Hakuna kosa wala dhambi kumkumbuka Magufuli, aliiweza nchi, kwa sasa kuwa na uhakika wa mambo ya kesho, haijulikani

Hakuna kosa wala dhambi kumkumbuka Magufuli, aliiweza nchi, kwa sasa kuwa na uhakika wa mambo ya kesho, haijulikani

As for now miradi inaendelea na mingine Mingi imeanzishwa Kwa nini saruji isiadimike?

Unakumbuka Dangote alitaka kutimkia? Mwendazake hakuna alivhoweza Kila mtu alikuwa mbaya kwake.

Wakitaka kumpora pesa Dangote shenzi zenu.

Mimi huwezi nidanganya awamu ya 5 Nina kumbukumbu vizuri.

Hata Mafuta ya kula yamianza kupanda 2019,Mafuta ya magari Kuna mwaka yaliadimika
Kosa la magufuli ni moja tu kwenu, kuwatimua wapumbavu wote waliokuwa wamejifanta wasomi kumbe vilaza wakubwa

Nyakati zile za kipumbavu, utamkuta Dkt akifanya opareshen ya kichwa ili hali mgonjwa alipaswa afanyiwe mguuni

Pumbavu zao vilaza wale! Sjui ndo kina nyie??
 
Kosa la magufuli ni moja tu kwenu, kuwatimua wapumbavu wote waliokuwa wamejifanta wasomi kumbe vilaza wakubwa

Nyakati zile za kipumbavu, utamkuta Dkt akifanya opareshen ya kichwa ili hali mgonjwa alipaswa afanyiwe mguuni

Pumbavu zao vilaza wale! Sjui ndo kina nyie??
Unamdanganya nani?
 
Magufuli ameacha nini? Ameacha wizi wa Tsh 2.4 Trilion, chuki dhidi ya upinzani, ubaguzi wa maendeleo kwa kupendelea Chato, umalaya kwa akina Jokate na Kairuki, matusi kwenye majukwaa, kuropoka, ubishi wa Corona mpaka imemuua, uuaji wa akina Ben Saanane na Azory Gwanda, utekaji wa akina MoDewji, maonezi kwa akina Eric Kabendera na Tito Magoti na dharau kwa wanawake tu.

Atakumbukwa kwa UDIKTETA, kukandamiza Demokrasia, Wizi wa uchaguzi Serikali za Mitaa 2019, wizi wa kura uchaguzi Mkuu 2020, kuvunja Katiba, kudhibiti Bunge na kuitishia Mahakama. Vilevile kuminya uhuru wa kujieleza na kuitishia vyombo vya habari.

Nani atanikamata leo nikisema Magufuli alikuwa muuaji? Hakuna kwa vile Rais SSH anakubali kukosolewa kwa misingi ya Sheria. Ila wapumbavu kama wewe wanafiriaalikuwa mtu wa maana
Mlimwagwa mitandaoni kama utitiri Kwa sababu ya kupambana na marehemu tu!!!

Mwanaume kama binti
 
Acha shobo bei iliwahi fika 4,000 Mkoani huko Dar ilikuwa kati ya 3000-35000 wakawa wanasema bei elwkesi ni 2700-2800 lakini wapi.
Acha uwongo kijana hii ya 4000 ni yenu msiojali maisha ya wananchi, mnajali wizi na kutetea mafisadi

Hivi ile ripoti ya CAG mbali na kelele za bunge lenu la maccm imefikia wapi?
 
Magufuli alikuwa ni disaster;
1.Alitangaza vita vya vyeti fake huku akilinda baadhi ya watumishi wakuu na idara nyingine wasiguswe.
2.Alihubiri kuangamiza rushwa lakini akiwaruhusu traffic police kupewa pesa za hongo alioiita pesa ya kupiga brush viatu.
3.Alianzisha elimu bure matokeo yake darasa la kwanza wanafunzi kwenye chumba kimmoja walijaa zaidi ya 200.
Hata pale vilipopatikana au kujenga vyumba vya madarasa hakuajiri walimu wapya kuendana na wingi wa madarasa.
4.Aliomba mkopo/msaada wa Elimu wenye thamani ya 400 million dollars uliokuwa na sharti ya kuruhusu waliozaa kurudi shuleni kuendelea na masomo,lakini ulipokuwa tiyari akauruka kimanga.

5.Akiwa waziri wa miundo mbinu wakati wa Jk,aliufagilia mradi wa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo,lakini alipoukwaa uraisi akaukana kabisa.
6.Alitumia pesa nyingi kujenga uzio wa kuzunguka eneo zima la madini ya Tanzanite huko Merelani ili kudhibiti utoroshaji wa madini hayo,kumbe wajanja wakachimba mahandaki kama ya wa Palestine ukanda wa Gaza,wakaendelea kutorosha madini hayo kwa njia za chini kwa chini.

7.Alihamia Dodoma kwa kuhamisha serikali yake na Taasisi mbali mbali tokea Dar kwa kile alichodai makao makuu ya nchi,lakini kwa nyakati mbali mbali akaifanya Chato kufanya shughuli mbali mbali za kitaifa hata kuliko Dodoma.
8.Hakupenda kukosolewa lakini yeye akiwakosoa waliomtangulia na viongozi wengine kwenye serikali yake.
9.Alikataa safari za kwenda nchi za nje za mbali akidai anapunguza matumizi kumbe alikuwa na kitufe Pacemaker chenye kurekebisha mapigo ya moyo ambacho kinaweza kuadhirika sana kwasababu ya mitambo ya electronic ya ndege.
10.Tuliambiwa tunadai ushuru wa makanikia sh 360 trillion tukaambuli sh 700 billion hata trillioni mmoja haijafika.
Kibaya zaidi Barrick waliitoa pesa hiyo kwa awamu wakisema ni msaada wa maendeleo wala si kodi ya makanikia hawadaiwi.
11.Alituhamasisha ataleta maendeleo kwa wananchi wote, kuwa hajali mwananchi anatokea chama gani lakini wakati mwingine akidai kuwabomolea nyumba ambao hawakumchagua.
12.Takwimu za viwanda alivyodai 8000 vimejengwa wakati wa utawala wake haikuwa sahihi.
Yule mtu angeendelea angeharibu Nchi harafu awe anawaambia wapumbavu eti Mabeberu wanamuonea wivu anajenga Sgr 😂😂

Hakuna mtu mwenye akili anaweza acha Nchi iwe kama Zimbabwe kisa tabia za kishenzi za mtu mmja tuu.
 
Sukari ilipanda bei kipindi chake, bundle lililpanda bei kipindi chake, au ulikua nchi gani?
Mgao ulikuwepo sema tu ulikua hautangazwi, mfano nikiwa Dar between 2017 na 2019 tulikua hatupati umeme jumamosi na jumapili wakisema wanatengeneza "mradi mkubwa kigamboni".

Kipindi cha Covid 19 bei ya mafuta ilishuka sana maana demand ilikua hamna. Sasa mafuta utamuuzia nani bei ya juu wakati wazungu wote walikua kwa lockdown?

Nani kakukataza? Mlifanya maadhimisho ile 17 March pale chato ila hamkufika watu 60!! Badala ya kelele nyingi humu nendeni Chato mkaadhimishe sio mnajazana upepo humu alafu ikifika 17 March mkawa busy kujadili kifo cha Bob Junior mkamsahau JPM!!
Wewe ndo ulikuwepo nchini peke ako?
 
Unaona unacjokifanya hapa
Chuki mby sn
Chuki au naweka sawa ukweli? 😂😂😂

Kumbe mbapenda sifa tuu ila mlipoharibu hamtaki 🤣🤣

Bora bwana yule aendelee kuongoza malaika mbinguni kama alivyosemaga yeye au nasema.uongo ndugu zangu?
 
Mlimwagwa mitandaoni kama utitiri Kwa sababu ya kupambana na marehemu tu!!!

Mwanaume kama binti
Wako tayari kutetea ujinga na upuuzi wa utawala huu! Lakini wao wanaona sawa tu!
Mtu mweusi kumtenganisha na upumbavu sio rahisi!
 
Huyu mama ananikumbusha awamu ya kikwete. Hapa ni sawa na ulikuwa unatumia Itel unaamua kubadili simu unachukua Tecno
 
Hatupaswi kukumbuka aliyofanya JPM! Tunalinda heshima ya Mama!
Ndivyo utamaduni wetu ulivyo! Yale mazuri aliyofanya JPM tunahesabu yamefanywa na Mama! Yaliyofanywa na JMK tulihesabu yalifanywa na JPM! Yaliyofanywa na BWM tunahesabu yalifanywa na JMK. na kurudi nyuma huko!
Kwa hiyo kwa sasa sifa zote ziende kwa Mama! Tatizo la Umeme litaisha na maisha yataaendelea!
 
Aliyesababisha Hadi Sukari kutoa 1500-2000 Hadi 3000-3500 ni Magufuli.

Huko kwenye umeme hakuna miujiza yeyote sana sana ni kwamba matumizi ya umeme yalipungua Kwa sababu watu walikimbia na kufunga biashara hivyo grid haikuwa na pressure tofauti na Sasa ambako kila kitu kimefunguka.

Hakuna wakati wowote Nchi hii Iko pazuri kushinda awamu ya 6,Kumlinganisha mtu aliyepora pesa za wafanyabiashara na Watumishi Kwa sababu ya kufilisika ni kumkosea heshima Samia.

Mwisho hakuna mtu anakukataza kumuwaza Mwendazake,wenzako wanaomtumia kama.kete ya siasa Kwa wajinga wewe unamkumbuka kushinda Muumba wako,hapo ndipo laana itakutafuna.
huyu wa sasa hakuna jipya zaidi anafuata nyayo za mwanaume kiufupi ni mtumwa wa ilani iliyoandaliwa na jembe mwamba tingatinga bulldozer kiboko ya mashoga kiboko ya majizi majambazi maporaji maharamia makuwadi mazezeta matoto ya mama uenye vyeti feki mazembe mazururaji mababaishaji masaliti yalikiri yakakiri yakaduwaa mbele ya Simba Tai fastjet
 
huyu wa sasa hakuna jipya zaidi anafuata nyayo za mwanaume kiufupi ni mtumwa wa ilani iliyoandaliwa na jembe mwamba tingatinga bulldozer kiboko ya mashoga kiboko ya majizi majambazi maporaji maharamia makuwadi mazezeta matoto ya mama uenye vyeti feki mazembe mazururaji mababaishaji masaliti yalikiri yakakiri yakaduwaa mbele ya Simba Tai fastjet
🚮🚮🚮 Kama anafuata nyayo unasikia vyuma kukaza au watu kutekwa na kupotea?

That dude was useless 😂😂
 
🚮🚮🚮 Kama anafuata nyayo unasikia vyuma kukaza au watu kutekwa na kupotea?

That dude was useless 😂😂
Kwa hiyo saizi hawatekwi? Hao vijana wa vingunguti Waliouawa juzi hapa,Kijana wa mbezi week ilopita kaonekana ameuliwa!
Wale vijana wa Kariakoo wa tano mpaka leo hawajawahi kuonekana, Geita nako watu wamepotea!
Mauaji kila kona ya nchi huyaoni wewe punga?
Mauaji vituo vya polisi na Wagonjwa kupata mateso mahospitalini na kufa kwa uzembe husikii?
Yaani wewe akitekwa mmoja mwanasiasa ndo jambo hatari ila wakitekwa na kuuliwa wananchi wa kawaida sawa tu!
Jinga kabisa!
 
Back
Top Bottom