Hakuna kiongozi au binadamu aliyekamilika, leo imedhihirika JPM alikuwa anakubalika kwa wanyonge na sio kwa mafisadi na matapeli ya kisiasa

Hakuna kiongozi au binadamu aliyekamilika, leo imedhihirika JPM alikuwa anakubalika kwa wanyonge na sio kwa mafisadi na matapeli ya kisiasa

Itakuwaje nn????hao ni wale uwezo wao wa kufikir upo chini kama vp naww ukufe bc ili ucshuhudie itakuwaje????na ukasaidie kubeba makabrasha ya kiongozi mtarajiwa wa malaika
Unapoteza mb na muda wako kupost ujinga. Kila mtu anahoji itakuwaje maana JPM ameondoka. Tumia akili hatanya kuazima
 
Nyerere aliacha Wosia, Mkapa aliacha kitabu na Magufuli ameacha makaburi.

Kaka yangu aliuawa kikatili kwa Mapanga, Ubongo ukachuruzika mithili ya supu nzito ya nguruwe, Polisi bila hata uchunguzi wakatoa statement kwamba kauawa kwa ugomvi wa mapenzi pamoja na kuwaonesha meseji nyingi za vitisho kutoka kwa CCM na ambazo kabla marehemu aliripoti mwenyewe polisi hakuna hata mmoja aliyekamatwa.

Kisa ni kaka kuwa Diwani kupitia chadema, wakaamua kumuua kikatili kwa mapanga. RIP bro, RIP Azory Gwanda, RIP Ben Saanane

Lala milele Dikteta Jiwe, Usiamke tena na uwe kuni huku uendako
Pole sana ndugu yangu kwa kumpoteza Kaka yako. Lakini ufarijike katika Bwana maana wauaji hawataikwepa hukumu wala laana mpaka kizazi cha 4.

Nduguyo kwa udhalimu aliotendewa uamini kuwa yupo kwa Bwana wetu, miongoni mwa wanaoizunguka meza ya Bwana, wakimsifu na kumwabudu usiku na mchana, huku watesi wake wakiionja jehenam ya mateso.

Tusiogope anayeteketeza mwili bali yule aharibuye roho.
 
Nyerere aliacha Wosia, Mkapa aliacha kitabu na Magufuli ameacha makaburi.

Kaka yangu aliuawa kikatili kwa Mapanga, Ubongo ukachuruzika mithili ya supu nzito ya nguruwe, Polisi bila hata uchunguzi wakatoa statement kwamba kauawa kwa ugomvi wa mapenzi pamoja na kuwaonesha meseji nyingi za vitisho kutoka kwa CCM na ambazo kabla marehemu aliripoti mwenyewe polisi hakuna hata mmoja aliyekamatwa.

Kisa ni kaka kuwa Diwani kupitia chadema, wakaamua kumuua kikatili kwa mapanga. RIP bro, RIP Azory Gwanda, RIP Ben Saanane

Lala milele Dikteta Jiwe, Usiamke tena na uwe kuni huku uendako
Nyerere aliacha Wosia, Mkapa aliacha kitabu na Magufuli ameacha makaburi.
 
Wengi wanaotaka kuaminisha umma kuwa hayati JPM alikuwa kiongozi asiyefaa imegundulika ni wapuuzi wa huko Twita, wanasiasa njaa/matapeli ambao wananchi hawawataki. Hawa wanataka kila mtu aamini kuwa hakuwa mtu wa haki na utawala wake ulijaa udhalimu.

Lakini leo hii tumepata picha kamili, wazalendo, wamachinga, wakinamama tumeshudia wakilia na kugaagaa mabarabarani hii ni kwa sababu wanajua pengo lake litakuwa ngumu kuzibwa.

Mabaradhuli na mafedhuli mnapoteza muda maana nyie ni kama 1% ya wanaoichukia Tanzania. Maana 99% wanaipenda Tanzania na leo mmeshuhudia.
Uliona msafara wa Lipumba siku anarudi ulaya kipindi kile?
Uliona msafara wa Ruge akipokewa siku anapokewa akiwa marehemu toka south?


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wahindi na waarabu siwaoni kwenye kuaga

Mama Samia naomba tenda zote ukishika madaraka usimpe mhindi wala mwarabu hadi muda huu masaa kibao sijaona mhindi au mwarabu akimuaga Marehemu Magufuli.Akufaaye kwa dhiki ndie Rafiki naona wahindi na waarabu wametususia watanzania ngozi nyeusi.Sio kesi .Wanajitia watanzania wenzetu msibani hadi muda huu hawajatokea .Heri utoe tenda kwa waswahili kuliko hawa wahindi na waarabu

Mabalozi wa nje pia kuna aliyewaona kuaga? ili tumshauri vizuri Raisi wetu?
 
Nyerere aliacha Wosia, Mkapa aliacha kitabu na Magufuli ameacha makaburi.

Kaka yangu aliuawa kikatili kwa Mapanga, Ubongo ukachuruzika mithili ya supu nzito ya nguruwe, Polisi bila hata uchunguzi wakatoa statement kwamba kauawa kwa ugomvi wa mapenzi pamoja na kuwaonesha meseji nyingi za vitisho kutoka kwa CCM na ambazo kabla marehemu aliripoti mwenyewe polisi hakuna hata mmoja aliyekamatwa.

Kisa ni kaka kuwa Diwani kupitia chadema, wakaamua kumuua kikatili kwa mapanga. RIP bro, RIP Azory Gwanda, RIP Ben Saanane

Lala milele Dikteta Jiwe, Usiamke tena na uwe kuni huku uendako
Kumbe ni polisi ndio waliua Sasa unamuhusisha vp hayat jpm
 
Umeandika nini? Hakuwa Tanzania una maana gani? Mtu kama hakuwa mtu mwema watu wangemlilia leo?
Kama alikuwa mwema au mbaya, kwa sasa hayo yapo mbele ya Muumba wake. Sisi tunamsindikiza tu aende kwa amani kule ambako kila mmoja wetu ataenda.

Lakini tutambue kuwa kila mtu, hata awe mbaya vipi, kuna watakaomlilia. Kuna msemo wa Kiswahili, 'baniani mbaya kiatu chake dawa', maana yake hakuna aliye mbaya akakosa uzuri. Jambazi anaweza kuwa mbaya kwa anaowaibia, lakini akawa mwema kwa watoto wake maana akiiba, alichoiba anaenda kukitumia kwa manufaa ya familia yake.

Wapo wanaohuzunika kwa sababu kweli wameguswa na mazuri ya marehemu. Wapo wanaohuzunika kwa sababu hawana uhakika na manufaa waliyokuwa wanayapata kwenye utawala wa Magufuli, kama watayapata tena, na hawa ni wengi sana.

Wapo waliomchukia kwa sababu aliwatenda isivyo haki. Lakini pia wapo waliomchukia kwa sababu uwepo wake uliwazuia kupata manufaa binafsi, yawe ya halali au ya dhuluma.

Ukweli unabakia pale pale, katika misiba mikubwa mitatu tuliyoipata - Mwalimu, Mkapa na Magufuli; hakika Mwalimu alililiwa na wote, japo hakuwa madarakani. Sikuwahi kumsikia hata mmoja akinena kuwa, ni aheri Mwalimu ametutoka. Mwalimu kabla ya kifo chake alisema, 'najua watanzania watanililia sana, lakini nami nitawaombea kwa Mungu'. Kwa matendo na unyofu wake, alikuwa na uhakika atamfikia Mungu.

Mwalimu alipostaafu, alipewa zawadi mbalimbali na taasisi mbalimbali lakini ama alizikataa ama alizipokea na kuzigawa. Nakumbuka alipokea trekta toka JKT kisha akakipatia kijiji ili wawe wanasombea maji. Kwa maneno yake alisema, 'Biblia inasema, ni aheri kwa ngamia kupenya tundu la sindano kuliko tajiri kuuona ufalme wa mbingu. Mnanipa vitu vyote hivi, mnataka niwe tajiri? Mimi nautamani ufalme wa mbinguni'.

Msiba huu ndiyo msiba pekee ulioonesha hali ambayo siyo ya kawaida kabisa, siyo hali ya kawaida mtu akifariki. Kuna watu wamesema wazi kabisa kuwa wanamshukuru Mungu amezisikia sala zao. Maana yake walikuwa wakiombea asiwepo Duniani!!!

Siwezi kusema neno hasa. Wala siwezi kuwalaani watu hao maana huna uhakika walipitia kwenye tanuru la namna gani wakati wa utawala wa Magufuli.

Huwezi kuelewa magumu aliyopitia Tundu Lisu, ni yeye na Mungu wake ndio wanajua.

Huwezi kujua wala kuhisi simanzi na magumu waliyoyapitia wazazi, wadogo na ndugu wa karibu wa Ben Saanane. Ni Mungu pekee yake ndiye anajua.

Ni vigumu kujua mateso ya nafsi waliyopitia wanafamilia wa Azory, yule diwani aliyeuawa na wanaCCM katili Dar, yule diwani aliyeuawa Kilosa, na yule mwenyekiti wa CHADEMA liyekatwa shingo kwa msumeno kule Arusha.

Fikiria mtoto wako, kaka yako, baba yako, mdogo wako - anauawa kwa kutakatwa na msumeno. Halafu hawa wote wakaambiwa kuwa ndugu yenu ameuawa na wanaCCM, na wauaji hawataguswa kwa sababu ndiyo watawala. Je, watu hawa watasikitikia vifo vya watawala ambao wanaamini walikuwa na mkono kwenye kifo cha ndugu yao? Hawa si ajabu, wakapiga magoti na kusema, 'Bwana tunakushukuru, kwa kuwa sauti ya mtu mnyonge imepata thamani mbele yako Bwana wa majeshi'.

Lakini hakika, ninyi nyote mlioguswa na magumu ya utawala wa marehemu kwa kuonewa, thawabu yenu ni kubwa mbinguni kama mtaweza kunena katika nafsi zetu, 'hakika bwana tuliumia na kuhuzunika sana lakini kwa kuwa wewe Yesu Kristu Bwana wetu, hata wakati ukiyandea mauti, ukiwa juu ya msalaba ulisema, Baba uwasamehe kwa kuwa hawajui watendalo. Basi nasi kwaajili ya neno hili, tunasema tumeyasamehe yote maana ni katika kusamehe, nasi tunasamehewa.
 
Lets be honest hivi nyomi ya huu msiba utaufananisha na ule wa kanumba?
 
Hata usiangaike na hao wanafiki wafata mkumbo, hawanaga Hoja zaidi kuvizia Lisu kasema nini nayeye atembee nalo ukiamua kuwapa jina zuri basi waite wajinga wafata mkumbo.

Na kwa sababu ujinga wao umeota mizizi miilini mwao basi hujiona wako wengi pale wanapoona welevu wamekaa kimya.

Usishangae wajinga hawa kumkubali kikwete nyakati hizi na kusahau matapishi yao.

Basi vile vile usishangae kesho kuwasikia wajinga hawa wakisema tulijua tu huyu mama hawezi kuyaenzi aliyoacha mzee.
Mzee gani? Amka wewe kichaa kumekucha bado unaota saa hizi!
 
Back
Top Bottom