After two weeks utamkumbuka.
Hata wabaya wanakumbukwa, Magufuli kafanya mazuri mengi nafahamu lakini ana mabaya yake.
Tatizo lenu wapambe na wanaccm wanafiki hamtaki kukiri madhaifu ya Magufuli kama binadamu mwenzetu. Mnalazimisha kumhubiri kama Mungu kwamba hakosei.
1. Kuongeza riba ya HESLB kutoka 8% hadi 15% kibabe bila kujali hajaongeza mshahara, hili namlaumu mpaka naingia kaburini. Kubariki 6% ya value retention fee namlaumu mpaka kiama, sisi wengine tumesoma kwa mbinde sana na maisha tunayaanza from scratch kufanya hivyo ni kutuumiza tusipige hatua tubaki kuwa maskini.
2. Watu kufa na kuokotwa ufukweni, watu kutekwa na wengine kupotea, watu kujeruhiwa na yeye kama Rais anakaa kimya bila kuviwajibisha vyombo vya ulinzi na usalama au kuviagiza vifanye uchunguzi, hapa tunabaki na maswali mengi, Magufuli aliteleza ukweli lazima usemwe.
3. Kufanya siasa za kibabe dhidi ya vyama vingine na dhidi ya wananchi, mfano kuwaambia wananchi msipochagua ccm sileti maji hapa, huu ni ubabe dhidi ya wananchi na kuvunja demokrasia ya nchi.
4. Kujibu watu majibu ya kejeli wanapokuwa na majanga, refer case ya Kagera wakati wa tetemeko, alaf siku chache mbeleni akatoa chakula cha msaada kupeleka nchi jirani baada ya nchi hiyo kukumbwa na janga la mafuriko
5. Kutokuhudhuria msiba mkubwa baada ya meli kuzama kule Ukerewe badala yake siku hiyo akaita askari trafiki nchi nzima akanywa nao chai ikulu wakati taifa lina majonzi, huu sio utanzania tuliozoea kuuona pamoja na umri wangu mdogo hapa duniani.
6.Kubariki watu wakamatwe hata wakihoji jambo dogo, wakimkosoa n.k huu ni uonevu, watu lazika wawe huru kukosoa kwenye nchi yao, Magufuli alijengea watu hofu kubwa wakaishi kama wako Afghanistan huko kwenye machafuko ya kila siku.
Baadhi ya mazuri yake ninayomkubali:
1. Kutekeleza miradi kama Nyerere hydropower station maarufu kama Stigler's gorge
2. Kufufua ATCL
3. Kujenga vituo vya afya
4. Kujenga SGR
5. Kujaribu kupambana na rushwa na kurejesha heshima kwa serikali, hususan watu matajiri walikuwa na dharau sana dhidi ya watendaji wa serikali
Yako mazuri mengi lakini mturuhusu kusema na mabaya yake, yeye ni binadamu kuna makovu kaacha kwenye mioyo ya watu