss tulipoteza mali na muda mwingi kuji rescue na ku maintain uchumi na wakat huo hali ya uchumi ilikuwa mbaya sana !!

Hiyo haitoshi ,ndg zangu kenya iko juu kulinganisha nasi kwa sababu hii pia , Tanganyika kipindi kile cha vuguvugu la kumuondoa mkoloni barani afrika sisi tulikuwa msitari wa mbele kabsa tukiongozwa na baba wa taifa JK Nyerere ,akina Emerson Mnagangwa ( Zimbabwe) ,vyama kama.FLERIMO nk vyote hv vilianzishwa hapa nchin na watu wengi ambao leo n viongoz huko.kusini mwa afrika wametokea hapa ,Jacob Zuma.walikaa Bagamoyo nk hvyo kwa vyovyote vile lazima kenya awe juu yetu !! Hii ndio maana mikoa yote ya kusini Tz maendeleo yake yako chini sababu kubwa ilikuwa ni "War Zone" hvyo maendeleo ingekuwa ngumu ambapo sasa sera yetu kubwa inatakiwa ijikite kuimarisha uchumi wetu!

Kingine kuhusu suala.la demokrasia nilisema japo kwa ufupi kwamba Njia ya kenyatta kuelekea ikulu inahistoria kubwa sana ambayo ilimpelekea hadi kwenda ICC Kwa mtu mwelewa ataelewa kwann huyu bwana anakuwa hivi leo!! Rejea maandamano ya kumpokea Mhasimu wake Raila Odinga kipindi kile pale airport ambapo mara ya kwanza alizuia kulakiwa na umati wa watu au wafuasi wake lakn baada ya kusoma upepo hakukuwa na namna bali kukubali hali ile yote haya inaweza ikawa ni maumivu na kumbukizi za nn kinaweza tukia endapo ange react kwan ashaonja pepo la icc !!! Kwa hali hii huwezi kumlinganisha na magufuli!

Nakataa na sikubaliana na hoja ya baadhi ya watu kusema ati magufuli kwa sababu anatokea familia masikini ndio maan anakuwa hvyo hii ni Big no!!na mimi nadhani tatzo siyo magufuli kwan anayotekeleza mengi ni agizo la chama chake na ndo alichokuwa akikinadi kwenye kampeni mambo kama ku fire out wafanyakazi aliyasema , ku deal na watu mafisadi yote aliyasema na tukakubali sera zake ndo maana ni Rais , hvyo kunautofaut huo kati yetu na wenzetu lakn sisi tumepiga hatua sana kwenye mambo ya ukabila hatuna kabisa !!! Kumbukeni pia ss ndo taifa pekee nadhani afrika linalohifadhi wakimbizi wengi hivyo nasi tunachakujidai licha ya kwamba uchumi wetu unayumba lakn hali hyo huwa n kawaida siku zote ham wezi mkawa at the right position , ni sawa na mgonjwa kuanza kupona haponi siku moja!!

Pasaka njema!
 
  • Thanks
Reactions: Oii
"Nchi ya democrasia Ile uwezi linganisha na nchi ya kidicteta"

Wewe utalinganisha mtu wa democrasia na mtu mtu dicteta jinsi wanavyokaa na kuonekana never"

Niliishi na wakikuyu sana Nairobi ni watu wakarimu sana wanaipenda nchi yao sio kwamba wana ukabila kama tunavyoaminishwa na watu wengine makabila mabaya kenya ni yale madogo madogo yanajihisi yanatengwa katika utawala wa kenya kitu ambacho sio kweli leo hii kenya maendeleo yapo mikoa yote.

Sio kama kipindi cha Moi alivyokuwa anawabagua wakikuyu na makabila mengine ndio maana unaona sasa hivi Ruto itakuwa ngumu kwake kwenda Ikulu 2022 kwa sababu ya historia yake kwenye kuwasababisha wakikuyu wengi kauawa mwaka 2007.

Uhuru ni presidential material watamkumbuka sana wakenya siku akiondoka sioni kabisa wa kuja kuziba pengo lake exactly 100%.

Kenya bado kuna hazina kubwa ya viongozi wenye busara mfano wa Uhuru Kenyatta viongozi wapo, wapo wengi kuna Msalia Mudavadi, Kalonzo Mosyoka, Peter Kenneth, Raila Odinga, Moses Wetangula, Wamalwa, na Gedion Moi.

William Ruto ni kiongozi mwenye akili nyingi sana lakini anatuhumiwa sana kwa ufisadi. Pia tatizo lake lingine kulingana na midia mbali mbali ni kwamba hana uvumilivu wa kisiasa.

Hata hivyo, wanasiasa hawa wote ukimuondoa Raila Odinga wamepikwa kisiasa na Moi. Ukijaribu kuangalia Moi hakuwa kiongozi mbaya kiasi hicho bali jaribio la mapinduzi la 1982 ambalo kina Raila na Ochuka walihusishwa ndio iliyombadilisha Moi. Hali ile ili mfanya Rais Daniel Arap Moi apunguze upole wake na kuongeza ukali kidogo ili kurudisha nchi katika njia ilionyooka.

Leo hii moi pamoja na uzee wake bado ana ushawishi mkubwa katika siasa za Kenya ndiyo maana wanasiasa wengi wanaotaka kugombea urais 2022 wengependa kuonana naye ili kuchota busara na baraka zake. Pia kuna tetesi kwamba 'handshake' ya Raila na Kenyatta ina baraka zote za mzee Moi.

Kuhusu maendeleo ya nchi Moi aliweza kujenga shule nyingi kuliko kiongozi yeyote yule. Alijenga shule nyingi za msingi, sekondari na vyuo vikuu. Hata pale ambapo aliona serikali haikuwa na uwezo wakujenga vyumba vya madarasa ya kutosha aliwahimiza sekta binafsi hasa taasisi za dini kushirikiana na serikali ili kuboresha elimu. Kwa upande wake serikali iliendelea kuwalipa walimu mishahara utaratibu huu ulianzishwa wakati wa Moi na viongozi waliofutata Kibaki na Uhuru waliundeleza huu utaratibu kwa maslahi mapana ya nchi yao.
 
Kuna kitu nmejifunza kupitia comment yako hii naomba nichangie nami kidogo!!

Kuna sehemu nadhani tunachanganya mambo na kushindwa kuelewa tunahitaji nn hasa ktk suala la Rais,, leo kupitia hii clip kenyatta kawa predential material!!! Nmeshtuka kidg uliposema kwamba kule hakuna ukabila na mle.mle ukadai kwamba tatzo n vikabila vidogo vilivyopo kenya nikashangaa kidogo kwamba huenda hujui maana ya ukabila!!! Ulichokisema kuhusu hayo makabila madogo dogo ndo ukabila wenyewe maana nijuavyo mm kitendo cha makabila hayo kujiona yanakandamizwa huo ndo ukabila!!

Umesema pia kwamba n propaganda tu huko ukabila upo naona kwa uelewa mpana unataka kusema huku Tz ndo upo pole saaana !!! Tz ni nchi ambayo kiongozi yeyote haulizwi Tribal make up yake ,,,ni nchi ambayo watz wanaoana pasipokuangalia anatokea kabila gan leo hii unaandika maneno kama haya????

Kingine umesema kenya ni nchi ya kidemokrasia ??? Kwa maneno yako Rais wa tz mfano Magufuli angekuwa katokea familia kama ya kenyatta ambaye baba yake aliwahi kuwa Rais wa kenya ungetoa matusi sana ndg lakn najua kwann umesema hvyo,,, naomba ufatilie utajiri alionao kenyatta then njoo u comment kwamba nchi ile kuna haki !!! Unasahau hata historia ya kenyatta ktk kuelekea kwenye urais wake unaandika tu!!! Hatari

Kingine labda nitoe ufafanuzi , kuna kitu tunakosea ,in africa there is no dictatorship !!! Labda hapo nyuma lakn we have elements of dictatorship ,,,,afrika tuna elements tu za udikteta ..mfano magufuli anaitwa dikteta hebu jaribu kusoma historia ya nchi zilizowah kuongozwa kidikteta hasa Ujerumani na nchi ya uitaliano then njoo useme ss huku n madikteta !!!

Mwisho ulichoandika umeandika kwa sababu fulani lakn unajua kabsa uongo na ukweli wa maneno yako lakn sishangai maana kwenye tafakuri huwa kuna mawazo kinzani na kila mtu anatafakuri yake lakn ukweli huwa unabaki pale pale tu !!

Kila kiongozi anaeneo lake la kusifiwa na eneo la kupewa lawama kwan kiongozi ni binadam si mkamilifu ,,,magufuli atatoka ,,tutaacha kusema pengine kwa sabab katoka maana hatumpendi lakn atakuja mwingine nae tutamsema kwa sababu zetu wenyewe lakn wote hao kuna chembe tu ya jambo jema ambalo kamwe hatutalisahau !!!!

pasaka njema !!!
[emoji16][emoji16][emoji16]umeandika yanayowachukiza, hawatapenda.

Hizi ndio akili za watz wavivu waliokata tamaa, kazi yao huwa ni kujadili maisha ya ulaya na kwingineko kwa mitizamo ya pepo.

Magu angekuwa ni chinga achia mbali kuwa mtoto wa mkapa hapa tz kuna watu wangekunya wakitembea kwa sababu ni tz, ila kenya ewalaaaa ni nchi ya kidemokrasia.
 

Nimeona hii na kutofautisha na wengine wa East Africa hasa wa kwetu.
Kwa nini hatujifunzi kwake?

Naunga mkono hoja, kuna viongozi it's easy to talk to, they are very much reachable,

lakini kuna viongozi, they are unreachable unresolvable!
The excuse is security concerns!
Security concerns my foot!.
Tena viongozi wetu ni wa ajabu kweli, tukitoka nao nje ya nchi, they are so reachable!, lakini Bongo, hata kumkaribia tuu, unaonekana kama suicide bomber!.

P.
 
Hebu angalia yeye na Odinga ni wapinzani wa jadi kweli lakini wanaheshimiana maana uhasama wao sio binafsi Bali katika kugombea kuwaongoza watu kwenda kwenye neema
Chakaza respect mkuu. Wewe ni mmoja ya wana JF wenye michango mizuri japo mara nyingi ni ya kukosoa lakini still uko vizuri. Lakini subiri kidogo: hivi siasa za Kenya unazielewa kwa undani? Nashangaa sana watanzania wengi wameingia kwenye mkumbo wa kuona Kenya na viongozi wake kama watu wa mfano! Ndugu yangu, siasa za Kenya zisikie hivyo hivyo. Ni kifo mkononi. Hakuna demokrasia kama wengi mnavyofikiri. Kilichotokea kwa Lissu Kenya ni jambo la kawaida kabisa. Kenya utaachiwa kufanya mambo yale ambayo hayana madhara kwa establishment lakini kuna mstari ukiuvuka kaburi ni halali yako.
 
Back
Top Bottom