Hakuna Mlipa Kodi anayependa kodi! Serikali na wananchi wajue hili

Hakuna Mlipa Kodi anayependa kodi! Serikali na wananchi wajue hili

Uzuri ni kuwa hawa sioni kama wanaonewa,ila wanakubali kwa hiyari yao kuwa waimba mapambio au kuimbishwa mapambio tena kwa sauti kuu huku wakidhulumiwa na kuporwa haki zao za msingi,hata wanaojitokeza kuwasaidia wanaona hawana maana.

Upande wa huyo bwana nasisi bila shaka na wewe umo.

Gharama ya magari yale si mcheza na mzigo wa yale mengine:

IMG_20210716_182538_628.jpg


Wewe unaona wapi?
 
Waswahili wana msemo wao kwamba ukitaka kuruka hakikisha unaagana na nyonga yako. Watanzania tulio wengi tunapenda kuyasikia maendeleo mazuri lakini hatuko tayari kuyagharamia. Waingereza wana msemo wao kwamba No Free Lunch. Bajeti kuu ya serikali ya mwaka 2021/2022 imetengeneza mazingira ya kila mwananchi ahusike kulipa kodi.

Taifa lolote imara mapato yao makubwa hutegemea kodi. Na nchi nyingi zilizoendelea kwao huwa ni fahari mtu kulipa kodi kwa ajili ya taifa lake. Lakini kwetu Afrika mtu anaona fahari kukwepa kodi wakati wenzetu kukwepa kodi ni fedheha sana katika taifa lako.

Tuna miaka 61 tangu tupate uhuru lakini maendeleo tuliyo nayo kama taifa hayaendani na umri wetu. Tukitaka mambo rahisi taifa letu litazidi kuwa maskini. Kodi ya mwaka huu inamfanya kila mwananchi ahusike kuijenga nchi yake ambayo itamfanya kuwa na wivu na taifa lake na atakuwa sehemu ya ujenzi wa taifa lake.

Kwenye hizi kodi watu wengi tumekimbilia kushambulia viongozi wetu na kusahau kuangalia faida itakayopatikana baada ya makato hayo. Barabara vijijini zitaboreshwa na zahanati nyingi zitajengwa kutokana na kodi hizo. Hii itapelekea nchi yetu kukua kwa kasi. Lazima kila mwananchi afunge mkanda ili tuyafikie maendeleo tunayoyakusudia kama taifa.

Wakati tunashangilia kwamba kila kijiji kinatarajia kuwa na umeme ni hizo kodi zetu zilizokatwa kwenye mafuta. Kwanini tusiendelee kukaza mkanda ili taifa letu tulitoe kwenye ombwe la umaskini.

Taifa letu inabidi likue tusitegemee sana misaada ya wenzetu. Mtegemea cha nduguye hufa maskini. Hii kodi imeitwa solidarity fund ambapo itapelekea nchi yetu kukua kwa kasi kimaendeleo.
Mimi siyo mtaalamu wa uchumi ila naiona nia ya dhati ya serikali ya kuwakomboa wananchi wote kwenye mazingira yao.

Haya mambo hatukayazoea ya kukatwa hela hizo lakini hiyo ndio njia nzuri ya kufanikiwa. Hatuwezi kubaki na mawazo yaleyale kama taifa halafu tukawaza kusonga mbele. Hii tusiichukulie kama adhabu bali tuone ni fahari kulipa kodi kwa ajili ya taifa letu.
Tanzania itajengwa na watanzania wenyewe.
#lipakodibilashuruti
#tanzaniaitajengwanawatanzania
 
Wabunge mishahara yao haikatwi kodi.

Siyo wazalendo?
 
Waswahili wana msemo wao kwamba ukitaka kuruka hakikisha unaagana na nyonga yako. Watanzania tulio wengi tunapenda kuyasikia maendeleo mazuri lakini hatuko tayari kuyagharamia. Waingereza wana msemo wao kwamba No Free Lunch. Bajeti kuu ya serikali ya mwaka 2021/2022 imetengeneza mazingira ya kila mwananchi ahusike kulipa kodi.

Taifa lolote imara mapato yao makubwa hutegemea kodi. Na nchi nyingi zilizoendelea kwao huwa ni fahari mtu kulipa kodi kwa ajili ya taifa lake. Lakini kwetu Afrika mtu anaona fahari kukwepa kodi wakati wenzetu kukwepa kodi ni fedheha sana katika taifa lako.

Tuna miaka 61 tangu tupate uhuru lakini maendeleo tuliyo nayo kama taifa hayaendani na umri wetu. Tukitaka mambo rahisi taifa letu litazidi kuwa maskini. Kodi ya mwaka huu inamfanya kila mwananchi ahusike kuijenga nchi yake ambayo itamfanya kuwa na wivu na taifa lake na atakuwa sehemu ya ujenzi wa taifa lake.

Kwenye hizi kodi watu wengi tumekimbilia kushambulia viongozi wetu na kusahau kuangalia faida itakayopatikana baada ya makato hayo. Barabara vijijini zitaboreshwa na zahanati nyingi zitajengwa kutokana na kodi hizo. Hii itapelekea nchi yetu kukua kwa kasi. Lazima kila mwananchi afunge mkanda ili tuyafikie maendeleo tunayoyakusudia kama taifa.

Wakati tunashangilia kwamba kila kijiji kinatarajia kuwa na umeme ni hizo kodi zetu zilizokatwa kwenye mafuta. Kwanini tusiendelee kukaza mkanda ili taifa letu tulitoe kwenye ombwe la umaskini.

Taifa letu inabidi likue tusitegemee sana misaada ya wenzetu. Mtegemea cha nduguye hufa maskini. Hii kodi imeitwa solidarity fund ambapo itapelekea nchi yetu kukua kwa kasi kimaendeleo.
Mimi siyo mtaalamu wa uchumi ila naiona nia ya dhati ya serikali ya kuwakomboa wananchi wote kwenye mazingira yao.

Haya mambo hatukayazoea ya kukatwa hela hizo lakini hiyo ndio njia nzuri ya kufanikiwa. Hatuwezi kubaki na mawazo yaleyale kama taifa halafu tukawaza kusonga mbele. Hii tusiichukulie kama adhabu bali tuone ni fahari kulipa kodi kwa ajili ya taifa letu.
Tanzania itajengwa na watanzania wenyewe.
#lipakodibilashuruti
#tanzaniaitajengwanawatanzania
Unaufahamu uzalendo wewe? Au umeandika tu ili ufurahishe genge?

Uzalendo ni kuhamasisha watu wa kipato cha kawaida walipe kodi halafu wa kipato cha juu mfano Wabunge, Rais, nk wasilipe?

Uzalendo ni kuona watoto wa maskini wakisoma shule za kata halafu watoto wa viongozi kusoma shule za international?

Unaongelea uzalendo, au UNAFIKI? Yaani unaongelea Uzalendo na wakati huyo mwigulu na Rais wake kila kitu kwao ni bure tu! Hawanunui muda wa maongezi, hawanunui mafuta ya Ma V 8 yao, hawajui kodi ya pango ikoje! Mishahara yao ni minono!!

Hauko serious hata kidogo.
 
Tartiiiiiiiiibu CCM Inaenda Kujimaliza Yenyewe.
HAKUNA mlala hoi hata mmoja ambaye hili halitamgusa. Na kwa Kuwa Linawagusa Wengi usidhani Wataendelea Kukuchekea..... ! Take care
 
Mamluki. Kodi ambayo hatujui inakwenda wapi? Ridhikeni msijifanye wakoloni mana hii ni kama kodi ya kichwa tu...
 
Tartiiiiiiiiibu CCM Inaenda Kujimaliza Yenyewe.
HAKUNA mlala hoi hata mmoja ambaye hili halitamgusa. Na kwa Kuwa Linawagusa Wengi usidhani Wataendelea Kukuchekea..... ! Take care
Mama nchi ishamshinda aachie ngazi
 
Tartiiiiiiiiibu CCM Inaenda Kujimaliza Yenyewe.
HAKUNA mlala hoi hata mmoja ambaye hili halitamgusa. Na kwa Kuwa Linawagusa Wengi usidhani Wataendelea Kukuchekea..... ! Take care
Mama nchi ishamshinda aachie ngazi
 
Waswahili wana msemo wao kwamba ukitaka kuruka hakikisha unaagana na nyonga yako. Watanzania tulio wengi tunapenda kuyasikia maendeleo mazuri lakini hatuko tayari kuyagharamia. Waingereza wana msemo wao kwamba No Free Lunch. Bajeti kuu ya serikali ya mwaka 2021/2022 imetengeneza mazingira ya kila mwananchi ahusike kulipa kodi.

Taifa lolote imara mapato yao makubwa hutegemea kodi. Na nchi nyingi zilizoendelea kwao huwa ni fahari mtu kulipa kodi kwa ajili ya taifa lake. Lakini kwetu Afrika mtu anaona fahari kukwepa kodi wakati wenzetu kukwepa kodi ni fedheha sana katika taifa lako.

Tuna miaka 61 tangu tupate uhuru lakini maendeleo tuliyo nayo kama taifa hayaendani na umri wetu. Tukitaka mambo rahisi taifa letu litazidi kuwa maskini. Kodi ya mwaka huu inamfanya kila mwananchi ahusike kuijenga nchi yake ambayo itamfanya kuwa na wivu na taifa lake na atakuwa sehemu ya ujenzi wa taifa lake.

Kwenye hizi kodi watu wengi tumekimbilia kushambulia viongozi wetu na kusahau kuangalia faida itakayopatikana baada ya makato hayo. Barabara vijijini zitaboreshwa na zahanati nyingi zitajengwa kutokana na kodi hizo. Hii itapelekea nchi yetu kukua kwa kasi. Lazima kila mwananchi afunge mkanda ili tuyafikie maendeleo tunayoyakusudia kama taifa.

Wakati tunashangilia kwamba kila kijiji kinatarajia kuwa na umeme ni hizo kodi zetu zilizokatwa kwenye mafuta. Kwanini tusiendelee kukaza mkanda ili taifa letu tulitoe kwenye ombwe la umaskini.

Taifa letu inabidi likue tusitegemee sana misaada ya wenzetu. Mtegemea cha nduguye hufa maskini. Hii kodi imeitwa solidarity fund ambapo itapelekea nchi yetu kukua kwa kasi kimaendeleo.
Mimi siyo mtaalamu wa uchumi ila naiona nia ya dhati ya serikali ya kuwakomboa wananchi wote kwenye mazingira yao.

Haya mambo hatukayazoea ya kukatwa hela hizo lakini hiyo ndio njia nzuri ya kufanikiwa. Hatuwezi kubaki na mawazo yaleyale kama taifa halafu tukawaza kusonga mbele. Hii tusiichukulie kama adhabu bali tuone ni fahari kulipa kodi kwa ajili ya taifa letu.
Tanzania itajengwa na watanzania wenyewe.
#lipakodibilashuruti
#tanzaniaitajengwanawatanzania
Mbona kodi zinalipwa tatizo ni aina zipi za kodi zilipwe , pia kodi iwiane na maendeleo na matumizi, hata ulipe kodi vipi kama matumizi yasiyo ya msingi ni makubwa basi kodi inakuwa haina maana kwa kuleta maendeleo, uzalendo uanzie kwanza kwa hao hao wanaosema tulipe kodi, nadhani umeona matumizi yao.
 
Toka karne nyingi zilizopita suala la ulipaji kodi limekuwa likikwepwa sana na raia wa mataifa mbali mbali hadi kupelekea kutungwa sheria kali za kuwabana walipa kodi.

Nchi yetu Tanzania ina nguvu kazi kubwa na hazina ya vijana ambao wengi hawashiriki kikamilifu kulipa kodi.

Mfumo wetu wa ulipaji kodi unawalenga tu wafanyabiashara wakubwa na wafanyakazi walio kwenye mfumo rasmi huku ikiwaacha mamilioni ya watanzania nje ya mfumo wa kodi.

Ukiacha VAT inayolipwa na wote kuna makundi mfano:-

Bodaboda hawalipi kodi, japo wanaingiza kipato kwa mwezi mara nyingine kuliko hata mwalimu.

Wamachinga zaidi ya mchango wa 20,000 za kipindi cha Magufuli hakuna kodi nyingine wanalipa.

Wakulima nao hali kadhalika, kodi zao ni kwa wakulima wakubwa tu ambao ni wachache mno.

Na hawa ni wengi sana. Je nchi itapigaje hatua bila kutafuta kodi itakayo wahusisha wote? Jibu ni rahisi maana asilimia kubwa ya hili kundi linatumia mitandao ya simu kufanya miamala basi tuwafuate huko huko.

Wanaopinga tozo za miamala Je mnataka nchi isonge mbele kwa kodi za nani?

Angalia toka asubuhi hadi jioni ni fedha kiasi gani umekatwa kama kodi na je zinatosha kukuletea huduma unazohitaji?

Rais Magufuli alikamua kodi mpaka mwisho lakini aliishia kupata 1.2 Trillion kwa mwezi ambazo hazitoshi kabisa.

Tutakapolipa wote kodi, uchungu wa kuzifuatilia utaongezeka na maendeleo yatapatikana. Kuliko wachache wanaumia kulipa kodi, wengine wanashinda instagram kupromote udaku.
 
Kweli bhana tulipe ili na viongozi waongeze misafara hata kuzindua vyoo
 
ulipe kodi kwenye serikali inayopanga bajeti ya kipuuzi ya 80% matumizi ya kawaida na 20% maendeleo?

hii siyo kodi. ni dhulma.

wanajua hawana uwezo wa kuwadai kodi wafanyabiashara wakubwa kama alivyokuwa anafanya Rais Magufuli sasa wanaonea watu wa hali ya chini.
 
Tartiiiiiiiiibu CCM Inaenda Kujimaliza Yenyewe.
HAKUNA mlala hoi hata mmoja ambaye hili halitamgusa. Na kwa Kuwa Linawagusa Wengi usidhani Wataendelea Kukuchekea..... ! Take care
Mama nchi ishamshinda aachie ngazi
 
Back
Top Bottom