Hakukuwa na sababu ya Profesa Mkenda kuzungumza aliyoyazungumza hadharani. Kiongozi ni kuwa na Kifua na Uvumilivu

Hakukuwa na sababu ya Profesa Mkenda kuzungumza aliyoyazungumza hadharani. Kiongozi ni kuwa na Kifua na Uvumilivu

Kwani akiwa waziri anapoteza hisia na maumivu akitendewa mabaya?
Au ni mwiko kwa mwana ccm kukisema vibaya hilo genge lenu?
Ukiwa kiongozi wa ngazi ya juu kama vile Waziri haupaswi kufanya mambo na maamuzi kwa hisia.
 
Paragraph moja ilitosha naona umerudiarudia maelezo

Mkenda sio mjinga kuamua kusema hali anazopitia kwenye uongozi. Huenda hata lengo si kumfikishia ujumbe number moja bali umma wa watanzania. Kaamua liwalo na liwe.
Andiko langu limeeleza kwa kina maana ya kuwa kiongozi. Nafikiri hata waziri Mwenyewe atajutia na amejutia kauli yake na kutambua makosa yake.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Sote tumeyasikia maneno na kauli za Waziri wa Elimu Mheshimiwa Profesa Adolph Mkenda akilalamika kuwa alizungushwa kupata nafasi ya kuonana na Mheshimiwa Rais wetu Mpendwa na Jemedari wetu kipenzi cha watanzania Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan.

Mimi Mwashambwa nimejiuliza maswali ya je kulikuwa na sababu zipi za kuyaongea hayo masuala hadharani? Yalikuwa na umuhimu upi na sababu zipi? Alishindwa nini kuyaongea faragha alipopata nafasi ya kuongea na kuonana na Mheshimiwa Rais?

Je waziri hana njia nyingine za kuwasiliana na kufikisha ujumbe wake kwa Rais? Je waziri hawezi kuwasilisha jambo hilo kwenye kikao cha Baraza la mawaziri na kutoa dukuduku lake na kero yake ili mambo yazungumzwe na kuonyana humo humo badala ya kuleta hadharani?

Juu ya Waziri Wa Elimu kuna Naibu Waziri Mkuu, Waziri Mkuu ,Makamu wa Rais kabla ya kumfikia Rais Mwenyewe. Sasa kwanini asingemtumia hata mmoja wapo kati ya hao kupeleka jambo lake na kero yake hiyo?

Hata alipopelekewa kikaratasi mezani kwake kwanini na kulikuwa na sababu gani ya kujibu kwa jeuri kuwa yale aliyokuwa anayaongea yalikuwa ni Sehemu ya hotuba yake? Kwanini alikuwa anaonyesha kana kwamba yupo kwenye mgogoro na wasaidizi wa Rais na sasa anataka kuwachongea na kutunishiana misuli hadharani? Yalikuwa na sababu gani hadi ya kusema kuwa tuliambiwa tuongee kwa saa mbili tu?

Kwanini Waziri ambaye ni Profesa kabisa anakosa kifua na uvumilivu pamoja na subira ya mambo madogo kama hayo? Kama jambo dogo kama hilo linamshinda kuvumilia na kukaa kimya bila kuonyesha hasira zake hadharani,anaweza vipi vumilia mambo makubwa na kukaa nayo mpaka anaingia kaburini? Unapokuwa kiongozi mkubwa ni pamoja na kubeba maumivu na kutunza siri kwa gharama kubwa na Maumivu.

Hivi kama Rais Samia Mama yetu kipenzi asingekuwa na kifua na uvumilivu na kuamua kuzungumza kila kitu hadharani. Unafikiri angezungumza mangapi mazito baada ya kuapishwa kwake kuwa Rais? Au mmesahau ni nini Mkuu wa Majeshi wetu mstaafu Mheshimiwa Jenerali Venance Mabeyo alichokisema na kilichotokea baada ya kifo cha Hayati Mwalimu Daktari John Pombe Joseph Magufuli?

Mmesahau Kauli ya Jenerali Mabeyo kuwa kuna watu walisahau katiba inasema nini na kwamba akawakumbusha Matakwa ya Katiba mara baada ya kufa kwa Rais? Hivi mnaichukuliaje kauli hiyo? Mnaelewa Maana yake? Mnataka niwafungulie mabano ili muelewe?

Je mnafikiri watu hao waliosahau matakwa ya katiba Hawapo hai? Mnafikiri hawapo Tanzania? Mnafikiri hawapo serikalini?? Mnafikiri Mama yetu Mpendwa hawafahamu? Mnafikiri Mama yetu kipenzi hafahamu kilichotokea baada ya kifo cha Hayati? Au mnafikiri amekaa kimya kwa sababu hajui kitu?

Jibu ni kuwa anafahamu kila kitu na ameamua kukaa kimya na kuendelea na kazi kwa sababu anajua maana ya uongozi. anajua maana ya kutunza siri. Anajua Ukubwa ni jalala. Anajua jambo gani linapaswa kuzungumzwa hadharani na lipi halipaswi kuzungumzwa hadharani. Anajua kuna mambo yanapaswa kukaa kifuani na kubakia kama siri mpaka Kifo.

Na huo ndio uongozi. Ndio Ukubwa.Ndio uongozi unavyotaka hivyo kwa kiongozi wa juu kuwa na kifua ,kutunza siri,kuwa na subira, uvumilivu na kujizuia kuongea vitu kwa msukumo wa hasira,jazba, mihemuko na kukurupuka. Kama Rais Samia angetaka kuongea kila kitu hadharani basi Nchi ingesimama. Nasema tena kuwa NCHI ingesimama hii.

Viongozi wetu jifunzeni kuwa na siri,vifua, uvumilivu na subira. Tumieni busara na hekima katika kuzungumza hadharani na chagueni maneno ya kuzungumza mbele ya hadhira. Na ikiwezekana someni hotuba mlizoandaliwa kuliko kutumia hisia bila mantiki kuzungumza na kujikuta mkiharibu na kuleta taswira mbaya kwa jamii .

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Wee nae upo kama shoga angalia mabasha wa ccm wasije wakakutia ukuni wa Kwa mpalange, maana naona ndo unakoelekea Sasa, uchawa Gani huo unafanya uchawa mpaka unavuka mipaka, wewe marinda yako rehani chunga sana.
 
Wee nae upo kama shoga angalia mabasha wa ccm wasije wakakutia ukuni wa Kwa mpalange, maana naona ndo unakoelekea Sasa, uchawa Gani huo unafanya uchawa mpaka unavuka mipaka, wewe marinda yako rehani chunga sana.
Embu acha maneno ya kihuni huni. Jikite kwenye hoja au waachie wenye akili Timamu wajadili hoja
 
Prof amefanya vyema..amevumilia mengi.. ameamua kujitibu kwa kusema ukweli hadharani.. ila hakuwataja wahusika (upungufu kwenye hotuba yake)..
 
Acha ushamba, wewe una akili kuliko Profesa Mkenda?.
Kwani wewe unajua ukubwa wa akili zangu upoje? Au wewe mtu akiwa waziri unafikiria anakuwa tayari na akili nyingi kuliko watanzania wote hapa Nchini?
 
Prof amefanya vyema..amevumilia mengi.. ameamua kujitibu kwa kusema ukweli hadharani.. ila hakuwataja wahusika (upungufu kwenye hotuba yake)..
Aliyoyafanya hayapaswi kufanywa na kiongozi wa ngazi yake
 
Andiko langu limeeleza kwa kina maana ya kuwa kiongozi. Nafikiri hata waziri Mwenyewe atajutia na amejutia kauli yake na kutambua makosa yake.
Kuwa mtu mzima, msomi na kiongozi haiondoi ubinadamu wake wa kawaida mkuu.
 
Mmesahau Kauli ya Jenerali Mabeyo kuwa kuna watu walisahau katiba inasema nini na kwamba akawakumbusha Matakwa ya Katiba mara baada ya kufa kwa Rais? Hivi mnaichukuliaje kauli hiyo? Mnaelewa Maana yake? Mnataka niwafungulie mabano ili muelewe?
Hivi hawa watu walikuwa akina nani? Mimi huwa nasikia fununu tu wakiwa wanamsingizia MUNGAI, lakini hadi leo sijwahi kuwafahamu kabisa
 
Aliyoyafanya hayapaswi kufanywa na kiongozi wa ngazi yake
Angekuwa kama bi mkubwa..'na haya mkayatazame'..Hapana,sio kwenye jambo la elimu. Prof yuko sahihi.. elimu yetu haimsaidii mhitimu kupambana na maisha/ hakuna ubunifu..ni kukariri tu..
 
Kuna mambo ya kuficha na mambo ya kuongea wazi wazi. Kama waziri amekosewa sana, protocol haikufuatwa. Nani ans mandate ya kumzuia waziri kuzungumza na raisi?🤔 Ni jambo la ajabu sana kuwahi kutokea.

Inaonekana huko ikulu hivi sasa kuna watu wa hovyo sana ambao hawakutakiwa hata kuwa wasimamizi wa vyoo vya stand.
 
Paragraph moja ilitosha naona umerudiarudia maelezo

Mkenda sio mjinga kuamua kusema hali anazopitia kwenye uongozi. Huenda hata lengo si kumfikishia ujumbe number moja bali umma wa watanzania. Kaamua liwalo na liwe.
Nimekuwa nasisitiza hili hapa mara kadhaa lakini mtoa maada kajitoa akili.
 
Back
Top Bottom