Hakuna kiongozi au binadamu aliyekamilika, leo imedhihirika JPM alikuwa anakubalika kwa wanyonge na sio kwa mafisadi na matapeli ya kisiasa

Hakuna kiongozi au binadamu aliyekamilika, leo imedhihirika JPM alikuwa anakubalika kwa wanyonge na sio kwa mafisadi na matapeli ya kisiasa

Hata usiangaike na hao wanafiki wafata mkumbo, hawanaga Hoja zaidi kuvizia Lisu kasema nini nayeye atembee nalo ukiamua kuwapa jina zuri basi waite wajinga wafata mkumbo.

Na kwa sababu ujinga wao umeota mizizi miilini mwao basi hujiona wako wengi pale wanapoona welevu wamekaa kimya.

Usishangae wajinga hawa kumkubali kikwete nyakati hizi na kusahau matapishi yao.

Basi vile vile usishangae kesho kuwasikia wajinga hawa wakisema tulijua tu huyu mama hawezi kuyaenzi aliyoacha mzee.
Nani anamkubali JK, ukiona watu wanamsifia JK ujue wanampaka mafuta kwa mgongo wa chupa ili kumnanga huyo muovu.
 
labda wewe mtoa mada na shangazi zako ndio mliokuwa mnagaagaa huko barabarani kwa wasiwasi wa kutoijua hatima yenu ya baadaye kwa kuukosa ulaji.Hao unaowaita wanyonge kama Jiwe wako ambaye ameshasagika,wana nini haswa?.
Hii mijamaa na wenzake kina Makonda, Musiba and Co ndio walizidi kumharibia mzee wa watu kwa maupuuzi yao, yalikuwa yanafanya madudu halafu inaonekana kama mzee kayatuma, sasa yanavuna aibu yanajifanya kuja kulia lia hapa.
 
Nakubaliana na wewe Magufuli kama binadamu hakuwa mkamilifu. Kosa la Magufuli ni kuwa alipewa mamlaka asimamie haki sawa kwa raia wote. Yeye akatumia nafasi hiyo kuacha wengine waonewe, wengine wauliwe bila kuchukua hatua na kudhani yeye peke yake ndiye pekee mwenye kuweza kuiongoza nchi. (Na amewahi kuuliza kama yupo atakayeweza kufanya yale anayofanya)

Sasa Mungu kamchukua ili aone kuwa wapo wengine watafanya kama yeye na zaidi bila hata kuonea na kusababisha maumivu kwa wengine.

Shida nyingine Magufuli kila alipofungua mdomo wake hakuwa mtu wa kuongea maneno ya faraja wala kuleta tumaini. Mara nyingi ametumia mdomo wake kukwaza watu na kutoa maneno ya kejeli na kuudhi. Cha kusikitisha zaidi hotuba yake ya mwisho mtaani alimwambia yule bwana anayejiita "Trump" aliyehoji kuhusu malipo ya choo maneno ambayo hayapaswi kutamkwa na kiongozi wa nchi hadharani

Mimi kama binadamu mwenzake namwombea tu awe alitafuta amani na Mungu wake katika siku zake za mwisho. Na Mungu amsamehe na kumpa pumziko la milele
Uonevu na ubaguzi ndio kimemharibia sana Magu.Angekuwa mtu wa haki basi angekuwa ni mmoja ya watu waliofanya vizuri sana
 
After two weeks utamkumbuka.
Hata wabaya wanakumbukwa, Magufuli kafanya mazuri mengi nafahamu lakini ana mabaya yake.
Tatizo lenu wapambe na wanaccm wanafiki hamtaki kukiri madhaifu ya Magufuli kama binadamu mwenzetu. Mnalazimisha kumhubiri kama Mungu kwamba hakosei.

1. Kuongeza riba ya HESLB kutoka 8% hadi 15% kibabe bila kujali hajaongeza mshahara, hili namlaumu mpaka naingia kaburini. Kubariki 6% ya value retention fee namlaumu mpaka kiama, sisi wengine tumesoma kwa mbinde sana na maisha tunayaanza from scratch kufanya hivyo ni kutuumiza tusipige hatua tubaki kuwa maskini.

2. Watu kufa na kuokotwa ufukweni, watu kutekwa na wengine kupotea, watu kujeruhiwa na yeye kama Rais anakaa kimya bila kuviwajibisha vyombo vya ulinzi na usalama au kuviagiza vifanye uchunguzi, hapa tunabaki na maswali mengi, Magufuli aliteleza ukweli lazima usemwe.

3. Kufanya siasa za kibabe dhidi ya vyama vingine na dhidi ya wananchi, mfano kuwaambia wananchi msipochagua ccm sileti maji hapa, huu ni ubabe dhidi ya wananchi na kuvunja demokrasia ya nchi.

4. Kujibu watu majibu ya kejeli wanapokuwa na majanga, refer case ya Kagera wakati wa tetemeko, alaf siku chache mbeleni akatoa chakula cha msaada kupeleka nchi jirani baada ya nchi hiyo kukumbwa na janga la mafuriko

5. Kutokuhudhuria msiba mkubwa baada ya meli kuzama kule Ukerewe badala yake siku hiyo akaita askari trafiki nchi nzima akanywa nao chai ikulu wakati taifa lina majonzi, huu sio utanzania tuliozoea kuuona pamoja na umri wangu mdogo hapa duniani.

6.Kubariki watu wakamatwe hata wakihoji jambo dogo, wakimkosoa n.k huu ni uonevu, watu lazika wawe huru kukosoa kwenye nchi yao, Magufuli alijengea watu hofu kubwa wakaishi kama wako Afghanistan huko kwenye machafuko ya kila siku.

Baadhi ya mazuri yake ninayomkubali:
1. Kutekeleza miradi kama Nyerere hydropower station maarufu kama Stigler's gorge
2. Kufufua ATCL
3. Kujenga vituo vya afya
4. Kujenga SGR
5. Kujaribu kupambana na rushwa na kurejesha heshima kwa serikali, hususan watu matajiri walikuwa na dharau sana dhidi ya watendaji wa serikali

Yako mazuri mengi lakini mturuhusu kusema na mabaya yake, yeye ni binadamu kuna makovu kaacha kwenye mioyo ya watu
 
Hata alipokuja lisu barabara zilijaa pia na watu kulia,
Huyu ni kiongozi na wengi wameenda kuangalia namna dikteta alivyofumba macho
Wengi wanaotaka kuaminisha umma kuwa hayati JPM alikuwa kiongozi asiyefaa imegundulika ni wapuuzi wa huko Twita, wanasiasa njaa/matapeli ambao wananchi hawawataki. Hawa wanataka kila mtu aamini kuwa hakuwa mtu wa haki na utawala wake ulijaa udhalimu.

Lakini leo hii tumepata picha kamili, wazalendo, wamachinga, wakinamama tumeshudia wakilia na kugaagaa mabarabarani hii ni kwa sababu wanajua pengo lake litakuwa ngumu kuzibwa.

Mabaradhuli na mafedhuli mnapoteza muda maana nyie ni kama 1% ya wanaoichukia Tanzania. Maana 99% wanaipenda Tanzania na leo mmeshuhudia.
 
Huo upuuzi wa kuita wajinga wanyonge peleka hukohuko kwenu sio hapa
Watu wasioelewa umuhimu CAG kuhoji upotevu wa matrilioni/ kuzuiwa kipiga mahesabu migodini, bunge kuhoji ununuzi wa midege/ kujenga uwanja wa ndege n.k
Watu wasioelewa umuhimu wa mzunguko wa fedha
Watu wanaofurahia matajiri kuporwa mitaji, kufilisiwa, kunyanyaswa ili wafanane na wao kitu ambacho hakiwezekani
Watu hao ndo mnaita wanyonge, mnatumia udhaifu wa uelewa wao kushinda kisiasa. Nyinyi ni watu wabaya sana
Badilisheni mfumo wa elimu, shule za msingi watumie kiingereza Kama lugha ya kufundishia, alafu muone moto wake baada ya miaka kadhaa

Kula tano mwanangu, kwao mnyonge ni mtu asiyeweza kuhoji zaidi ya kumsifia Magufuli. Mtu yoyote mwenye kuweza kuhoji hasa haki yake, huyo ni mchochezi, fisadi na sio mzalendo.
 
Unapoteza mb na muda wako kupost ujinga. Kila mtu anahoji itakuwaje maana JPM ameondoka. Tumia akili hatanya kuazima
Unataka kila mtu akubaliane na wewe kuwa anakubalika, they are fox in sheep , Hata Mimi nikiwa na walio na udhuni ndauzunika nikiwa na walio na furaha ndafurahi, wengi wanalia kinafki.
Kama unaingia kwenye moyo wao Basi endelea kujifariji

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shida nyingine waliyonayo MATAGA ni kukatika mishipa ya aibu na kujifanya hamnazo.Watu kama mtoa mada,tayari wanafanya mazoezi ya kuanza kuusifu na kuuabudu utawala wa mama Samia kwa masilahi yao na sio vinginevyo.Mapambio mengi saana yatapigwa.
 
Nyerere aliacha Wosia, Mkapa aliacha kitabu na Magufuli ameacha makaburi.

Kaka yangu aliuawa kikatili kwa Mapanga, Ubongo ukachuruzika mithili ya supu nzito ya nguruwe, Polisi bila hata uchunguzi wakatoa statement kwamba kauawa kwa ugomvi wa mapenzi pamoja na kuwaonesha meseji nyingi za vitisho kutoka kwa CCM na ambazo kabla marehemu aliripoti mwenyewe polisi hakuna hata mmoja aliyekamatwa.

Kisa ni kaka kuwa Diwani kupitia chadema, wakaamua kumuua kikatili kwa mapanga. RIP bro, RIP Azory Gwanda, RIP Ben Saanane
😢
😢
😢

Lala milele Dikteta Jiwe, Usiamke tena na uwe kuni huku uendako
We kenge kufa kama umeumia sana...ufatane nae huko jehanam
 
Mtu muovu angependwa na wanyonge namna hii?

Hakuna anayependwa wala kuchukiwa na watu wote, hata upendwe na watu wengi kiasi gani, hiyo haiondoi ukweli kuwa ni mtu muovu.
 
Hata wabaya wanakumbukwa, Magufuli kafanya mazuri mengi nafahamu lakini ana mabaya yake.
Tatizo lenu wapambe na wanaccm wanafiki hamtaki kukiri madhaifu ya Magufuli kama binadamu mwenzetu. Mnalazimisha kumhubiri kama Mungu kwamba hakosei.

1. Kuongeza riba ya HESLB kutoka 8% hadi 15% kibabe bila kujali hajaongeza mshahara, hili namlaumu mpaka naingia kaburini. Kubariki 6% ya value retention fee namlaumu mpaka kiama, sisi wengine tumesoma kwa mbinde sana na maisha tunayaanza from scratch kufanya hivyo ni kutuumiza tusipige hatua tubaki kuwa maskini.

2. Watu kufa na kuokotwa ufukweni, watu kutekwa na wengine kupotea, watu kujeruhiwa na yeye kama Rais anakaa kimya bila kuviwajibisha vyombo vya ulinzi na usalama au kuviagiza vifanye uchunguzi, hapa tunabaki na maswali mengi, Magufuli aliteleza ukweli lazima usemwe.

3. Kufanya siasa za kibabe dhidi ya vyama vingine na dhidi ya wananchi, mfano kuwaambia wananchi msipochagua ccm sileti maji hapa, huu ni ubabe dhidi ya wananchi na kuvunja demokrasia ya nchi.

4. Kujibu watu majibu ya kejeli wanapokuwa na majanga, refer case ya Kagera wakati wa tetemeko, alaf siku chache mbeleni akatoa chakula cha msaada kupeleka nchi jirani baada ya nchi hiyo kukumbwa na janga la mafuriko

5. Kutokuhudhuria msiba mkubwa baada ya meli kuzama kule Ukerewe badala yake siku hiyo akaita askari trafiki nchi nzima akanywa nao chai ikulu wakati taifa lina majonzi, huu sio utanzania tuliozoea kuuona pamoja na umri wangu mdogo hapa duniani.

6.Kubariki watu wakamatwe hata wakihoji jambo dogo, wakimkosoa n.k huu ni uonevu, watu lazika wawe huru kukosoa kwenye nchi yao, Magufuli alijengea watu hofu kubwa wakaishi kama wako Afghanistan huko kwenye machafuko ya kila siku.

Baadhi ya mazuri yake ninayomkubali:
1. Kutekeleza miradi kama Nyerere hydropower station maarufu kama Stigler's gorge
2. Kufufua ATCL
3. Kujenga vituo vya afya
4. Kujenga SGR
5. Kujaribu kupambana na rushwa na kurejesha heshima kwa serikali, hususan watu matajiri walikuwa na dharau sana dhidi ya watendaji wa serikali

Yako mazuri mengi lakini mturuhusu kusema na mabaya yake, yeye ni binadamu kuna makovu kaacha kwenye mioyo ya watu
Jibu unalo wema wake unaoutweigh mapungufu yake.
 
Kula tano mwanangu, kwao mnyonge ni mtu asiyeweza kuhoji zaidi ya kumsifia Magufuli. Mtu yoyote mwenye kuweza kuhoji hasa haki yake, huyo ni mchochezi, fisadi na sio mzalendo.
Washenzi sana hawa jamaa, mabingwa wa reverse 😂😂
 
Hakuna anayependwa wala kuchukiwa na watu wote, hata upendwe na watu wengi kiasi gani, hiyo haiondoi ukweli kuwa ni mtu muovu.
Hajafikia hatua ya kuwa kwenye kundi la muovu.
 
Mtu pekee niliyemuona akilia ni Harmonize akiwa amejipost instagram. Wengine wanasema tu wamelia na matusi kwa wingi na kulaani ila ni bwana Rajab tu ndiye alilia
 
Mapenzii hayalazishw we nguchiro
Wengi wanaotaka kuaminisha umma kuwa hayati JPM alikuwa kiongozi asiyefaa imegundulika ni wapuuzi wa huko Twita, wanasiasa njaa/matapeli ambao wananchi hawawataki. Hawa wanataka kila mtu aamini kuwa hakuwa mtu wa haki na utawala wake ulijaa udhalimu.

Lakini leo hii tumepata picha kamili, wazalendo, wamachinga, wakinamama tumeshudia wakilia na kugaagaa mabarabarani hii ni kwa sababu wanajua pengo lake litakuwa ngumu kuzibwa.

Mabaradhuli na mafedhuli mnapoteza muda maana nyie ni kama 1% ya wanaoichukia Tanzania. Maana 99% wanaipenda Tanzania na leo mmeshuhudia.
 
Back
Top Bottom