Pre GE2025 Hakuna mwana CCM yeyote zaidi ya Rais Samia atakayechukua fomu ya Urais wala kutia nia 2025 kwasababu ya utamaduni wetu

Pre GE2025 Hakuna mwana CCM yeyote zaidi ya Rais Samia atakayechukua fomu ya Urais wala kutia nia 2025 kwasababu ya utamaduni wetu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Soma nilichoandika na siyo kutoa maoni yao bila kulielewa andiko langu.sheria katika nini? Nimekuandikia andiko langu na kuweka hadi mifano na ufafanuzi wa kina.
Zingatia katiba ya nchi na katiba ya chama, kinacho fuatwa ni katiba ya chama inasemaje sio utamaduni wa maneno, utanielewa hukooo mbele mbele huko
 
Nyie watu mmegeuka machawa wa Rais mnaongea mengi ya kumsifia na kumaoaka mafuta kwa mgongo wa chupa lakini kiuhalisia hamna Nia njema kwa yeye Rais wala nchi.

Kesi ya Rais Samia ya kulazimishwa agombee pekeyake asiwe na mpinzani huko sisiem inafanana na kesi yangu enzi nipo shule.

Kipindi hiko nipo zangu form three nikachaguliwa monitor wa darasa. Hali haikuwa nzuri darasani kwa sababu nilikuwa mpole sana na nilishindwa kuwacontrol wale wanafunzi wahuni na watukutu hivyo darasa na uongozi ikawa kama unanielemea.

Matokeo yake nikawa napata adhabu Kila mara kutoka kwa walimu kwaakosa ya watu wengine ambao nilishindwa kuwacontrol (ulikuwa ni uzembe na kutowajibika vema).

Cha ajabu,tulipofika form four darasa Zima wakasema niendelee Mimi na nipite bila kupingwa, na Kuna watu walikuwa wanapigwa mikwara ya chinichini wasigombee umonita maana Mimi natosha. Nilipita Tena kwa kishindo.

Ila kiuhalisia wale wanafunzi wenzangu ambao walikuwa wababe hadi kuwanyamazisha wengine wasigombee kwa mabiti ya chini chini waliona udhaifu wangu ni nafuu kwao.

1. Walikuwa wanapiga kelele sana darasani.
2. Wanafika muda wanaotaka na wanaondoka Munda wanaotaka.
3. wakipewa adhabu alafu Mimi nisimamie walikuwa wnafurahi maana sikuwa kiongozi Bora wa kusimamia na kuwawajibisha vema.
4. Walifeli mtihani wa mwisho.

Wale wanafunzi ndiyo nyie sisiem mnajifanya kumsifia mama anaupiga mwingi na kuwachimba mikwara wengine wasigombee.kumbe za ndani mna agenda zenu za kuibomoa nchi maana mnajua kiongozi aliye madarakani mnammudu.
Embu acha utoto wa kutuletea habari za kitoto za shuleni kwenye jukwaa la watu wazima,wasomi na wenye kupevuka akili .hizo habari nenda kajadiliane na wenzako wa rika lako na siyo kutuchukulia sisi kama wanafunzi wenzako wenye mawazo ya kiwanafunzi.hapa tunajadili mstakabali wa Taifa letu.
 
Zingatia katiba ya nchi na katiba ya chama, kinacho fuatwa ni katiba ya chama inasemaje sio utamaduni wa maneno, utanielewa hukooo mbele mbele huko
Kwani ni wapi katiba ya Nchi inamzuia Mama yetu shujaa wa Afrika kuongoza Muhula wa pili?taja hicho kifungu
 
Mwaka 2025 Mama atagombea kwa Tiketi ya CCM na akishinda Uchaguzi ambao ni obvious atashinda hicho ndicho kitakuwa kipindi chake cha kwanza Rasmi cha miaka mitano !
Kisha 2030 akitaka kugombea tena kipindi cha pili atafanya hivyo !

Hapo vipi kwa wale wenye kuumezea mate Uprezidaaa ndani ya Chama letu ???!
Nadhani wengi wao Umri utakuwa umeshawatupa mkono 😳🙄

Ama kweli Waswahili walisemaga “ mkamia maji hayanywi “ 😅😂🙌👍

Au nasema uongo ndugu zanguni ???! 😱 !
 
Mi wala sikulaumu, ni kiwango cha njaa zako na dignity level uliyonayo inaamua uwe mwanaume au mtu na utu wake, au uuze utimamu wako!

Speaking of high level bullshit, nafikiri wewe unaongoza!

Lucas Mwashambwa
Mimi nimefanya kazi ya kuwapeni Elimu juu ya utaratibu na utamaduni wetu CCM
 
Ndugu zangu Watanzania,

Napenda kuwaelezeni na kuwapeni Elimu ndogo tu ya kuwa kwa utamaduni wetu CCM na wana CCM.ni kuwa hapo Mwakani hakutakuwa na Mwana CCM atakaye chukua fomu ya kugombea Urais .wala hakutakuwa na mtu yeyote yule mwanachama wa CCM atakaye tia nia wala kuonyesha kutia nia wala kutamka hadharani au mahala penginepo pale popote pale .

kuwa anataka kuchuana na Rais wetu Mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan katika kuomba ridhaa ya kupeperusha Bendera ya CCM.

Hii ni kwa kuwa kwa utamaduni wetu CCM ni kuwa mgombea wa CCM atakuwa ni Rais Samia pekee ambaye atachukua na kurejesha Fomu ya Urais,ni Rais Samia pekee ndiye atakaye achiwa nafasi ya kuchukua Fomu hiyo ya Urais,Ni Rais Samia pekee ambaye atakuwa na nafasi ya kuendelea na muhula wa pili wakuongoza Taifa letu,ni Rais Samia pekee ndiye anayetarajiwa kuiwakilisha CCM katika uchaguzi Mkuu hapo Mwakani dhidi ya vyama dhaifu na vilivyokosa Dira na muelekeo aina ya CHADEMA.

Pia soma: Kuelekea 2025 - Aliyekuwa mwanachana wa CHADEMA Mbunge Jesca Kishoa aomba 2025 itolewe Fomu 1 tu ya Urais kwa Samia Suluhu Hassan

Imekuwa hivyo kwa CCM tangia kuanza kwa mfumo wa vyama vingi hapa Nchini.Imekuwa hivyo wakati wa Hayati Benjamini Mkapa mwaka 2000,Imekuwa Hivyo kwa Mheshimiwa Daktari Jakaya Mrisho Kikwete 2010,Imekuwa hivyo kwa Hayati Mwalimu Daktari John Pombe Joseph Magufuli 2020 Na itakuwa hivyo kwa Mheshimiwa Rais wetu Mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan 2025.

Na ndio Maana mpaka sasa upinzani umejikatia tamaa kabisa ya hata kutafuta mtu wa kushindana na Rais Samia katika sanduku la kura.maana wanajuwa hawana mtu mwenye uwezo wala nguvu wala ubavu wala ushawishi wa kuweza kushindana na Mama huyu imara,hodari, shupavu na madhubuti kwelikweli.

Kwa sababu mtu yeyote yule mwenye akili Timamu na anayejitambua na asiye na upofu wa akili na macho anatambua kazi kubwa iliyofanywa na Rais Samia na serikali yake ya CCM iliyogusa Maisha ya watu na kuleta tabasamu na matumaini kwa mamilioni ya watanzania.

Ndio sababu ya kuona kwa sasa upinzani kama CHADEMA Wamekata tamaa hata ya kufanya mikutano ya hadhara.huwaoni hata wakifanya hamasa ya jambo lolote lile kama zamani.ndio maana unaona akina Mbowe wapo kama hawapo,huku watu kama lissu wakiwa mguu pande na njia pande kuendelea kukaa na kusalia CHADEMA au kutafuta makazi mapya.Ndio maana chama kinakwenda kama kipofu gizani.

Rais Samia amefanikiwa kuyaleta makundi yote kwa pamoja na kupata uungwaji mkono kwa kila kundi,kuanzia kwa vijana,wazee,akina mama kwote huko Mama Samia anakubalika na kuungwa sana mkono.huku CHADEMA ikisusiwa na kupuuzwa na watanzania.ndio maana mliona waliopoitisha hata maandamano aliishia kujitokeza Mbowe na mwanae tu ,huku Mke wake akiwa haieleweki kama alikuwa anakwenda kazini au kuwaomba majirani waandamane.Huku Mbowe akiwaomba waandishi wa habari akina Salimu KIkEKE waandamane naye.View attachment 3141244View attachment 3141254

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Wewe kweli ni chawa mkosa weledi. Tangu lini wewe ukawa msemaji wa wanaCCM wote? Ni wapi na lini mlifanya mkutano wa wanaCCM wote, halafu kukawa na maamuzi hayo, na wewe ukachaguliwa kuwa msemaji wao?

Au ni lini ilithibitika kuwa anachowaza Lucas ndiyo wanachowaza wanaCCM wote? Kwa nini usingekuwa unatafuta hoja zinazoonesha una upeo wa akili kuliko kudhalilisha utu wako kwa hoja za kipuuzi? Kwa nini uwadhalilishe wazazi wako kwa kiwango hiki!!
 
Wewe kweli ni chawa mkosa weledi. Tangu lini wewe ukawa msemaji wa wanaCCM wote? Ni wapi na lini mlifanya mkutano wa wanaCCM wote, halafu kukawa na maamuzi hayo, na wewe ukachaguliwa kuwa msemaji wao?

Au ni lini ilithibitika kuwa anachowaza Lucas ndiyo wanachowaza wanaCCM wote? Kwa nini usingekuwa unatafuta hoja zinazoonesha una upeo wa akili kuliko kudhalilisha utu wako kwa hoja za kipuuzi? Kwa nini uwadhalilishe wazazi wako kwa kiwango hiki!!
Umesoma andiko langu au umekimbia mbiombio kutoa maoni yako kama kawaida yenu Upinzani msiojitambua?
 
hakutakuwa na Mwana CCM atakaye chukua fomu ya kugombea Urais .wala hakutakuwa na mtu yeyote yule mwanachama wa CCM atakaye tia nia wala kuonyesha kutia nia wala kutamka hadharani au mahala penginepo pale popote pale .
Kwani wewe unawajua wana ccm wote hadi uwasemee?!!

Akijitokeza mtu kuchukua fomu ya kugombea dhidi ya Sa100 mtamteka?
 
Tufuate utamaduni au katiba, haki na uhuru?
 
Akijitokeza mtu kuchukua fomu ya kugombea dhidi ya Sa100 mtamteka?
Majibu yako yapo katika andiko langu.Lakini kila mwana CCM anafahamu utaratibu wa CCM.huwezi ukawa mwana CCM hai na usielewe jambo dogo kama hilo kuwa Mwakani anayestahili kuchukua Fomu ya Urais ni mmoja tu ambaye ni Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Napenda kuwaelezeni na kuwapeni Elimu ndogo tu ya kuwa kwa utamaduni wetu CCM na wana CCM.ni kuwa hapo Mwakani hakutakuwa na Mwana CCM atakaye chukua fomu ya kugombea Urais .wala hakutakuwa na mtu yeyote yule mwanachama wa CCM atakaye tia nia wala kuonyesha kutia nia wala kutamka hadharani au mahala penginepo pale popote pale .

kuwa anataka kuchuana na Rais wetu Mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan katika kuomba ridhaa ya kupeperusha Bendera ya CCM.

Hii ni kwa kuwa kwa utamaduni wetu CCM ni kuwa mgombea wa CCM atakuwa ni Rais Samia pekee ambaye atachukua na kurejesha Fomu ya Urais,ni Rais Samia pekee ndiye atakaye achiwa nafasi ya kuchukua Fomu hiyo ya Urais,Ni Rais Samia pekee ambaye atakuwa na nafasi ya kuendelea na muhula wa pili wakuongoza Taifa letu,ni Rais Samia pekee ndiye anayetarajiwa kuiwakilisha CCM katika uchaguzi Mkuu hapo Mwakani dhidi ya vyama dhaifu na vilivyokosa Dira na muelekeo aina ya CHADEMA.

Pia soma: Kuelekea 2025 - Aliyekuwa mwanachana wa CHADEMA Mbunge Jesca Kishoa aomba 2025 itolewe Fomu 1 tu ya Urais kwa Samia Suluhu Hassan

Imekuwa hivyo kwa CCM tangia kuanza kwa mfumo wa vyama vingi hapa Nchini.Imekuwa hivyo wakati wa Hayati Benjamini Mkapa mwaka 2000,Imekuwa Hivyo kwa Mheshimiwa Daktari Jakaya Mrisho Kikwete 2010,Imekuwa hivyo kwa Hayati Mwalimu Daktari John Pombe Joseph Magufuli 2020 Na itakuwa hivyo kwa Mheshimiwa Rais wetu Mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan 2025.

Na ndio Maana mpaka sasa upinzani umejikatia tamaa kabisa ya hata kutafuta mtu wa kushindana na Rais Samia katika sanduku la kura.maana wanajuwa hawana mtu mwenye uwezo wala nguvu wala ubavu wala ushawishi wa kuweza kushindana na Mama huyu imara,hodari, shupavu na madhubuti kwelikweli.

Kwa sababu mtu yeyote yule mwenye akili Timamu na anayejitambua na asiye na upofu wa akili na macho anatambua kazi kubwa iliyofanywa na Rais Samia na serikali yake ya CCM iliyogusa Maisha ya watu na kuleta tabasamu na matumaini kwa mamilioni ya watanzania.

Ndio sababu ya kuona kwa sasa upinzani kama CHADEMA Wamekata tamaa hata ya kufanya mikutano ya hadhara.huwaoni hata wakifanya hamasa ya jambo lolote lile kama zamani.ndio maana unaona akina Mbowe wapo kama hawapo,huku watu kama lissu wakiwa mguu pande na njia pande kuendelea kukaa na kusalia CHADEMA au kutafuta makazi mapya.Ndio maana chama kinakwenda kama kipofu gizani.

Rais Samia amefanikiwa kuyaleta makundi yote kwa pamoja na kupata uungwaji mkono kwa kila kundi,kuanzia kwa vijana,wazee,akina mama kwote huko Mama Samia anakubalika na kuungwa sana mkono.huku CHADEMA ikisusiwa na kupuuzwa na watanzania.ndio maana mliona waliopoitisha hata maandamano aliishia kujitokeza Mbowe na mwanae tu ,huku Mke wake akiwa haieleweki kama alikuwa anakwenda kazini au kuwaomba majirani waandamane.Huku Mbowe akiwaomba waandishi wa habari akina Salimu KIkEKE waandamane naye.View attachment 3141244View attachment 3141254

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Usiusemee moyo
 

Attachments

  • 5744975-8bcb85f1807b40dfe9b1bdf5a6eabbb0.jpg
    5744975-8bcb85f1807b40dfe9b1bdf5a6eabbb0.jpg
    8 KB · Views: 5
Back
Top Bottom