Hakuna mpinzani mwenye uwezo wa kushindana na Rais Samia kwenye jukwaa wala ndani ya sanduku la kura

Hakuna mpinzani mwenye uwezo wa kushindana na Rais Samia kwenye jukwaa wala ndani ya sanduku la kura

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
28,722
Reaction score
20,610
Ndugu zangu watanzania,

Huo ndio ukweli kuwa kwa Sasa Hakuna mpinzani au mtu yeyote kutoka upinzani mwenye uwezo wa kushindani na Rais Samia Jukwaani Na hata katika sanduku la kura, kwa Sasa Rais Samia ndiye kiongozi mwenye ushawishi mkubwa Sana hapa Barani Afrika na ukanda huu wa Afrika mashariki.

Ni kiongozi ambaye Kuna nchi zinatamani angezaliwa kwao ili aweze kuwatumikia Kama ambavyo anatutumikia watanzania,wanatamani wapate kiongozi msikivu, mnyenyekevu,mchapa kazi ,mzalendo,mwana demokrasia,mwana diplomasia, mcha Mungu na mwenye hofu ya Mungu Kama Rais wetu.

Wanatamani wangekuwa na Rais Samia nchini kwao atakaye wasikiliza sauti zao na kuwatazama shida zao,lakini kwa bahati Nzuri Ni kuwa Rais Samia alizaliwa Tanzania na kuinuliwa na Mwenyezi MUNGU kwa ajili ya kuwatumikia Watanzania kutoka katika umaskini na kusonga mbele kimaendeleo na kiuchumi.

Ni kiongozi Ambaye watanzania wanatamani kumsikiliza muda wote,wanatamani kumuona akifika maeneo yao kwa kuwa wanajuwa Kuna Tumaini jipya juu ya kero na changamoto zao afikapo Rais wao, Wanajuwa kuwa watasikilizwa na kupewa majibu ya kuridhisha.

Kila anapokuwa mh Rais na kutoa hotuba yake inakuwa Ni hotuba iliyo jaa matumaini kwa watanzania wote,inakuwa Ni hotuba inayojibu maswali ya watanzania wote,anaweza akawa Dodoma lakini hotuba yake ikajibu maswali na kutoa matumaini kwa wakulima wa Mbozi mkoani Songwe au wafanyabiashara na vijana wa Tunduma mkoani Songwe.

Ni kiongozi ambaye maneno yake yanaponya wenye kuumizwa na kero mbalimbali,yanaleta faraja na matumaini kwa waliokata Tamaa,Yanaleta matumaini kwa walio poteza Dira,yanaamsha ari na nguvu ya kufanya kazi kwa walio nyong'onyea,Yanaleta ujasiri na kutia hamasa kwa walio kaa chini.

Rais Samia Amewafanya watanzania wasitamani hata kufanyika kwa uchaguzi maana wanaona Ni upotevu wa pesa kwa kuwa wameridhishwa na utendaji kazi wake na wangependa aendelee kuwatumikia kwa kuwa ameonyesha dhamira ya dhati katika kumfanya kila mtanzania awe na Tabasamu la kiuchumi na kumgusa kila mtu kiutendaji.

Kazi alizozifanya mh Rais ndani ya muda mfupi zimeikonga mioyo ya watanzania, Zimewagusa kila watu, zimeamsha matumaini katika kila secta, zimeleta amani na utulivu kwa watumishi wa umma, zimewainua na kuwaheshimisha wakulima na kilimo.

Zimeamsha matumaini kwa wanafunzi wanao pata Elimu bure,zimeleta Tabasamu kwa wafanya Biashara, zimekuwa chambo kwa wawekezaji na watalii kumiminika na kufurika nchini, zimeleta umoja na mshikamano miongoni mwa watanzania, zimeiheshimisha nchi yetu na kuifanya kuheshimika kimataifa.

Ni wapi na secta ipi ambako Rais Samia Hajafika? Ni Nani ambaye hajafikiwa na Rais Samia? Ni wapi na mkoa upi ambao haujapelekewa maendeleo na mabillioni ya pesa?

Ni mwananchi yupi ambayeAmeonewa au kuumizwa kimaneno na kimatendo na Rais Samia na serikali Yake? Ni Nani ambaye ndoto zake zinakwama kwa sababu ya serikali ya Rais Samia?

Kazi Iendeleee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu. 0742-676627
 
Ndugu zangu watanzania,

Huo ndio ukweli kuwa kwa Sasa Hakuna mpinzani au mtu yeyote kutoka upinzani mwenye uwezo wa kushindani na Rais Samia Jukwaani Na hata katika sanduku la kura, kwa Sasa Rais Samia ndiye kiongozi mwenye ushawishi mkubwa Sana hapa Barani Afrika na ukanda huu wa Afrika mashariki.

Ni kiongozi ambaye Kuna nchi zinatamani angezaliwa kwao ili aweze kuwatumikia Kama ambavyo anatutumikia watanzania,wanatamani wapate kiongozi msikivu, mnyenyekevu,mchapa kazi ,mzalendo,mwana demokrasia,mwana diplomasia, mcha Mungu na mwenye hofu ya Mungu Kama Rais wetu.

Wanatamani wangekuwa na Rais Samia nchini kwao atakaye wasikiliza sauti zao na kuwatazama shida zao,lakini kwa bahati Nzuri Ni kuwa Rais Samia alizaliwa Tanzania na kuinuliwa na Mwenyezi MUNGU kwa ajili ya kuwatumikia Watanzania kutoka katika umaskini na kusonga mbele kimaendeleo na kiuchumi.


Ni kiongozi Ambaye watanzania wanatamani kumsikiliza muda wote,wanatamani kumuona akifika maeneo yao kwa kuwa wanajuwa Kuna Tumaini jipya juu ya kero na changamoto zao afikapo Rais wao, Wanajuwa kuwa watasikilizwa na kupewa majibu ya kuridhisha.

Kila anapokuwa mh Rais na kutoa hotuba yake inakuwa Ni hotuba iliyo jaa matumaini kwa watanzania wote,inakuwa Ni hotuba inayojibu maswali ya watanzania wote,anaweza akawa Dodoma lakini hotuba yake ikajibu maswali na kutoa matumaini kwa wakulima wa Mbozi mkoani Songwe au wafanyabiashara na vijana wa Tunduma mkoani Songwe.

Ni kiongozi ambaye maneno yake yanaponya wenye kuumizwa na kero mbalimbali,yanaleta faraja na matumaini kwa waliokata Tamaa,Yanaleta matumaini kwa walio poteza Dira,yanaamsha ari na nguvu ya kufanya kazi kwa walio nyong'onyea,Yanaleta ujasiri na kutia hamasa kwa walio kaa chini.

Rais Samia Amewafanya watanzania wasitamani hata kufanyika kwa uchaguzi maana wanaona Ni upotevu wa pesa kwa kuwa wameridhishwa na utendaji kazi wake na wangependa aendelee kuwatumikia kwa kuwa ameonyesha dhamira ya dhati katika kumfanya kila mtanzania awe na Tabasamu la kiuchumi na kumgusa kila mtu kiutendaji.


Kazi alizozifanya mh Rais ndani ya muda mfupi zimeikonga mioyo ya watanzania,Zimewagusa kila watu, zimeamsha matumaini katika kila secta,zimeleta amani na utulivu kwa watumishi wa umma,zimewainua na kuwaheshimisha wakulima na kilimo,zimeamsha matumaini kwa wanafunzi wanao pata Elimu bure,zimeleta Tabasamu kwa wafanya Biashara,zimekuwa chambo kwa wawekezaji na watalii kumiminika na kufurika nchini,zimeleta umoja na mshikamano miongoni mwa watanzania, zimeiheshimisha nchi yetu na kuifanya kuheshimika kimataifa.


Ni wapi na secta ipi ambako Rais Samia Hajafika? Ni Nani ambaye hajafikiwa na Rais Samia? Ni wapi na mkoa upi ambao haujapelekewa maendeleo na mabillioni ya pesa? Ni mwananchi yupi ambayeAmeonewa au kuumizwa kimaneno na kimatendo na Rais Samia na serikali Yake? Ni Nani ambaye ndoto zake zinakwama kwa sababu ya serikali ya Rais Samia?


Kazi Iendeleee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu. 0742-676627
Una bidii kweli ya kutafuta kuolewa karibu utapata mume
 
Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu. 0742-676627
Pole Sana ndugu. Yaelekea una damu ya kunguni na nyota ya gundu.

Unakaribia kutujazia server hapa JF kwa kuandika ujinga na kuambatanisha namba yako lkn huteuliwi.

Mwenzako Kafulila ameandika miezi michache tu na Sasa kapewa shavu.
 
Pole Sana ndugu. Yaelekea una damu ya kunguni na nyota ya gundu.

Unakaribia kutujazia server hapa JF kwa kuandika ujinga na kuambatanisha namba yako lkn huteuliwi.

Mwenzako Kafulila ameandika miezi michache tu na Sasa kapewa shavu.
Mimi Kam mpig Kura niliyepiga na kuipigia CCM Kura katika ngazi zote ninakuwa sijatenda kosa nikimpongeza mh Rais kwa utendaji kazi wake uliyo tukuka na wenye kuleta matumaini ndani ya muda mfupi wa uongozi wake.
 
Wewe sasa unakoelekea si kuzuri!
Watanzania gani wamekwambia hawataki tena uchaguzi?!
Uchawa unalipa lakini wanatakiwa pia Chawa wenye maarifa siyo chawa wa kutia aibu kama wewe!
Unasifia mpaka unapitiliza!
Vipi jana umemsikia Rais Ruto wa Kenya akihojiwa na wanahabari wenye maarifa kuhusu kukopa na madeni ya Taifa hilo?!
Amesema boldly kabisa kwamba hawezi kuendesha Nchi kwa kutegemea mikopo kwani Kenya inaweza kufilisika ( run bankrupt)!
Chawa mwenzako David Kafulila kalamba uteuzi leo kwa kusifia ukopaji!
Ebu na wewe tafuta topic nzuri usifie vizuri utateuliwa maana namba yako ya simu tayari imeshachukuliwa!
 
Una bidii kweli ya kutafuta kuolewa karibu utapata mume
Kwani wewe hunaga hoja mbadala,.kazi alizozifanya mh Rais zinaonekana hata kwa kugusa na kusikia kwa mtu Ambaye Ni kipofu wa macho, kila sehemu Ni kazi za Rais Samia,hata wanafunzi wanatambua kazi kubwa alizozifanya mh Rais,ipo Siku utakubalii tuu utendaji kazi wa Rais
 
Wewe sasa unakoelekea si kuzuri!
Watanzania gani wamekwambia hawataki tena uchaguzi?!
Uchawa unalipa lakini wanatakiwa pia Chawa wenye maarifa siyo chawa wa kutia aibu kama wewe!
Unasifia mpaka unapitiliza!
Vipi jana umemsikia Rais Ruto wa Kenya akihojiwa na wanahabari wenye maarifa kuhusu kukopa na madeni ya Taifa hilo?!
Amesema boldly kabisa kwamba hawezi kuendesha Nchi kwa kutegemea mikopo kwani Kenya inaweza kufilisika ( run bankrupt)!
Chawa mwenzako David Kafulila kalamba uteuzi leo kwa kusifia ukopaji!
Ebu na wewe tafuta topic nzuri usifie vizuri utateuliwa maana namba yako ya simu tayari imeshachukuliwa!
William Ruto anafata njia za Rais wetu katika kujenga Taifa ,maana amewaambia wakenya kuwa Ni lazima kila mtu alipe ushuru na Kodi Jambo ambalo sisi watanzania chini ya uongozi shupavu na madhubuti wa Rais Samia Tulishalianza muda katika kuhakikisha kuwa tunajenga nchi yetu kwa mikono yetu wenyewe kwa kuchangia kupitia vipato vyetu kwa kadri kila mmoja wetu anavyo pata na kukaliwa na Mwenyezi MUNGU,ndio maana uliona kupitia Tozo serikali yetu ilijenga vituo vya Afya 234 nchini,hapo bado sijazungumzia kwenye secta nyingine Kama Elimu n.k
 
Jamani mamlaka za uteuzi naomba huyu Lucas Mwashambwa mumteue haraka jamani!
Huyu mtu anazidi kujidhalilisha hivi na nyie mnamwangalia tu!
Basi mpigieni hata simu kwamba njaa yake ya uteuzi mnaifanyia kazi,namba zake amewawekea hapo!
Huyu jamaa nadhani siko pekee yangu, AMETUCHOSHA NA KILIO CHAKE CHA UTEUZI!!!
 
Jamani mamlaka za uteuzi naomba huyu Lucas Mwashambwa mumteue haraka jamani!
Huyu mtu anazidi kujidhalilisha hivi na nyie mnamwangalia tu!
Basi mpigieni hata simu kwamba njaa yake ya uteuzi mnaifanyia kazi,namba zake amewawekea hapo!
Huyu jamaa nadhani siko pekee yangu, AMETUCHOSHA NA KILIO CHAKE CHA UTEUZI!!!
Asikilizie tangazo la kesho 🤣🤣🤣
 
Jamani mamlaka za uteuzi naomba huyu Lucas Mwashambwa mumteue haraka jamani!
Huyu mtu anazidi kujidhalilisha hivi na nyie mnamwangalia tu!
Basi mpigieni hata simu kwamba njaa yake ya uteuzi mnaifanyia kazi,namba zake amewawekea hapo!
Huyu jamaa nadhani siko pekee yangu, AMETUCHOSHA NA KILIO CHAKE CHA UTEUZI!!!
Nani kakwambia kuwa haya maoni yangu Ni Barua ya maombi ya uteuzi,Hapa Ni jukwaa huru mahali pa kuwasilisha mawazo na siyo posta ya kutuma Barua
 
Nani kakwambia kuwa haya maoni yangu Ni Barua ya maombi ya uteuzi,Hapa Ni jukwaa huru mahali pa kuwasilisha mawazo na siyo posta ya kutuma Barua
Wewe hata ndugu zako wa damu wanakuona kinyaa maana unawaaibisha kwa huu upuuzi wako.
 
Back
Top Bottom