Uchaguzi 2020 Hakuna pingamizi atawekewa mgombea wa CHADEMA

Uchaguzi 2020 Hakuna pingamizi atawekewa mgombea wa CHADEMA

Trust me wale wagombea wengine waliopewa kipaumbele na kuharibu ratiba wakaingia fasta wakapokelewa na kupitishwa haraka wamefanya makosa mengi ya kisheria..na hili litawagharimu pakubwa.
Acha kufikiria kwa kutumia mapigo ya moyo
Mnajitia hofu isiokuwepo,hakatwi mtu hapa hata likitoka pingamizi,tunata mshindwe mapema tena bila visingizio
 
Ni kujipa moyo tu kwa CDM. hakuna mambo ya kiroho uliyoyaelezea. Siasa ni sayansi na inataka mipango. Sasa wewe danganya watu na habari za kiroho ni dalili njema. CDM wajipange kwa kila hatua. Ambao hawakupita mikoani walijipanga pia kwa sababu zao kadhaa lakini pia hakukua na haja.

Tundu Lissu ange save the last dance for wakati wa kuomba kura. Watu wangejawa na shauku kubwa zaidi ya kumwona wakati wa kampeni.but pia ange save gharama zisizo na sababu.

Tufikie hatua tuwe tunaandika kisayansi na si kihisia na kujidai tunafahamu mambo ya rohoni.hayo ni siri kubwa anayoijua Mungu tu.
 
Sheet hole ndo nini? Badala uwekeze kwenye elimu unakuja jaza server hapa na kuandika utumbo.

Aibu hata enzi ya chama kimoja Nyerere alikuwa anashindanishwa na kivuli chake ndiyo inapatikana hiyo % sasa leo wajumbe 150 ndiyo wanatupa Mbunge Aibu Sheet hole kweli kweli halafu tunasema tuna wasomi karne hii vitu vya ajabu hapo hata helkopta ya mabua hatuwezi tengeneza
 
Na watu wanajipanga hujui watakuja kwa njia gani. Lissu mwenyewe kasema sasa anajiandaa kwa ajili ya pingamizi. Yeye ambaye anajielewa. Haya mambo yanataka uelewe sayansi ya siasa.
 
Majimbo aliyozunguka Lisu kutafuta wadhamini Ni 20 CCM tayari imeshachukua majimbo 22 ambayo wabunge wa CCM wanepita bila kupingwa

Hapo unaweza kuona kuwa ziara zake Ni hopeless sababu Hadi Sasa Hana mbunge kote alikozunguka

1598411302592.jpeg
 
Majimbo aliyozunguka Lisu kutafuta wadhamini Ni 20 CCM tayari imeshachukua majimbo 22 ambayo wabunge wa CCM wanepita bila kupingwa

Hapo unaweza kuona kuwa ziara zake Ni hopeless sababu Hadi Sasa Hana mbunge kote alikozunguka
Tupu zenu ziko nje

1598411399625.jpeg
 
Sharti ilikuwa wasiopungua 200 kila mkoa bila kizuizi hata wadhamini wakiwa 10,000 kila mkoa hivyo kuwa na Amani kila mkoa Tundu Lissu alipata wadhamini kwa mamia ya makumi, ndiyo maana hata Tume ilipelekewa Maboksi na Maboksi . Hilo la wadhamini wala usitie shaka lori semi trela lenye nyaraka lipo Dodoma.
Nasema kama wanafikiria kuwawekea pingamizi wagombea wengine, nawashauri wafanye hivyo. Lisu katekeleza vema sharti la wadhamini!
 
Na ningekuwa Lissu ningeweka pingamizi kwa wagombea wote,

Mshana Jr hela ya kampeni humu jf tunatosha kuchangia, waseme tu halafu waone. Tena hata yule dada wa kwa trump hatumtaki achangishe haeleweki.

Unasema moshwari leo kuko kimya, duuu, nshasema nikifa nizikwe on the sport sitaki uje kunibaka nikiwa maiti looooh.
 
Umeandika vema, well articulated.
1. Inahitajika timu ya watu tangu jana alipoitishwa kupitia jina kwa jina na kupiga smu kuhakiki kama hao bado wanaishi.. unawapigia simu wote kuona atakaye pokea au ambazo hazitapokelewa zitakuwa ngapi. Ukipata 10% hzijapokelewa, then unaweka pingamizi
2. Wanasheria kupitia fomu za waliopitishwa kuzihakiki.. kutafuta dosari kama zipo....sijui taratibu huwa zinakuwaje , unapewa kila kopi ya aliyepitishwa?

LAKINI: Mshana jr was it deliberate kutohakikiwa mikoani au walikuwa hawajui? Kama walikuwa hawajui, that is a grave mistake to recorn!
I think that was a tricky bro ....ile walichokifanya chadema ni bonge moja la akili kwa sababu kadhaa .
1.kuwafanya wawe kwenye midomo ya watu na media for a long time before selection kuliko vyama vyingine..hili wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa sana.
2.kuchelewesha zoezi la wao kutangazwa ili kuepusha wale wenye mapingamizi wasije kuwa na mda wa kufanya hivyo.
3. Hili linaweza kuwa halikuwa kwenye sababu za kwanini hawwakuhakiki huko majimboni nalo ni kuwakeep busy watu wa nec na chadema pekee maana chadema walikuwa na uhakika na kazi yao
4.kama wangepitishwa mchana kama ilivyokuwa kwa chauma au act etal isingekuwa breaking news kama ambavyo umetokea ....hapa haiihitaji ushahidi kulitambua......yote Tisa, Kumi ni hili la kutuweka roho juu Takriban masaa sita aisee that was tough time amongst the tough time ever...Hali ya jana sikumbuki ni lini katika maisha yangu nimewahi kuwa nayo ...nadhani asingepita ningeumia sana lakini yawezekana mimi ni strong ila kunawatu wengezimia kama siyo kufa....

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Majimbo aliyozunguka Lisu kutafuta wadhamini Ni 20 CCM tayari imeshachukua majimbo 22 ambayo wabunge wa CCM wanepita bila kupingwa

Hapo unaweza kuona kuwa ziara zake Ni hopeless sababu Hadi Sasa Hana mbunge kote alikozunguka
Lengo la kuzunguka lilikuwa ni kutafuta wadhamini. Sisi tumepata hao wabunge kwa figisu figisu za kishamba kama za kule Ruangwa na Mtama. Hili si la kujisifia hata kidogo, ni la kufikirisha sana na linahitaji hofu ya Mungu kuliepuka. Tujiandae kwa kampeni zitakazotupa wakati mgumu kujibu baadhi ya mashambulizi, yaani tulijua vita imekwisha tukapiga maji tukalala, adui aliyekuwa mahututi kaibuka na kutushtukiza sasa tuna muda mchache wa kujipanga na atatusumbua kwa kweli. Mechi imebadlika dakika za majeruhi, wachezaji wa akiba tushawaweka wote, refa na washika vibendera plus kamisaa wa mechi ni wa kwetu lakini bado tunambwela mbwela na kufanya mambo ya kitoto.
 
Hivi huwa ukiandika unafikiri kweli au unaandika tu almradi uonekane umeandika!?
Wew ni fala kweli yaani anazunguka halafu anaachakufanya yale ya msingi yanayomhusu ,? Ni akili za wapi kila kitu kipo clear unazunguka halafu hao wadhamini wanahakikiwa na mkurugunzi wa uchaguzi kwa jimbo husika?
 
Chadema wajipange na kampeni tu sasa. And vile vile waweke pingamizi kwa hawa waliopita bila kupingwa.
Kwanini wapite bila kupingwa, ccm wanaogopa uchaguzi? Hili halikubaliki, tunawanyima wananchi haki yao
 
Umeandika vema, well articulated.
1. Inahitajika timu ya watu tangu jana alipoitishwa kupitia jina kwa jina na kupiga smu kuhakiki kama hao bado wanaishi.. unawapigia simu wote kuona atakaye pokea au ambazo hazitapokelewa zitakuwa ngapi. Ukipata 10% hzijapokelewa, then unaweka pingamizi
2. Wanasheria kupitia fomu za waliopitishwa kuzihakiki.. kutafuta dosari kama zipo....sijui taratibu huwa zinakuwaje , unapewa kila kopi ya aliyepitishwa?

LAKINI: Mshana jr was it deliberate kutohakikiwa mikoani au walikuwa hawajui? Kama walikuwa hawajui, that is a grave mistake to recorn!
Watakuambia ni nguli wa sharia sasa ntashindwaje kungamua swala dogo kiasi hicho
 
Tundu ni mtu wa pekee sana, ana utofauti na hao wengine wagombea, sikuwahi sikia hata mkuu wa nchi kuzunguka kutafuta saini mbali na pale alipopokea lile gimbi. Hivi hakujua mtaani au kijijini mtu mpaka ufuge gimbi lifikie pale linakuwa limebeba maroho yote, hili mtani utalijua kiroho.

Gimbi linaona watu wakizaliwa, wakiroga, wakitambika, wakifa, limeshughudia misiba limesikia watu wakisema na linaongea na ardhi, leo hii mkuu top leader unalishika kwenye kadamnasi, haikuwa nzuri.

Mwalimu Nyerere alipokuwa anapewa zawadi walikuwa wanampokelea. Na akitoka hapo anaenda kwa kiongozi wa mila kusema naye.

Anyways hayatuhusu,

Ya Lissu leo ni makubwa, ni nini kimewalazimisha kushezesha orodha? Suala la kiroho sana hilo.

Je hao wagombea wengine waliopitishwa tu yaani bora liende si ni lazima watakuwa bora liende, tutaona.

Ni nini kilikusudiwa kimtokee, mpaka ikafika tunaona namba za magari kuwa yanamngoja nje tukasikia mengi mengi vile.

Mwisho nguvu zao zikamezwa, Ikawa kimyaaa.

Sitaki kumalizia kuandika kitu ambacho kilishaandikwa, ardhi ni shahidi. We will see.

Mshana Jr hulali ?
Tundu Lissu anaona mbali...... Matukio mengi machafu amesha ya pre empty kabla hata hayajatokea huyo ndio Tundu Lissu kipenzi cha watz

Mbona magufuli yuko bize makanisani na misikitini anagawa rushwa takukuru wako kimya?
 
Majimbo aliyozunguka Lisu kutafuta wadhamini Ni 20 CCM tayari imeshachukua majimbo 22 ambayo wabunge wa CCM wanepita bila kupingwa

Hapo unaweza kuona kuwa ziara zake Ni hopeless sababu Hadi Sasa Hana mbunge kote alikozunguka

Kwa nini unatumia neno "Hopeless" ikiwa hujui maana yake? Weka Kiswahili tu.
 
Back
Top Bottom