Hakuna haja ya kuandika Wosia kama Mahakama inaubatilisha

Hakuna haja ya kuandika Wosia kama Mahakama inaubatilisha

Kwenye kesi Mzee Erasto Msuya, baba yake ambaye yuko hali alikuwa anadai miongoni mwa Mali zilizoshikiliwa na mashemeji wa marehemu ni Mali zake alizomrisisha marehemu akitegemea zitakuja kuwafaa wajukuu zake lakini ghafla Mali zinahamia ukweni.. Jmn sio Jambo jepesi. Kama mnasema waache kulilia Mali za marehemu watafute zao kwanini na upande mwingine nao wasitafute zao wang'ang'anie Mali za marehemu. Tuwe na huruma kumbuka marehemu ana ndugu, wazazi, watoto iweje wewe uchukue zote?
 
Tuwe na huruma kumbuka marehemu ana ndugu, wazazi, watoto iweje wewe uchukue zote?
Ndugu....watafute zao. Kwann washobokee mali za marehemu?

Wazazi ......hawa muda wao wa kuishi umeisha. Mali wapewe za nn?

Watoto....wale wenye miaka chini ya 25 wapewe kwa kadri marehemu alivyowmua. Lkn watoto wenye miaka 25+ wasipewe hata senti. Wapambane kivyao.
 
Ila tuwe wakweli tu! Ishu ya Doreen Wa Mrema ina makanganyiko. Yaani watu wameishi miezi kadhaa!! Mwanamke kamkuta mzee wa watu na mali zake, halafu leo na yeye apange mstari kudai mirathi!!

The same to Jackline Ntuyabaliwe! Amemkuta Mzee Mengi na mali zake alizochuma na mke wake wa kwanza, pamoja na watoto wake! Leo anakuja na sound za kutaka kumiliki kirahisi tu, kila kitu!! Kisa amezaa na marehemu watoto wawili mapacha!!

Wosia wa aina hii lazima ulete tu utata. Ifikie wakati tujifunze kutafuta vya kwetu, huku tukiwa na wenzi wetu. Mambo ya kitumia njia za mkato, hayana tija kwenye hii dunia ya kidijitali.
Ilikuwa kimkakati..wachaga sio wa ki spot spot 😂 😂 😂 😂 😂 😂
 
Nashkuru kuzaliwa Muislamu
katika Uislamu hili ni jambo dogo sanaaa wala halihitaji complication ya aina yyte ile

Kamuulize Sheikh yyte yule alosoma dini vizuri hilo suala halina complication yyte ile kwenye Uislamu

Uislamu ni dini yangu
Am proud to be Muslim
 
Ndugu mtoa mada, napenda kukupongeza kwa kutoa mada nzuri, Kwa hakika maoni yako ni mazuri sana.

Lakini, Kabla ya kufikia hitimisho lako yatupasa tukumbuke kuwa mara nyingi mahakama za Tanzania zimekuwa zikiheshimu mapendekezo ya marehemu juu ya nani apewe nini kwenye mali zake.

Mara nyingi mgogoro huwa inatokea pale inapoonekana wazi kabisa hata Kwa mtu wa tatu (Reasonable man test) kuwa mgawanyo wa mali aliofanya marehemu ni wa ajabu na mtu yeyote mwenye akili ya kawaida tu asingeweza kufanya hivyo.

Mfano katika hali ya kawaida mtu hawezi kuacha kuwarithisha wanae wa kuwazaa mali zake na badala yao amrithishe Jirani au mke mdogo pekee, katika akili ya kawaida hii inakataa.Ndo maana hata sheria yenyewe mfano sheria za kimila zinakataza kum disinherit mwanao wa kumzaa isipokuwa Kwa sababu zifuatazo; Awe alitembea na mama yake (mke wako),Awe alitaka kukuua Ili arithi Mali,Awe hakukuhudumia wakati unaumwa haliyakuwa uwezo alikuwa nao.

Lakini pia endapo mahakama itajiridhisha wosia ulikuwa una mapungufu ya kisheria au labda mtoa wosia hakuwa katika hali nzuri ya kiakili,mahakama huingilia kati ili kulinda maslahi ya watu wengine waliotakiwa kuwa wafaidika.

KWENYE ISSUE YA MAREHEMU MREMA.

Kwa kuwa bado ni tetesi, Kwa kiasi kikubwa tunazoandika hapa ni hisia tu.

Labda inawezekana wosia wa mzee Mrema umeacha mali nyingi Kwa bi mdogo na haujaacha chochote Kwa Watoto. Kiubinadamu hata kama watoto tayari ni wakubwa na wana mali zao lazima itawauma na watachallenge huo wosia na wanaweza hata kuutilia shaka kama umeandikwa na baba yao.

Lakini pia Kwa sasa Kuna trend mbaya inaendelea ya mabinti wadogo kuolewa na vikongwe, Kwa kiasi kikubwa jamii hutengeneza dhana kuwa mabinti hao hufuata Mali, Kama itakuwa si kweli na badala yake hufuata mapenzi tujaribu kukuuliza kwanini mzee akiondoka tu wanaanza kugombea Mali. Kama ulimfuata mtu na mtu huyo hayupo kwanini usiondoke kimya kimya tu bila kudai chochote?

Wanaume tuache kuandika wosia tukiwa vifuani Kwa wake zetu (Joke).
Asante. Hapo ndio unapoona umuhimu wa mirathi kwa waislam
 
Nashkuru kuzaliwa Muislamu
katika Uislamu hili ni jambo dogo sanaaa wala halihitaji complication ya aina yyte ile

Kamuulize Sheikh yyte yule alosoma dini vizuri hilo suala halina complication yyte ile kwenye Uislamu

Uislamu ni dini yangu
Am proud to be Muslim
Asante umemaliza mkuu. Nami najivunia kuwa muislamu na nitaishi maisha ya kiislamu na. Namuomba Allah anifishe nikiwa muislam. Amiin
 
Nafikiri pesa ndio imebatilisha sio mahakama. Pesa ni kama ccm inachoshindwa ni kumfufu mfu tu.
Dah! Kwa mtazamo wangu naona umekosea sana kuifananisha pesa na hiyo takataka aisee!

Siku zote hiyo takataka huwa inafananiswa na vitu vya uharibifu tu kama fisi, mchwa, ukoo wa panya, majambazi, mafisadi, majangili, nk.

Pesa ina hadhi yake mkurugenzi.
 
Asante umemaliza mkuu. Nami najivunia kuwa muislamu na nitaishi maisha ya kiislamu na. Namuomba Allah anifishe nikiwa muislam. Amiin
Waislam nao wanapelekena Mahakamani siku hizi, ingawa sheria zao za kiislam ziko wazi na zeny mashiko sana, kuliko hizi sheria za mahakama za kawaida.
 
Asante umemaliza mkuu. Nami najivunia kuwa muislamu na nitaishi maisha ya kiislamu na. Namuomba Allah anifishe nikiwa muislam. Amiin
Kwa waislamu ishu ya mirathi sio kubwa sana Kwa sababu zifuatazo;

Sheria ya kiislamu imeweka ukomo wa uhuru wa mtoa wosia kugawa mali zake. Muislamu anaruhusiwa kugawa 1/3 pekee ya Mali zake.

Mgawanyo wa mali zinazobaki unakuwa umeelezwa bayana kwenye Quran na Qiyas etc.
 
Ila tuwe wakweli tu! Ishu ya Doreen Wa Mrema ina makanganyiko. Yaani watu wameishi miezi kadhaa!! Mwanamke kamkuta mzee wa watu na mali zake, halafu leo na yeye apange mstari kudai mirathi!!

The same to Jackline Ntuyabaliwe! Amemkuta Mzee Mengi na mali zake alizochuma na mke wake wa kwanza, pamoja na watoto wake! Leo anakuja na sound za kutaka kumiliki kirahisi tu, kila kitu!! Kisa amezaa na marehemu watoto wawili mapacha!!

Wosia wa aina hii lazima ulete tu utata. Ifikie wakati tujifunze kutafuta vya kwetu, huku tukiwa na wenzi wetu. Mambo ya kitumia njia za mkato, hayana tija kwenye hii dunia ya kidijitali.
Kwani yeye alikuwa kama Dada wa kazi au mke? Maana mke anamhudumia mmewe, Dada wakazi anamshahara na mke vipi, huo muda si angetafuta pesa zake!
 
Ndugu mtoa mada, napenda kukupongeza kwa kutoa mada nzuri, Kwa hakika maoni yako ni mazuri sana.

Lakini, Kabla ya kufikia hitimisho lako yatupasa tukumbuke kuwa mara nyingi mahakama za Tanzania zimekuwa zikiheshimu mapendekezo ya marehemu juu ya nani apewe nini kwenye mali zake.

Mara nyingi mgogoro huwa inatokea pale inapoonekana wazi kabisa hata Kwa mtu wa tatu (Reasonable man test) kuwa mgawanyo wa mali aliofanya marehemu ni wa ajabu na mtu yeyote mwenye akili ya kawaida tu asingeweza kufanya hivyo.

Mfano katika hali ya kawaida mtu hawezi kuacha kuwarithisha wanae wa kuwazaa mali zake na badala yao amrithishe Jirani au mke mdogo pekee, katika akili ya kawaida hii inakataa.Ndo maana hata sheria yenyewe mfano sheria za kimila zinakataza kum disinherit mwanao wa kumzaa isipokuwa Kwa sababu zifuatazo; Awe alitembea na mama yake (mke wako),Awe alitaka kukuua Ili arithi Mali,Awe hakukuhudumia wakati unaumwa haliyakuwa uwezo alikuwa nao.

Lakini pia endapo mahakama itajiridhisha wosia ulikuwa una mapungufu ya kisheria au labda mtoa wosia hakuwa katika hali nzuri ya kiakili,mahakama huingilia kati ili kulinda maslahi ya watu wengine waliotakiwa kuwa wafaidika.

KWENYE ISSUE YA MAREHEMU MREMA.

Kwa kuwa bado ni tetesi, Kwa kiasi kikubwa tunazoandika hapa ni hisia tu.

Labda inawezekana wosia wa mzee Mrema umeacha mali nyingi Kwa bi mdogo na haujaacha chochote Kwa Watoto. Kiubinadamu hata kama watoto tayari ni wakubwa na wana mali zao lazima itawauma na watachallenge huo wosia na wanaweza hata kuutilia shaka kama umeandikwa na baba yao.

Lakini pia Kwa sasa Kuna trend mbaya inaendelea ya mabinti wadogo kuolewa na vikongwe, Kwa kiasi kikubwa jamii hutengeneza dhana kuwa mabinti hao hufuata Mali, Kama itakuwa si kweli na badala yake hufuata mapenzi tujaribu kukuuliza kwanini mzee akiondoka tu wanaanza kugombea Mali. Kama ulimfuata mtu na mtu huyo hayupo kwanini usiondoke kimya kimya tu bila kudai chochote?

Wanaume tuache kuandika wosia tukiwa vifuani Kwa wake zetu (Joke).
Ulichokiandika hakina uhalisia wa maisha na ndo mawazo haya yanaleta matatizo nchi nyingi za ki maskini.Kama mtu mwenye mali kaamua kuoa mwenye umri mdogo kuliko yeye na AKENDA KWA MWANASHERIA,na kumuandikia urithi wa mali zote huyo mpenzi wake,wengine inawahusu nin.Mambo ya kuandika urithi ni mambo ya kisheria,inabidi yaheshimiwe hata kama kwa ndugu jamaa na jamii kwa ujumla hatuyaelewi.Hao ndugu kwa nin walishindwa kumwambia awaandikie watoto zake au jamaa zake wengine wakati yupo hai?mali ni zake kama kaamua kuhonga,kupeleka kwenye mizimu,kutupa ni zake hili inabidi lieleweke! Hayo mambo ,sijui alichuma na nani mara ohhh kuna watoto wengine kwani marehemu alikuwa hayajui yote haya au alisahau kama alizaa si alikuwa anajua,na pamoja na yote akaamua kumwachia mimali huyo demu,labda ana sababu zake,matakwa yake yaheshimiwe.
 
Tunaaminishwa kwamba ili kuondoa migogoro ya kugombea mali za Marehemu ni muhimu kuandika wosia.

Maana ya wosia: refers to the document written by a testator that details what is to happen to property owned by that testator upon death.

Kwa mantiki hiyo wosia ni matakwa ya mwenye mali kuamua ibakie kwa nani mara atakapokuwa amepumzika kwa amani. Sasa kwanini kuna mtu au taasisi inaingilia matakwa hayo?

Kilichofanywa na mahakama kwa Jacqueline Mengi kutengua wosia wa Mzee Mengi, ndiyo kinawapa nguvu familia ya Mrema kumfanyia vurugu mjane wake.

Mapendekezo:
Itungwe sheriaya ya kuzuia mtu mzima(miaka 25+) kugombea/kupewa mali za marehemu hata kama ni mtoto wa kuzaliwa.

Swali: Kama Mahakama inaweza kutengua wosia kizembe namna hii kuna haja gani ya kuandika wosia?
Tatizo unaandika Wosia baada ya kupewa mahaba na mchepuko, andika ukiwa na akili timamu
 
Wachaga shikilieni happo hapo,[emoji106]

Mmetusaidia sana kunyoosha Hawa wajasilia mwili sampo za kina mtoa mada[emoji4][emoji116]

Wajasiria mwili wanataka kula bila jasho. Wanakuja jua ndio linazama halafu wapate share nono hapana aisee.
 
Hakuna neno sipendi kulisikia kama WAKRISTU badala ya WAKRISTO
Pitia huu uzi kwanza
[emoji1484][emoji1484][emoji1484][emoji1484]

 
Nimeshangaa sana mtu tajiri anakufa watu wanazozana kuhusu mali. Huu ni ubinafsi wa aliyekufa kwa watoto wake. Angewapa mapema kila mtu chake na mkewe pia kwa ratio.

Naanza kuwa na mashaka na utajiri wa mizimu🤣🤣🤣
 
Tunaaminishwa kwamba ili kuondoa migogoro ya kugombea mali za Marehemu ni muhimu kuandika wosia.

Maana ya wosia: refers to the document written by a testator that details what is to happen to property owned by that testator upon death.

Kwa mantiki hiyo wosia ni matakwa ya mwenye mali kuamua ibakie kwa nani mara atakapokuwa amepumzika kwa amani. Sasa kwanini kuna mtu au taasisi inaingilia matakwa hayo?

Kilichofanywa na mahakama kwa Jacqueline Mengi kutengua wosia wa Mzee Mengi, ndiyo kinawapa nguvu familia ya Mrema kumfanyia vurugu mjane wake.

Mapendekezo:
Itungwe sheriaya ya kuzuia mtu mzima(miaka 25+) kugombea/kupewa mali za marehemu hata kama ni mtoto wa kuzaliwa.

Swali: Kama Mahakama inaweza kutengua wosia kizembe namna hii kuna haja gani ya kuandika wosia?
Sheria kuhusu mirathi na wosia zipo zaidi ya 5 Tanzania, na sheria hizi zote zinaongelea namna ya kuandika wosia na namna ya kugawa mali.

Inapotokea sheria hizi haijafuatwa na mtu amabaye ndio anaandika wosia huweza kupelekea wosia huo kukataliwa na mahakama,

Baadhi ya sababu hizo ni
- kuto kumtaka msimamizi wa mirathi
-Kutokutaka mali zako zote.
-Kutokutaja Watoto/ Mama kama warithi
-Kutokuwa na umri unaoruhusiwa 18+
-Kutokuwa katika hali ya utimamu wa akili wakati ukiandika Wosia (Example mengi case)
- kutokufuata utaratibu wa uandishia wa wosia (example Muslim hutakiwi kuweka mali zako zote Wakfi lazima kiasi cha mali kibaki kwa ajili ya familia.

#CJ
 
Tunaaminishwa kwamba ili kuondoa migogoro ya kugombea mali za Marehemu ni muhimu kuandika wosia.

Maana ya wosia: refers to the document written by a testator that details what is to happen to property owned by that testator upon death.

Kwa mantiki hiyo wosia ni matakwa ya mwenye mali kuamua ibakie kwa nani mara atakapokuwa amepumzika kwa amani. Sasa kwanini kuna mtu au taasisi inaingilia matakwa hayo?

Kilichofanywa na mahakama kwa Jacqueline Mengi kutengua wosia wa Mzee Mengi, ndiyo kinawapa nguvu familia ya Mrema kumfanyia vurugu mjane wake.

Mapendekezo:
Itungwe sheriaya ya kuzuia mtu mzima(miaka 25+) kugombea/kupewa mali za marehemu hata kama ni mtoto wa kuzaliwa.

Swali: Kama Mahakama inaweza kutengua wosia kizembe namna hii kuna haja gani ya kuandika wosia?
Lakini nadhani kuna kipengele kinasema lazima muandika wosia awe na akili timamu ya kujitambua na bila shuruti
 
Back
Top Bottom