Hakuna mchezaji aliyefikia kiwango cha Pele?

kipindi de lima na zizou walipochukua ballorn d'or mara tatu tatu dunia ikajua hakuna mwingine ambae anaweza akavunja rekodi za magwiji hao
lakini kumbe kapo haka kajamaa mdogo kwa umbo mkubwa kwa mambo messi mahatrick!
rekodi anazoweka nahisi itapita miaka 1000 kuvunjwa
nani mwingine atakuja kuchukua ballorn d'or mara tano?????
sahau kuhusu world cup hiyo itakuwa kama additional qualification on his already impressive cv
messi mahatrick hana mpinzani
 
Hapana aisee, unapozungumzia skills na ufungaji dinho ni nyoko. Kwa skills huyu jamaa hakuna mtu aliyefikia level yake.
 
Until he wins World Cup he can't be compared to Maradona or Gaucho to say the least

Si sababu w/cup..sikatai pele ana mengi kutokana na ushindi usiokuwa na mvuto kiasi icho(offside free).. lkn kaachwa mbali mno na de D10s, na Isitoshe pia kaachwa mbali na zizle! Na hapo sijui utaniambia nini! Hapo messi nimemweka PENDING
 

Asante sana mkuu kwa kuwaelewesha..hapo watakuwa wamekuelewa vyakutosha na wameshajitambua
 
Uliowataja walikuwa wachezaji wazuri lakini sio kwa level Ya Maradona

MARADONA HABARI INGINE..Hao aliowataja namuongeza na REDONDO,MARIO KEMPES waargentina wengine hawa walikuwa wakali ile mbaya kipindi cha maradona, Beckenbauer mjerumani huyu alikuwa na yeye fimbo wa kuotea mbali..sasa hawa wa3 dinyo wenu bado kufikia kiwango chao zaidi ya kurukaruka uwanjani tu utafikiri mnyama flani ivi wa baharini aitwaye PENGUIN
 
Ni kumkosea CR7 heshima kumlinganisha na Neymar kwa sasa ila Neymar ni very promising naamini atavunja records nyingi

Neymar ana mambo mengi, anahitaji kocha wa kumfundisha kuwa na concentration.

By the way vipaji siku hizi hakuna kabisa.
 
Hakuna kama mtakatifu Dinho Gaucho Mnyama,huyu ni Nabii na Mtume wa mwisho kwenye Soka,hatatokea mwingine kama kabla ya miaka 2000 kuisha.

Kwa kipi alichokifanya chamaana mpaka umtukuze kiasi icho, kukenua meno?kurukaruka uwanjani ka mnyama PENGUIN? kukatika (mauno) kipi unamaanisha? hakuna mchezaji yeyote ulimwenguni na hakuna ataekuja kutokea baada ya miaka 1000 kufikia uwezo wa maradona na messi huu ndio ukweli.
 
Pele na Maradona ni malegendary wa soka katika dunia hii. Ronaldinho Gaucho kaja na ufundi kwenye kabumbu.

Hawa kina messi, CR7 tunawazungumzia kwasababu ndio kipindi/zama zaotu. Hawamfikii Gaucho.

Mkuu mi nataka tu ututhibitishie kwa kipi dinyo kamzidi messi? Lete record zote za dinyo mpaka alipoenda kujifia huko ac milan then kakimbilia brazil kwao.then lete na za KING MESSI hapo ndio ntakuona wa maana! Nasubiri
 
Mkuu mi nataka tu ututhibitishie kwa kipi dinyo kamzidi messi? Lete record zote za dinyo mpaka alipoenda kujifia huko ac milan then kakimbilia brazil kwao.then lete na za KING MESSI hapo ndio ntakuona wa maana! Nasubiri
Gaucho is a World Cup winner, the ultimate prize which every player dreams about
Messi ataiangalia World Cup kwenye runinga tu
 
Ukichaa wako wa kuzaliwa au kulogwa?kama ni kurogwa tukupeleke kwa Sangoma.

Umeona eee hizo ni dalili za kuwakubali hao niliowataja,maneno machafu hayasaidii kitu..hahaahaaaa messi ataendelea kuwapa hat attack
 
Ronaldo de Assis Morreira, best ever, wengine nawapa heshima ila huyu ndo mchezaji wangu bora wa muda wote!

Tatizo lenu mnapenda ushabiki! Mkiambiwa leteni records zake alivoanza mpaka alipojifia huko alipo ooh mnabaki dinyo bana acha kabisa yule jamaa hakunaga... sasaa sisi tunataka vitu vyote vya maana alivyomzidi huyu kiumbe magician! Kama unavyo lete hapa! Kama ni world cup kuchukua dinyo alikuwepo lkn hakuisaidia timu yake chochote kile zaidi ya de lima na rivaldo ndio waliofanya kazi ya ziada pale
 
Sasa zilikuwa vipi offside kama offside hazikuwepo?

Ulikuwa unanyonya bado! Angalia clip zake utaona facts..na maprofessional wamelizungumzia sana hilo la offside free, ukipigia hesabu ya harska haraka utapata magoli yake ya kihalali si chini ya 600, ingekuwa ni free mpaka sasa maradona, messi,suarez aguero,nk may be 2000 goals to now
 
pele kacheza mpira kipindi ambacho ni kigumu sana, ambacho sheria nyingi zilikua bado kutungwa ambazo kwa sasa zinamlinda mchezaji, zidane, ronadinho wamecheza mpira kipindi ambacho dunia ilikua na wachezaji wenye viwango bora ambao ni wengi sana, messi na ronaldo wa ureno wanacheza mpira kipindi ambacho dunia imekosa kutoa wachezaji wenye viwango sawa vya ubora ndo maana wataonekana ni bora zaidi ya kizazi cha kina de lima, nakata na kile cha kina pele ambacho kilikua na watu wengi wenye ubora zaidi kuliko kile kizazi cha maradona
 
Punguza povu basi mkuu, umekisoma vizuri nilichoandika kweli, Sawa Dinho hakufanya kitu kule Korea na Japan, ila kamuulize David Seaman yule Goalkeeper wa England, Dinho ni nani? Zingatia sana neno HESHIMA, na neno langu sio Sheria
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…